Bungeni Leo: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atoa maelekezo mapya uendeshaji wa treni ya SGR

Bungeni Leo: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atoa maelekezo mapya uendeshaji wa treni ya SGR

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Uchukuzi kuendelea kulisimamia kwa karibu Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kuhakikisha huduma za treni ya SGR zinaboreshwa.

Pia, Majaliwa ameagiza miundombinu ya mradi huo inaimarishwa ili uweze kudumu kwa muda mrefu. Kauli ya Majaliwa inakuja wakati baadhi ya wadau wakiwemo watumiaji wa usafiri huo wakipongeza huku wengine wakilalamikia huduma duni ndani ya usafiri huo.

Tayari Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Morogoro, ilibaini kuwepo kwa baadhi ya abiria wanaohujumu mradi huo kwa kulipa nauli pungufu na kuishauri TRC hatua za kuchukua kudhibiti hali hiyo.

Waziri Mkuu Majaliuwa amesema katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali itaendeleza sekta ya uchukuzi ambapo pamoja na mambo mengine itasimamia sekta ya reli ikiwemo ujenzi wa SGR na uendeshaji wake kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma.

Pia Soma
Utendaji wa Train ya SGR uboreshwe
 
Akiwa anahutubia bungeni leo Septemba 6, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Uchukuzi kuendelea kulisimamia kwa ukaribu Shirika la Reli Tanzania (TRC) ili kuhakikisha huduma za treni ya SGR zinaboreshwa.

Aidha Majaliwa ameagiza miundombinu ya mradi huo kuimarishwa ili uweze kudumu kwa muda mrefu.

Kauli ya Waziri Mkuu Majaliwa inakuja katika kipindi ambacho baadhi ya wadau wakiwemo watumiaji wa usafiri huo wakipongeza huku wengine wakilalamikia huduma duni ndani ya usafiri huo.

Tayari Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Morogoro, ilibaini kuwepo kwa baadhi ya abiria wanaohujumu mradi huo kwa kulipa nauli pungufu na kuishauri TRC hatua za kuchukua kudhibiti hali hiyo.

Soma pia: Utendaji wa Train ya SGR uboreshwe

Waziri Mkuu Majaliuwa amesema katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali itaendeleza sekta ya uchukuzi ambapo pamoja na mambo mengine itasimamia sekta ya reli ikiwemo ujenzi wa SGR na uendeshaji wake kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma.

photo_5969614786499036066_x.jpg

Majaliwa ameyasema hayo leo Ijumaa, Septemba 6, 2024 wakati wa kuahirisha Mkutano wa 16 wa Bunge jijini Dodoma.

“Naomba kulitaarifu Bunge lako tukufu kuwa, safari za treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam - Morogoro zilianza Juni 14, 2024 na Julai 25, 2024 uendeshaji wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma ulianza,” amesema.

Amesema treni hiyo inaendelea kutoa huduma kwa wananchi na imechangia kuimarisha sekta ya usafirishaji.

“Kipekee ninaomba kumpongeza Rais Samia kwa kusimamia maono yake na kwa kweli anaahidi, anatekeleza, Kazi Iendelee”.

Source: Mwananchi News
 
Hakika na sense ya ownership iwepo, huu mradi ni muhimu sana kuliko kiongozi yeoyete wa Taifa hili.
 
..Sgr inapaswa kuwa ya MIZIGO.

..biashara ya abiria itabidi shirika lipewe ruzuku.

..na nimeona kuna matumizi yasiyo ya lazima ikiwemo kuajiri mamia ya wahudumu
ktk treni.
We jamaa wahudumu nashauri wawepo wengi pale stesheni mana unakuta watu kibao alafu wahudumu hamna
 
..sisemi wahudumu waondolewe wote.

