Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha Sheria inayotoa mamlaka kwa mtu kujipima UKIMWI

Jela miaka 30 lakini huyo huyo binti wa miaka 15 anapewa kifaa na serikali ili asiambukizwe maambukizi. Hapa mbona kama tunawinda wenyewe kwa wenyewe sasa!!!!
 
Hahahaa Baharia tulia! Nasikia ukifika siku hizi ukitaja hilo Jina unakamatwa! Nenda hadi mitaa ya Stendi pale kisha mtafute Baharia muelewa muulize....ni jirani tu
MAKEI inapatikana maeneo gani hapo Mafinga Mkuu wa Kikosi? Nataka nikafanye utafiti kidogo.
 
Angalizo: Kuna watu wakishapima wanapata shock iwapo majibu yatakuwa tofauti na matarajio,chondechonde usichukue maamuzi yeyote mpaka uonane na daktari.
 
Na kwenye vipimo ivyo waweke kabisa alama + au - kumaanisha positive au negative.
 
Kuna issue ya Takwimu,idadi ya walioambukizwa itakuwa ngumu kupatikana hivyo kuathiri utungaji wa sera,

Pili, kutokana na kupima nyumbani kutakuwa hakuna ushauri nasaha karibu., mtu anaweza kuchukua hatua za kujidhuru na hata kujiua pindi anapojua ameathirika.
 
Kwa hiyo hivi vipimo havitauzwa kwa kificho tena?
 
Wakuu mwenye uelewa afafanue matumizi ya kipimo hicho na upatikanaji, pia kinywa ina maana denda, mate yanaweza onyesha!?
 
Sijui lengo haswa ya maamuzi haya ni nini, kuna changamoto nyingi sana kwenye utekelezaji wa upimaji na hatimae ufuatiliaji wa matumizi ya dawa, ni miezi zaidi ya miwili sasa upimaji umesimama kwa ukosefu wa Unigold, dawa za kuzuia maambukizi ya Tb ( IPT ) upatikanaji wake ni tatizo, huduma za upimaji ( Liver and Renal function tests, viral load, CD4 na vingine havifanyiki kama miongozo Inavyotaka) kwa nini wizara isitatue kwanza changamoto zilizopo kabla ya kuanzisha hili jipya?
 
Pamoja na Kondom
 
Waungwana, salama!

Kwa mujibu wa hii sheria mpya, unaweza kununua na kuhifadhi vipimio vya ‘HIV’ ndani kwako kwa ajili ya matumizi binafsi na ya kifamilia, wapo wanaopongeza hatua hiyo na wengine kusimama kinyume.

Pamoja na ukweli kwamba suala la maambukizi ya virusi ‘vinavyoweza’ kusababisha UKIMWI (VVU) ni tatizo kubwa, elimu ya kujikinga na kujiepusha na maambukizi mapya bado haipewi uzito unaostahili, hivyo kupelekea kasi ya maambukizi kuendelea kupanda kila kukicha.

Elimu inayotolewa bado haijawafikia walio wengi ukiacha ile kidogo ya awali ambayo wengi tumeipata tungali wadogo sana shule ya msingi, kwa wakati huo tuliamini na kuogopa kweli kweli lakini kumbe ni kwa vile tu tulikuwa hatujaonja asali. Waathirika wakubwa ni ‘watu wazima’ ambao kwa asilimia kubwa hawana tena muda wa kuendelea kupatiwa elimu sahihi hivyo hujikuta katika hatari zaidi ya kuambukizwa na kusambaza.

Kumekuwa na changamoto katika upimaji wa afya kwenye vituo husika, huku ikiripotiwa kuwa wanaume sio wengi wanaojitokeza kwa hiari huku wanawake wakilazimika kufanyiwa vipimo hasa kipindi wanapokuwa wajawazito na hata hao wanaolazimika kupima (ME/KE) inapotokea upenyo wengi wao hukimbia ‘majibu’ au huwa hawapo tayari kujua ukweli.

Sasa kwa sheria hii inaruhusu upatikanaji ‘holela’ wa vifaa vya kupimia VIRUSI, mtu kwa hiari yake ataweza kujipima na kujipa majibu akiwa amejifungia au akiwa na watu ambao mwenyewe karidhia kuwa nao, lakini je elimu inatosha juu ya kupokea matokeo ya vipimo?

Imeshawahi kunitokea mimi enzi za ujana wangu, japo ilikuwa kinyume na sheria ila nilifanikiwa kuwa na vipimio ndani na mara kadhaa nilikuwa naibuka mshindi kwa kutengeneza matokeo CHANYA kabla ya mechi, ila siku moja ikatokea mambo yakasoma ‘kekundu’ kwa huyu ‘mshirika’ ambaye umemshawishi na kumpima. Je, utakuwa katika nafasi gani kumfanya akubaliane?

Tunahitaji elimu, elimu, elimu.

UKIMWI upo, japo umepunguza sifa hivyo umetulia kama vile haupo ila takwimu ziko sahihi.

Pima. Jitambue. Ishi.
 
ELIMU NI MUHIMU SANA.

Ila napongeza uwepo wa vifaa madukani ambapo raia anaweza kununua kama panadol, nakumbuka enzi ulipotaka kununua condom ilikuwa mpaka watu watoke dukani ubaki na muuzaji au unaenda na kimemo.

So kwa hatua hii nadhani itasaidia wananchi kujitambua binafsi na baadhi watakwenda wenyewe kuchukua ARV kabla nazo hazijawekwa kwenye maduka.
 
kwanini nipime ukimwi
 
saivi kabla hujanipa hata ulimi wako

tutoboane kwanza,uuuuuuuh acha nifanye mazoezi ya udaktari

zero aikyu atatoboa wadada wa watu spati picha...
 
Hivi vipimo kila mwezi ndani kwangu nilikuwa napeleka nje kutupa dusbin limejaa kwenda kutupa baada ya kutumika, sio muumini wa condom hivi vipimo ndo vilikuwa kinga yangu, kwa vile wameruhusu sasa nitakuwa huru kununua tani nzima ya H.I.V test
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…