Buriani Salum Zahoro

Buriani Salum Zahoro

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
BURIANI SALUM ZAHORO

Makala hiyo hapo chini niliandika miezi miwili iliyopita.

Naiweka tena tuisome kama kumbukumbu ya Salum Zahoro aliyefariki jana na kuzikwa jana hiyo hiyo:

SALUM ZAHORO MWIMBAJI WA "TANGANYIKA NA UHURU" 1961 NI MGONJWA SANA ANAHITAJI MSAADA

Tarehe 9 Desemba TBC walirusha kipindi cha kumbukumubu ya uhuru kipindi kikijikita zaidi katika mchango wa watu walioishi Magomeni ya miaka ya 1950.

Niliwashauri TBC kutumia nyimbo ya Salum Zahoro na Kiko Kids, ''Tanganyika na Uhuru,'' katika kipindi chao na kwa hakika hili walilipenda sana na wakaipiga nyimbo hii wakati wa kumaliza kipindi.

Nimeweka clip fupi ya mwisho wa kipindi Salum Zahoro akiimba nyimbo hii.

Umri wa nyimbo hii ni sawasawa na umri wa miaka 59 kipindi cha uhuru wa Tanganyika.

Salum Zahoro aliimba nyimbo hiyo akiwa kijana labda wa miaka 20 akiwa kiongozi wa Kiko Kids Tabora.

Katika nyimbo hii utamsikia Salum Zahoro akiwataja viongozi wa Serikali ya Uhuru - Julius Nyerere, Abdallah Fundikira, Nsilo Swai, Tewa Said Tewa, Kawawa na wengineo.

Picha hii pamoja na nyimbo hiyo kaniletea Hamisi Delgado kutoka Ujerumani ambae ni mzaliwa wa Tabora na akimjua Salum Zahoro toka yeye bado kijana mdogo.

Nilimfahamisha Delgado maradhi ya Mzee Salum Zahoro alipokuja likizo na siku ya pili tu alikwenda kumjulia hali nyumbani kwake ambako alifahamishwa kuwa Mzee Salum Zahoro amelazwa Hospitali ya Amana.

Delgado alikwenda kumuona hospitali.

Inatia simanzi na kusikitisha kuwa wazalendo wetu waliojenga taifa hili hatuwathamini. Hapa sitasema mengi kwani tatizo hili kwa sasa ni maarufu hakuna asiyelijua.

Miezi michache iliyopita nilipokea simu usiku kutoka kwa Juma Mwapachu akaniambia kuwa yuko na Mzee Steven Hiza aliyetunga nyimbo, ''Tanzania Yetu ni Nchi ya Furaha,'' akiwa na Atomic Jazz Band ya Tanga.

Juma Mwapachu akanieleza masikitiko yake kwa hali ambayo amemkutanayo Mzee Hiza wakati nyimbo hii yake ndiyo imekuwa kama utambulisho wa taifa letu ukipigwa na steshini zote za radio na televisheni.

Aliniuliza nini tufanye ili Mzee Hiza na wanamuziki wetu walioitumikia nchi hii angalau waonje faida ya jasho lao lau kama tumechelewa.

Hii ndiyo hali ya mashujaa wetu waliohamasisha Watanzania katika kujenga taifa hili na kuleta maendeleo.

Picha ya Mzee Salum Zahoro akiwa amelazwa hospitali.

https://youtu.be/kb7etyo820c


1612414280002.png
 
Kwa kweli hali hii inasikitisha sana. Huyu Mzee Zohori aliumwa sana na pengine hakupata matibabu kwa wakati. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
 
R.I.P gwiji. Halafu hakuna kitu kinaitwa nyimbo hii ni wimbo huu.
 
R.I.P gwiji. Halafu hakuna kitu kinaitwa nyimbo hii ni wimbo huu.
Rufiji,
Hili la "nyimbo," na "wimbo," lilijitokeza hapa nami nikajieleza.

Mimi nazungumza Kiswahili cha Kidarasalama ambako ndiyo kwetu.

"Nyimbo," ndivyo nilivyokuta wazee wangu wakizungumza.

Nimekuta wakisema, "saa," si "masaa."
Wakisema, "upungufu," si "mapungufu."

Hii ndiyo tofauti baina yetu.
 
