Buriani Amina Chifupa!

Status
Not open for further replies.
mie nnauliza ni sawa kujitokeza hadharani kwa sasa kama alivyofanya?, na huu mfuko wa amina mnauonaje?
 
Baada ya kumsoma huyu mzee, nashawishika kushauri kwamba Huyu mzee anapaswa kushtakiwa kwa kuua bila kukusudia.
 
Baba mjinga sana huyu!!!

Mjinga = asiyejua
mimi siamini kama huyu mzee hajui kitu, anajua mengi,
atakuwa amekuwa betrayed somewhere by somebody. nasema hivi kwasababu huyu ndiye alikuwa wa kwanza kusema mwanae kafa kifo cha kawaida; kitendo cha yeye leo kuibuka na jipya kinaonyesha kuwa wakati anatoa zile statement za kwanza ama alifanya hivyo under undue influence, au alifanya hivyo akitegemea kuwaridhisha watu fulani ili baadae wawe naye vizuri, yaani, alitegemea kupata payback kwa kufunika mambo aliyoyajua. kumbuka huyu ndo alikimbia haraka haraka kwenda kumzuia mwanae asitoe maelezo yake kwa waandishi wa habari; ni kitu gani kilimfanya achukue hatua hiyo ikiwa alikuwa hajui kilichokuwa kinaenda kusemwa? lazima alitumiwa na mtu/watu fulani kumzuia. Na kama ndivyo, basi aliahidiwa au alitegemea jambo fulani toka kwao waliomtumia.
Bada ya kifo bado akawa hajakata tamaa kwa kujua kuwa suala la mwanae lina uzito so akiwafichia atapata uswahiba nao na pengine kanafasi fulani ndani ya mtandao; naamni baada ya haya yote ameachwa solemba ndo maana anaamua ku-spill the beans kidogokidogo, soon atsema jingine tena..hiyo ndio faida ya usanii
 
Bigman,
Poa kwa kutuletea hiyo message lakini naona hata Mzee Chifupa hajafanya lolote, huenda na yeye anawaogopa hao watu. Hakuna lolote la maana alilosema, angesema wazi aliyosema Amina, ili tujue nini ni nini na wapi ni wapi
 
sasa waungwana hili la kuenda kwenye kadamnasi ya waandishi wa habari na kuzungumza alioyazungumza mnayapemaje?


na huu mfuko wa amina mnaowonaje? au ndio njia ya wengine kutokea hapo? akiwamo baba mtoto?
 
Hivi, si hawa hawa wanafamilia waliotuma barua Bungeni ati habari za kifo cha mtoto wao zisiandikwe magazetini, halafu wakati huo huo wanaenda maelezo kuelezea mambo ya ushirikina? Something is very wrong.... Angalia habari hizi ambazo zote ziko kwenye gazeti moja:

1. 2007-07-12 22:02:07 (Nipashe)
Na Mwanaidi Swedi, Dodoma


Familia ya aliyekuwa Mbunge wa Viti- Maalum kupitia Umoja wa Vijana wa CCM, Marehemu Amina Chifupa, imekuja juu ikitaka mpendwa wao asiendelee kuandikwa kwenye vyombo vya habari.

Katika kuhakikisha hilo linatekelezwa, familia hiyo imetuma ujumbe maalum Bungeni, uliosomwa na mmoja wa waheshimiwa wabunge.

Salam hizo za wana familia ziliwasilishwa Bungeni na Mbunge wa Mbinga Magharibi, CCM, Kapten (Mstaafu) John Komba.

Wakati anatoa salam hizo ilikuwa jana yapata saa moja hivi usiku.

Kapteni Komba alifikisha ujumbe huo wakati alipopewa nafasi ya kutoa mchango wake kwenye bajeti ya Wizara ya Miundombinu.

Akasema kuendelea kuamuandika Marehemu Amina Chifupa wakati akiwa tayari ameshatangulia mbele ya haki, ni sawa na kuwakumbusha machungu ndugu na jamaa zake.

Mheshimiwa Amina Chifupa alifariki Juni 26 mwaka huu katika hospitali ya Jeshi Lugalo ambako alilazwa tangu Juni 8 mwaka huu.

Halafu siku moja baadaye,

2007-07-13 10:44:20
Na Lucy Lyatuu


Mzazi wa aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Vijana (CCM), Marehemu Amina Chifupa, ameishauri serikali kuwataja viongozi wanaoshiriki katika sakata la dawa za kulevya ikiwa ni njia mojawapo ya kumuenzi mtoto wao.

Baba wa Amina, Bw. Khamis Chifupa alitoa rai hiyo, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam jana.

