Bunge Lakatizwa Ghafla!

sababu ni nini?

any update please
 
Mitambo ya kunasa sauti imeleta hitlafu. Walihamia kwenye ukumbi wa zamani wa Pius Msekwa. Source; Radio One
 
utamaduni wa kutakiana radhi ulishakwisha siku nyingi, ndio maana umeme, maji, vinaweza kukatika ghafla na kurudi tena ghafla bila maelezo.bad habit zinajijenga taratibu na kuwa normal habit. Japo TBC1 sio wazuri sana kuna wakati walikuwa wanarusha matangazo ya waziri mkuu bungeni halafu ilivyofika ya kambi ya upinzani ambapo Dr Slaa alikuwa anataka kuwasilisha ya kambi ya upinzani matangazo yakakatwa ili watanzania tusione jinsi jamaa anavyochachafya serikali. Lets wait and see.
 
TBC wametangaza kwenye taarifa yao mchana kuwa kikao kiliahirishwa kwa muda kutokana na matatizo ya mawasiliano ila kiliendelea kwenye ukumbi wa Msekwa.
Naomba tusiwalaumu sana, kumbe plan B. ilikuwepo.
Mode: Naomba rekebisha headline, hii sio breaking news tena.
 
Tuliambiwa kuwa huo mjengo ni hakuna Sub-Sahara - mwisho wa siku hamna hata "BCP"!
 
kwanini usanii hata kwenye mambo ya maana ccm watatumaliza hawa
 
oya hii ni Bongo ya wanganyenyi kisha watawaleni inji hii ni ya wadanganyika tumezoea sio bunge tu hata maji, umeme kama kawa na siku hizi mi voda utasikia haipatikani bila sababu za msingi
 
Ukiona wanaanza na longo longo ya kuwa kuna hitilafu ya mitambo ujue kuna jambo nyeti linatakakujadiliwa na ili kuficha aibu yao , hawataki wananchi waone uoza wao!! Wanabodi si mnakumbuka wakati Dr. Slaa alipotaka kuijibu risala ya serikali wakati wa budget iliyopita; mara tu alipoanza kutoa hotuba yake TV zote zikawa blank!! Hizo ndio mbinu za watawala wetu kutunyima haki yetu ya msingi ya kupata habari zinazohusu maisha yetu!!
 

Mimi sijaelewa..................bunge limehairishwa au ma-TV yameharibika..????
 
Mimi sijaelewa..................bunge limehairishwa au ma-TV yameharibika..????

Ngalikihinja, liliahirishwa kwa muda kutokana na hitilafu ya virekodi sauti vya Bunge na sio camera, likaendelea ukumbi wa Msekwa ambako hakuna camera set-up, hivyo liliendelea bila kuonekana live, lets hope saa 10 hii, litaendela salama.
 
Ngalikihinja, liliahirishwa kwa muda kutokana na hitilafu ya virekodi sauti vya Bunge na sio camera, likaendelea ukumbi wa Msekwa ambako hakuna camera set-up, hivyo liliendelea bila kuonekana live, lets hope saa 10 hii, litaendela salama.

Haikai akilini............. kwa jinsi niijuwavyo TZ......... HAPO LAZIMA KUNA KITU CHA MOTO kilikuwa kinafuata........ so badala ya kutupa first hand information, tutapewa second hand ambayo itakuwa hatuna uhakika nayo ..............TZ HOYEEEEEEEEE
 
Kumbe wanatosha na kuna vyombo vinavyohitajika kwenye ukumbi wa zamani? Sasa mpya ulijengwa kwa ajili gani yarabi katika nchi 'maskini' kama yetu? Kama huo si ufujaji wa mali za umma, ni nini?
 
Tunadumisha mila zetu bwana.

Rahisi sana kulaumu wengine lakini tujiulize kwenye kila wabongo 10 ni wangapi wana fire extinguisher kwenye makazi yao? Au kwenye wabongo wenye majumba yenye thamani ya mil. 300 kuendelea wangapi wana bima?

Ukipata haya majibu rudi uwaseme bunge na plan B, a.k.a DRP/BCP.
 
Kumbe wanatosha na kuna vyombo vinavyohitajika kwenye ukumbi wa zamani? Sasa mpya ulijengwa kwa ajili gani yarabi katika nchi 'maskini' kama yetu? Kama huo si ufujaji wa mali za umma, ni nini?


Hili ndio swali la hekima.. sasa najua tunaweza kuwa na Bicameral House.. tuwe na Wabunge na Maseneta.. kumbe kumbi zote mbili zinaweza kutumika... Najua wamekuwa wakiutumia huo wa Msekwa kwa semina n.k na uko updated.. now we have a reason to reduce MPS from 323 hadi 200 tu halafu tuchague maseneta 50 hivi..
 
Bunge ni kijogoo hapa bongo. Huna ruhusa kuquestion maamuzi yabunge nje ye bunge kisheria. Wakiamua kuwa na majengo kila wilaya ruksa, wakiamua kukaa vikao kwa mzunguko kila jimbo ruksa, bunge ndio watunga sheria na wala hawatungiwi wao. Mtu wa kawaida ndiye mvujaji mali ya umma, sio Bunge ambalo ni jicho la matumizi ya pesa ya umma kwa wale wanaopewa kibali cha matumizi ya pesa ya umma. NDIO MAANA MAPROFESA wanakimbilia bungeni ambako ndiko hasa jiko kuu la ulaji, angalau kwa miaka mitano.
 

Mlo wenyewe kuupata ni shida,au hata hela ya kwenda hospitali hawana sasa watakumbuka wapi fire extinguisher.
 


Kuna umuhimu gani wa kuwa na mfumo wa Senetors?
 
'Kipya kinyemi ingali kidonda.' Hiki ndicho kilichotokea. Tanzania hatuna utamaduni wa matayarisho makini kabla ya shuguli zetu - say preparedness and constant surveilance. Na sio hili tu, hata kwa watangazaji wetu wa habari, inaonekana swala la kuzingatia sheria stahiki za mawasiliano nazo hawakuzizingatia au pengine tuseme kuna ka-uzembe kwenye utendaji wetu wa kazi! Angalau kusema basi, 'Watazamaji na wasikilizaji kuna tatizo limetokea hapa na tutashindwa kuwepo hewani kwa muda usiojulikana hadi tatizo hilo litakapotatuliwa! Na hili liliwashinda kusema kama watangazaji, au mpaka mruhusiwe na Bunge! Call a spade a spade and not a big spoon.... basi huu ni uzembe wa vyombo vya habari.
 
Hakuna lolote hawa wanataka kupitisha swala la EAC kwa ushabiki. Wabunge wasikubali ushabiki wa CCM na makuwadi wake wa kuridhia swala la EAC, sisi sio shamba la bibi. Natumaini wabunge wengi watapinga hili swala kwa niaba ya wanaowawakilisha. Tanzania hatuwezi kuwakaribisha manyang'au na vikaragosi vyao kuja kuchuma ambako hawakupanda.

Hata USA hawawakubali Mexicans kuingia na kufanya wanalotaka, au UK au nchi yoyote ile duniani. Kenya ambao hivi majuzi tu wamechinjana kama kuku wanatafuta mahali kwa kukimbilia Amani yetu tuliyoijenga hatukuwajengea wageni bali Watanzania na vizazi vyao vijavyo. Wao waendelee kuwa manyang'au hadi kiama hatuwezi kuuza utu wetu kwa vipande vya fweza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…