Butiku na wenzake ni 'wahaini'



Mkuu kuichambua si kosa ila kuweka matusi ni tatizo hapo.kwa uchambuzi wa Tadea na wengine binafsi nauukubali,kwani kufanya hivyo ni kuatarisha amani ya nchi.kwa viongozi wakuu wastaafu kuikosoa serikali kwa njia kama ile ni hatari sana.wao naamini wananjia nzuri tu ya kupeleka mawazo kwa serikali iliyopo madarakani.

wamekiuka miiko na viapo walivyokula wakati wanahika nyadhifa zao.

Bravo TADEA NA WENZIO
 
Dang,

I can't even tell who is CCM and who is opposition, especially after these CCM stalwarts attacking Kikwete and these fake opposition leaders singing Kikwete's song, reversal of roles.

That wouldn't be much if it didn't carry some undertones of totalitarianism of an Orwellian par. I mean even Kikwete himself has been benevolently (or is it cowardly?) observing freedom of speech.

Unless these are stage puppets running on a string from Kikwete it doesn't even make sense.These are the ghost kind of opposition "leaders" who can't even get 1% out of presidential elections and no parliament seat.Why should we listen to them?
 

Njaa zinawasumbua!
 
Hizi njaa zimewafanya baadhi yetu kuvamia siasa bila kuwa na utaratibu.Tunaishia kuwa vituko tu.JK hahitaji watu wa aina hii wamsafishe.Si aende CCM ambako wote hawa wanaosemwa yeye ndio mwenyekiti wa chama chao? Imagine, eti nao ni vyama vya upinzani!!
 
Nafikiri hawa viongozi wa vyama pinzani vya kufikirika wanashindwa kuelewa tofauti kati ya kukosoana kwa minajili ya kuleta maendeleo. Maana kama kuna udhaifu wa kiuongozi kama ilivyo sasa na watu waendelee na wimbo wa kumpamba na kumtukuza mkuu wa nchi itabidi ichunguzwe dhamiri inayowasukuma kufanya hayo. Hawa ni viongozi wa vyama ambavyo kimsingi vishajifia havipo lakini ingelikuwa vizuri na tungewaunga mkono kama wangezijadili hoja zilizotolewa na jukwaa la taasisi ya jkn kwa hoja. Pia kuna hao walioandalia maandamano ya j/mosi kujinadi kama viongozi wa dini. Hawa nao wanafahamika vizuri. Ni waalimu wa ile mihadhara ya usiku inayoanza saa 1 usiku hadi saa sita. Watakuwa hawana jipya ila kujadili watu. Sidhani kama hapa tutapata mjadala wa hoja kupanguliwa kwa hoja.
 
Makuwadi wa siasa kipindi cha mavuno kimeshafika,bado tutasikia wengi watakuja na staili tofauti tofauti.

waliowatuma wakati huu watakuwa wanajilaumu sana,unajua wamekuja na staili ya kitoto kiasi kwamba inakera na kutia kinyaa.
 
Hivi huyu ndiye amerithi chama kilichoanzishwa na Kambona?
Alianzisha yeye hicho chama pamoja na Kambona. Alifungwa miaka mingi na Nyerere kwa uhaini pamoja na akina Otini Kambona na Bibi Titi. Hawa ndio old time wapinzani ambao walipambana na Nyerere toka 60s. Kachoka mzee kwa sasa. Kachoka sana Chipaka. Tumpuuze tu katika haya aliyoyasema maana ni dhahiri ya kutumwa
 
VYAMA vya The Tanzania Democratic Alliance (Tadea) na United Peoples Democratic (UPDP)
Bila kutaja majina, walisema kutokana na viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuutangazia umma kuwa CCM imepoteza dira ni vema wakaondoka kwenye chama hicho na kujiunga kwenye vyama vingine au kuunda chama chao ambapo wasisitiza

Kwa hili, sioni kilichobaki kwa hawa viongozi kuvunja vyama vyao na kujiunga na ccm, kwani upande walikosimama sio sahihi. Kwani kina Bujiku hawawezi kutoka ccm na kuingia kwenye vyama vyao kwani wao tayari ni copy ya ccm!
 
