CAG, Prof. Mussa Assad, Atoa Dawa ya Kutibu Ugonjwa Hatari wa Deni la Taifa, ni Nidhamu ya Matumizi kwa Kubudget Kutumia Kile tuu Tutachokipata

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Moja ya ugonjwa mkubwa na mbaya kuliko magonjwa yote yanayolikabili taifa letu, ni ugonjwa wa kukua kwa deni la taifa, ambalo linakuwa kwa kasi kubwa kuliko uchumi wetu. Ukuaji wa uchumi wetu wa taifa ni wastani wa asilimia 7% kwa mwaka, wakati ukuaji wa deni la taifa ni asilimia 20% kwa mwaka!. Rate hii ikiendelea, tutafikia kiwango ambacho deni litakuwa halihimiliki kwa kufikia kiwango cha mwisho cha uwezo wa kukopesheka, hivyo taifa letu kuwa halikopesheki.

Sababu kubwa ya kukua kwa deni la taifa ni kutokana na nchi yetu kupanga bajeti tegemezi ambayo ni bajeti kubwa kuliko makusanyo yetu, hivyo bajeti yetu ziku zote inategemea mikopo na misaada ya nchi wafadhili, inapotokea nchi wafadhili wamepunguza misaada, nchi yetu hujikuta inalazimika kukopa ili kutekeleza bajeti, both recurrent, na development.

CAG Prof. Mussa Assad ambaye kitaaluma ni mchumi, hapa anatoa dawa ya kutibu ugonjwa huo wa kutegemea budget tegemezi.
Msikilize.
Paskali.
 
Asante ndugu Paskali binafsi nafurahishwa na,mabandiko yako humu jukwaani nikiona post yako naacha kila kitu nasoma kwanza ulichoandika ninini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namtafakari mtu aliyetuletea heshima kubwa kama hii, kutaka kuletewa figisu kwa kuusema ukweli wa udhaifu wa Bunge!.

Hivi kitu ambacho ni ukweli kabisa kina udhaifu na kila mtu anaona udhaifu huo, akitokea mtu bold na kuusema ukweli ni kukidhalilisha?.

Ili hili likifanikiwa la CAG kumgolewa, then nitaamini ile spika ya kule Dodoma, ni wireless speaker tuu na kazi ya spika kutoa sauti tuu, lakini mwenye sauti haswa ni aliyeshika ile wireless microphone.

P.
 
Wanaounga msimamo wa CAG wanaitwa kamati ya maadili.

Umejiandaa??

"Heri mbwa hai kuliko Simba mfu"
 
Nitamani huyo alieshika wireless microphone afanye kama yale yaliyofanywa kule kucheleee!
 
Wakuu Bajeti ya serikali imesomwa jana, kuna kitu muhimu kwenye bandiko hili, CAG, alishauri kuhusu bajeti.

Katika bajeti ya mwaka 2018-2019 serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi Trilioni 32.48 kutoka katika vyanzo vyote vya ndani na nje, mchanganuo wa mapato yaliyopatikana hadi April, 2019 ni Trilioni 12.9 sawa na 87.4%
Mkuu Beth, asante kwa bajeti ya serikali, enzi za JK, budget day huwa ni siku muhimu sana, siku hiyo rais hapangiwa shughuli zozote hata kama kuna ugeni, haupangiwa kuja on budget day.

Hizi hesabu zimekaaje? au mimi ndio nazeeka nashindwa kufanya calculus?. Umepanga kukusanya tirilioni 32.48, ukafanikiwa kukusanya tirilioni 12.9 tuu, hata nusu haijafika, halafu unatuambia hii ni.87.4%?!

Tuelewesheni maana sisi wengine hesabu ni mbingu na nchi, tumekuwa tukipanga budget kubwa kuliko uwezo wetu wa makusanyo na badala yake tunashindwa kuitekeleza, na matokeo yake ni kulazimika kukopa.
Kwa nini tupange kutumia kitu ambacho hatuna?.

P
 
Kuhusu deni la taifa, ushauri huu ufuatwe.
P
 
Tanzania tuna viongozi wachache sana wanaojielewa, wengi waliokua wanajielewa zamani wanapoteza muelekeo kwa kulinda UGALI.

Ila huyu PROF. ASSAD ana vinasaba vyote vya kua RAIS WA KIHISTORIA AFRICA, kama atapewa nafasi ya kuwania kiti cha urais, basi atakua rais ambae anaweza kulitoa taifa letu gizani na kulipeleka kwenye mwangaza (he is one of the smartest minds in Tanzania).

MTAZAMO WANGU WA #2020 UCHAGUZI. . . . . Mh Magufuli kuonesha na kuthibitisha "UZALENDO NA MAPENZI" yake kwa taifa letu, avunje ile mila ya CCM kuwania urais kwa mihula miwili, na amuachie huyu mtu kijiti cha kuwania Urais. Atatufikisha mbali sana Prof Assad akiwa Rais wa Tanzania. Hata sisi tusioikubali CCM tutaipenda bila shuruti.
 
Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
 
Ondoa kichere weka kuchele, mambo ni kuslide tu sasa,

1.5 hatutaisikia tena
 
Mkuu Capt Tamar ,
Asante,
Ubarikiwe
Japo sina uhakika, kwavile siwezi kusoma mabandiko ya watu wote humu, lakini humu JF, mimi ni miongoni mwa tuliomuongelea sana CAG, Ofisi ya CAG na Ripoti za CAG!.
Nakutakia Jumapili Njema
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…