Bwana harusi aliyedaiwa kutekwa apatikana Kigamboni, alijificha kwa Mganga wa Kienyeji

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Taarifa ya Jeshi la Polisi

Your browser is not able to display this video.

==

Ndugu wa Vincent Masawe, bwana harusi anayedaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha wamethibitisha kupatikana kwa ndugu yao.

Kwa mujibu wa ndugu hao, Vincent yupo katika kituo cha polisi kilichopo Kigamboni, mkoani Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Vick Massawe amethibitisha kupatikana kwa ndugu yao jana asubuhi Desemba 16, 2024.

Pia, Soma: RC Chalamila: Hajatekwa, amejipoteza mwenyewe

Taarifa za kupotea kwa Vincent zilifikishwa Kituo cha Polisi Kigamboni Novemba 19, 2024 na mke wake. Jeshi la Polisi katika taarifa lilisema upelelezi ulianza mara moja.
 
Huyo bi arusi naye atakuwa wa kifala kama ataolewa na huyu jamama. Kama bwana harusi ameshawasha taa nyekundu mwanzo kabla ya kuingia ndoani, si itakuwa balaa hapo mbeleni kwenye maisha ya ndoa?
 

Mangi ameanza kwa kufeli...uuze mali ya mtu halafu ukimbilie kwa mganga. That is how low our thinking has become these days.

Tunaamini katika ushirikina na shortcut. Mtu hafanyi kazi ila anaenda kumuhonga Nabii au Mtume ampe hela na mali. Mtu anaibia watu, halafu anajidanganya kuna mganga atamfanyia zindiko kesi ipotelee hewani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…