Business partner needed

mayome

Member
Joined
Jan 17, 2012
Posts
62
Reaction score
21
Habari zenu wanajamii wenzangu

Mimi ni kijana wakiume kwa sasa Shughuli yangu ni usindikaji vinywaji vyenye vileo ( pombe). Katika biashara yangu hii changamoto kubwa ambayo naipata ni ufinyu wa mtaji nilio nao na hivyo kunifanya nishindwe kujitanua na kufanya vizuri zaidi kwenye biashara. Kufuatia changamoto hiyo nimeamua kutafuta mtu/watu wenye pesa au uwezo wa kukopa ili tushirikiane.
Kwa yeyote alie tayari mambo ya muhimu hapa ni kama ifuatavyo:-

  1. Bidhaa inayotengenezwa ni kilevi ( POMBE) kwa hiyo usiwe na pingamizi kiimani. Vile vile bidhaa imekua sokoni kwa miezi mine tu hadi sasa.
  2. Biashara iko MBEYA MJINI TANZANIA ,Kama partner unaweza kushiriki katika uendeshaji wa biashara au usishiriki tegemeana na nafasi yako.
  3. Unahitaji kua na mtaji wa shilingi za Tanzania Million hamsini hadi milioni mia mbili (50,000,000/= to 200,000,000/=)
  4. Kwa yule ambaye hana pesa lakini ana Dhamana ya kuweza kupata mkopo anakaribishwa kwakua kuna mpango wa biashara/business plan ambayo tayari imeandaliwa.
Ambaye atavutiwa na post yangu na akitaka kujua zaidi anitumie private massage au anipigie kwa namba yangu +255712244831. Atakaye hitaji tuonane ili tuzungumze kwa ukaribu zaidi nitakua tayari, na nitakua Dar tangu leo hadi 29/08/2012 baada ya hapo nitarudi Mbeya.


NOTE: Tafadhalini wana jamii hili tangazo niliwahi kuliweka hapa lakini niliishia kusumbuliwa kwa coments zenye maswali mengi yaliyonitaka kujibu na wengine walituma private massages lakini hawakua sereous. Naombeni kama unaona post sio ya aina yako huna haja ya reply/comment, tambua kua hauwezi kua mjuaji wa kila kitu na pia upo kwenye uwanja wa GREAT THINKERS jaribu kua objective.
 
Unaeleweka vema kiasi, unaweza pia kuuza hisa za kampuni hiyo(equity finance), Ubia partinership au join venture, vile vile hapa Tz inasemekana zipo Capital Venture zaidi ya 20 Tafuta mojawapo, HAYA YOTE NI RAHISI SANA KAMA KWELI HIYO BIASHARA NI VIABLE (inalipa)
 
Good initiative, the good idea would be to engage many people because there are very few individuals who can afford to give 50.m
 
Good initiative, the good idea would be to engage many people because there are very few individuals who can afford to give 50.m

Una deal na pombe aina gani na je we umewekeza kiasi gani hadi kufikia hapo deal nimelipenda ila hiyo partner's capital range inalet down aisee
 
pombe halali kwa biashara tanzania inatokana na matunda mchanganyiko
 
Aina ya pombe ni pombe ya matunda mchanganyiko kuhusu kuingage watu wengi zaidi naona kama yaweza leta shida badae kwasababu wengine wanaweza kua sumbufu na hivyo kurudisha nyuma mradi huu.
 
Good initiative for self employment, unaweza kuregister kwenye SME'S FORUM kupitia Tanzania Chamber for Comerce Industry and Agriculture (TCCIA), utapata msaada wa kutosha na maelekezo ya jinsi ya kukuza mtaji wako.
 
Why don't you open the public company where many people can contribute capital? unaweza ukafungua kampuni kama NICOL watu wengi watachangia mtaji na watapata gawiwo (dividend) pindi kampuni itakapoanza kupata faida. Hii itasaidia kwa maana kwamba wanahisa hawatataka faida ya haraka. I know the corporate culture in Tanzania is still at its infancy but that is the simple and effective way of acquiring capital.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…