BURIANI Sultan Jamshid BIN Abdulla BIN Khalifa (1926 - 2024)

BURIANI Sultan Jamshid BIN Abdulla BIN Khalifa (1926 - 2024)

Mbona kama Mzee Said anatuvuruga? @ Paschal tunaomba utunyooshee maelezo na historia iwekwe sawa.....ina maana Sultan hakufanya ...udhalimu unaosemwa na kuandikwa sana? Heshima ya mapinduzi Matukufu kumbe ni uongo? Utumwa dhuluma udhalilishaji mateso etc....tunaomba sana tuwekane sawa hapa....
Pascal Mayalla
 
Mzee@Mohamed Said,niliwahi kuzungumza na Mzee mmoja Mzanzibari Chotara kuhusu Mapinduzi na utawala wa kisultan maana alikuwepo.
Alichoniambia,ni kwamba Waarabu waliishi kwa Amani na Wazawa ijapokuwa waliishi madaraja tofauti.
Waarabu walikuwa Raia wa Daraja la Juu na Wazawa wakiwa Raia wa Daraja la chini.
Na ubaguzi ulikuwepo.
Lakini alilalamikia Mapinduzi,kuwa Wazawa walimwaga Damu nyingi ya Waarabu mpaka kupelekea wengine kukimbia na manusura waliobakia ndio watu kama wao ambao Waarabu walizaa na wanawake wa kiswahili.
Kwa kifupi;
kwa mtazamo wangu Mapinduzi yalikuwa Muhimu ili kuondokana na Unyonyaji wa Waarabu na tabia zao za ukabaila za kukodisha ardhi kwa Wazawa wenye ardhi Yao na kuwatoza Kodi.
Pia kukomesha madaraja baina ya Waarabu na watu weusi.
Inasikitisha kiwango cha umwagaji damu uliotokea lakini lazima tukubaliane kwamba silaha zilitumika na pande zote Mbili,Wazawa wangezembea wao ndio wangekufa wengi.
Nayasifu MAPINDUZI maana sultan hakuwa na Haki ya kutawala na alikuwa mvamizi.
Ukiwavamia watu na ukawatawala kimabavu ni lazima siku Moja watakutoa tu,kama alivyotolewa sultan.
Labda Jemshid alikuwa mtu mzuri lakini historia ya watawala waliopita ilimponza,manyanyaso na ubaguzi vina tabia ya kuchosha watawaliwa.
Tabia hiyo ya Ubaguzi imeota mizizi mpaka Leo Zanzibar,Muunguja anambagua mpemba,Wazanzibar wanatubagua Wabara na kutuita majina ya kutweza,watu wengi wenye asili ya kiarabu na ngozi nyeupe nao huwaona watu weusi kama wewe kuwa si kitu.
Yote kwa yote,ni historia tu na inabidi tujifunze na tujirekebishe kwayo.
MAPINDUZI DAIMA.
Wasalaam.
 
Abdulatif...
Kwanza muhimu uelewe hakuna Mzanzibari Chotara wala Mzanzibari Mweusi.

Wazanzibari hawajapata kujinasibu kwa hivyo.

Hili la rangi na matabaka lilikuwapo enzi za Sultan kama lilivyo duniani kote na lipo hadi leo Tanzania.

Ukileta suala la uzawa Zanzibar utapata shida kubwa kupita kiasi kwani utawakuta Waafrika koo zao haziendi nyuma hata kizazi kimoja na utawakuta wengine wana damu ya Kiomani na Kimanyema wanakwenda nyuma vizazi hadi saba na pengine zaidi.

