Can we BRING MAMA LWAKATARE back to THE FORUM?

uttoh2002

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2012
Posts
17,060
Reaction score
32,400
Waungwana na wakubwa zangu kwa heshima kubwa ninaomba nimrudishe huyu Mana kwenye majadiliano yetu ya kila siku, pengine wengi mmesikia mambo yake, wengine mmetetea tusimnyoshee mtumishi wa Mungu vidole etc! mimi ni Mkristo na kwa kweli namheshimu Mungu, He is the reason of who I am right now, he has been so good to me.

Lakini kitu kinachoniuuuuma sana ni watu wanafiki wanaomtumia Mungu kwa mambo yao wenyewe, narudia huu usemi tena "Enyi wote mnajiita manabii, watumishi, waheshimiwa na Malaika" mjue kuna siku na tena haiko mbali mtakutana na huyu mnayemtangaza kinafiki na kwa maslahi yenu uso kwa uso, na sijui mtamueleza nini"

Kwangu mimi aheri na fisadi kabisa anayetumia wadhifa wake kuiba, kuliko Mchungaji anayekusanya watu wa watu, wakiwa na nia ya kumtafuta Mungu, lakini kumbe wako ki Maslahi yao na wana mambo yao Binafsi ("Hili halikubaliki kabisa wandugu")

Nimepata bahati ya kusikiliza hii clip:

Bomu la kakobe the Part2 - YouTube

Hemu jamani msikilizeni huyu mtumishi anayejiita wa Mungu ambavyo anaweza kukaa chini na kupanga hila kiasi chote hiki, hili kwa ukweli haliwezi kuelezeka hata kidogo wandugu,

Maswali Machache:


  1. Ni watu wangapi nchi hii wanaojitahidi kumtafuta Mungu and they ended up kuwa chini ya wachungaji kama hawa?
  2. Ni watu wangapi wenye mapenzi na Mungu na wa kipato cha chini wanaotoa pesa zao kwa kumpenda Mungu ambazo zinaishi kwenye hizi hila?
  3. Kwa nini mtu uwe na nyadhifa 3 kubwa? Mchungaji "ana upako" ila hana mda wa kukaa na kumtafuta Mungu, Mfanya biashara Mashuhuru - Lazima awe na corner nyingi na mtoa rushwa mzuri, Mbunge - Hili ndo balaa la mwisho?

My take:

Mungu yupo, na atafutwe, ila ninawaomba watu kidogo tuwe pia tunatumia akili na logic zetu kichwani, tusiwe tunaenda kama makondoo.

Nomba kuwasilisha na kufungua mjadala wakubwa.

Kind Uttoh 2002 Zanzibar.
 
Uwezi ukatumia akili zako mwenyewe na ukeikwepa mitego ya hawa watu. Unatakiwa umuombe Mungu katika Jina la Yesu Kristo akupe busara ya kuelewa maelekezo yake period.

Namshukuru Mungu na bwana wangu Yesu Kristo kwa kuniweka huru dhidi ya uongo wote.
 
Du huyu mama ni hatari. Naoa dunia imemteka nyara! angefikiria na umri basi kuwa cku za kuishi zishaisha amrudie muumba wake!.
 
Mhh while listening to this clip.....
I am more than shocked na hawa watumishi wa mungu.

I have no comments.
Mambo mengi sana kwa maisha ya binadamu ni maigizo!
creating stages....

Masikini Tanzania
Dini ni maigizo.......
Siasa ni maigizo.....
Uchumi na maisha ya kila siku ni maigizo....
 
Mungu alitupatia akiri ya kujua mema na mabaya. Yesu Kristo akatuonya kwamba siku za mwisho watazuka MANABII wengi wa UONGO kwa JINA lake. I'm not saying Mama Lwakatare is a false prophet.

Kwa hiyo tumia vizuri akili zako, Sio wote wanaosema YESU, YESU ni wafuasi wake!

BTW, mara ya mwisho nilisoma kwamba Mama Lwakatare alipeka swali bungeni kuichongea JF ifungiwe kwasababu inasema UKWELI SANA "unaowaumiza" viongozi. JUST imagine MTUMISHI wa MUNGU anaogopa UKWELI! Be the jurry yourself.
 
Watakuja wengi Romani catholic itadumu
mbishi abishe lakini ukweli ndo huo. Hivi tangu makanisa haya ya uwongo yamekuja ni lipi limekuwa kubwa kama Rc.kazi yao kuwaibia waumini wao kwa kuwaambia toa toa mpaka wanakuwa maskini huku wao wakitajirika sana. Wanatembelea vx za ml 300 we kila siku unawapelekea sadaka.. Kumbukeni mahubiri yao makubwa ni kutoa sadaka! Mungu kakupa akili ya kutambua. Tafakarini mchukue hatua ndg zangu.
 
ni hatari sana kwa taifa la Mungu ila iko siku Mungu atawaumbua hadharani kweupe
 
Tatizo mtu akienda kusali anataka baada ya misa tu apate maombi aliyopeleka kwa Mungu. Asipopata anakuwa frustrated na kutoliamini kanisa lake, pale anapokosa imani na kuanza kuhangaika ndiyo anakutana na mashehebu yanayopokea waumini walio FRUSTRATED kama Mwingira, Lwakatare, Kakobe na Gwajima. Hasa wanawake ni wahanga wakubwa wa matapeli hawa
 
Huwa nasgangaani kwanini watu bado kila siku wanaenda hukohuko, wanapeleka pesa n akuaa masikini akati wenzao wanatajirika tu. Haiitaji hata nguvu kutoka mbinguni kukwambia kwamba hawa watu wanakudanganya ni akili kidoogo tu inahitajika kugundua hilo. waache wajinga waliwe.
 

People are frasturated. There are so many problesm facing the peoople, hawajui pa kwenda. Makanisa za siku zote kama RC and mengine yanaonekana kuwa slow sana kuwasaidia watu. Hapo ndio the LWAKATALE's have capitalized on it.
Kwa kweli inatisha na kuhuzunisha sana.
 
Lwakatale ni taperi kama mataperi wengine,ila yeye utapeli wake anatumia mgongo wa Mungu kuwatapeli watu,
Huyu ni mtu mwenye mawazo finyu sana kwa sababu hajui ya kwamba,saa yoyote Mungu anaweza kufanya lolote juu yake, na hizo hela anazowatapeli watu zisimsaidie chochote,
Mali zote tutaziacha hatutakwenda nazo peponi,namshauri afanye kama Zakayo awarudishie watu mali/hela zao ili abaki salama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…