Alikuwa akitoa shukrani zake kwa watu walioshiriki kwa njia moja au nyingine kufanikisha msiba wa mtoto wake.

Mapema kabla ya kuanza mkutano huo, waandishi wa habari walisimama kwa dakika moja na kusali na kutoa heshima kwa marehemu ambaye kitaaluma alikuwa mwandishi wa habari na mtangazaji wa radio.

Alisema familia yake iko tayari kusikia taarifa zozote zinazohusiana na viongozi wanaojihusisha kwa njia moja au nyingine katika sakata la dawa za kulevya na akaiomba serikali kutokuwa na kigugumizi kuwataja wahusika bila kujali nyadhifa zao kisiasa au kijamii.
Hata hivyo, aliishukuru serikali kwa mchango wake ilioutoa katika kipindi chote cha majonzi.

``Tunamshukuru sana Rais Jakaya Kikwete kwa mchango wake alioutoa ikiwa ni pamoja na kutoa ndege yake kwa ajili ya kusafirisha mwili wa marehemu hadi kijijini Ihanjo wilayani Njombe. Hatuna cha kuwalipa ila tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu,`` alisema Bw. Chifupa.

Alisema familia yake haiwezi kusema serikali ichunguze kifo hicho ila kama kuna mtu mwenye taarifa au anayejua mazingira ya kifo hicho anaweza kutoa taarifa kwa serikali ili wanaohusika wachukuliwe hatua.

``Ninatoa kauli hii kwa kuwa wapo wanaosema kifo cha Amina kinahusishwa na kupewa sumu, wengine uchawi kutokana na kupiga vita dawa za kulevya, jambo ambalo hatuna uhakika nalo,`` alisema.

Hata hivyo, alisema katika kumuenzi mtoto wake, familia itaendeleza mfuko wa Amina Foundation na kuwataka watu wote waliokuwa na mapenzi mema na Amina kuuchangia ili uweze kutekeleza ahadi zote alizokuwa amewaahidi.

``Amina Foundation itaongozwa na mjomba wake, Bw. Solomon Mmbanga, akishirikiana na wajumbe wengine kutoka Bungeni na kamati iliyokuwa ikiandaa msiba wake.

Bw. Chifupa alisema yeyote anayetaka kuuchangia mfuko huo atumie akaunti iliyoko katika tawi la CRDB Kijitonyama yenye namba 01J1014153400.

Alisema marehemu Amina alianza kuumwa Mei 8 mwaka huu mara baada ya kwenda nyumbani kwake akitokea kwa aliyekuwa mume wake, Bw. Mohamed Mpakanjia.

Aliongeza kuwa mwanae aliugua maradhi ya ajabu ambapo alikuwa akitaja baadhi ya viongozi kuwa ndio waliomsababishia tatizo la kuugua.

Hata hivyo, kwa kipindi chote Amina alikuwa hali chakula chochote ndipo tulipojua kuwa yalikuwa mambo ya Kiswahili hivyo ikabidi kumhudumia Kiswahili.

Bw. Chifupa alisema baada ya kumpeleka hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo aligundulika kuwa na ugonjwa wa kisukari kilichofikia 400 kikichanganyikana na homa, ambavyo vyote kwa pamoja vilikuwa havishuki.

``Akiwa hospitalini Amina alizungumza maneno mengi (hakuyataja) ya ajabu na mazito mengine yakiashiria kifo chake,`` alisema.

Katika hatua nyingine, Bw. Chifupa alimetoa ruksa kwa wote wanaoendelea kumuandika mtoto wake lakini waandike yaliyo ya kweli peke yake.

Marehemu Amina alikufa Juni 26, mwaka huu saa 8:45 usiku akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo na kuzikwa kijijini Ihanjo wilaya ya Njombe mkoa wa Iringa.
 



Very strange and disgusting! Those who said silence is golden had brains!
 
Ni nani aliyempa ujumbe Kapteni Komba kutoa Bungeni, I'll bet you ni yule yule mtajwa tajwa sana kwenye sakata hili.
 
Baba mjinga sana huyu!!!

Mzee huyu alikuwa Brigedia wa Jeshi la Wananchi Tanzania, kwa hiyo siyo mjinga vile, inawezekana kuna jambo. Ninahishi vile vile sasa hivi anasumbuliwa na kitendo cha kumkosa binti yake.
 
Amina Chifupa: Wazazi wake wajaa hofu

2007-07-13 17:22:00
Na Mwandishi wetu, Jijini

Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalimu kupitia Umoja wa Vijana wa CCM, marehemu Amina Chifupa, kimezidi kuzua mapya huku kikileta hofu kubwa katika familia yake.