Sultani hakuvamia Zanzibar aliombwa na Wazanzibari wenyewe kuja Zanzibar kuwaondoa Wareno walioivamia Zanzibar wakaikalia kwa nguvu na kuupiga vita Uislam.
Mzee@Mohamed Said,niliwahi kuzungumza na Mzee mmoja Mzanzibari Chotara kuhusu Mapinduzi na utawala wa kisultan maana alikuwepo.
Alichoniambia,ni kwamba Waarabu waliishi kwa Amani na Wazawa ijapokuwa waliishi madaraja tofauti.
Waarabu walikuwa Raia wa Daraja la Juu na Wazawa wakiwa Raia wa Daraja la chini.
Na ubaguzi ulikuwepo.
Lakini alilalamikia Mapinduzi,kuwa Wazawa walimwaga Damu nyingi ya Waarabu mpaka kupelekea wengine kukimbia na manusura waliobakia ndio watu kama wao ambao Waarabu walizaa na wanawake wa kiswahili.
Kwa kifupi;
kwa mtazamo wangu Mapinduzi yalikuwa Muhimu ili kuondokana na Unyonyaji wa Waarabu na tabia zao za ukabaila za kukodisha ardhi kwa Wazawa wenye ardhi Yao na kuwatoza Kodi.
Pia kukomesha madaraja baina ya Waarabu na watu weusi.
Inasikitisha kiwango cha umwagaji damu uliotokea lakini lazima tukubaliane kwamba silaha zilitumika na pande zote Mbili,Wazawa wangezembea wao ndio wangekufa wengi.
Nayasifu MAPINDUZI maana sultan hakuwa na Haki ya kutawala na alikuwa mvamizi.
Ukiwavamia watu na ukawatawala kimabavu ni lazima siku Moja watakutoa tu,kama alivyotolewa sultan.
Labda Jemshid alikuwa mtu mzuri lakini historia ya watawala waliopita ilimponza,manyanyaso na ubaguzi vina tabia ya kuchosha watawaliwa.
Tabia hiyo ya Ubaguzi imeota mizizi mpaka Leo Zanzibar,Muunguja anambagua mpemba,Wazanzibar wanatubagua Wabara na kutuita majina ya kutweza,watu wengi wenye asili ya kiarabu na ngozi nyeupe nao huwaona watu weusi kama wewe kuwa si kitu.
Yote kwa yote,ni historia tu na inabidi tujifunze na tujirekebishe kwayo.
MAPINDUZI DAIMA.
Wasalaam.
 
Much...
Mipango ya mapinduzi ilifanyika Tanganyika na Zanzibar.

Tanganyika sehemu inayoitwa Kipumbwi, Tanga iliwekwa kambi ya Wamakonde kutoka Shamba la Mkonge la Sakura kuwafunza mbinu za kupigana.

Hawa Wamakonde walivushwa kuingia Zanzibar kushiriki uchaguzi na mwaka wa 1964 walishiriki kama askari mamluki kupindua serikali ya Sheikh Mohamed Shamte.
Kwa ufupi serikali ya Shamte na utawala wa Jamshid ulipinduliwa na mamluki kutoka Tanganyika na sio wazanzibari ?
 
Abdulatif...
Kwanza muhimu uelewe hakuna Mzanzibari Chotara wala Mzanzibari Mweusi.

Wazanzibari hawajapata kujinasibu kwa hivyo.

Hili la rangi na matabaka lilikuwapo enzi za Sultan kama lilivyo duniani kote na lipo hadi leo Tanzania.

Ukileta suala la uzawa Zanzibar utapata shida kubwa kupita kiasi kwani utawakuta Waafrika koo zao haziendi nyuma hata kizazi kimoja na utawakuta wengine wana damu ya Kiomani na Kimanyema wanakwenda nyuma vizazi hadi saba na pengine zaidi.

Sultani hakuvamia Zanzibar aliombwa na Wazanzibari wenyewe kuja Zanzibar kuwaondoa Wareno walioivamia Zanzibar wakaikalia kwa nguvu na kuupiga vita Uislam.
Ahsante kwa kunielimisha zaidi,Sina ninalojua zaidi yako Mzee wangu.
Huu ni mtazamo wangu tu kutokana na uzoefu wangu wa Maisha ya visiwani pamoja na story za wazee huko kwenye maskani zao.
 
Mtu mwema au ufalme utokanao na watu kamwe hauwezi pata upinzani au mapinduzi kutoka kwa watu wake.

Ukiona ufalme umepinduliwa jua ni ufalme aliojipa madaraka wenyewe,umeua na kuumiza,umeleta madhira kwa watu hadi watu wakauchoka na kuamua kuleta mapinduzi.

Huyo sultan ni moja kati ya watawala walio umiza sana wazanzibar kwa kuwafanya watumwa katika nchi yao,wakati huo yeye sio mzawa halisi wa visiwa hivyo bali ni uzao wa watesi kutokea omani.

Daima mapinduzi matukufu ya enziwe kutoa utawala haramu wa sultani.
Kwan serikali ipi ilipinduliwa Zanzibar?
 
