Watanzania ni wasahaulifu.. Yaani mmesahau kuwa Simba ilishawahi kufika fainali ya kombe la CAF? Siku ya fainali ndio Simba ikatolewa tena inasemekana ilikua ni hujuma ya mfadhili wa Simba kuahidi zawadi ya Kia moja moja? Baada ya kuona Simba wanakaribia kuchukua kombe kibao kikageuka akaona ubahili kutimiza ahadi yake, lakini Yanga haijawahi fika mbali kwenye kombe la Caf ndio maana record yake iko chini sana yaani haitambuliki, labda viligi vya hapa nyumbani ndio inajikongoja kiaina.