Baba mzazi wa marehemu Amina, Luteni Mstaafu Hamis Gabriel Chifupa, amesema anahofia usalama wa familia yake iwapo atatangaza majina ya watu aliotajiwa na mwanae kabla ya kifo chake kwamba wanahusika kwa njia moja ama nyingine na maradhi yake.

``Kabla hajafa alikuwa akitaja majina ya baadhi ya viongozi, wengine ninyi waandishi mmekwishawataja, lakini wengine bado, pamoja na hayo mimi siwezi kuwataja kwa kuhofia usalama wangu na familia yangu, naiachia Serikali ifanye kazi hiyo,`` akasema Mzee Chifupa.

Akasema mwanae aliugua maradhi ya ajabu ambapo alikuwa akitaja majina ya baadhi ya viongozi kuwa ndio waliomsababishia tatizo la kuugua.

Akasema katika kipindi hicho chote Amina alikuwa hali chakula chochote na ndipo walipobaini kuwa yalikuwa mambo ya kiswahili, hivyo ikabidi kumuhudumia kiswahili.

Hata hivyo huduma hizo za kiswahili hazikufua dafu na ndipo walipoamua kumpeleka katika Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo.
Mzee Chifupa akasema akiwa hospitalini Amina aliendelea kutamka maneno mengi mazito na ya ajabu yaliyoashiria kifo chake.

``Familia haiwezi kusema Serikali ichunguze, ila kama kuna mtu mwenye taarifa au anayejua mazingira ya kifo cha mwanangu anaweza kutoa taarifa serikalini ili wanaohusika wachukuliwe hatua,`` akasema.

Amina Chifupa alifariki dunia Juni 26 mwaka huu katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo, alikokuwa akipatiwa matibabu.
  • SOURCE: Alasiri
 
I have really being saddened by the fact that her dad decided to to treat her "kiswahili" what the hell is that? in one way or another the family is to blame for delaying proper medical attention. I'm totally flabbergasted by this revelation.
 
.... (Mzee Chifupa)...Akasema mwanae aliugua maradhi ya ajabu ambapo alikuwa akitaja majina ya baadhi ya viongozi kuwa ndio waliomsababishia tatizo la kuugua. [*]SOURCE: Alasiri[/LIST]


Ugonjwa huu mpya ambao aliugua Bi. Chifupa na uliosababisha mauti yake kwa jina la kitaalamu hujulikana kama Uumbuajiasis Viongozitanzanialitis Hadharanum. Ugonjwa huu unatokana na kufuatilia mambo ya serikali na viongozi kwa karibu kiasi cha kutaka kuweka ubovu wao hadharani. Dalili kubwa za ugonjwa huu ni hizi:

a. Kupenda nchi zaidi kuliko chama
b. Kuwa tayari kutetea mali ya Taifa na kuilinda mali hiyo
c. Kutoogopa yatakayokukuta
d. Kuanza kuweka hadharani ubovu na siri za viongozi hasa kwa jamaa yako karibu
e. Kutosikiliza ushauri wa kutakiwa kukaa kimya na wakubwa wako
f. Kuwa kimbelembele kuzungumza na kukemea maovu kila upatapo nafasi
g. Kuwa mtetezi wa Katiba na mkosoaji wa jamii
h. Kutolegeza msimamo hadi kifo.

Maambukizi
Ugonjwa huu unaambukiza watu wachache kwani watu wengi wameshapatiwa kinga yake. Kwa wale wanaombukizwa wanafanya hivyo zaidi kwa kusoma habari za ufisadi, rushwa, na ubadhirifu katika serikali yao. Kwa kupitia mitandao, vitabu, na vyombo vya habari virusi vya ugonjwa huu vinajipenyeza katika akili za watu na kusababisha kusisimka kwa ubongo. Wale waliombukizwa ugonjwa huu hujikuta wakitafuta habari za kila namna na kushiriki mijadala yenye kutafakari mustakabali wa Taifa lao.

Kinga:
Ugonjwa huu kinga yake kubwa hujulikana kwa kitaalamu kama Mrungura. Kinga hii hutolewa kwa wale wote wenye kuanza kuonesha dalili za kukumbwa na ugonjwa huu. Kinga hii huwekwa kwenye mabenki na maofisi mbalimbali ili kuzuia viongozi wakubwa wasipatwe na virusi vya ugonjwa huu. Kinga hii pia hufanya kazi kwa wale walioanza kuonesha dalili kama kina Phillip Marmo, Chrisant Mzindakaya n.k Pindi mtu akishapatiwa kinga hii HAWEZI kuipinga serikali!

