Burundi: Tume ya Uchaguzi yamtangaza Evariste Ndayishimiye kama mshindi wa urais

Burundi: Tume ya Uchaguzi yamtangaza Evariste Ndayishimiye kama mshindi wa urais

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
1590420190335.png

Tume ya uchaguzi nchini Burundi imemtangaza mgombea wa chama tawala Evariste Ndayishimiye kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika juma lililopita.

Jenerali mstaafu ameshinda kwa 68.72% ya kura zilizopigwa, wakati Agathon Rwasa, kutoka chama kikuu cha upinzani akipata 24.19% ,matokeo yaliyotangazwa na tume hiyo hii leo.

Kwa kuwa Ndayishimiye amepata zaidi ya 50% ya kura, ameepuka kufanyika kwa duru ya pili ya uchaguzi.

Haya ni matokeo ya awali ya uchaguzi , ambapo matokeo ya mwisho yatatangazwa na mahakama ya kikatiba tarehe 4 mwezi Juni.

Jenerali Ndayishimiye liteuliwa kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.

Bwana Ndayishimiye ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri katika siasa za Burundi walio karibu na Pierre Nkurunziza, ambaye uamuzi wake wa kuwania madaraka kwa muhula wa tatu kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 ulisababisha mzozo na mgomo wa upinzani.

Wagombea wengine waliochuana kwenye kinyang'anyiro hicho ni pamoja na;

Gaston Sindimwo (Uprona) - 1,64%

Domitien Ndayizeye (Kira Burundi) - 0,57%

Léonce Ngendakumana (FRODEBU) - 0,47%

Nahimana Dieudonné - 0,42%

Francis Rohero - 0,20%

Chanzo: BBC Swahili

=======

Burundi's election commission has declared the governing party's candidate, Evariste Ndayishimiye, as the winner of the country's presidential election last week.

The retired army general won 68.72 percent of the votes, while Agathon Rwasa, the main opposition leader, received 24.19 percent, the body said on Monday. Since Ndayishimiye has received over 50 percent of the vote, he has avoided a runoff.

Ndayishimiye was picked by the governing CNDD-FDD party to succeed outgoing President Pierre Nkurunziza, whose controversial decision to seek a third term in the last election in 2015 sparked mass unrest and an opposition boycott.

Rwasa has already alleged foul play, saying early numbers showing his National Congress for Liberty party heading for a bruising defeat are a "fantasy".

The May 20 vote, which was contested by seven presidential hopefuls, is meant to usher in the first democratic transfer of power in 58 years of independence.

There were few international election monitors on Wednesday after the government said they would have to spend 14 days in quarantine to prevent the spread of the coronavirus.

Rwasa has already hinted he would not take to the streets in protest and would appeal to the Constitutional Court, though he considers the process imperfect. The final election results will be declared by the Constitutional Court on June 4.

Ndayishimiye is expected to be sworn in for a seven-year term in late August, when Nkurunziza's term ends.

It is unclear whether Ndayishimiye would be able to rule free from interference by Nkurunziza, who in February was elevated by Parliament to the rank of "supreme guide for patriotism" and will remain chairman of the party's highly influential council of elders.

Al-Jazeera
 
Kwahiyo Nkurunziza sio Rais tena popote pale humu duniani, ila si ndio nilisikia alibadili katiba kama sharti la kutogombea akajiweka kuwa supreme ambae kiuhalisia yuko juu ya Rais
 
Heko kwao, wengi walikuwa macho pima kusubiria majanga. Piere heko umejua kuzichanga.
 
Wakuu ,habarinii ..

Nmekutana na hii taarifa nikaona vyema nshare nanyi wakuu..

Mgombea urais wa chama tawala nchini Burundi Evariste Ndayishimiye ametangazwa mshindi leo kwenye kinyang’anyiro hicho ambacho kimedaiwa kukumbwa na visa vya udanganyifu.

Ndayishimiye ametangazwa kushinda baada ya kupata asilimia 68.72 ya kura zilizopigwa. Tume ya uchaguzi nchini Burundi ambayo imetangaza matokeo hayo moja kwa moja kupitia vyombo vya habari nchini humo, imesema Agathon Rwasa wa chama cha National Freedom Council (CNL) ambaye ndiye mshindani mkuu wa Ndayishimiye amepata asilimia 24.19 ya kura.

Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi, asilimia 87.7 ya wapiga kura waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo. Hapo awali, msemaji wa Rwasa alisema kilichotokea kwenye uchaguzi huo ni mpango uliosukwa vyema na chama tawala wa kung'ang'ania madaraka.


Africa ;

Sent using Tecno Y3+
 
Kwa Africa hii ni Mzee Kaunda tu ndiye Mwaninifu..aliona kura zake hazikutosha haya ma vyeo ya duniani ni ya kupita tu hayana maana yeyote ..badala ya kumwaga damu kama wapambe wake walivyotaka iwe akawakatalia kabisa akakaa pembeni akakabidhi nchi kwa mshindi....Viongozi wa Africa karibia wote walimshangaa sana...wakimwambia yaani una dola unashindwaje uchaguzi....

Hongera sana Kenneth Kaunda..
 
Wakuu ,habarinii ..

Nmekutana na hii taarifa nikaona vyema nshare nanyi wakuu..

Mgombea urais wa chama tawala nchini Burundi Evariste Ndayishimiye ametangazwa mshindi leo kwenye kinyang’anyiro hicho ambacho kimedaiwa kukumbwa na visa vya udanganyifu.

Ndayishimiye ametangazwa kushinda baada ya kupata asilimia 68.72 ya kura zilizopigwa. Tume ya uchaguzi nchini Burundi ambayo imetangaza matokeo hayo moja kwa moja kupitia vyombo vya habari nchini humo, imesema Agathon Rwasa wa chama cha National Freedom Council (CNL) ambaye ndiye mshindani mkuu wa Ndayishimiye amepata asilimia 24.19 ya kura.

Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi, asilimia 87.7 ya wapiga kura waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo. Hapo awali, msemaji wa Rwasa alisema kilichotokea kwenye uchaguzi huo ni mpango uliosukwa vyema na chama tawala wa kung'ang'ania madaraka.


Africa ;

Sent using Tecno Y3+


Waangalizi/Wasimamizi kutoka nje wanasemaje au hawakuwepo kabisa kwa sababu ya Corona?
 
Waangalizi/Wasimamizi kutoka nje wanasemaje au hawakuwepo kabisa kwa sababu ya Corona?
hawakuwepo mkuu ,na corona hii nani anawez kufatilia hilo..na inasemekan uchguz wenyew magumashi ,,, mpinzani awali alionekana akiongozaa lakini ..mwishoni imekuwa vice versa
 
Kila laheri Rais Mteule, ni vyema kipaumbele chako cha Kwanza kiwe kuimarisha uhusiano mzuri na nchi jirani hasa Rwanda.
 
Rwanda kwao!! True!!
Rwanda sio kwao.

ila akishaapishwa rasmi anaweza kujaribu kupunguza hali ya uhasama na uadui kati ya nchi yake na serikali ya Kagame kwa manufaa ya mataifa yote mawili.
 
Wapigakura Wana akili sana kamwe hawawezi kumpigia kura mtu mwenye mawazo ya msituni kuwa kiongozi
 
Rwanda sio kwao.

ila akishaapishwa rasmi anaweza kujaribu kupunguza hali ya uhasama na uadui kati ya nchi yake na serikali ya Kagame kwa manufaa ya mataifa yote mawili.
Kwenye East Africa Union Kenya na Rwanda wana work Plan...Uganda halijojo, Burundi, Sudan nao ni kama sisi tu hawajui wanahitaji nini ili wasonge mbele...no priorities...linalotokea asubuhi ndilo hilo hilo.
 
Kwenye East Africa Union Kenya na Rwanda wana work Plan...Uganda halijojo, Burundi, Sudan nao ni kama sisi tu hawajui wanahitaji nini ili wasonge mbele...no priorities...linalotokea asubuhi ndiyo hilo hilo.
Kenya na Rwanda hawapakani, hiyo work plan itakayowatenga Uganda na Tz unafikiri inaweza kufanikiwa?
 
Back
Top Bottom