Bunge litunge Sheria ili mali ambazo hazikuandikiwa wosia zimilikiwe na Serikali inapotokea mmiliki amefariki

Bunge litunge Sheria ili mali ambazo hazikuandikiwa wosia zimilikiwe na Serikali inapotokea mmiliki amefariki

Championship

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2019
Posts
5,500
Reaction score
10,616
Hii itasaidia kila mtu mwenye mali sehemu awe anatunza wosia na kuufanyia marekebisho mpaka siku anapofariki.

Wosia uandaliwe kwa kufuata matakwa ya kisheria na ikiwezekana kuwe na centralized electronic database ya kutunza wosia. Mahakama ndio itoe idhini ya kufungua akaunti ya marehemu kujua wosia unasemaje.

Itasaidia sana kuondoa migogoro inayofuatia baada ya mtu kuaga dunia. Itaboresha mahusiano baina ya ndugu.

Serikali itakuwa imeongeza chanzo cha mapato ikiwa watu hawataandika wosia. Kimsingi faida kubwa zaidi kwa serikali ni uwepo wa mahusiano mazuri katika jamii baada ya misiba.
 
Kwa hiyo kama mzee ana nyumba na watoto, akifa ghafla bila wosia, serikali ichukue nyumba ifanye NHC,
Kwa waislamu wana taratibu zao za miradhi,
Pendekezo lililopo sio hasa kuchukua mali ya mtu bali kuhakikisha kila raia anaandika wosia na kuutunza sehemu salama.
 
Hatuko nyuma kiasi hicho. Waafrika wengi wanataratibu za kimila- labda kama wewe unazipiga vita mila za kabila yako.
Haujui tu yanayoendelea mtu akifa ghafla , hoja ya mtoa mada ipo Sawa kabisa , taratibu za kimila Kwa sasa hazina nguvu, Mkono wa serikali ndo utakaotiisha , watu Wanauana Sana .... Wosia unatakiwa uwe updated kila mwaka
 
... labda kama marehemu hakuacha mtoto, mke/mume, au mzazi hapo sawa. Ila kama hao wapo hata kama hakuandika wosia how comes serikali itaifishe mali za marehemu wakati ndugu zake wa karibu wapo? It is not fair; ni wizi wa mchana kweupe!

Ambacho ninge-suggest, ni endapo marehemu hakuacha wosia na ameacha watoto na wameshindwana kufuata taratibu za kimila au kidini katika kugawana mali basi mali hiyo igawanywe sawa sawa kwa watoto wote na mke/wake regardless of gender.

Kama hajaacha watoto ila mke/mzazi/wazazi wapo (whoever exists) basi mali igawanywe sawa baina yao. Kama hajaacha yeyote katika hao na hakuna wosia, basi mali hiyo ichukuliwe na kabidhi wasii mkuu.
 
Hii itasaidia kila mtu mwenye mali sehemu awe anatunza wosia na kuufanyia marekebisho mpaka siku anapofariki.

Wosia uandaliwe kwa kufuata matakwa ya kisheria na ikiwezekana kuwe na centralized electronic database ya kutunza wosia. Mahakama ndio itoe idhini ya kufungua akaunti ya marehemu kujua wosia unasemaje.

Itasaidia sana kuondoa migogoro inayofuatia baada ya mtu kuaga dunia. Itaboresha mahusiano baina ya ndugu.

Serikali itakuwa imeongeza chanzo cha mapato ikiwa watu hawataandika wosia. Kimsingi faida kubwa zaidi kwa serikali ni uwepo wa mahusiano mazuri katika jamii baada ya misiba.
Akili za CCM hizi ...na tunajua ccm ni mafii .
 
Hii itasaidia kila mtu mwenye mali sehemu awe anatunza wosia na kuufanyia marekebisho mpaka siku anapofariki.

Wosia uandaliwe kwa kufuata matakwa ya kisheria na ikiwezekana kuwe na centralized electronic database ya kutunza wosia. Mahakama ndio itoe idhini ya kufungua akaunti ya marehemu kujua wosia unasemaje.

Itasaidia sana kuondoa migogoro inayofuatia baada ya mtu kuaga dunia. Itaboresha mahusiano baina ya ndugu.

Serikali itakuwa imeongeza chanzo cha mapato ikiwa watu hawataandika wosia. Kimsingi faida kubwa zaidi kwa serikali ni uwepo wa mahusiano mazuri katika jamii baada ya misiba.
Kwa uoande wa Waislam hili tatizo halipo kwa sababu kila kitu kipo wazi
nani anarithi
nani harithi
anarithi kiasi/rate gani

Na ndio maana kule Uswazi, utasikia Mwanamke kama kafiwa na Mume wake anasema "Nasubiri Kisumni changu"
Sumni => 1/8 ya mali aliyoacha mumewe
Muislam atawajibika kutamka/kuandika Wasia pindi tu atakapotaka kiasi fulani cha mali aliyoacha iende nje ya familia yake (warithi halali kulingana na Qur'an na Sunnah) kama kupeleka Wakfu kwa ajili ya Watoto Yatima au Msikiti. Ambayo vilevile (hiyo thamani ya Wakfu) haitakiwi izidi 1/3 ya mali yote aliyoacha marehemu
Baada ya kuitoa hiyo mali ambayo marehemu ame dedicate kwa ajili ya Wakfu mali yote iliyobaki ratio ziko very clear, nani apate kiasi gani
 
Hii itasaidia kila mtu mwenye mali sehemu awe anatunza wosia na kuufanyia marekebisho mpaka siku anapofariki.

