Butiku na wenzake ni 'wahaini'


Watanzania wengi hawana uti wa mgongo (not assertive) na ndiyo maana mtu akikosoa kidogo kunakuwa na 'reaction' kubwa. Mimi naamini wanaokosoa wana hoja na wanaomtetea Jakaya Kikwete/Serikali wanadhani kukosoa ni kumumaliza/kuimaliza Serikali. Hii inapelekea watu wengi kuwa wanafiki, wakidhani 'flattery' ndiyo njia ya ku'survive'.

Mawazo yangu ni haya: kama kundi moja la watu linakosoa basi kundi jingine lisije na kuwapinga waliokosoa. Kama wanataka waanze kuelezea mema ambayo kundi la kwanza halikuona. Lakini kurudiarudia tu maneno na kuanza kuaanika maovu ya wakosoaji kunaonyesha tu jinsi tunavyo'abuse' uwezo wetu wa kufikiri. Tuwaache watu waseme kero zao - wenye kusifia acha wasifie na wenye kukosoa acha wakosoe! Hii ndiyo njia sahihi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…