Busara na Hekima ya Easther Bulaya kwa wanaohama Vyama

tripof

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2024
Posts
829
Reaction score
1,120

Easther Bulaya

Nimemsikiliza mara kadhaa Bulaya kuhusu hekima ya kuhama vyama wakati wa Lijualikali na pia kwa Msigwa, ana hoja na ukomavu wa siasa.

Ninamuunga mkono kuwa ukihama siyo lazima kukitukana au kukashifu chama chako cha siasa cha awali.

Huyu mama yuko vizuri kichwani ni hazina nzuri kwa Chadema kwa baadaye.
 
Huyu Dada ni CCM sio @chedema
 
Nimemsikiliza Upendo Peneza leo Segerea hawa watu hawana hoja kabisa eti anazungumzia Rushwa ya ngono nikashangaa ameijuaje kama hakushiriki kuinawirisha. wanajimaliza na kuonekana pumba kwenye majukwaa. wabadilishe mkakati
 
Hivi huyu dada kaolewa au ana mtu, mwambieni kuna mtu hapa ana uhitaji naye.
 
Nimemsikiliza Upendo Peneza leo Segerea hawa watu hawana hoja kabisa eti anazungumzia Rushwa ya ngono nikashangaa ameijuaje kama hakushiriki kuinawirisha. wanajimaliza na kuonekana pumba kwenye majukwaa. wabadilishe mkakati
Huyo Upendo wamemtafuna sana hapo Lumumba mpaka amekongoroka na kuzeeka amebakishiwa komwe tu.
 
Kweli kabisa. Na hata katika matatizo hayo ya sasa sijamsikia na wenzake wakiwatukana viongozi wa chama kilichowatema. Nakumbuka Halima aliwahi kusema kuwa walifanyiwa uhuni kitu ambacho sio tusi.

Amandla...
 
Lowasa hakuwatukana CCM hata Magufuli alithibitisha hilo. Kutukana siyo sera ya CCM,Wawaachie upinzani siasa chafu. Wao waendelee kuwa role model wa siasa safi zisizo za kuchafuana
 
Lowasa hakuwatukana CCM hata Magufuli alithibitisha hilo. Kutukana siyo sera ya CCM,Wawaachie upinzani siasa chafu. Wao waendelee kuwa role model wa siasa safi zisizo za kuchafuana

..mbona kila kukicha wana-ccm wanatukana wapinzani?

..kuna kipindi tulishuhudia hata wabunge wa Ccm wakitukana na kudhalilisha wapinzani ndani ya bunge.

..ni uongo wa wazi kudai kwamba Ccm hawatukani.
 
Naunga mkono hoja, hiki ni kichwa cha ukweli, na mimi ni miongoni mwa watu walio ki sport tangu kitambo Mbunge wa CCM, Esta Bulaya, Afanya Tukio la Kishujaa Mjini Dodoma!
P.
 
Ukihama chama huwezi kukisema vibaya, ila ukihamishwa chama, lazima waliokuhamisha wakutumie kuchafua chama chako ulichohama. Na hakuna jinsi lazima ufanye watakavyo ili wakuwezeshe njia yako ya kwenda chooni isiote majani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…