Katiba ya Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 ibara ya 143(1) kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu atakuwa na jukumu juu ya mambo yafuatayo;
(a) kuhakikisha kwamba fedha zozote zinazokusudiwa kutolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina na serikali matumizi yake yameidhinishwa ba kwamba zitatolewa kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 136 ya Katiba hii, na iwapo atatosheka kwamba masharti hayo yatatekelezwa ipasavyo,basi ataidhinisha fedha hizo zitolewe.
(b) kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo matumizi yake yameidhinishwa yatokane na fedha zilizomo katika mfuko Mkuu wa hazina ya serikali au fedha ambazo matumizi yake yameidhinshwa na sheria iliyotunhwa na Bunge, na ambazo zimetumika ,zimetumiwa kwa ajili ya shughuli zilizohusika na matumizi ya fedha hizo na kwamba matumizi hayo yamefanywa kwa kufuata idhini iliyotolewa kuhusu matumizi hayo;na
(c)angalau mara moja kila mwaka kufanya ukaguzi na kutoa taarifa juu ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya Jamhuri ya Muungano,hesabu zinazosimamiwa na watumishi wote wa serikali ya Jamhuri ya Muungano nahesabu za mahakama zote za Jamhuri ya Muungano na zinazosimamiwa ba Katibu wa Bunge.
Sasa kwa majukumu haya ya Kikatiba aliyonayo CAG, nani wa kumtishia maisha zaidi ya wanaokaguliwa naye?
Kwa kitendo hiki tu, sio ilitosha kusikia kuna mtu/watu wamekamatwa kwa kutenda kosa la namna hii?
Gazeti kubwa kama hili linaloongozwa na Mzee mbobevu na Wakili wa Mahakama KUU kamwe haliwezi kutunga hekaya, lazima kuna jambo;
Ni imani yangu vyombo husika vitalifanyia Kazi jambo hili;
CAG ndio jiicho la walipa kodi na katika mazingira ya kawaida, huwezi kukusanya kodi za watu wako halafu ukakubali zichezewe ; hata Donors hupata confidence ya mikopo/misaada yao kwa kazi nzuri ya CAG na Tanzania ilikuwa ni miongoni mwa Nchi zenye mifumo/systems imara in Africa.
Pamoja na salamu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ........................................Kazi indelee