Bunge la bajeti 2011/2012 na yatokanayo

Bunge la bajeti 2011/2012 na yatokanayo

Sijawaelewa hapo why wasamehewe kodi hii si itaongeza gape kubwa sana kati ya walionacho na wale wasionacho?
 
Badala ya kutengeza budget itakayo saidia utengenezaji wa barabara na kupunguza kero ya usafiri, polisi nao wanapewa mgao wa kujipatia kipato
 
https://www.jamiiforums.com/busines...-watumishi-wa-serikali-na-mashirika-yake.html


Tafsiri yangu kutokana na kutotoza kodi kwenye posho za watumishi wa serikali na taasisi nyingine zinazopata ruzuku ya serikali ni kuwa "watawala wameungana na wafanyakazi wao na wanasiasa" kutekeleza sheria ya mapato ya mwaka 2004 kibaguzi. Nasema hivi kwa sababu mabadiliko hayo yatawahusu:
(i) Viongozi wakuu wa serikali ambao mbali na mishahara yao wana posho mbalimbali zinazozidi hata mishahara ambazo kwa mujibu wa sheria ya mapato ya mwaka 2004 zinatakia kulipiwa kodi lakini kwa kuwa wao ndio walioshika mpini wameamua kutokulipa kodi;


(ii) Wafanyakazi wa serikali na taasisi zake nao wanaungana na watawala kutokulipa kodi. Kwa tafsiri hii watajipangia mishahara midogo na sehemu nyingine kujilipa kama posho na hivyo kutokulipa kodi;

(iii) Wanasiasa - kutokana na vyama vya siasa kupata ruzuku ya serikali watawalipa watumishi wao posho badala ya mishahara na hivyo kutokulipa kodi kabisa.

Matokeo hasi ya mabadiliko haya ni kuwa

(a) Utendaji wa TRA kwenye kuhimiza ulipaji wa kodi za mishahara kwenye sekta binafsi hasa kwenye posho utapata upinzani, ilitakiwa wadai kodi wakionyesha mfano wa wao kulipa hizo kodi kinyume chake wao hawatalipa bali watawataka wafanyakazi wa sekta binafsi walipe. Wakati wa utawala wa Mh. Mwinyi, serikali ilifuta kodi kwenye posho na matokeo yake Mh. Mustafa anafahamu kwani Serikali ilikuwa na hali mbaya sana kifedha na

(b) Nia ya serikali kukuza sekta binafsi itafifishwa na rekebisho hili kwani nguvu kazi kubwa itapendelea kufanya kazi kule ambako watalipa kodi kidogo

(c) Kutakuwepo tofauti ya mapato kwa watu wa kada moja mfano nesi anayefanya kazi serikalini posho zake za night allowance hazitatozwa kodi lakini nesi ambaye yuko hospitali binafsi posho zake za night allowance zitatozwa kodi.

Mtazamo wangu ni kuwa rekebisho hili ni mtego mkubwa kwa wabunge wetu. Endapo watapitisha rekebisho hili, ina maana wako bungeni kwa maslahi binafsi kwani wao na vyama vyao ni sehemu ya watu watakaofaidika na rekebisho hili. Kwa upande mwingine, chama cha waajiri Tanzania na vyama vya wafanyakazi ambao si wa sekta ya umma ni wakati mwafaka kujitokeza na kupinga rekebisho hili kwa ajili ya ustawi wa nchi yetu.
 
tuzingatie sheria na magari mabovu yasiingie barabarani maana ajali zimezidi mkuu
 
Nani msemakweli - maneno ya mdomoni ya waziri Mkulo au taarifa iliyoandikwa na yeye mwenyewe? Ina maana hakusoma kilichoandikwa; je achukuliwe hatua gani?
84. Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani, Sura, 168 ili kuongeza ukomo wa kiwango cha faini inayotozwa kwa kufanya makosa wakati wa uendeshaji gari barabarani (Traffic Notification Fee) kutoka shilingi 20,000 hadi shilingi 300,000.

ndo hapa sasa umakini hamna kabisa kwa watawala wetu...
 
Hapa ndio uwa naona siasa za Tanzania ni Controversy tu, hamna kitu chochote, wakati wa kampeni mnapita kwenye majimbo mnatoa ahadi za matumaini ili tuwachague kumbe ilikuwa usanii?
 
