CAG mstaafu Uttoh: Hakuna Shirika lolote la ndege duniani lililopata faida baada tu ya kuanzishwa, ATCL haijawahi kulipa Gawio Serikalini

CAG mstaafu Uttoh: Hakuna Shirika lolote la ndege duniani lililopata faida baada tu ya kuanzishwa, ATCL haijawahi kulipa Gawio Serikalini

Thanks!
Nice, logical and factual argument. Akili kubwa!
Tatizo watanzania wengi, hata waliosoma ni mateka wa propaganda.

Maisha kipindi cha JPM yalikuwa na unafuu mkubwa sana kwa watanzania walio wengi.
Miaka ya nyuma walio faidi keki ya taifa walikuwa wachache sana. Mijini watu walikuwa wanajirusha, wanashinda night clubs na kupangia nyumba mademu hata 4 kwa mpigo, wakati ukienda kijijini hupati change ya sh 10,000.00.

Watanzania wa vijijini walikuwa wanakumbwa na njaa na hwana fedha ndogo ya matibabu. Ndiyo mana kipindi cha mavuno sababu ya madeni na mahitaji ya muhimu hasa matibabu walikuwa wanauza mazao yote kwa bei ndogo na kisha hao hao wakulima wenye kipato kidogo wanakuja kulazimika kununua mazao kwa ajili ya chakula kwa bei kubwa sana. Aliyekuwa anafaidi, mfanyabiashara!
Na kwakua hao wachache ambao wanadhani ni first class citizen ndiyo ambao wana tablets na internet connections basi wanaaminisha watu kuwa ni watanzania kumbe majoritarian hawana hata basics...Hataree sana hivi virus kuliko corona!
Hayati JPM alijali welfare ya kila kundi na siyo ambap wanajua kupiga makelele ndiyo maana katika msiba wake wale disadvantaged ndiyo waliotandika nguo zao barabarani....
 
Maelezo ya kifundi...
Ila maelezo ya ujumla uko sawa..
Ndugu maana ya faida ni (Mapato - Matumizi) hapo kwenye matumizi no pamoja na running costs kwahiyo huwezi kusema unapata faida lakini inamezwa na running costs that's called loss mzee
 
CPA Uttoh amesema kimsingi mashirika ya umma hayapaswi kulipa dividend kwa sababu hayafanyi biashara na ametoa mfano UDSM wanalipa dividend serikalini kwa biashara gani wanayofanya?

Source: ITV kipindi cha Kipima Joto
Mlimani City Shopping Malls zimejegwa ndani ya eneo la UDSM
 
KAKURUPUKA huyo Mkuu. Hakuwahi kuendesha shirika la ndege popote pale duniani hiyo conclusion yake ni UCHWARA halafu kaminya kuhusu faida itapatikana baada ya muda gani.
Wewe ulishawahi kuendesha shirika la ndege wapi?
 
CAG mstaafu mh Uttoh amesema hakuna shirika la ndege lolote duniani lililowahi kupata faida katika miaka ya mwanzo ya operations zake.

Kuhusu gawio mh Uttoh amesema dividend hutolewa baada ya biashara kupata faida na huamuliwa na bodi kiasi gani cha faida kigawiwe kama dividends.

Uttoh amesema kwa uelewa wake ATCL haijawahi kulipa dividend kwa serikali, na kama kuna fedha ziligawiwa kwa serikali na ATCL hicho ni kitu kingine siyo dividend

CPA Uttoh amesema kimsingi mashirika ya umma hayapaswi kulipa dividend kwa sababu hayafanyi biashara na ametoa mfano UDSM wanalipa dividend serikalini kwa biashara gani wanayofanya?

Source: ITV kipindi cha Kipima Joto
Alishakagua mashirika mangapi ya ndege nje ya nchi ili kuthibitisha anachozungumzia?
 
