beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
Tume ya uchaguzi nchini Burundi imemtangaza mgombea wa chama tawala Evariste Ndayishimiye kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika juma lililopita.
Jenerali mstaafu ameshinda kwa 68.72% ya kura zilizopigwa, wakati Agathon Rwasa, kutoka chama kikuu cha upinzani akipata 24.19% ,matokeo yaliyotangazwa na tume hiyo hii leo.
Kwa kuwa Ndayishimiye amepata zaidi ya 50% ya kura, ameepuka kufanyika kwa duru ya pili ya uchaguzi.
Haya ni matokeo ya awali ya uchaguzi , ambapo matokeo ya mwisho yatatangazwa na mahakama ya kikatiba tarehe 4 mwezi Juni.
Jenerali Ndayishimiye liteuliwa kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.
Bwana Ndayishimiye ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri katika siasa za Burundi walio karibu na Pierre Nkurunziza, ambaye uamuzi wake wa kuwania madaraka kwa muhula wa tatu kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 ulisababisha mzozo na mgomo wa upinzani.
Wagombea wengine waliochuana kwenye kinyang'anyiro hicho ni pamoja na;
Gaston Sindimwo (Uprona) - 1,64%
Domitien Ndayizeye (Kira Burundi) - 0,57%
Léonce Ngendakumana (FRODEBU) - 0,47%
Nahimana Dieudonné - 0,42%
Francis Rohero - 0,20%
Chanzo: BBC Swahili
=======
Burundi's election commission has declared the governing party's candidate, Evariste Ndayishimiye, as the winner of the country's presidential election last week.
The retired army general won 68.72 percent of the votes, while Agathon Rwasa, the main opposition leader, received 24.19 percent, the body said on Monday. Since Ndayishimiye has received over 50 percent of the vote, he has avoided a runoff.
Ndayishimiye was picked by the governing CNDD-FDD party to succeed outgoing President Pierre Nkurunziza, whose controversial decision to seek a third term in the last election in 2015 sparked mass unrest and an opposition boycott.
Rwasa has already alleged foul play, saying early numbers showing his National Congress for Liberty party heading for a bruising defeat are a "fantasy".
The May 20 vote, which was contested by seven presidential hopefuls, is meant to usher in the first democratic transfer of power in 58 years of independence.
There were few international election monitors on Wednesday after the government said they would have to spend 14 days in quarantine to prevent the spread of the coronavirus.
Rwasa has already hinted he would not take to the streets in protest and would appeal to the Constitutional Court, though he considers the process imperfect. The final election results will be declared by the Constitutional Court on June 4.
Ndayishimiye is expected to be sworn in for a seven-year term in late August, when Nkurunziza's term ends.
It is unclear whether Ndayishimiye would be able to rule free from interference by Nkurunziza, who in February was elevated by Parliament to the rank of "supreme guide for patriotism" and will remain chairman of the party's highly influential council of elders.
Al-Jazeera