Bunge limejaa vilaza uwezo wa kujadili bajeti kwa mustakabali wa nchi hawana sasa wafanyaje? Ni aibu wangeishia kulala na kukoroma sishangai sana, wabunge wetu umuhimu wanauona ni kutetea posho za vikao, labda watanzania watalichukulia kama ni funzo kwa chaguzi za baadae, haya tuliyasema sana darasa la saba na ubunge wapi kwa wapi? Mawaziri na Ph.d za kupika wabunge std 7; kazi tunayo mwaka huu.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Nahisi wabunge wa CCM wamekacha, baada ya kuona hamna la maana linaloendelea maana bajeti ni ile ile ya miaka zote, hakuna mbadala zaidi ya kuongeza Faini kwa madereva, Kodi katika bidhaa ambazo ni muhimu kwa maisha ya kila siku ya mwananchi, nawapa Big UP wana Magamba kama mlikacha kwa yale ambayo nimeyaanisha hapo juu,
 
https://www.jamiiforums.com/busines...-watumishi-wa-serikali-na-mashirika-yake.html


Tafsiri yangu kutokana na kutotoza kodi kwenye posho za watumishi wa serikali na taasisi nyingine zinazopata ruzuku ya serikali ni kuwa "watawala wameungana na wafanyakazi wao na wanasiasa" kutekeleza sheria ya mapato ya mwaka 2004 kibaguzi. Nasema hivi kwa sababu mabadiliko hayo yatawahusu:
(i) Viongozi wakuu wa serikali ambao mbali na mishahara yao wana posho mbalimbali zinazozidi hata mishahara ambazo kwa mujibu wa sheria ya mapato ya mwaka 2004 zinatakia kulipiwa kodi lakini kwa kuwa wao ndio walioshika mpini wameamua kutokulipa kodi;


(ii) Wafanyakazi wa serikali na taasisi zake nao wanaungana na watawala kutokulipa kodi. Kwa tafsiri hii watajipangia mishahara midogo na sehemu nyingine kujilipa kama posho na hivyo kutokulipa kodi;

(iii) Wanasiasa - kutokana na vyama vya siasa kupata ruzuku ya serikali watawalipa watumishi wao posho badala ya mishahara na hivyo kutokulipa kodi kabisa.

Matokeo hasi ya mabadiliko haya ni kuwa

(a) Utendaji wa TRA kwenye kuhimiza ulipaji wa kodi za mishahara kwenye sekta binafsi hasa kwenye posho utapata upinzani, ilitakiwa wadai kodi wakionyesha mfano wa wao kulipa hizo kodi kinyume chake wao hawatalipa bali watawataka wafanyakazi wa sekta binafsi walipe. Wakati wa utawala wa Mh. Mwinyi, serikali ilifuta kodi kwenye posho na matokeo yake Mh. Mustafa anafahamu kwani Serikali ilikuwa na hali mbaya sana kifedha na

(b) Nia ya serikali kukuza sekta binafsi itafifishwa na rekebisho hili kwani nguvu kazi kubwa itapendelea kufanya kazi kule ambako watalipa kodi kidogo

(c) Kutakuwepo tofauti ya mapato kwa watu wa kada moja mfano nesi anayefanya kazi serikalini posho zake za night allowance hazitatozwa kodi lakini nesi ambaye yuko hospitali binafsi posho zake za night allowance zitatozwa kodi.

Mtazamo wangu ni kuwa rekebisho hili ni mtego mkubwa kwa wabunge wetu. Endapo watapitisha rekebisho hili, ina maana wako bungeni kwa maslahi binafsi kwani wao na vyama vyao ni sehemu ya watu watakaofaidika na rekebisho hili. Kwa upande mwingine, chama cha waajiri Tanzania na vyama vya wafanyakazi ambao si wa sekta ya umma ni wakati mwafaka kujitokeza na kupinga rekebisho hili kwa ajili ya ustawi wa nchi yetu.

hapo lazima tujue kama tuna vichwa bungeni au matumbo ...........wasindikizaji na wabinafsi.!
 
Wakubwa wanakubali kuwa gharama za maisha zimekuwa juu na hivyo wamebuni mbinu ya kupunguza makali hayo kwa wao wenyewe, kwa hiyo wategeuza malipo yao mengi yawe kwenye category ya posho na hiyo kukwepa makato. Wananchi watabaki kuwa 'cash cow'.
 
Nami naona nijadili machache juu ya bajeti:

"Mheshimiwa Spika, ili kupunguza makali ya ongezeko la bei ya mafuta nchini, Serikali imeamua kufanya mapitio ya namna ya kukokotoa tozo zinazotozwa na Mamlaka mbalimbali kwa lengo la kuzipunguza na zoezi hili litakamilika katika mwaka wa fedha 2011/12."

Hizi ni blabla za kisiasa tu. Yaani mapitio na namna ya kukotoa ndiyo yatakamilika 2011/2012, siyo urekebishaji wa tozo hizo! Hivyo bei ya mafuta uko pale pale

".kuingiza sekta isiyo rasmi kwenye mfumo wa kodi;"
Hata kwa tafsiri ya neno lenyewe (sekta isiyo rasmi) ina maana ya sekta isiyo na utaratibu rasmi. Hawana kumbukumbu, leo wapo kwenye biashara kesho hawapo, hawana maeneo maalum nk. Kwa vyovyote kodi za sekta hii zitakuwa ni za kukadiria tu – hapo ndipo rushwa itakapokithiri. Ebu fikiria unamtozaje kodi mama-ntilie!
Je hatua hii inapunguza ukali wa maisha?