Mkuu, viapo vyao vili-expire baada ya kuacha madaraka waliyokuwa nayo. Hivyo wana haki ya kutoa maoni yao kama mtu mwingine yeyote.

Kwa kweli sioni tatizo la mtu kusema mapungufu ya serikali na viongozi wake (kama yapo na anayaona). Haiwezekani kusubiri kusemewa wakati mambo yanaharibika. Vile vile, sidhani kama kilichosemwa na viongozi hao hakijawahi kusemwa na watu wengine katika mijadala ya kawaida. Ni mambo ambayo yamesemwa na wengi sana kabla ya kufika kwenye kongamano hilo. Tofauti iliyopo katika kauli hizo, ni nani aliyesema tu.

Nadhani ni vyema kusubiri kusikia hao wanaoandamana wanataka kutoa ujumbe gani.
 
Mpaka hapo tutakapoondoa woga na kuwa tayari kwa lolote, hakuna jema litakalotokea. Tusitarajie CCM na vibaraka wake wajiondoe na kukaa pembeni bila kulazimishwa kuondoka. Tusitarajie kuwa tutaitoa CCM kwa kutumia 'chaguzi' endapo mfumo uliopo unaipa fursa ya kushinda bila kushindana. Vyama vya upinzani vimejaa ubinafsi na havishughulikii mambo ya msingi zaidi ya kupigania ruzuku. Kuna haja ya kusema imetosha, liwalo na liwe...tuweke uzalendo mbele, masilahi binafsi nyuma...longolongo haitatufikisha popote...kuna haja ya kupambana na ndiyo njia pekee ya kubadili utawala uliopo. Vinginevyo tutulie tuli na waendelee kutunyoa kwa kutumia kipande cha chupa!
 
Du kazi kweli nchi hii ina mijitu ya hovyo hovyo kuliko wanaadamu wote kwenye sayari hii.
 

- Well, hoja zijibiwe kwa hoja sio viroja kama hawa wakuu, eti mnawaita ni opposition hawa? No wonder CCM itaendelea kushinda daima, I mean hawa kweli ni wenyeviti wa kuchaguliwa? Yaani na wao kama Kikwete, wameshindwa kujibu hoja za Butiku na Quaresi, badala yake wanajibu yale yale ya chuki na wivu kama Bibi Sophia!

- Unajua kwa mara ya kwanza nimeielewa case ya Chadema kukataa kujiunga na vyama vingine, hivi unawezaje kujiunga na vyama mufilisi namna hii? Hawa nao ni mafisadi hawa, hivi wamewahi kugombea nini katika taifa hili mbona hatujwahi kuwasikia? garademiti!

- Ujumbe wangu kwa Rais na washauri wako, acha kutumia hawa wachovu, nilijua huwezi kujibu kama ulivyoahidi sasa umeamua kutumia zile njia zako kama za kamati ya madini, it won't work, sasa do all of us wananchi a big favor, stand up as man kubali mapungufu yako kiuongozi, and then do something about it, au kama huwezi jiuzulu, waachie wengine, wapo wengi sana wanaoweza na usipoangalia very soon wananchi tutaamua bora shetani Lowassa! Kutumia wachovu katika jamii kujaribu kujisafisha kisiasa ina gharama zake kwa taifa, na moja ambayo ni mbaya kuliko zote ni kuigawa jamii katika makundi yanayopingana bila sababu, umeigawa CCM sasa unataka kuligawa taifa, please onea huruma watoto na wajukuu wetu, maana ukiendelea hivi hakitabaki kitu kwa taifa!

- Wakuu sio siri kwamba sasa huu ndio ule Mtandao, tayari umeanza kazi wanayoijua best ya kuchafua yoyote aliyeko kwenye njia yao, sasa ni vyema wananchi tukawa careful na kutokuangukia kwenye mitego yao, tujitahidi kuwa one step ahead huku tukiwaambia ukweli kwamba kama wameshindwa uongozi waondoke lakini hatuwezi kudanganywa kirahisi hivi, shame on you Kikwete na hizi very cheap politics!