..mimi nadhani idadi yao imezidi mahitaji.
Joka kuna uchawi sio bure mbona mimi juzi kati hapo stesheni kuu ya daslamu wahudumu wa kukatisha tiketi ilikua mtiti mpaka madirisha mengine yakawa yako wazi tu wahudumu wawili mfoleni huoo
 
Hakika na sense ya ownership iwepo, huu mradi ni muhimu sana kuliko kiongozi yeoyete wa Taifa hili.
Kwa uzoefu wangu, na tabia ya watanzania kwa mali za umma, it's just a matter of time, itakuwa kama UDART au kuendeshwa kwa hasara kama CAG anavyoliripoti ATCL,TTCL etc...ningeweza kuekewa kidogo kama main objective ya SGR ingekuwa kusafirisha mizigo halafu hii ya abiria iwe ni additional. Ina maana usafirishaji wa mizigo ungeweza pia kuiendesha treni ya abiria kwa kuongezea some running costs. Kingine hii reli inatakiwa private sector waruhusiwe kuleta treni zao za mizigo na abiria na wawe wanailipa serikali Kodi ya kutumia SGR.
 
Joka kuna uchawi sio bure mbona mimi juzi kati hapo stesheni kuu ya daslamu wahudumu wa kukatisha tiketi ilikua mtiti mpaka madirisha mengine yakawa yako wazi tu wahudumu wawili mfoleni huoo
Hili pia ni kosa lingine,tena la kujitakia. Serikali ndiyo imeamuru mabus yote tiketi zikatwe kwa mtandao. Mimi sikumbuki ni lini nimeenda stendi kukata tiketi. Natumia simu tuu na wananitumia tiketi yangu, tena makampuni mengine hata huna haja ya kuprinti hard copy...
 
Joka kuna uchawi sio bure mbona mimi juzi kati hapo stesheni kuu ya daslamu wahudumu wa kukatisha tiketi ilikua mtiti mpaka madirisha mengine yakawa yako wazi tu wahudumu wawili mfoleni huoo
Watu waelimishwe wakate ticket kwa njia ya mtandao. Sioni haja ya watu kuwa na misurur kwenye madirisha ya wakata ticket.
 
Hili pia ni kosa lingine,tena la kujitakia. Serikali ndiyo imeamuru mabus yote tiketi zikatwe kwa mtandao. Mimi sikumbuki ni lini nimeenda stendi kukata tiketi. Natumia simu tuu na wananitumia tiketi yangu, tena makampuni mengine hata huna haja ya kuprinti hard copy...
Hata treni huna haja ya printed copy ukikata kwa njia ya mtandao.

Wana scan soft copy bila shida. Kikubwa ni watu wapate elimu na taarifa sahihi.
 
Watu waelimishwe wakate ticket kwa njia ya mtandao. Sioni haja ya watu kuwa na misurur kwenye madirisha ya wakata ticket.
We jamaa mbona kama huelewi au mimi ndio sielewi mana pale ukikata mtandaoni watakuambia upitie dirishani waiprint tena unafahamu?
 
Hili pia ni kosa lingine,tena la kujitakia. Serikali ndiyo imeamuru mabus yote tiketi zikatwe kwa mtandao. Mimi sikumbuki ni lini nimeenda stendi kukata tiketi. Natumia simu tuu na wananitumia tiketi yangu, tena makampuni mengine hata huna haja ya kuprinti hard copy...
We kariri tu mambo ya mabusi basi pale kuna watu wamekata kupitia mitandaoni na wakawa wamepanga foleni waiprint iwe kwenye mfumo wa ticket ya karatasi sasa kama unaona tunajitakia lipia hapo kwenye simu alafu nenda
 
Hivi watu mnakaa kabisa mnapoteza muda kuwasikiliza hao wajingawajinga majambazi waliojikusanya kihuni na kuniita bunge.
 
We jamaa mbona kama huelewi au mimi ndio sielewi mana pale ukikata mtandaoni watakuambia upitie dirishani waiprint tena unafahamu?
Mimi nimetumia SGR na sikuwa na karatasi. Tiket yangu waliiscan ikiwa kama PDF kwenye Simu ya mkononi.
 
Toka aseme rais yupo anapanga mafaili ofisini siwez mwamini kamwe
 
Back
Top Bottom