Mzee Uttoh yuko sahihi kabisa, mashirika yote ya ndege huwa hayaleti faida ya moja kwa moja kwa taifa. Biashara ya usafirishaji wa ndege kama yenyewe huwa haiingizi faida, ila faida zake huja kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi ambazo safari hizo za ndege hufanikisha ndani ya nchi husika.

Mfano mzuri shirika kubwa kama la Fly-Emirates au Air-China hayapati faida za moja kwa moja, lakini shughuli za kiuchumi ambazo haya mashirika yamezifanyikisha ndizo huingiza faida. Fly-Emirates linafanikisha shughuli za kiutalii na biashara ya kimataifa ndani ya ile falme ya Kiarabu.

Faida ambazo zinapatikana kutoka kwenye utalii na biashara ya kimataifa ndiyo hutumika kufidia (Compensate) gharama ya uendeshaji wa shirika la Fly-Emirates. Biashara ya ndege ina gharama kubwa sana kuendesha, na mashirika yanayoingiza faida kama Ethiopian Airlines hayaingizi kutokana na safari za anga pekee, bali kazi nyingine (Kufundisha marubani na wahudumu, pamoja na kufanya marekebisho ya ndege) ambazo shirika hufanya.

Ambacho sisi hatukukubaliana na Raisi Magufuli ni ile tabia ya kusema unanunua ndege kwa pesa taslimu kuinua UTALII nchini, ilhali umeweka sera mbovu ambazo zinawakimbiza watalii: Hata mpango-mkakati wa biashara (Business Plan) hajatupa wananchi. Kila jambo linafanyikia gizani tu....

Lingine ni hili la kununua ndege kwa pesa taslimu bila kuweka wazi mikataba yake linatia ukakasi sana. Halafu shirika bado liko kwenye majaribio ya kufufuliwa na halijasimama vizuri: Tungejaribu kwanza kuchukua ndege chache chini ya Lease (Dry or Wet Leases ) huku tukipima upepo unaendaje.....
Miaka hamsini bado tuwe tunajaribu tu si ndio...? Hivi ni lini watanzania tutakuwa na uthubutu wa kufany mambo? Hivi ulisikia hata mwenyekiti wako alimsifia magufuli kuwa ni mtu mwenye uthubutu... woga wa nini kila siku... na ndo maana daima hatufanikiw kwa sababu ya kukosa uthubutu.

Kila kitu tunajaribu, kisa kuogopa hasara. Na ndio maana hata hatufanikiw maisha yanazidi kuwa duni tu. Inabdi ifike mahala tujue namna ya kulazimisha kuyatafuta mafanikio... fanya kazi... kazi kazi kazi kazi na kuacha kupiga domo...

Pia, tuache maisha ya kupiga dili.. ndo maana tukipewa kaz tuisimamie tunawaza kuiba na uvivu... hujui tu ulivyonikera... fanyeni kazi...

VIJANA TUACHE NA MAWAZO MUFILISI... I WISH MZEE ANGEKUWA HAI HATA SASA.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Tukisema jiwe Alikua msanii Watu wanabisha. Tulikokua tunaenda hata hospitali na shule za msingi na sekondari zingetakiwa kutoa gawio. Ovyo sana
 
ATCL pengine ilitoa contributions and not dividend to the Govt. Fatilieni msichanganye mambo.
Uko sahihi. Kilicholipwa na ATCL hakikupaswa kuitwa Dividend..........
(Dividends are paid to the shareholders of a company out of profits or reserves. So, a lossmaking company with no reserves cannot pay a dividend. That means, unlike a salary, contractors and other business owners can only pay a dividend when their company is profitable.)
 
Watu hawaelewi Mkuu KUKURUPUKA kwa huyo mwendazake kulivyoathiri uchumi wa nchi katika miaka mitano. Mwenyezi Mungu katunusuru sana 🙏🏾Watanzania. Imagine miaka mitano hali iko kama hivi je angekaa miaka 10 au milele kama maccm walivyotaka akae madarakani mpaka achoke mwenyewe au afariki si uchumi badala tu ya kuuangusha angeua kabisa uchumi.
BAK yupo sahihi kabisa na ukosoaj8 wako haupo technical. Ambacho unapaswa ufahamu hao 11% ndio wanaweza expand au contract uchumi.