Respect.


FMEs!
 

Na hii hapa je ?
Kwamba Kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation liligeuzwa jukwaa la wehu na wahaini - duh, kaazi kweli kweli !
 
Na hii hapa je ?
Kwamba Kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation liligeuzwa jukwaa la wehu na wahaini - duh, kaazi kweli kweli !

Hii ni satire.. sijui umeelewa hilo ? Ukisoma vyema utaona wamemtukana sana Makamba na mtandao wa Kikwete wanaodai eti ukosoaji ni uhaini! Na wajue 2010.. bado mapema... watasikia mengi... watanzania si mabwege tena.....
 
Hii ni satire.. sijui umeelewa hilo ? Ukisoma vyema utaona wamemtukana sana Makamba na mtandao wa Kikwete wanaodai eti ukosoaji ni uhaini! Na wajue 2010.. bado mapema... watasikia mengi... watanzania si mabwege tena.....

Nilielewa sana ila na mimi nilikuwa nazidi kupigilia msumari wa mwisho kwani Makamba ni karani mkuu na mpishi mkuu wa JK na CCM. Swali ni je, chakula anachowapikia Makamba wanakifurahia ? Vinjonjo wanavyoongezea akina Chipaka wa Tadea na Dovutwa wa UPDP wanavi enjoy ? Na vibwagizo vinavyotolewa na akina Chifu Msopa, Shehe Mwaipopo, Mch. Bulegi na kubarikiwa na Kamanda Kenyela wa jeshi la polisi vinamezeka ? Surely the country has gone to the dogs and they are fighting for the pieces of her poor torn body. Only a revolution can save us now - nothing less, nothing more.
 
Huyu mwandishi nae unaweza sema chizi mwingine tu. Anasema kikwete anataka ku promote demokrsia; alafu hapo hapo anasema wanaotoa maoni yao ni wahaini wanao staili kusfunguliwa mashtaka.

Where does freedom of speech falls into au demokrasia kwetu ina maana nyingine; maana ana sound as if hawa jamaa wame commit high treason ukati Kikwete and co ndio wanaweza hukumiwa kwa kesi hii.

Kama jamaa ni weak ni weak tu its obvious; wanasema litakua gwaride bovu iwapo kiongozi anakosea routine zake. Iwapo gwaride huushuudiwa na mamia anachosema mhudhuria mmoja ujue kimeshudiwa na wengi anawakilisha tu/

If he has to be taken serious he has to be serious mfano kwanini Tz maskini sijui; ukati leo hii tunasoma BoT inatoa mikopo kwa wakazi wake ili wajenge nyumba aihitaji muelevu kuelewa asilimia kubwa ya hawa watu wananyumba tayari. What does he do the next day anawaalika Mamiss sijui nini IKULU

Huu ujinga kiasi MKANDARA asuse
 
Inaonekana na ni wazi kwamba mtoa mada ya uhaini ni kati ya wale Asilimia 70 wanaofuata upepo maana ukisoma kwa makini hata uhaini waliofanya akina Butiku hauelezeki au hajaelezwa...

Ni kweli kwamba asilimia 30 ya misaada yote hutafunwa na wajanja mkulu amesema hayo na akiambiwa achukue maazmuzi magumu anasuasua... sasa uhaini uko wapi...

Ukweli siku zote unauma full stop
 

Heshima kwako FMEsm

Nimependa andiko lako kwa kweli Muungwana kashikwa pabaya mbaya zaidi bado anafikiria Watanzanda ni mabwege.Kwa mara ya kwanza nadhani Muungwana anamuhitaji Ngoyai amsaidie kuweka mambo sawa,Ngoyai angekuwepo asingekubali hizi cheap propaganda kuwatumia kina Chipaka na maandamano ya waislam jumamosi ni makosa ya kuwa na timu ya watu wa hovyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…