BURIANI SALUM ZAHORO

Makala hiyo hapo chini niliandika miezi miwili iliyopita.

Naiweka tena tuisome kama kumbukumbu ya Salum Zahoro aliyefariki jana na kuzikwa jana hiyo hiyo:

SALUM ZAHORO MWIMBAJI WA "TANGANYIKA NA UHURU" 1961 NI MGONJWA SANA ANAHITAJI MSAADA

Tarehe 9 Desemba TBC walirusha kipindi cha kumbukumubu ya uhuru kipindi kikijikita zaidi katika mchango wa watu walioishi Magomeni ya miaka ya 1950.

Niliwashauri TBC kutumia nyimbo ya Salum Zahoro na Kiko Kids, ''Tanganyika na Uhuru,'' katika kipindi chao na kwa hakika hili walilipenda sana na wakaipiga nyimbo hii wakati wa kumaliza kipindi.

Nimeweka clip fupi ya mwisho wa kipindi Salum Zahoro akiimba nyimbo hii.

Umri wa nyimbo hii ni sawasawa na umri wa miaka 59 kipindi cha uhuru wa Tanganyika.

Salum Zahoro aliimba nyimbo hiyo akiwa kijana labda wa miaka 20 akiwa kiongozi wa Kiko Kids Tabora.

Katika nyimbo hii utamsikia Salum Zahoro akiwataja viongozi wa Serikali ya Uhuru - Julius Nyerere, Abdallah Fundikira, Nsilo Swai, Tewa Said Tewa, Kawawa na wengineo.

Picha hii pamoja na nyimbo hiyo kaniletea Hamisi Delgado kutoka Ujerumani ambae ni mzaliwa wa Tabora na akimjua Salum Zahoro toka yeye bado kijana mdogo.

Nilimfahamisha Delgado maradhi ya Mzee Salum Zahoro alipokuja likizo na siku ya pili tu alikwenda kumjulia hali nyumbani kwake ambako alifahamishwa kuwa Mzee Salum Zahoro amelazwa Hospitali ya Amana.

Delgado alikwenda kumuona hospitali.

Inatia simanzi na kusikitisha kuwa wazalendo wetu waliojenga taifa hili hatuwathamini. Hapa sitasema mengi kwani tatizo hili kwa sasa ni maarufu hakuna asiyelijua.

Miezi michache iliyopita nilipokea simu usiku kutoka kwa Juma Mwapachu akaniambia kuwa yuko na Mzee Steven Hiza aliyetunga nyimbo, ''Tanzania Yetu ni Nchi ya Furaha,'' akiwa na Atomic Jazz Band ya Tanga.

Juma Mwapachu akanieleza masikitiko yake kwa hali ambayo amemkutanayo Mzee Hiza wakati nyimbo hii yake ndiyo imekuwa kama utambulisho wa taifa letu ukipigwa na steshini zote za radio na televisheni.

Aliniuliza nini tufanye ili Mzee Hiza na wanamuziki wetu walioitumikia nchi hii angalau waonje faida ya jasho lao lau kama tumechelewa.

Hii ndiyo hali ya mashujaa wetu waliohamasisha Watanzania katika kujenga taifa hili na kuleta maendeleo.

Picha ya Mzee Salum Zahoro akiwa amelazwa hospitali.

https://youtu.be/kb7etyo820c


View attachment 1693896
Jamii yetu ikiwemo wewe na mimi, hili linatuhusu. Hakuna wa kumnyooshea kidole.
Nakubaliana na Mzee Mwapachu, nini kinahitajika kufanyika kuwasaidia na kuwaenzi wazee hawa?
 
Rufiji,
Hili la "nyimbo," na "wimbo," lilijitokeza hapa nami nikajieleza.

Mimi nazungumza Kiswahili cha Kidarasalama ambako ndiyo kwetu.

"Nyimbo," ndivyo nilivyokuta wazee wangu wakizungumza.

Nimekuta wakisema, "saa," si "masaa."
Wakisema, "upungufu," si "mapungufu."

Hii ndiyo tofauti baina yetu.
Sadaktaa Sheikh Mohammed.

Hayo ya 'wimbo' ni kiswahili cha kisasa siyo cha wenyeji kindakindaki.
 
