Burkina faso yaanzisha utaratibu wa kurusha mubashara ( live) kesi zinazohusu ubadhirifu/ wizi wa fedha za umma

Burkina faso yaanzisha utaratibu wa kurusha mubashara ( live) kesi zinazohusu ubadhirifu/ wizi wa fedha za umma

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Burkina Faso iliyo chini ya utawala wa kijeshi wa Kapteni Ibrahim Traore imeanzisha utaratibu wa kurusha live kesi zote zinazohusu ubadhirifu wa fedha za umma.

Utaratibu huo umeanza mwezi Novemba 2024 na watuhumiwa walioanza nao ni maafisa wa wizara ya misaada ya kibinadamu wanaotuhumiwa kuiba fedha zilizotolewa kwa ajili ya kusaidia wananchi waliokimbia makazi yao kutokana na sababu za kiusalama.

Kesi hizo zinarushwa live kwenye vituo mbalimbali vya Televisheni, Chaneli za YouTube pamoja na kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii ili kuwawezesha wananchi wote kujionea mwenendo wa kesi hizo.

Katika mwenendo wa kesi inayowahusu maafisa wa wizara ya misaada ya kibinadamu,leo tarehe 17 Disemba 2024 mmojawapo wa watuhumiwa aitwaye Amidou Tenya amekiri kuiba kiasi cha CFA Francs milioni 44 ambazo ni sawa na shilingi Milioni 12 za Tz katika nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2023 na 2024.

Amidou amesema kwamba alitumia pesa hizo kwa ajili ya kununua shamba, jumba la kifahari pamoja na kumjengea nyumba baba yake aliyepo nchini Ivory Coast.

Amidou amekiri kuiba kiasi hicho cha fedha ingawa anatuhumiwa kuiba kiasi kikubwa zaidi ya alichotaja na kutumia kujenga hotel ya vyumba 20, mabwawa mawili ya kuogelea, kiwanda cha kuzalisha chakula cha mifugo, kuchimba visima virefu vinne ,kununua shamba na kuanza ufugaji wa wanyama mbalimbali kama ng'ombe, swala pamoja na ndege aina ya mbuni, kununua magari ya kifahari pamoja na kununua wanyama kama ng'ombe na ngamia waliotumika kwenye ibada ya "zindiko" ili kuzuia serikali kutambua wizi alioufanya.

Watuhumiwa wengine walikana mashtaka yao na kesi imeahirishwa hadi hapo itakapotajwa tena. Endapo watuhumiwa hao watakutwa na hatia, watakabiliwa na adhabu mbalimbali ikiwemo mali zao kuuzwa ili serikali iweze kurudisha kiasi kilichoibiwa.

Kwa upande mwingine mawakili wa upande wa utetezi wameomba utaratibu wa kurusha kesi mubashara ukomeshwe kwa madai kuwa unawadhalilisha watuhumiwa wao .

Chanzo: YouTube Channel ya Shirika la habari la Burkina Faso ( RTB)
 
Hakuna kitu hapo. Ukiona hivyo uchaguzi unekarinia; the ruling regime wants to be back in power. Changa la macho kwa wajinga hilo kiki mzuka.
Serikali ya kijeshi na uchaguzi wapi na wapi? Huyo kutoka mpaka apende mwenyewe.
 
Isiwe tu kama ile movie ya Ousmane Sembene.
 
Wakipigiwa sana kelele wanajifanya kugombea kiraia.
Hata wakigombea wakaamua kuiba kura Huwezi kufanya chochote. So hapo hesabu kutoka ni hadi apende mwenyewe. Halafu ECOWAS ndio walikuwa wanawapigia kelele lakini wamejitoa ECOWAS. AU waliwasimamisha uanachama na wanapeta tu. Wananchi wakichoka watamtoa wenyewe kama walivyomtoa Blaise Compaoré
 
Hata wakigombea wakaamua kuiba kura Huwezi kufanya chochote. So hapo hesabu kutoka ni hadi apende mwenyewe
Umeeleza vizuri. For your info tawala zote hakuna inayopenda kujionesha ni dhalimu. Always ita-side na wananchi kujionesha it is there for public interest but in reality it might be quietly different! Stuka!
 
Umeeleza vizuri. For your info tawala zote hakuna inayopenda kujionesha ni dhalimu. Always ita-side na wananchi kujionesha it is there for public interest but in reality it might be quietly different! Stuka!
Cha muhimu kiongozi awe mzuri na mzalendo basi. Thomas Sankara alikuwa mjeda na alifanya mambo mazuri kwa muda mfupi ndio maana Ufaransa wakatumia mtu kumuua. Lakini pia kuna mifano mingine ya viongozi wanajeshi walionyonya nchi kama Mobutu na wengineo. Kwahiyo binafsi nawatakia heri. Kama anafanya kazi nzuri sio lazima atoke hata Angela Merkel aliongoza nchi kwa miaka karibu 20.
 