Wosia uandaliwe kwa kufuata matakwa ya kisheria na ikiwezekana kuwe na centralized electronic database ya kutunza wosia. Mahakama ndio itoe idhini ya kufungua akaunti ya marehemu kujua wosia unasemaje.

Itasaidia sana kuondoa migogoro inayofuatia baada ya mtu kuaga dunia. Itaboresha mahusiano baina ya ndugu.

Serikali itakuwa imeongeza chanzo cha mapato ikiwa watu hawataandika wosia. Kimsingi faida kubwa zaidi kwa serikali ni uwepo wa mahusiano mazuri katika jamii baada ya misiba.
Halafu serikali uchukue pia jukumu la kuwatunza hao mayatima!
 
Mkuu Mimi mbona sijaelewa hapa, yaani Nina Nyumba yangu mke na watoto , baadaye nife ghafra halafu serikali itaifishe Mali yangu kisa sikuandika wosia!!! vipi kuhusu mke na watoto wangu?
 
Ipo sheria ya kabidhi wasii mkuu (The Administrator General Act) ambayo kwa Sasa sheria hiyo inasimamiwa na RITA, everything has been covered, Kila kitu kimeshafanyiwa kazi. Nenda google utaikuta sheria hiyo.

Haya mambo yameanza Karne nyingi zilizopita, yameanzia uingereza, yakapelekwa India, baadae katika makoloni yetu.

Japo kama hakuna wosia si lazima ziende kwa kabidhi wasii mkuu.

Wanaukoo wanaweza kuzigawa wa wanaostahili baada ya kufuata taratibu zote za mirathi,ikiwemo kikao Cha ukoo na kuthibitishwa na mahakama

Serikali na jamii Ina maslahi na Mali za wanajamii, sheria inaweka utaratibu mzuri wa kuzifanya ziwe salama kwa maendeleo ya taifa
 
Hii itasaidia kila mtu mwenye mali sehemu awe anatunza wosia na kuufanyia marekebisho mpaka siku anapofariki.

Wosia uandaliwe kwa kufuata matakwa ya kisheria na ikiwezekana kuwe na centralized electronic database ya kutunza wosia. Mahakama ndio itoe idhini ya kufungua akaunti ya marehemu kujua wosia unasemaje.

Itasaidia sana kuondoa migogoro inayofuatia baada ya mtu kuaga dunia. Itaboresha mahusiano baina ya ndugu.

Serikali itakuwa imeongeza chanzo cha mapato ikiwa watu hawataandika wosia. Kimsingi faida kubwa zaidi kwa serikali ni uwepo wa mahusiano mazuri katika jamii baada ya misiba
Haya yangesemwa na mtu ambaye hajawahi kufiwa labda ingeeleweka. Yangesemwa na mtu asiyejua wizara yetu ya ardhi ifanyavo kz, angeeleweka. Nje ya hapo huenda aliyeandika ni mwajiriwa wa hiyo wizara au hajafanya utafiti wa kutosha.

Haijui hii nchi ipasavyo. Hajui uelewa wa haya mambo kw wanaoishi vjjn ukoje, hajui ubaya/uzuri wa sheria za kimila zikoje wala hajui sheria zilizopo zimekwamia wp au kama hazitumiki, ni kw sbb gani.

Kuna migogoro kibao ya watu kunyang'anywa ardhi na kuuziwa wengine hata kbla hawajafa na hata wngn kuzuiwa kuitumia ardhi zao watakavyo. Zipo hata nyngn zlizouzwa bila taarifa.

Labda kipengele ch kuongeza mapato-iwe Kw afsa ardhi binafsi au Kw serkali, wala hili halina mahusiano yyt mazr/mabaya ktk jamii. Badala yake ni kuongeza kero tu kwa wananchi, ni kuongeza urasimu uxio wa lazma Kw waTz ambayo pia ni mojawapo wa mambo yanayotukera Kw sana. Hakuna msaada wwt watakaopata wafiwa toka serikalini. fuatilia Kw watu waliofiwa uje na mifano toshelezi, hususan vjjn halafu andka upya.

Mwisho toa mifano ya jinsi serikali itakavoongeza mahusiano mazuri kutokana na uporaji huo wa ardhi za wafiwa, bila hivo, wngn hatutakuelewa
 
Back
Top Bottom