Ndege za trillion 3 plus pesa inaenda Canda huko lakini Trillion 3 ikitumika ndani whether kulipa wazabuni au kuajiri/kupandisha mishahara ina maana pesa itazunguka kwenye uchumi na kuchochea biashara kupitia spillover effects.

Na ndio maana duniani mabillionea na washika mitaji wakubwa hawafiki 5% lakini dunia nzima tunawategemea kwa kila kitu kuanzia ajira mpaka supply ya bidhaa muhimu so uchumi hauangalii namba ya direct wanufaika bali inaangalia wale wanufaika watatawanyaje pesa baada ya kuzipata.

Ndio maana mwaka juzi Prof.Luoga alishusha reserve ratio requirement ya benki za biashara pale BOT ili kwamba benki za ndani ziwe na ukwasi ziweze kuajiri,kukopa,kuwekeza n.k ili pesa zitoke kwenye mashelf ya BOT ziende kwa raia kuchochea biashara mpaka ya boda boda na mama ntilie!! Uchumi unafanya kazi hivyo
 
Janga lingine la KUKURUPUKA kwa mwendazake kuhusu manunuzi ya korosho na dhuluma kubwa aliyowafanyia Wakulima wa Korosho hii hapa. Halafu kuna wapuuzi wanataka eti kumuenzi huyu. Kuna cha kuenzi kwenye mediocre performance, dhuluma na udhalimu!?
BAK yupo sahihi kabisa na ukosoaj8 wako haupo technical. Ambacho unapaswa ufahamu hao 11% ndio wanaweza expand au contract uchumi.


Ndege za trillion 3 plus pesa inaenda Canda huko lakini Trillion 3 ikitumika ndani whether kulipa wazabuni au kuajiri/kupandisha mishahara ina maana pesa itazunguka kwenye uchumi na kuchochea biashara kupitia spillover effects.

Na ndio maana duniani mabillionea na washika mitaji wakubwa hawafiki 5% lakini dunia nzima tunawategemea kwa kila kitu kuanzia ajira mpaka supply ya bidhaa muhimu so uchumi hauangalii namba ya direct wanufaika bali inaangalia wale wanufaika watatawanyaje pesa baada ya kuzipata.

Ndio maana mwaka juzi Prof.Luoga alishusha reserve ratio requirement ya benki za biashara pale BOT ili kwamba benki za ndani ziwe na ukwasi ziweze kuajiri,kukopa,kuwekeza n.k ili pesa zitoke kwenye mashelf ya BOT ziende kwa raia kuchochea biashara mpaka ya boda boda na mama ntilie!! Uchumi unafanya kazi hivyo
 
ATCL pengine ilitoa contributions and not dividend to the Govt. Fatilieni msichanganye mambo.
Ila siku wanatoa liliitwa gawio huku TV zikiwa mubashara na wananchi kupongeza kwani ilionekana miaka ya nyuma yalikuwa yanaingia mitini ila wataalamu wa mambo walihoji inakuwaje mashirika ya Umma yanatoa gawio huku vitabu vya mahesabu vinaonyesha hasara
 
Tatizo la ATCL ni jinsi fedha za wananchi zilivyotumika bila weledi katika uwekezaji wa jinsi ndege zilivyonunuliwa na sequencing ya ununuzi wa ndege hizo!!! Kulikuwa na uharaka gani wa kununua dreamliner wakati safari za local na regional zilikuwa bado kutoshelezwa? Matokeo yake ndege kuota jua kiwanjani na kutengeneza hasara!!!
Na kupelekwa Mwanza kila siku badala ya kuruka majuu huku nyingine (Air Bus) badala kuwa busy na kusafirisha abiria, inapata nafasi mpaka ya kusafirisha msafara wa Rais (kwa kigezo hiki tu inaonyesha ndege ni nyingi kuliko abiria)
 
Back
Top Bottom