Championship
JF-Expert Member
- Aug 7, 2019
- 5,500
- 10,616
- Thread starter
-
- #61
Asante mkuu kwa kuleta mwongozo.Sheria zinazohusu mirathi Tanzania
Hii hutumika pale ambapo marehemu aliishi kwa kufuata mila na desturi za kabila lake. Sheria ya kimila itatumika pale tu wahusika wa mirathi hiyo wanatoka katika kabila moja na si vinginevyo.
- Sheria za kimila
Kanuni za Urithi (Tangazo la serikali Na.436/1963).
Sheria hii itatumika pale endapo itabainika kuwa marehemu alikuwa hafuati sheria za Kiislamu wala taratibu za kimila. Sheria hii inaitwa Sheria ya Urithi ya India ya 1865 (inatumika na watu wanaofuata dini ya Kikristo).
- Sheria za Serikali
- Kama marehemu ameacha mjane na watoto mgao utakuwa 1/3 kwa 2/3
- Kama marehemu hakuacha watoto mjane atapata ½ na ½ nyingine hugawanywa sawa kati ya wazazi, kaka na dada za marehemu.
Sheria hizi zinabainishwa katika Quran Tukufu na zinafuatwa na waumini wa dini ya Kiislam. Mgawanyo wake ni kama ifuaatavyo;
- Sheria za dini ya kiislamu
Aina za Mirathi
- Warithi wakuu katika sheria hii ni mke au wake, baba,mama na watoto
- Watoto wa kiume wanapata mara 2 ya watoto wa kike
- Wajane/mjane wanapata 1/8 ya mali ya marehemu kama kaaacha watoto.
- Mwosia haruhusiwi kutoa wosia zaidi ya 1/3 ya mali yake.
- Mirathi palipo na wosia: hutokea wakati marehemu kabla ya kufariki aliacha maandishi/matamshi au maelezoya namna mali yake itakavyoshughulikiwa/itakavyomilikiwa baada ya kifo chake.
- Mirathi pasipo na wosia: hapa marehemu hakuacha wosia yaani tamko au maandishi hivyo warithi hulazimika kuchagua msimamizi au wasimamizi kupitia mahakama.
Kimsingi hapa kuna mkanganyiko. Mfano mtu ambaye ni muislam lakini kaacha wosia inashughulikiwaje?
Kwenye hili pendekezo sijazingatia sana mhusika atataka mirathi ifuate utaratibu gani. Nadhani hapa kila mtu apewe uhuru wa kuchagua anaandika wosia kwa kufuata utaratibu upi aidha kimila au kidini.
Hoja yangu kwenye bandiko ni kuiweka utaratibu wa kilazima kwa kila mtu kuandika wosia kulingana na matakwa mahususi yatakayowekwa na sheria yenyewe.