Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais Madarakani, lakini ni ngumu sana

Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais Madarakani, lakini ni ngumu sana

Safi sana JokaKuu. Hili ni jambo linaloonesha kabisa kuwa hakuna check-and-balance na hivo katika ngapi za juu hakuna aliye na maamuzi juu ya matendo ya mwingine. Mara Rais anaweza kuvunja Bunge, Bunge linaweza kumwondoa Rais, lakini Rais ndiye anayechagua hata Jaji Mkuu. Na kama haitoshi, hata maRais na waziri wakuu waliopita bado wanaweza kushiriki katika mchakato rasmi wa kuteua Rais wa siku za usoni. Maana yake makosa yao madarakani yanaweza kulindwa na maRais wa siku za usoni!!

Madaraka ya Rais ni mengi na makubwa kuliko inavohitajika. Wananchi hawana mamlaka mara baada ya kufanya uchaguzi! Pathetic!!

..unajua Watz kwa muda mrefu tumefundishwa kwamba sisi si lolote au chochote mbele ya watawala.

..Yaani tumeaminishwa kwamba hatuna mamlaka yoyote mbele ya viongozi tunaowachagua kwenda kuongoza serikali inayoendeshwa kwa kodi zetu.

..Wabunge, ambao ni wawakilishi wetu na watunga sheria hawatekelezi jukumu lao la kuisimamia serikali.

..Badala yake wabunge wamegeuka kuwa ombaomba wa miradi ya maendeleo kwa viongozi wa serikali. Imani ya wabunge ni kwamba bila kuwa "ombaomba" mzuri basi jimbo husika linaweza lisipate miradi ya maendeleo.
 
Mkizingua analivunja bunge .....kura za maoni anawatosa wabunge wote kabisa watakuja wapya.....mna swali lingine nani atakuwa ameshinda? Qnawakamata wote ikiwemo Ndugai nabkundi lake anawapa kesi uhaini kutaka kupindua nchi kesi miaka 10 haijaisha.....muache choko choko
 
KATIBA INARUHUSU LAKINI NI NGUMU SANA BUNGE KUMWONDOA RAIS MADARAKANI

Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi,

Leo nimeona nije na hili jambo la kusisimua lililopo kwenye katiba yetu lakini lisilotekelezeka. Halitekelezeki kwa sababu CCM haijawahi teua mgombea mwenye matatizo yasiyo ya kawaida kufikia hatua ya kufikiria kumwondoa madarakani. Lakini kwa upande mwingine tuchangamshe akili zetu na kuona jinsi gani hili suala lilivyo gumu kutekelezeka hasa nyakati hizi CCM ikiwa inaongoza.

Katiba kupitia ibara ya 46A imeweka wazi taratibu za kufuatwa. Imeandikwa hivi;
Ibara ya 46A.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.

(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Rais.

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;

(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba, au

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano, na haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.

Baada ya hili azimio la bunge kuna taratibu zimeelezwa hadi kufikia hatua ya Rais kuondolewa. Ugumu uko wapi? Ni kwenye kofia ya pili ya Rais kama mwenyekiti wa CCM. Hapa namaanisha baada ya rais kuondolewa madarakani atabaki na uenyekiti wa chama. Kama aliondolewa kwa fitna basi hao wabunge ambao pia ni wanachama wa CCM watakuwa katika wakati mgumu sana kulikwepa rungu la mwenyekiti.... uwezekano mkubwa ni wengi wao kufukuzwa uanachama. Ikumbukwe mojawapo ya hatua kwenye utekelezaji wa azimio hilo ni uwepo wa taarifa ya maandishi yenye sahihi za wabunge wanaounga mkono. Hakuna kujificha kwa waliohusika. Ila Tukumbuke ibara hii;

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-

(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;

Kwahiyo hakuna mbunge atapenda kujiingiza kwenye matatizo ya kuhatarisha ubunge wake kwa kuleta hoja ya kutokuwa na imani na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wake wa chama. Mwisho wa siku hiyo ibara itaendelea kutotumika. Binafsi nawapongeza sana viongozi wa CCM walioamua rais pia awe mwenyekiti wa CCM. Kuvaa hizi kofia mbili kwa mpigo imezuia hatari nyingi sana.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
Aah, Kamanda: ulitaka iwe rahisi? Leo Rais, kesho hakuna. The makamo,arud8she Waarabu, then ASP, fyekelea mbali. Ni lazima iwe ngumu, siyo blabla za kina tundulissu na wasaliti k8na Zitto WB. Au Mdude Chadema pia anafaa nara mojamoja.
 
Mtu akiisoma katiba yetu yote kuna mawili atapata majibu:-
La kwanza sisi wananchi ndiyo wenye matatizo au kama siyo sisi basi maRais wetu wanaotutawala ndiyo huwa mwenye shida

Hii Katiba ishapitwa na wakati kabisa, kwanza ilitakiwa iwe replaced wakati tulivyoamua kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi 1992.
Katiba hii Rais anapewa mamlaka kama ya wale Wafalme wa kale.
 
KATIBA INARUHUSU LAKINI NI NGUMU SANA BUNGE KUMWONDOA RAIS MADARAKANI

Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi,

Leo nimeona nije na hili jambo la kusisimua lililopo kwenye katiba yetu lakini lisilotekelezeka. Halitekelezeki kwa sababu CCM haijawahi teua mgombea mwenye matatizo yasiyo ya kawaida kufikia hatua ya kufikiria kumwondoa madarakani. Lakini kwa upande mwingine tuchangamshe akili zetu na kuona jinsi gani hili suala lilivyo gumu kutekelezeka hasa nyakati hizi CCM ikiwa inaongoza.