Burkina Faso iliyo chini ya utawala wa kijeshi wa Kapteni Ibrahim Traore imeanzisha utaratibu wa kurusha live kesi zote zinazohusu ubadhirifu wa fedha za umma.

Utaratibu huo umeanza mwezi Novemba 2024 na watuhumiwa walioanza nao ni maafisa wa wizara ya misaada ya kibinadamu wanaotuhumiwa kuiba fedha zilizotolewa kwa ajili ya kusaidia wananchi waliokimbia makazi yao kutokana na sababu za kiusalama.

Kesi hizo zinarushwa live kwenye vituo mbalimbali vya Televisheni, Chaneli za YouTube pamoja na kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii ili kuwawezesha wananchi wote kujionea mwenendo wa kesi hizo.

Katika mwenendo wa kesi inayowahusu maafisa wa wizara ya misaada ya kibinadamu,leo tarehe 17 Disemba 2024 mmojawapo wa watuhumiwa aitwaye Amidou Tenya amekiri kuiba kiasi cha CFA Francs milioni 44 ambazo ni sawa na shilingi Milioni 12 za Tz katika nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2023 na 2024.

Amidou amesema kwamba alitumia pesa hizo kwa ajili ya kununua shamba, jumba la kifahari pamoja na kumjengea nyumba baba yake aliyepo nchini Ivory Coast.

Amidou amekiri kuiba kiasi hicho cha fedha ingawa anatuhumiwa kuiba kiasi kikubwa zaidi ya alichotaja na kutumia kujenga hotel ya vyumba 20, mabwawa mawili ya kuogelea, kiwanda cha kuzalisha chakula cha mifugo, kuchimba visima virefu vinne ,kununua shamba na kuanza ufugaji wa wanyama mbalimbali kama ng'ombe, swala pamoja na ndege aina ya mbuni, kununua magari ya kifahari pamoja na kununua wanyama kama ng'ombe na ngamia waliotumika kwenye ibada ya "zindiko" ili kuzuia serikali kutambua wizi alioufanya.

Watuhumiwa wengine walikana mashtaka yao na kesi imeahirishwa hadi hapo itakapotajwa tena. Endapo watuhumiwa hao watakutwa na hatia, watakabiliwa na adhabu mbalimbali ikiwemo mali zao kuuzwa ili serikali iweze kurudisha kiasi kilichoibiwa.

Kwa upande mwingine mawakili wa upande wa utetezi wameomba utaratibu wa kurusha kesi mubashara ukomeshwe kwa madai kuwa unawadhalilisha watuhumiwa wao .

Chanzo: YouTube Channel ya Shirika la habari la Burkina Faso ( RTB)
Hapa kwetu itakuwa mwiba kwa mtu
 
Cha muhimu kiongozi awe mzuri na mzalendo basi. Thomas Sankara alikuwa mjeda na alifanya mambo mazuri kwa muda mfupi ndio maana Ufaransa wakatumia mtu kumuua. Lakini pia kuna mifano mingine ya viongozi wanajeshi walionyonya nchi kama Mobutu na wengineo. Kwahiyo binafsi nawatakia heri. Kama anafanya kazi nzuri sio lazima atoke hata Angela Merkel aliongoza nchi kwa miaka karibu 20.
If you read between the lines unaona kuna credits za bure wanataka ku-achieve from wananchi. Kuna maeneo mengine mengi ya muhimu kuliko kuonesha kesi za ubadhirifu live!
 
Hakuna kitu hapo. Ukiona hivyo uchaguzi umekaribia; the ruling regime wants to be back in power. Changa la macho kwa wajinga hilo kiki mzuka.
Kama sijakosea utawala ni wa kijeshi
 
Kama sijakosea utawala ni wa kijeshi
Hilo linaeleweka. Wanajenga mazingira fulani kuwahadaa wananchi huku wakijiandaa kugombea kiraia. Hizo ni ghilba za kisiasa kujifanya kuonesha kesi za ubadhirifu live! Katika matatizo yote yanayoikumba nchi hilo la kuonesha kesi live ndio la maana kweli? Hadaa tu hizo.
 
Wizi hauwezi kuisha maadam mnaojifanya masikini na kupokea hela za misaada basi mtakuwa majizi tu maana hamuoni uchungu nazo

Huyu dogo anajitahidi kwa nchi yake na anaona hiyo ndio njia nzuri ya kuzuia wizi
Maana ukiiba unawekwa live
 
Hakuna kitu hapo. Ukiona hivyo uchaguzi umekaribia; the ruling regime wants to be back in power. Changa la macho kwa wajinga hilo kiki mzuka.
well hao jamaa wamepata kiongozi majuzi, so ichaguzi hauja karibia
 
Back
Top Bottom