Bunge Letu Kibri na Jeuri ni Bunge Kweli la Kutunga Sheria au ni Bunge Ruber Stemp ya Serikali? Kwanini Linaogopwa Hivi na Mhimili wa Mahakama?

Naunga mkono hoja mkuu.
 
Kule data huwa hazizimiki, Tanzania internet huwa inasumbua naskia husaidia wanasiasa kufikiri vizuri.

Tangia awamu ya tano huwa nafurahia nikiwaona nyumbu wanavuka mto wenye mamba tena wenye njaa hasa pale ambapo hawaioni hatari ya kumezwa na mamba ama kujeruhiwa, ili mradi wafike huko wanakoongozwa waende hata kama watapitipa kwenye sehemu hatarishi, huu ndiyo mfano mzuri wa kujizima data, tuseme kuahirisha kufikiri kizalendo

Hii tabia ya kanyaga twende, (unyumbu), inapendwa sana na wanasiasa, (CCM), tuseme wanajizima data, ili kulitumikia kundi fulani kwamasilahi binafsi

Swali fikirishi je jamii za kiafrika zinahitaji tabia ya unyumbu wa kisiasa ili kutimiza majukumu yake hasa ya serikali
 
Paschal unapoteza muda wako tu!!

Toka nilivyoona Ndungai kalazimishwa kujiuzulu kisa tu Bibi hamtaki ndio nilijuwa kabisa bungeni hakuna kinachoendelea tunapoteza pesa tu!!

Rais na sipika kwa wenzetu kupishana ni kawaida

R.I.P Samwel Sitta!!
Na hata kama Ndugai angekataa kujiuzulu angefukuzwa uanachama wa CCM na ndiyo angekuwa amepoteza uspika na ubunge!
 
Jamaa anajifanya kujitoa ufahamu wakati kila kitu Kiko wazi.
Ameandika abstract.

Mahakama imesema hivii "Tumeamua suala hili mpaka tumechoka. Sasa, kuepusha mgogoro wa kikatiba utakaotokana na mzozo kati ya mahakama na bunge, na sisi mahakama tunakata rufaa kwa wananchi kama mnakubaliana na mahakama kuwa bunge limekosea mliwajibishe kwa kura ama vinginevyo".

Hii ni rufaa ya Mahakama ya Rufaa kwa wananchi.

Pascal Mayalla
 
Nimeacha kusoma nakala zako kwa kuwa kuna upotoshaji mwingi mno.
JF ni user generated forum inayoheshimu freedom of expression, ukiona mtu amepotosha kitu, dawa sio kususa au kuzira, watu wataendelea kupotoshwa, dawa ni kumweleza mpotoshaji amepotosha wapi na wewe kusawazisha hicho kilichopotoshwa.
Unaandika bila kufanya utafiti
Ni kweli mimi sio mtafiti hivyo sifanyi utafiti wowote, ninachofanya ni kusoma tuu katiba, kuleta kilichoandikwa na mtunga katiba na kukuwekea tafsiri yangu.
unatumia intuition na ni hatari kwa wasomaji
Ni kweli kuna maeneo natumia intuition, hii ni sauti ya kwake YEYE aliye ndani yangu, hivyo most intuitions
zangu zinakuja kuwa right, na kubwa kuliko ni HII ya 2025.
Unaweza kusoma baadhi ya intuitions zangu "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia kisha piga hesabu ya percetage ya ngapi zimekuwa kweli na zimekuja kutokea, utakubaliana na mimi I am very right.
P
 
JPM alishasema kuna mhimili mmoja umechimbiwa chini zaidi ila mkadharau. Pia mbunge wa darasa la 7 kama Shigongo anaweza kutunga sheria gani? Mtu kama Babutale anaweza kusoma muswada ulioandikwa kwa kiingereza? Kwenye katiba mpya tusiruhusu tena vilaza kuingia bungeni. Pia Spika asiwe na chama wala mbunge. Kikatiba Spika kung'olewa ni sekunde 2 tu endapo atavuliwa uanachama wa chama chake. Hivi ndo vitu vya kuongelea kwenye kudai katiba mpya ila CHADEMA kwa upumbavu wa hali ya juu wanang'ang'ania serikali 3 kama vile ndo tatizo kuu la kikatiba. Pumbavu sana.
 
Bila shaka mpumbavu mkubwa ni wewe! Mara zote Chadema wamekuwa wakisisitiza turudi kwenye mchakato wa kutengeneza Katiba mpya kuanzia rasimu ya Warioba na siyo uharo uliochakachuliwa na CCM wa Bunge la Katiba!
 
Bila shaka mpumbavu mkubwa ni wewe! Mara zote Chadema wamekuwa wakisisitiza turudi kwenye mchakato wa kutengeneza Katiba mpya kuanzia rasimu ya Warioba na siyo uharo uliochakachuliwa na CCM wa Bunge la Katiba!
Mungu atakuadhibu kwa kushindwa kutumia vizuri akili alizokupa bure. Unaongelea hii rasimu takataka ya Warioba yenye kasoro kibao? CHADEMA walichoongea si kuweka wagombea wawili kila jimbo la uchaguzi ili kubalance ishu za jinsia? CHADEMA wanataka katiba mpya ila mambo wanayoyataka ni ushuzi mtupu.
 
Pia Spika asiwe na chama wala mbunge. Kikatiba Spika kung'olewa ni sekunde 2 tu endapo atavuliwa uanachama wa chama chake.
Naunga mkono hoja Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?
Hivi ndo vitu vya kuongelea kwenye kudai katiba mpya ila CHADEMA kwa upumbavu wa hali ya juu wanang'ang'ania serikali 3 kama vile ndo tatizo kuu la kikatiba. Pumbavu sana.
Huna haja kuwatukana
P
 
BUNGE NDIO LINATUNGA SHERIA IWEJE UIITE BATILI??
BUNGE LINA HAKI YA KUTUNGA SHERIA HATA KAMA NI BATILI
 
Ungekuwa na akili usingebinua hilo domo lako! Unaelewa maana ya mchakato? Kama rasimu ya Warioba ni takataka si ndiyo hiyo ilitumika kuweka uharo wa CCM! Kwa nini CCM hawataki mjadala huru na wa kidemokrasia. Uchawa wa kipumbavu usinajisi ubongo wako uwe kama nguruwe 🐖 anayekula watoto wake!
 
BUNGE NDIO LINATUNGA SHERIA IWEJE UIITE BATILI??
BUNGE LINA HAKI YA KUTUNGA SHERIA HATA KAMA NI BATILI
Hiki ndicho ninachokifanya humu kuelimisha kuhusu ukuu wa katiba.
Katiba ndio sheria mama, sheria yoyote kinyume na katiba ni sheria batili. Bunge haliruhisiwi kutunga sheria batili.
P
 
kila kitu hapo jamhuri ya kihuni ni ubatili mtupu. taifa linaendeshwa kama familia. ni taifa la kipuuzi kwenye kila jambo
Sii kweli kuwa kila kitu kinaendeshwa kihuni. Katiba ndio ilibadilishwa kihuni, kuchomekea ubatili fulani ndani ya katiba. Vitu vingine vingi tuu viko sawa.
P
 
Kwa Tanzania Tuna muhimili Mmoja tu ambao ni Excutive na Muhimili huo ndo unatoa Maagizo kwa Mihimili mingine..hiyo inatokana na Kutokuwa na Msisitizo w Katiba yetu..
Nakubaliana na hii hoja....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…