Cameroon imemjibu Edo Kumwembe kwa kufuzu fainali

Bado Arsenal kumjibu Edo Kumwembe kwa kuchukua EPL msimu huu😉
 
muhimu sana kuweka akiba ya maneno
 
Mchambuzi si lazima mtazamo wake utimie. Maajabu hutokea. Hivyo mjifunze kazi za mchambuzi wa soka
 
Edo ni mchambuz wa kiwango cha juu.

Anakosea TB Joshua itakuwa Edo Kumwembe.

All of us makes mistakes in some situations.
 
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Edo ni mchambuzi mzuri wa mpira lakini wakati mwingine anajisahau sana kwa kuingiza hisia zake binafsi kwenye baadhi ya timu tofauti na wachambuzi wengine kama Mwalimu Kashasha, kwa mfano nakumbuka aliponda sana usajili wa Fernando Torres kwenda Liverpool kutoka Atletico Madrid lakini Torres msimu huo aliibuka kuwa striker tegemeo wa Liverpool mpaka kuwa mfungaji bora wa EPL.
Pia amekuwa akiisifu sana Barcelona inapofanya vizuri lakini ikipoteza mchezo anaponda.
 
Hii inaonesha ni jinsi gani mpira ulivyporomoka Afrika.. umekosa kabisa mvuto
 
Mchambuzi hutoa maoni yake kutokana na jinsi aonavyo. Hata ukicheki wachambuzi wa sky sport nao hutoa predictions zao nao pia huingia chaka vile vile.
Kama neno lenyewe Uchambuzi lilivyo ni maelezo au kuingia kwa kina ndani ya jambo fulani ambalo either limetokea au linaenda kutokea. Na katika mabo kama hayo kuna kupata na kukosea.
So msimuandame sana, sio mpiga ramli. Cheki hao waliocheza mpira kina Kuffor, Carregher, Neville na wengine wanavyopwaya sometimes.

Tena kwa case kama ya cameroon yani kwa mtu makini asingepishana na Kumwembe, ukiangalia hali halisi Cameroon kwenye mashindano haya hana kile kikosi ambacho kimezoeleka miaka mingi chenye majina ya wanaotamba kwenye ligi kadhaa kubwa duniani, ila wana timu nzuri inayoshirikiana kitu kinachowapa matokeo. sina hakika kwamba kuna kundi kubwa la wadau walioipa cameroon nafasi kubwa at expense of Ghana, Ivory coast na Algeria.
 
hata fugerson alisema chelsea haitaingia top 4 lakini cha kushangaza itachukua ubingwa, kumbe hata ulaya wapo wachambuzi uchwara
 
hata fugerson alisema chelsea haitaingia top 4 lakini cha kushangaza itachukua ubingwa, kumbe hata ulaya wapo wachambuzi uchwara
Kuna tofauti kati ya kutabili na kuponda..,yeye alikuwa anaiponda cameron
 
anaiponda kivipi mkuu ? maana hata fergurson aliiponda chese kwa namna moja au nyingine
anasema Cameron ni timu mbovu sana na ya kawaida sana eti haina wachezaji wanaocheza timu za maana ulaya.
Kwamba Cameron imekuwa simba wa shaba.
Bora na Ferguson alisema Chelsea ni timu nzuri lakini hawapi nafas ya ubingwa
 
Huyu jamaa namkubali ila sometimes anakosa cha kuandika,kuna siku aliandika eti kiungo wa Kati atakaefunga magoli matano atampa laki tano ,mbona kamusoko alifikisha halafu hajampa hata mia.hahah ningemuona ningemuambia
 
Anachambua utafikiri yy ndio anacheza aliwaponda sana kumbe watu wana mioango yao.
Cameroon ni wazuri na wamekuwa wakiimarika kila mechi na pia kumsoma adui kwa haraka sana.
Viva Indomitable Lions...!
 
binafsi nawapongeza cameroon kwa hatua walioifikia,kwani ni timu inayoundwa na vijana wengi wasio na majina makubwa,ila ni nafasi kwetu watanzania kujifunza,kuhusu @EddoKumwembe ule ni mtazamo wake na maoni yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…