"Maslahi ya Watumishi
68. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha maslahi ya watumishi kulingana na uwezo wa mapato yake kwa lengo la kuwawezesha kumudu gharama za maisha. Maeneo ambayo yatatiliwa mkazo ni pamoja na malipo ya mshahara na likizo kwa wakati, kuhakikisha watumishi wanalipwa mafao yao mara baada ya kustaafu, pamoja na pensheni zao za kila mwezi. Sambamba na hayo, Serikali itatoa mafunzo kwa maafisa wa Hazina ndogo na wa mahakama zote zinazoshughulikia mirathi, na kuweka mikakati ya pamoja kuwaondolea kero wasimamizi na warithi wa mali ya marehemu."
Watumishi hapa mmepigwa changa la macho. Serikali itaendelea kuboresha maslahi, lakini maeneo yatakayotiliwa mkazo si kuongeza mishahara! Poleni sana. Silaha ya mfanyakazi kuongezewa mshahara si kumbembeleza mwajiri bali kumshinikiza!


"Baadhi ya hatua zitakazochukuliwa, ni pamoja na: kuendelea kuboresha mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa mapato kutoka vyanzo vya Halmashauri; kupitia upya vyanzo vya Halmashauri vilivyofutwa; kupitia mfumo wa kodi ya majengo katika majiji, manispaa, miji, wilaya na miji midogo; na kuainisha mianya ya upotevu wa mapato na vyanzo mbadala vya kuongeza mapato ya Serikali za Mitaa."

Hapa waziri anataka baadhi ya vyanzo vilivyofutwa sasa virudishwe. Hii yaweza kuwa kodi ya maendeleo, gharama za leseni nk. Je ametafakari sababu zilizopelekea kuondolewa kwake. Je kuna mabadiliko ya mazingira kwamba zilipofutwa hali ilikuwa hivi na sasa imeboreka kiasi cha kurudisha kodi hizo? Je hii itapunguzaje ukali wa maisha? Kumbuka hapa inaongelewa kodi kwenye halmashauri ambako ndiko wananchi wanaishi!


"Kusamehe kodi ya mapato kwenye posho wanazolipwa wafanyakazi wa Serikali na wanaofanya kazi kwenye Taasisi zinazopata ruzuku kutoka kwenye bajeti ya Serikali.."

Huu ni ubaguzi wa wazi katika bajeti. Fikiria wewe ni mtumishi wa sekta isiyopata ruzuku ya serikali, unakwenda katika semina au warsha au mkutano ambao pia unahudhuriwa na watumishi wa serikali na mashirika yanayopata ruzuku ya serikali. Nyote mnalipwa posho ya Tshs 50,000 kwa siku. Wewe posho yako ihesabiwe kama sehemu ya mapato yako wakati wa kukokotoa kodi ya mapato lakini kwa hao wengine isihesabiwe hivyo! Nyote ni watanzania, mnakula chakula kile kile, mnalala sehemu ile ile. Huu si ubaguzi wa hatari?

"b)Halmashauri za Wilaya zitoze na kukusanya Ada ya leseni ya biashara ya shilingi 30,000 kwa mwaka kwa biashara zinazoendeshwa katika maeneo ya miji midogo na vituo vya biashara."
"c)Halmashauri za vijiji zitoze na kukusanya shilingi 10,000 kwa mwaka kwa kila biashara inayoendeshwa katika maeneo yake."

Ada ya leseni hizi ilifutwa huko nyuma baada ya kuonekana ni kero kwa wananchi. Je sasa sababu za kuifuta zimekwisha? Waziri anaweza kutueleza sababu hizo zimekwisha vipi? Halafu hizi ni flat rate – yaani kwa kila biashara, kana kwamba biashara zote zinafanana! Halafu hapo umepunguza ukali wa maisha!
"84. Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani, Sura, 168 ili kuongeza ukomo wa kiwango cha faini inayotozwa kwa kufanya makosa wakati wa uendeshaji gari barabarani (Traffic Notification Fee) kutoka shilingi 20,000 hadi shilingi 300,000."

Fursa za rushwa zimeongezwa! Hata kama itakuwa ni hiyo 50,000 aliyotamka waziri. Ni vizuri ikawa kila kosa na fee yake badala ya kujumuisha makosa yote. Fikiria mtu ambaye anaendesha pikipiki lakini kwa bahati mbaya amesahau kadi ya pikipiki au leseni nyumbani – fee 300,000! (maana sheria inasema lazima uwe navyo wakati wote iwe mvua au jua) Nadhani pia kuna kasoro kubwa katika utungaji wa sheria. Wanatunga sheria za magari halafu wanazihusisha na pikipiki. Kwa mfano road licence (kwa sheria) inatakiwa ibandikwe kwa ndani kwenye kioo cha mbele! Mwenye pikipiki kioo hicho ni kipi?
Kwa sasa naishia hapo; nitaendelea na uchambuzi kadri muda utakavyoruhusu.
 