Buriani Mzee Salum Zahoro

Hili la Wazee kutothaminiwa linatia uchungu. Mfano mzuri ni hiyo nyimbo ya Tanzania yetu ni nchi ya furaha' ambapo mtunzi hafaidiki na jasho lake kama walivyo wengi

Kuna sehemu nyingi ya tatizo.
Kwanza, ni kwa serikali zetu kutothamini watu waliotoa michango yao nyakati hizo.

Pili,ni watu waliokuwa madarakani 'wakalewa' na kujisahau leo wanatazama nyuma na kubaini tatizo.
Mfano, hivi Mzee Mwapachu, Mayor Sykes, Mayor Kitwana Kondo, akina Kandoro, Rais Kikwete n.k.ambao ni wenyeji wa maeneo wanayoishi hawa wazee hawakuliona tatizo hili wakiwa madarakani?
Walifanya nini wakati wakiwa na 'power' ?

Tatu, watu wanaowafahamu hawa wazee kama akina Mohamed Said wamefanya nini kuonyesha maisha yao ? Kuandika taarifa mzee akiwa Hospitali ni too late, kuandika Buriani ni jambo jema lakini linasaidiaje hali?


JokaKuu
 
Buriani Mzee Salum Zahoro

Hili la Wazee kutothaminiwa linatia uchungu. Mfano mzuri ni hiyo nyimbo ya Tanzania yetu ni nchi ya furaha' ambapo mtunzi hafaidiki na jasho lake kama walivyo wengi

Kuna sehemu nyingi ya tatizo.
Kwanza, ni kwa serikali zetu kutothamini watu waliotoa michango yao nyakati hizo.

Pili,ni watu waliokuwa madarakani 'wakalewa' na kujisahau leo wanatazama nyuma na kubaini tatizo.
Mfano, hivi Mzee Mwapachu, Mayor Sykes, Mayor Kitwana Kondo, akina Kandoro, Rais Kikwete n.k.ambao ni wenyeji wa maeneo wanayoishi hawa wazee hawakuliona tatizo hili wakiwa madarakani?
Walifanya nini wakati wakiwa na 'power' ?

Tatu, watu wanaowafahamu hawa wazee kama akina Mohamed Said wamefanya nini kuonyesha maisha yao ? Kuandika taarifa mzee akiwa Hospitali ni too late, kuandika Buriani ni jambo jema lakini linasaidiaje hali?


JokaKuu
Nguruvi3,
Misaada ya watu binafsi haikidhi pakubwa.

Jamii ina watu wengi mfano wa hawa na tunaishinao miaka yote.

Wenye kufanya watafanya kama ilivyo ada lakini haiondoi shida.

Ama ukiona jambo mwishowe limeanikwa hadharani ni kuwa msaada zaidi unahitajika na kwa hakika tumeishi na hawa wazee wetu miaka yoye katika kipindi hicho hawakuhitaji msaada wa yeyote.

Uzee ulipowatopea hapo ndipo matatizo yalipoanza.

Wizara husika na nambo haya ipo na tujaalie watachukua hatua stahiki.
 
Salum Zahoro nilipenda sana uimbaji wake wa kufungua koo lote; ningependa waimbaji wa sasa wamuige pia, siyo huu uimbaji wa kubanabana makoo na pua tu. Nitamkumbuka sana kwa nyimbo nyingi ile ule wa "Wamtetea Bure" huwa nausikiliza sana mpaka leo.

Kama kweli katangulia mbele ya haki, basi mola wetu ampumuzishe kwa amani huko atakakoona kunamfaa.

 
Rufiji,
Hili la "nyimbo," na "wimbo," lilijitokeza hapa nami nikajieleza.

Mimi nazungumza Kiswahili cha Kidarasalama ambako ndiyo kwetu.

"Nyimbo," ndivyo nilivyokuta wazee wangu wakizungumza.

Nimekuta wakisema, "saa," si "masaa."
Wakisema, "upungufu," si "mapungufu."

Hii ndiyo tofauti baina yetu.
Tuna rahis asiyejua historia na asiyejali kitu
 
Rufiji,
Hili la "nyimbo," na "wimbo," lilijitokeza hapa nami nikajieleza.

Mimi nazungumza Kiswahili cha Kidarasalama ambako ndiyo kwetu.