Tiba:
Hadi hivi sasa ugonjwa huu hauna tiba ya uhakika kwani wale ambao wameshaugua kwa muda mrefu hawako tayari kutibiwa kwani wanaona wanaishi vizuri tu na ugonjwa huu.

Karantini
Pindi baadhi ya wakubwa wakiona kuna mtu ambaye amefikia hatua ya juu kabisa ya ugonjwa huu basi kwa mbinu wanazozijua wenyewe wanamkarantini, na wakati mwingine anakuwa katika hali hiyo ya kutengwa hadi kifo ili asiendelee kuwaambukiza watu wengine.

Jihadhari
Kwa vile ugonjwa huu ni wa hatari, watu wabadhirifu, wezi wa mali ya umma, walaghai, na mafisadi hawawezi kuustahimili. Ugonjwa huu ni kinyume kabisa na watu hawa hivyo kama hutaki kuambuzizwa hakikisha unaendelea kujikita katika katika vitendo viovu vya kuharibu mali za umma na kuivunja vunja nchi huku ukishiriki katika kumegeana hadhina ya Taifa. Kwa vile ugonjwa huu unaendelea kuambukiza taratibu, kuna kila dalili hapo ulipo UNAISHI NA MWATHIRIKA!
 

You should patent this stuff man. Haya wale waliokuwa wanaamini Amina kauawa wamepata uthibitisho wao leo: kauawa kwa juju!

This is from the horses-mouth...hamna cha Mzee Mwanakijiji wala nini. Dingi anadai mwanaye karogwa...na wamemtibu "kienyeji" mpaka mahututi ndo wanampeleka hospitali. Tutatafuta mchawi mpaka asubuhi lakini tatizo hapa ni elimu ndogo na ujuha wa hali ya juu wa huyu Mzee. Cha kusikitisha ni kwamba kuna wasomi hapa wanakaa mamtoni na wana intaneti wanashindwa kumlaani huyu Mzee.

Mzee Mwanakijiji umekosa credibility kwa kutulea habari za uongo a couple of times humu.
 

Nakukubali ndugu Muhingo. Nadhani inafaa pia kuchunguza uhusiano kati ya Shigongo na hawa drug barons. Ule utajiri wake ni kwa kuuza udaku tu? Na ni roho gani aliyo nayo ya kuendelea "kumfunua maiti" hadi kuzimu?
 
Mmmmh Mzee Kichuguu napingana nawe kumpa uerevu huyu Mzee kwa sababu tu alikuwa "Brigedia wa Jeshi".Hakuna neno lolote linalomfaa Mzee Chifupa isipokuwa hilo Mjinga!.Kwa taarifa yako tu Mzee Kichuguu tumewahi kuwa na Mkuu wa Majeshi(Major General) asiyejua hata kuandika jina lake.

Sina budi kusema Mzee Chifupa ni Mjinga kwa sababu alijua Ukweli toka pale Amina aliposhindwa kwenda Mtwara kwa sababu ya maumivu makali ya kichwa.Amina alitaka kulizungumza suala zima Hadharani kwa Waandishi wa Habari,lakini Mzee huyu huyu alimkataza na kuwaambia waandishi wa Habari kuwa wamemaliza tatizo kifamilia.Kwa nini leo anakuja na kutueleza Upumbavu huu!!Eti Amina amekufa kwenye mazingira ya kiuchawi!,na kibaya zaidi amesema kwa mdomo wake kwamba licha ya Huyo Mjumbe wa NEC kuna Viongozi kadhaa Amina amewataja kabla ya kifo chake.P/se Mzee Chifupa tutajie majina hayo!.Hata kama yataleta mtafaruku kwa sababu ni viongozi wa serikali,lakini itakuwa tunamtendea haki Marehemu Amina, kwa sababu Umma wa Watanzania utajua "UKWELI".
 
Amina alikula sumu iliyokwenda kuharibu ini haraka sana - pure and simple.

Kama sumu ni kulogwa, basi amelogwa.
You can then throw in the - kuchanganyikiwa kwa akili kutokana na hali ya mambo ilivyokuwa imemzonga wakati huo, i.e., talaka n.k. There you have a perfect scenario ya kulogwa.

I think Mkjj was much closer to the truth than anyone else I have read here in JF.
 
The truth is that Amina died of AIDS. Hamna cha kulogwa wala nini!! Baba yake anaona aibu kusema ukweli ndio maana anaanza kutoa visingizio kibao mpaka anajichanganya mwenyewe. Kwa taarifa yenu ni kwamba madaktari wa Lugalo walishajua kuwa Amina atakufa and there was nothing they could do.

Hivi kama uchawi upo kweli kwanini tusiutumie uchawi kwa mambo ya maendeleo???
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…