Bunge la katiba: Kura ya uwazi (ccm) au siri (taasisi nyingine)

KURA IWE YA UWAZI AU SIRI


  • Total voters
    41
  • Poll closed .

Chadema Diaspora

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2010
Posts
480
Reaction score
644
Kwa nini wajumbe wote walio changia kutaka kura ya WAZI ni CCM, lakini wanao taka kura ya SIRI ni wanatoka makundi mbarimbari?

Hawa ni baadhi ya wanaotaka kura ya WAZI

1.Pfr.Anna Tibaijuka, (CCM)
2.Hawa Ghasia, (CCM)
3.Hamis Kigwangala, (CCM)
4.Henry Shekifu, (CCM) 5.Stephen Wassira, (CCM)
6.Willium Lukuvi (CCM) etc...

Hawa ni baadhi ya waliochangia kutaka KURA YA SIRI

1.Halima Mdee, (CHADEMA)
2.Hashim Rungwe, (NCCR)
3.Mch.Msigwa, (CHADEMA)
4.John Mnyika, (CHADEMA)
5.Esther Bulaya, (CCM)
6.Juma Haji Duni (CUF).
7.Prof.Juma Kapuya (CCM)

So observation ya haraka inaonesha KURA YA SIRI inaungwa mkono na makundi mbalinbali, wapo CHADEMA, CCM, CUF, NCCR, Taasisi za dini, NGOs, vyama vya hiari etc. Lakini KURA YA WAZI inaungwa mkono na kundi moja tu, CCM. We unadhani CCM na kura yao ya wazi watashinda, wakati wameanza kugeukana? Na ni kwa nini CCM peke yao ndo wanataka kura ya wazi? By Mtatiro

Source:Julius S. Mtatiro Facebook Wall
 
Utapigaje kura halafu iwe ya wazi?

Ni wachache sana wanaoweza kumpinga kiongozi wao hadharani.

Mimi najua tuko wana CCM wengi tusiopenda muungano lakini ni wachache wanaoweza sema hadharani kama mimi kuwa hatuutaki kwa kuogopa kuonekana wako tofauti na uongozi.

HILI BUNGE LIKO KWA FAIDA YA WATANZANIA SIO VYAMA.

Na kwa nini unataka ya wazi ? ili ujue nani anakupinga? halafu umfanyeje?
 

Good input Mr. Lukosi.
 
sometimes dude UNA AKILI!hakika ule ushauri wa Dr.PAULINE umefanya kazi........kwikwikwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!
 

Wewe vipi unapingana na chama chako?

 


Unauliza jibu? Ili upelekwe machinjioni hapo mabwepande!
 
Kwa mara ya kwanza Lukosi anatoa point. Mpigieni makofi
 

Kwa mara ya kwanza tangu nijiunge ndani ya JF, Chris Lukosi ameongea senses.
 

Kuna haja ya kuwa na kanuni kwamba ili jambo au hoja ipite ni lazima ikubaliwe na angalau 50% ya kila kundi. Si makundi yanayotuwakilisha Bungeni yanajulikana? Basi hiyo kanuni itungwe fasta na itakuwa imekata ngebe za CCM kutegemea wingi wao kama turufu ya kuburuza wengine.
 

Siamini macho yangu, ngoja nipanguse ukungu. Umezaliwa upya!!! Amen Amen. Haleluya.
 

Pokea Like yangu Chris Lukosi,sijajua kama ndio mara yangu ya kwanza kukupa like!!Penye ukweli lazima tuuseme,hongera sana mkuu,umekua sasa!
 
Last edited by a moderator:

Ni wewe au naota?au kaiba PW yako?
 
kura ipigwe kwa siri ila ihesabiwe kwa uwazi, nadhani wote watapata haki yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…