CAG: Mradi wa Umeme wa Julius Nyerere umekamilika kwa 48% badala ya 94% iliyopaswa. Mafuriko na Uviko vyatajwa kama sababu

CAG: Mradi wa Umeme wa Julius Nyerere umekamilika kwa 48% badala ya 94% iliyopaswa. Mafuriko na Uviko vyatajwa kama sababu

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Kwa tuliokuwa tunaulizia mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere ulipofikia, leo CAG ametoa majibu, hauna dalili ya kuisha, ndio kwanza umefikia asilimia 48, kwa hesabu za asilimia maana yake hata nusu haujafika.

Ujenzi wa mradi wa ufuaji umeme wa Mwalimu Nyerere ulianza mwaka 2019 na ulitarajiwa uwe umeanza kuzalisha megawati 2115 mwishoni mwa mwaka huu na kuendeshwa na TANESCO.

========

CAG: Kuchelewa kwa ujenzi wa mradi wa bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere kwa asilimia 46.45. Hadi kufikia tarehe 31 Oktoba 2021 mradi ulipangwa kukamilika kwa asilimia 94.47, hata hivyo nilibaini mradi ulikamilika kwa asilimia 48.02 ukiwa umechelewa kwa asimilia 46.45.

=>Ucheleweshaji umesababishwa na kuchelewa kuwasilishwa kwa usanifu wa mwisho wa mradi, janga la mafuriko kwenye mto Rufiji pamoja na janga la Uviko.

=>Pia kukatika katika kwa umeme kwenye eneo la mradi kunasababisha kuongezeka kwa gharama na muda wa kukamilisha mradi.

Pia, soma=> Rais Samia apokea ripoti ya CAG, deni bado ni himilivu. Mafao yazidi mapato ya mifuko ya hifadhi
 
Kulikuwa na uongo mwingi sana kwenye mchakato mzima wa hili bwawa
 
Nipo rufiji sasaivi kama site engineer, mradi upo zaidi ya 60%....View attachment 2250341View attachment 2250342View attachment 2250343

Sent from my SM-J415F using JamiiForums mobile app
Asante kwa kutupa habari za sasa "current status" ya mradi. Hivi upo utaratibu gani wa kupima hicho kiwango kilichofikiwa? Kuna Consultant anayetoa Certificate za kuelezea mahali mradi umefika? Umepima je hiyo percentage au kiasi kilichofikiwa? Na kwa mwendo huo mradi unakadiriwa kukamilika lini?
 
Huu mradi hautakaa ukamilike. Yale mabilioni tumezika bure tu pale
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Back
Top Bottom