Bunge limepitisha bajeti 2009/10

Bunge limepitisha bajeti 2009/10

Hatahivyo Wabunge wameichemsha Serikali kama ni sikivu wamesikia.
 
Inawezekana baada kueleweshwa na wabunge wenzao wakaelewa somo, tusiwaangalie negatively.
 
Tanzania Daima said:
LICHA ya baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuipinga kwa kauli nzito na kejeli hotuba ya bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2009/2010, imepitishwa kwa kishindo na wabunge wa chama hicho tawala.

Baada ya kutishwa na spika kwamba kwa mujibu wa ibara ya 90, kifungu kidogo cha 2(b) ya katiba ya nchi, rais hataweza kulivunja Bunge isipokuwa kama wabunge watakataa kupitisha bajeti ya serikali , wabunge 221, wote wa CCM, waliipitisha kwa kuitikia ‘Ndiyo', wabunge 33 wa kambi ya upinzani waliipinga kwa kusema ‘Hapana', huku wabunge wawili kutoka Chama cha Wananchi (CUF), wakipiga kura ya kutokuwa upande wowote.

Kupitishwa kwa bajeti hiyo kwa kishindo, kunaweza kuibua maswali mengi kwani tangu kuanza kwa mjadala wa bajeti hiyo, baadhi ya wabunge wa CCM, walionyesha dhahiri kuikamia kwa kutoa kauli nzito na kuapa kwamba kama haitafanyiwa mabadiliko makubwa, hawataipitisha.

CCM ni chuo cha kuzalisha, kulea na kukuza ufisadi kwa kutumia unafiki, ulaghai na utapeli. Kwa mtu yeyote kuweka matumaini ya taifa kujikwamua kutoka kwenye lindi la umasikini mikononi mwa CCM ni kulisaliti taifa. Kwa mwananchi yeyote kuwatetea baadhi ya hawa wanafiki ndani ya bunge na kuwaita watetezi wa wanyonge ni ujinga. Kwa mwana JF yeyote kung'ang'ania kutetea hawa ndumilakuwili na kuwaita mashujaa katika vita dhidi ya ufisadi ni ulimbukeni wa kutupwa.

Tumewashuhudia Wabunge Lucas Selelii na Kilontsi Mporogomyi wakikacha kupiga kura huku wabunge John Shibuda, Anne Kilango, Ole Sendeka wakiungana na wenzao Rostam Aziz, Andrew Chenge, Nizar Nkaramagi kuhakikisha bajeti hii ya kifisadi inapita. Sasa hapa hao wapiganaji na hao mafisadi tunawatofautisha kwa misingi gani.
CCM wote lao moja - kutetea Ufisadi, period.
 
Wewe na mimi tunaweza kufanya maajabu kwa kuchagua viongozi wazuri na kutoka upinzania na sio Kelele kama za wakina Shibuda na wengine hawana jipya hawa jamaa na zaidi ya hayahaya leo inahuzunisha sana
 
Wewe na mimi tunaweza kufanya maajabu kwa kuchagua viongozi wazuri na kutoka upinzania na sio Kelele kama za wakina Shibuda na wengine hawana jipya hawa jamaa na zaidi ya hayahaya leo inahuzunisha sana

Kama panya huuma na kupuliza na kama hukuzinduka kidole chote umepoteza. Wananchi kama hatutazinduka, tujue tumekwisha.
Wakati wa kuzinduka ni sasa.
 
Kama panya huuma na kupuliza na kama hukuzinduka kidole chote umepoteza. Wananchi kama hatutazinduka, tujue tumekwisha.
Wakati wa kuzinduka ni sasa.


Halafu FMES- mwanaCCM mkereketwa anasema anapigania maslahi ya taifa halafu wanaJF rrrrrrrrrrrr na thanks. Can't you people analyse mindsets za hawa wanaCCM?

Hivi hamjui yeyote anayejiita mwanaCCM ni mnafiki kwa wananchi? Niambie kama Mwakyembe aliipinga bajeti ya mwaka uliopita.

Kwa mwanaCCM maslahi ya chama mbele, wananchi (Taifa) baadae.
 
Last edited by a moderator:
Halafu FMES- mwanaCCM mkereketwa ansema anapigania maslahi ya taifa halafu wanaJF rrrrrrrrrrrr na thanks. Can't you people analyse mindsets za hawa wanaCCM?
Hivi hamjui yeyote anayejiita mwanaCCM ni mnafiki kwa wananchi? Niambie kama Mwakyembe aliipinga bajeti ya mwaka uliopita.
Kwa mwanaCCM maslahi ya chama mbele, wananchi (Taifa) baadae.

Na sasa baada ya kupitisha hii bajeti ya kifisadi, serikali imepiga marufuku mijadala bungeni kuhusu wizi kampuni za Meremeta, Tangold na Deep Green kwa kuwa inahusu mambo ya usalama wa taifa - yale yale ya Kagoda !!!
Serikali inalitumia bunge kuhalalisha wizi.
 
Back
Top Bottom