CAF: Yanga, Simba zipo uwanjani leo Septemba 10, 2022

CAF: Yanga, Simba zipo uwanjani leo Septemba 10, 2022

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Raundi ya Kwanza ya Michuano ya Afrika ngazi ya klabu inatarajiwa kuanza wikiendi hii ambapo timu za Tanzania pia zitakuwa uwanjani ndani na nje ya Nchi.

Leo Septemba 10, 2022, Yanga itavaana na Zalan ya Sudani Kusini kwenye Uwanja wa Mkapa, Simba ipo Malawi kucheza dhidi ya Nyasa Big Bullets.

KMKM ya Zanzibar itaikaribisha Al Ahli Tripoli ya Libya kwenye Uwanja wa Amaan, mechi zote zikiwa ni za Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, kesho Septemba 11, 2022, Kipanga ya Zanzibar itakuwa Sudan Kusini kucheza dhidi ya Al Hilal Wau South, Geita Gold ikiwa ugenini kukipiga dhidi ya Hilal Alsahil ya Sudan.
 
Raundi ya Kwanza ya Michuano ya Afrika ngazi ya klabu inatarajiwa kuanza wikiendi hii ambapo timu za Tanzania pia zitakuwa uwanjani ndani na nje ya Nchi.

Leo Septemba 10, 2022, Yanga itavaana na Zalan ya Sudani Kusini kwenye Uwanja wa Mkapa, Simba ipo Malawi kucheza dhidi ya Nyasa Big Bullets.

KMKM ya Zanzibar itaikaribisha Al Ahli Tripoli ya Libya kwenye Uwanja wa Amaan, mechi zote zikiwa ni za Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, kesho Septemba 11, 2022, Kipanga ya Zanzibar itakuwa Sudan Kusini kucheza dhidi ya Al Hilal Wau South, Geita Gold ikiwa ugenini kukipiga dhidi ya Hilal Alsahil ya Sudan.
Kazi ianze tumjue aliyejiandaa vizuri.
 
Naihurumia timu yangu ya Simba leo ni vigumu kuepuka kipigo
 
Kila la kheri wananchi, Yanga Africa na makolo, Simba Sports C. Mkashinde inshallah.
 
Unapozitaja hizi timu kwa pamoja..itifaki yake unaanza kuitaja Simba ndiyo inafuata hiyo timu nyingine..sawa.
 
Mimi Yanga ila natabiri simba atashinda Yanga pia atashinda kmkm itapoteza
 
Sisi Yanga leo lazima tupasuke kama kawa ma janjaweed yatatuua
 
Back
Top Bottom