Mzee@Mohamed Said,niliwahi kuzungumza na Mzee mmoja Mzanzibari Chotara kuhusu Mapinduzi na utawala wa kisultan maana alikuwepo.
Alichoniambia,ni kwamba Waarabu waliishi kwa Amani na Wazawa ijapokuwa waliishi madaraja tofauti.
Waarabu walikuwa Raia wa Daraja la Juu na Wazawa wakiwa Raia wa Daraja la chini.
Na ubaguzi ulikuwepo.
Lakini alilalamikia Mapinduzi,kuwa Wazawa walimwaga Damu nyingi ya Waarabu mpaka kupelekea wengine kukimbia na manusura waliobakia ndio watu kama wao ambao Waarabu walizaa na wanawake wa kiswahili.
Kwa kifupi;
kwa mtazamo wangu Mapinduzi yalikuwa Muhimu ili kuondokana na Unyonyaji wa Waarabu na tabia zao za ukabaila za kukodisha ardhi kwa Wazawa wenye ardhi Yao na kuwatoza Kodi.
Pia kukomesha madaraja baina ya Waarabu na watu weusi.
Inasikitisha kiwango cha umwagaji damu uliotokea lakini lazima tukubaliane kwamba silaha zilitumika na pande zote Mbili,Wazawa wangezembea wao ndio wangekufa wengi.
Nayasifu MAPINDUZI maana sultan hakuwa na Haki ya kutawala na alikuwa mvamizi.
Ukiwavamia watu na ukawatawala kimabavu ni lazima siku Moja watakutoa tu,kama alivyotolewa sultan.
Labda Jemshid alikuwa mtu mzuri lakini historia ya watawala waliopita ilimponza,manyanyaso na ubaguzi vina tabia ya kuchosha watawaliwa.
Tabia hiyo ya Ubaguzi imeota mizizi mpaka Leo Zanzibar,Muunguja anambagua mpemba,Wazanzibar wanatubagua Wabara na kutuita majina ya kutweza,watu wengi wenye asili ya kiarabu na ngozi nyeupe nao huwaona watu weusi kama wewe kuwa si kitu.
Yote kwa yote,ni historia tu na inabidi tujifunze na tujirekebishe kwayo.
MAPINDUZI DAIMA.
Wasalaam.
Nini maana ya uvamizi na nin maana ya mapinduzi?

Tuanzie hapa kwnz
 
Kwa ufupi serikali ya Shamte na utawala wa Jamshid ulipinduliwa na mamluki kutoka Tanganyika na sio wazanzibari ?
Proved,
Uongozi wa ASP ulishirikiana serikali ya Tanganyika kufanikisha Mapinduzi.

Halikadhalika Makomredi yaani Umma Party walitoa michango wao kuonyesha njia pale walipoingia kati kukomesha mauaji.
 
Mzee embu muogope Mungu wako,kwa hiyo unataka kutuambia kati yako wewe uliyehadithiwa kuhusu Mapinduzi na Wazanzibar wenyewe wakiongozwa na Abdulhaman Babu chini ya Umma party walioshiriki Mapinduzi nani ni mkweli katika Usahihi wa kufanya Mapinduzi hayo?
 
View attachment 3189131
(1929 - 2024)​

Hiyo taazia hapo chini niliandika majuma machache yaliyopita nilipopokea taarifa kuwa Sultan Jamshid kafariki.

Haukupita muda nikapokea taarifa kuwa si kweli yu hai.
Nilijisikia vibaya sana.

Ninachokumbuka ni kupokea ujumbe kutoka kwa rafiki yangu akiniambia nilifanya haraka kuandika.

Sikuwa na la kusema.
Nilibakia kimya.

Niliandika taazia wakati Sultan Jamshid yu hai.
Taazia niliyoiandika ni hiyo hapo chini:

Jana usiku ndugu yangu kaniletea ujumbe mfupi kuwa Sultan Seyyid Jamshid, Sultani wa mwisho wa Zanzibar kafariki.

Asubuhi ndugu yangu huyu akanipigia simu tukazungumza mawili matatu akanifahamisha kuwa yeye hakupata kuonana na Jamshid ila alizungumzanae mara moja kwa simu Jamshid alipokuwa anaishi Portsmouth.

Sasa nikawa najiuliza nini naweza kuandika kuhusu Sultan Jamshid.

Jamshid kaandikwa sana kiasi nimekumbuka maneno ya marehemu Bibi Titi Mohamed aliponiambia, "Bwana Mohamed kipi utakachoandika wewe kuhusu mimi ambacho bado hakijaandikwa?"

Kipi ninachoweza mimi hii leo kuandika kuhusu Sultan Jamshid ambacho bado hakijaandikwa?

Kipo cha kuandika kuhusu Sultan Jamshid bin Abdulla bin Khalifa ambacho bado hakijaandikwa.