"Nyimbo," ndivyo nilivyokuta wazee wangu wakizungumza.

Nimekuta wakisema, "saa," si "masaa."
Wakisema, "upungufu," si "mapungufu."

Hii ndiyo tofauti baina yetu.

Singular nouns (zinazohesabika) za kiswahili zinazoanza na "w," wingi wake huanza "ny." Kwa mfano Wimbo-Nyimbo (Albamu ina nyimbo nyingi zunri, ila kuna wimbo mmoja nilioenda sana) , Wembe-Nyembe (Kasha lina nyembe 12 lakini kinyozi hutumia wembe mmoja tu kumnyoa mteja wake), Wakati-Nyakati: kwa maana ya kipindi fulani kwa siku (Wakati wa usiku siyo muda mzuri kwenda nje ila kuna nyakati nyingi ambapo kunakuwa hakuna haja ya kutokwenda nje usiku). Kwa hiyo unaposema nyimbo una maana ya nyimbo nyingi, siyo wimbo mmoja.

1612729107632.png

1612729145935.png
 
Singular nouns (zinazohesabika) za kiswahili zinazoanza na "w," wingi wake huanza "ny." Kwa mfano Wimbo-Nyimbo (Albamu ina nyimbo nyingi zunri, ila kuna wimbo mmoja nilioenda sana) , Wembe-Nyembe (Kasha lina nyembe 12 lakini kinyozi hutumia wembe mmoja tu kumnyoa mteja wake), Wakati-Nyakati: kwa maana ya kipindi fulani kwa siku (Wakati wa usiku siyo muda mzuri kwenda nje ila kuna nyakati nyingi ambapo kunakuwa hakuna haja ya kutokwenda nje usiku). Kwa hiyo unaposema nyimbo una maana ya nyimbo nyingi, siyo wimbo mmoja.

View attachment 1697135
View attachment 1697136
Kichuguu,
Ahsante kwa.juhudi yako lakini zingatia kuwa hata hiyo "standard Kiswahili," imetuletea maneno ya "s" class na "u" class ambayo hayakuwa na plural ya wingi.

Leo tuna "masaa" na tuna, "mapungufu," maneno mimi nimeyakutakatika Kiswahili chetu cha Kidarisalama hayakupata kuwa na wingi.
 
Kichuguu,
Ahsante kwa.juhudi yako lakini zingatia kuwa hata hiyo "standard Kiswahili," imetuletea maneno ya "s" class na "u" class ambayo hayakuwa na plural ya wingi.

Leo tuna "masaa" na tuna, "mapungufu," maneno mimi katika Kiswahili chetu cha Kidarisalama hayakupata.kuwa na wingi.
Kuna maneno mengi kwenye kiswahili leo ni mapya kutokana na utamaduni kubadilika. Zamani sana watu walikuwa hawajali muda kwa hiyo inawezekana hawakuwa wanahesabu masaa; ni kama ambavyo hatukuwa na utamaduni wa kufanya matengenezo ya vitu vyetu mpaka viharibike kabisa, kwa hiyo hatukuwa na neno la ukarabati.

leo hii elewa kuwa neno saa lina maana mbili; maana moja ni ile ya kuonyesha muda (o'clock) ambalo halina wingi; Utaamka saa moja, ufike nyumbani kwangu mbili na nusu na kadhalika. Lakini vile vile neno saa lina maana ya kuonyesa urefu wa muda (hour) katika kipindi fulani, ambalo lina wingi: kutoka Dar kwenda Morogoro safari inachukua muda saa moja au inachukua muda wa masaa mawili. Hili neno liliwahi kujadiliwa zamani sana na Sheikh Suleiman Kilemile katika kipindi cha baraza la kiswahili RTD zaidi ya miaka 25 iliyopita kwa hiyo halina ubishi.

Hilo la upungufu na mapungufu pia nina imani liko hivyo hivyo unavyopinga kwa kufuata isimu ya kiswahili.
 