Wameona wahalalishe tu ndugu yangu. Ninavyofahamu mimi kuna posho nyingi sana wanalipwa huko serikalini ambazo hazikatwi kodi. Ni mashirika ya serikali na secta binafsi ambaso ndizo zinazolipwa kodi.
 
lets see what the impact will be and what are those taxes being talked about. i want to hear that they have done something on excise duty, fuel levy, EWURA charges, TBS charges, WMA charges, TPA charges, TCFB charges, IDF charges, etc.
 
Tangu nianze kufuatilia habari za bajeti ni mwaka wa 6 sasa. Serikali kuna baadhi ya miaka ilikuwa inakuja na bajeti tamu hadi unaona nchi sasa itaendelea. Mwaka huu pamoja na mapungufu ya ubunifu wa vyanzo vipya vya mapato na kuendelea kung'ang'ania vyanzo asili kama bia na sigara na kusahau maliasili yetu iliyojaa tele ambayo kama tungetoza kodi ipasavyo tungekuwa mbali, bajeti ni afadhali. Serikali inasema itapunguza posho mbalimbali, itanunua magari pale inapobidi kwa kibali cha PM, kodi kadhaa za mafuta ya petroli zitafutwa, etc.

Lakini siku zote maneno yamekuwa mengi bila utekelezaji. Naamini hata bajeti hii zitapigwa hadithi nyingi sana wakati wa utekelezaji na mwisho wa siku kutakuwa hamna kitu na mwakani serikali itarudi na hadithi kibao; mi nimesema tu ... au siyo waungwana
 
Hawa watu wanatumia matumbo kufikiria. Kwa hiyo mhudumu wa baa anapaswa kulipa kodi kwa pesa yote anayolipwa na bosi wake, lakini mfanyakazi wa TTCL asilipe kodi ya posho yake. Huu ni ukosefu wa kufikiria, ni njia ya kuua morari wa kulipa kodi na ni njia ya kuua sekta binafsi. Hawafikirii, kazi kukurupuka tu. Hivi huwa wanafanya kazi au huwa wanapanga bajeti kwa siku mbili. Siwezi amini mtu huyu kazi yake ni kufanya mipango na huu ndo mpango aliokuja nao. Huu ni uchafu!
 
Mungu Ibariki Tanzania. Utusamehe pale tulipokukosea naomba uwaongoze wale uliowaweka kutuongoza wafanye yale yakupendezayo wewe! Amen!
 
Chadema ni kama mwanamke mjamzito akifanyiwa zuri kwake karaha akifanyiwa baya ndio tabu! Sasa mnataka Serikali ipuuze kila linalosemwa na Upinzani!

BORA MJAMZITO...ni mimba changa.......perfume kichefuchefu....samaki rosti anatapika......labda UDONGO(pemba), NDIMU,MBILIMBI NA KACHUMBARI KWA MBAALI
 
Haya yote ni matokeo ya mdomodomo wa NAPE na kimbelembele cha TRA kuhusu mshahara na posho ya Dr. Slaa.

Ninavyofahamu viongozi wakuu wote wa serikali na wabunge wanalipwa mi-posho mingi ambayo haikatwi kodi kinyume na sheria hadi jana alipohalalisha Mkulo.

Dr. Slaa alikuwa anaandaa kumulipua JK kuhusu POSHO na MARUPURUPU anayolipwa kila mwezi ambayo hayakatiwi kodi. Alikuwa bado akikamilisha kukusanya hizo data. Pia Dr. Slaa alikuwa yuko njiani pia kuwalipuwa wabunge kuhusu POSHO wanazopokea ambazo hazilipiwi kodi e.g. subsistance allowance, Sitting allowance, posho ya mafuta, posho jimbo (kwa wenye majimbo) etc.

Ili kum pre-empty Dr. Slaa, Mkulo ameona ahalalishe huo ukwepaji wa kodi kabla Dr. Slaa haja open a pandora box. Kwa wale tusiokuwa wafanyakazi wa serikali na Taasisi zake TULIE tu. Kwani sasa hivi Serikali imehalalisha watumishi wake na Taasisi zake kukwepa kulipa kodi.

Sheria za nchi hii zina macho, kama suala ni kuwapunguzia wafanyakazi makali ya maisha kwanini basi iwe kwa wafanyakazi wa serikali tu na sio wafanyakazi wote including wa private sector? BE THE JUDGE YOURSELF!
 
Back
Top Bottom