Jamshid kaondoka Zanzibar baada ya mapinduzi nafsi yake ikiwa imesalimika.
Jamshid anakwenda kwa Mola wake vidole vyake vikiwa safi havichuruziki damu.

Hakuna Mzanzibari anaeweza kusimama akasema Sultani ameniulia ndugu yangu au Sultani kanidhulumu haki yangu hii au ile.

Jamshid kaondoka Zanzibar hakuacha jela za mateso.
Jamshid hakuacha jela za mateso kwa kuwa hakurithi jela ya mateso.

Jamshid hakupata kukalia kiti cha enzi kilicholowa damu.
Hakika lipo la kuandika na la kusema kuhusu Jamshid.

Nimeingia Maktaba.
Natalii farahasha ya kitabu cha Harith Ghassany, "Kwaheri Uhuru Kwaheri Ukoloni."

Nataka nijikumbushe.

Najikumbusha kwa kuwa nilikuwa msaidizi wa Dr. Ghassany wakati wa utafiti wa kitabu hiki chake.

Nasoma yaliyomfika Jamshid halikadhalika nayasoma yale waliyopitia Wazanzibari waliokuwa nje ya Zanzibar mapinduzi yalipotokea.

Nayasoma na kuona kama vile ndiyo kwanza hayo nisomayo nayasikia leo.
Sultan Jamshid kapewa hifadhi Dar es Salaam yeye na familia yake na baadhi ya watu.

Wako wamejibanza kwenye nyumba mbili jumla yao watu 43.
Serikali ya Tanganyika inafanya mawasiliano na Waingereza kuhusu Sultan Jamshid.

Jamshid Sultan wa Zanzibar ni mtu masikini kwani hana fedha nje ya Zanzibar hata senti moja.

Sultan hana nauli ya kumfikisha Uingereza.

Nimetosheka.
Navuta kitabu kingine ninachokumbuka kuna habari za Sultan Jamshid.

Hili ni buku la mapicha kutoka matoleo ya gazeti maarufu DRUM lililokuwa likimilikiwa na Jim Bailey kutoka Johannesburg, Afrika Kusini.

Nilisaidia kuhariri na kuchapwa kwa kitabu hiki.

Katika kitabu hiki kuna makala ya Jamshid akiwa na watu wapatao 500 wananchi wa kawaida wanaingia porini kuwinda nguruwe.

Sultan Jamshid anaingia porini kwenye msitu mzito bila ulinzi wowote kuwinda pamoja na wawindaji wenzake wamemzunguka wamebeba mikuki.

Hakika yako mengi ya kusema kuhusu Jamshid.

Sura inayofuatia katika DRUM ni kuhusu mapinduzi chenye kichwa cha habari, "Bloodshed on the Spice Isle."

Nahitimisha safari yangu Maktaba kwa kitabu muhimu sana katika historia ya masultani: "Omani Sultans in Zanzibar," kilichoandikwa na Ahmed Hamoud Al Maamiry.

Mwanzo wa kitabu mwandishi anasikitika kuhusu damu iliyomwagika katika mapinduzi.
Siku zote historia ya mapinduzi itakuacha na majonzi.

Mwenyezi Mungu amfanyie wepesi hisabu yake ndugu yetu Sultan Jamshid bin Abdulla bin Khalifa.

View attachment 3189147

Huyu mzee amepata hitilafu kabisa kiakili!
Anamlilia mkoloni kwakuwa tu ni mwisilamu mwenzake na mwarabu!? Aibu gani hii kwa Mwafrika!!

Waafrika Imani hizi za kigeni zililetwa kutupiga pingu za ubongo.
 
Huyu Mzee kila siku anamdisi Mwalimu Nyerere aliyeongoza harakati za uhuru wetu, ila huyu hapa anamsifia Sultani aliyepinduliwa kwa kuwanyima haki za kisiasa n.k wazanzibar.
Kisa na mkasa; Dini.
Huyu mzee ni mhaini na mkosi mkubwa kwa taifa letu! Ni zaidi ya gaidi sijui kwanini serikali inamwangalia tu.

Sina lugha nyingine juu yake zaidi ya hiyo.
 
Proved,
Uongozi wa ASP ulishirikiana serikali ya Tanganyika kufanikisha Mapinduzi.

Halikadhalika Makomredi yaani Umma Party walitoa michango wao kuonyesha njia pale walipoingia kati kukomesha mauaji.
Hao ASP na umma party walikuwa watanganyika?
 
Back
Top Bottom