Kuna maneno mengi kwenye kiswahili leo ni mapya kutokana na utamaduni kubadilika. Zamani sana watu walikuwa hawajali muda kwa hiyo inawezekana hawakuwa wanahesabu masaa; ni kama ambavyo hatukuwa na utamaduni wa kufanya matengenezo ya vitu vyetu mpaka viharibike kabisa, kwa hiyo hatukuwa na neno la ukarabati.

leo hii elewa kuwa neno saa lina maana mbili; maana moja ni ile ya kuonyesha muda (o'clock) ambalo halina wingi; Utaamka saa moja, ufike nyumbani kwangu mbili na nusu na kadhalika. Lakini vile vile neno saa lina maana ya kuonyesa urefu wa muda (hour) katika kipindi fulani, ambalo lina wingi: kutoka Dar kwenda Morogoro safari inachukua muda saa moja au inachukua muda wa masaa mawili. Hili neno liliwahi kujadiliwa zamani sana na Sheikh Suleiman Kilemile katika kipindi cha baraza la kiswahili RTD zaidi ya miaka 25 iliyopita kwa hiyo halina ubishi.

Hilo la upungufu na mapungufu pia nina imani liko hivyo hivyo unavyopinga kwa kufuata isimu ya kiswahili.
Kichuguu,
Mimi sina tatizo na Kiswahili anachozungumza mzaliwa wa bara kwake yeye, "darasa," anaweza akatamka kama, "dalasa."

Hivyo ndivyo alivyojfunza na ndivyo anavyozungumza.

Anaweza kutamka, "masaa," "lisaa" nk.
Sina tatizo asilani.

Kama ulivyosema hicho ni Kiswahili kipya.
 
Kichuguu,
Mimi sina tatizo na Kiswahili anachozungumza mzaliwa wa bara kwake yeye, "darasa," anaweza akatamka kama, "dalasa."

Hivyo ndivyo alivyojfunza na ndivyo anavyozungumza.

Anaweza kutamka, "masaa," "lisaa" nk.
Sina tatizo asilani.

Kama ulivyosema hicho ni Kiswahili kipya.
Siyo swala la kiswahili cha bara wala cha Dar es salaamu au cha Mombasa au cha Tanga au cha Zanzibar, bali tunaongelea kiswahili kufuatana na isimu ya lugha yenyewe kama inavyotambulika na BAKITA. Kiswahili cha makabila mbalimbali kinaweza kuwa kinachanganya na lugha zao za asili lakini kiswahili cha BAKITA ni hicho tunachokuambia, inawezekana na wewe unaongea kiswahili cha kabila lako kwa hiyo hufuati isimu ya kiswahili bila kujielewa. Nimeishi na wamarekani wengi ambao hawana lugha nyingine bali ni kiingereza tu lakini wanaongea kiingereza broken sana, kwa mfano anaweza kupinga jambo kwa kusema "I don't know nothing!" Kwa hiyo na wewe inawezekana umeazaliwa na kukulia dar es Salaam na unajua kiswahili tu, lakini ni hicho kiswahi cha "I don't know nothing"

Kubali tu mzee mwenzangu kuwa inawezeka umekulia katika kiswahili kisichofuata isimu ya kiswahili na hilo lisiwe tatizo la kukufanya upinge kuwa wanonyoosha kiswahili chako ni watu wa bara tu wasiojua kiswahili ilihali hata wataalamu akina Sheikh Kilemile waliwahi kuliweka hilo bayana.
 
Tuna rahis asiyejua historia na asiyejali kitu

Ni kweli huyu Rais haijui historia sio ya chama anachokiongoza tu bali hata historia ya nchi anayoiongoza!! Nadhani kutoa Marais waliopita ni wazee wachache sana walioitumikia nchi hii na bado wako hai wanatambuliwa na serikali yake. Hawa wazee ni hazina kubwa sana ambayo ilitumiwa vizuri na watangulizi wake na ndio maana kwa mfano marehemu Mkapa alikuwa anawapa msamaha wa tozo kama zile za nyumba zao wanazoishi kitu ambacho sidhani kama serikali hii ina busara ya kufanya. Hawa wazee wenye miaka 70 na na ushee sio wengi kwani wengi wao wametangulia mbele ya haki hivyo si vizuri kuwaona wakisumbuliwa na kodi katika umri wao huo. Hapo hapo hawa wazee wanasumbuliwa kupata mafao yao ya uzeeni bila mafanikio kwani mifuko ya hifadhi ya jamii haina fedha za kuwalipa!!!
 
Back
Top Bottom