Katiba kupitia ibara ya 46A imeweka wazi taratibu za kufuatwa. Imeandikwa hivi;
Ibara ya 46A.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.

(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Rais.

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;

(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba, au

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano, na haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.

Baada ya hili azimio la bunge kuna taratibu zimeelezwa hadi kufikia hatua ya Rais kuondolewa. Ugumu uko wapi? Ni kwenye kofia ya pili ya Rais kama mwenyekiti wa CCM. Hapa namaanisha baada ya rais kuondolewa madarakani atabaki na uenyekiti wa chama. Kama aliondolewa kwa fitna basi hao wabunge ambao pia ni wanachama wa CCM watakuwa katika wakati mgumu sana kulikwepa rungu la mwenyekiti.... uwezekano mkubwa ni wengi wao kufukuzwa uanachama. Ikumbukwe mojawapo ya hatua kwenye utekelezaji wa azimio hilo ni uwepo wa taarifa ya maandishi yenye sahihi za wabunge wanaounga mkono. Hakuna kujificha kwa waliohusika. Ila Tukumbuke ibara hii;

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-

(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;

Kwahiyo hakuna mbunge atapenda kujiingiza kwenye matatizo ya kuhatarisha ubunge wake kwa kuleta hoja ya kutokuwa na imani na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wake wa chama. Mwisho wa siku hiyo ibara itaendelea kutotumika. Binafsi nawapongeza sana viongozi wa CCM walioamua rais pia awe mwenyekiti wa CCM. Kuvaa hizi kofia mbili kwa mpigo imezuia hatari nyingi sana.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
Bunge lipi ?
 
Una mshitaki vipi na wapi MTU mwenye kings kikatiba.

Spika fomu zinapita kwa Mkiti CCM

NCHI HII TUNA MFUMO WAKISHETANI SANA.

Bora kuishi na korona siyo huu mfumo
Acha Ufala wewe Yaan Corona mi Afadhali utawala?.. Fala sanaa
 
Aah, Kamanda: ulitaka iwe rahisi? Leo Rais, kesho hakuna. The makamo,arud8she Waarabu, then ASP, fyekelea mbali. Ni lazima iwe ngumu, siyo blabla za kina tundulissu na wasaliti k8na Zitto WB. Au Mdude Chadema pia anafaa nara mojamoja.
Umeandika nini hapa?
 
Na Rais anaweza kulivunja bunge!

Na kila siku wabunge wa CCM wanatishwa kwamba Rais anaweza kulivunja bunge.

Sijawahi kusikia wabunge wakiambiwa wanaweza kumuondoa Rais madarakani.
Yule ndiyo mwenyekiti wao na Rais vilevile, pia hatuna mahakama tuna mashina ya CCM tupu
 
Kwa Hilo bunge linalotokana na kura za magumashi hakuna mbuge wa kuwajibisha raisi maana hawana ushawishi kwenye sanduku la kura
 
Mbona mwendazake alifanya hovyo Kika eneo hawakuona?

..waliona ila waliamini hali siyo mbaya kiasi cha wao kushindwa kuidhibiti.

..hali ingekuwa mbaya basi ungeona wanamuondoa kwa mtindo uliotumika Zimbabwe dhidi ya Mzee Mugabe.

..Au, wangetafuta mkakati wa kuachia madaraka ya kisiasa, bila kupoteza nguvu za kiuchumi , kama ilivyotokea Afrika Kusini walivyokubali utawala wa walio wengi.
 
..waliona ila waliamini hali siyo mbaya kiasi cha wao kushindwa kuidhibiti.

..hali ingekuwa mbaya basi ungeona wanamuondoa kwa mtindo uliotumika Zimbabwe dhidi ya Mzee Mugabe.

..Au, wangetafuta mkakati wa kuachia madaraka ya kisiasa, bila kupoteza nguvu za kiuchumi , kama ilivyotokea Afrika Kusini walivyokubali utawala wa walio wengi.
Kwahiyo waliidhibiti?
 
Na kwenye uchaguzi hao wabunge wanamkuta huyo rais ndo mwenyekiti wa chama hivyo majina yanakatwa LIVE.
Na wakileta chokochoko wanamkuta ndye amiri jeshi wa majeshi yote nchini[emoji23][emoji1787]
 
..waliona ila waliamini hali siyo mbaya kiasi cha wao kushindwa kuidhibiti.

..hali ingekuwa mbaya basi ungeona wanamuondoa kwa mtindo uliotumika Zimbabwe dhidi ya Mzee Mugabe.

..Au, wangetafuta mkakati wa kuachia madaraka ya kisiasa, bila kupoteza nguvu za kiuchumi , kama ilivyotokea Afrika Kusini walivyokubali utawala wa walio wengi.
Watanzania wengi hatuzijui haki zetu, na hata wachache wanaozijua wanaonekana kama hawajali. Juzi hapa Chahali kaanzisha mada muhimu sana kuhusu mjadala wa katiba mpya unaoendelea.

Alichoambulia humu ni kushambuliwa na matusi kibao. Tunao ujuaji mwingi usiotusaidia.
 
Watanzania wengi hatuzijui haki zetu, na hata wachache wanaozijua wanaonekana kama hawajali. Juzi hapa Chahali kaanzisha mada muhimu sana kuhusu mjadala wa katiba mpya unaoendelea.

Alichoambulia humu ni kushambuliwa na matusi kibao. Tunao ujuaji mwingi usiotusaidia.

..kweli kabisa.

..haki za Watz zinakanyagwa na wale wanaozijua.

..halafu kuna mashabiki ambao wanaona Watz wenzao wakionewa halafu wanashangilia uonevu na uovu huo.
 
Back
Top Bottom