Canada yahitaji zaidi watu (soma)

Canada yahitaji zaidi watu (soma)

Myahudi Jr II

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2016
Posts
6,816
Reaction score
8,809
Habari wana Jamii Forums,

Leo napenda kuwashirikisha ndugu zangu ninyi mambo kadha wa kadha juu ya uhamiaji.

Najua Tanzania tuna watu wengi sana wanapenda kufanya kazi nje, pia ukosefu wa ajira ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu, na pia hata walioajiriwa bado hawana tofauti na wasiyo na ajira (wao pia hulalamika maisha magumu). Afadhali yao na wasiyoajiriwa ni moja tu wameridhika.

Tanzania ukitaka ufurahie maisha na ajira hakikisha unakua 'single', usiwe na mtoto, wala usiwe na wanaokutegemea, yaani pesa yako ni wewe tu. Hakika utafurahia kidogo ulambishwacho.
  • Daktari analia hana ajira na mshara hautoshi.
  • Injinia nao wanalia.
  • Manesi na wakunga wanalia.
  • Wachumi nao wanalia n.k.
Ndugu zangu tuchangamkieni fursa za uhamiaji (information is power), ninayoandika hapa jitahidi ufanye mwenyewe kama utaweza.

Canada wameongeza orodha ya kuhitaji nguvu kazi katika nchi yao, ni kweli wanahitaji, Watanzania tuchangamke ndugu zanguni, Wahindi wanatumia hizi fursa sana. Sasa hivi wnaruhusiwa kujiunga na Jeshi kwa walio na ukazi wa kudumu na hata Kingereza ni tatizo ila wanatoboa.

1668647304981.jpeg

1668647329974.jpeg


Ukifika hapa nakuhakikishia baada ya miaka 4 toka umefika tu wewe siyo huyo, yaani nyumbani utarudi kutalii tu, mfano ($ in CAD)
  • Mshahara wa daktari kwa mwaka (general doctor) ni $260,000.00.
  • Mfamasia $90,000 kwa mwaka.
  • Nesi $75,000 kwa mwaka.
  • Injinia $109,000 CAD.
  • Mwalimu $70,000.
  • Dereva wa lori $45,000 kwa mwaka.
  • Fundi seremala $43,100 CAD kwa mwaka.
  • Mmwaga zege $45,187.
  • Mpiga rangi $38,400.
  • Kibarua wa ujenzi $38,026.
  • IT $100,000.
Hapa kuna 'child support' ni;
  • $6,997 kwa mwaka($583.08 per month) kwa kila mtoto anayestahiki chini ya miaka 6.
  • $5,903 kwa mwaka ($491.91 per month) kwa kila mtoto anayestahiki mwenye miaka 6 mpaka 17.
Hapo huduma za kijamii zote ni uhakika kwa 100%, kwa hapa swala la afya ni changamoto kidogo, madaktari ni wachache kuliko watu kwa afya 60%. Unaweza kwenda kumuona daktari saa 3 asubuhi ukatoka saa 10 jioni, hadi umeenda kwa daktari wewe unaumwa kweli, wengi naona huwa wanaenda kutibiwa kwao au wengi wanaenda Dubai.

Hivi mtu una GPA ya 3.5+ unalia Tanzania,wakati wewe ni lulu kwa jirani?!

Unatakiwa vitu wiwili 2 tu;

1) Nenda British Counsil pale kafanye IELTS score band 7+ hakikisha unajiandaa kweli, usiende kupoteza 700,000 yako,

2) Unatakiwa uwe na “Educational credential assessment (ECA)” hii ni kama TZS 550,000 ndani ya miezi 5 unakua tayari kwa kuomba “Ukazi wa kudumu”.

Watakuja wazee wanaochaji watu TZS 10,000,000 kuwaombea kusema nimekurupuka, bado kuna vitu vingi. Hivyo vitu vingi kikubwa ni pesa ya kuonesha unaweza kuishi mwaka mmoja ambacho wanataka CAD 12,000 sawa na TSH 17,000,000.00, uoneshe benki (kwa mfanya kazi wa serikali unakopa unaweka bank, kuna wazazi wana pesa wanaweza kuwapa watoto wao), wengineo anzeni na hivyo vya juu kwanza kuna njia za wahindi wanatumia, nitawaeleza wakati mwingine.

Watakuja tena watu ukiwa na hiyo pesa si bora ubaki bongo, utatoboa, Bongo kutoboa mpaka uibe na rushwa

Siku ukiwa na IELTS 7band nitakuelekeza jinsi ya kuomba LCA, ambayo ni wewe, chuo na Ubalozi wa Canada. Malipo unalipia kwa kadi, wala usije hangaika lipa mamilioni kufanyiwa wakati ni vitu rahisi.
 
Hata Tanzania nayo inahitaji watu.

Canada ya leo kuna watu walitoka jasho na damu kuifikisha hapo na ni mababu wa hao unaowaona leo.

Tanzania ili itoke hapa ije kufanana na Canada 2100 inahitaji watu watakaokubali kutoka jasho na damu leo hii ili baadaye wajukuu wafaidi matunda.
 
Tatizo wabongo hawapendi kufanya kazi, wenye kazi wapo tu kuskizia deal na michongo, hawafanyi kazi kwa moyo😂

Wanasaisa ni madili kwenda mbele, hawafanyi kazi wanafanyia party matumbo yao.
 
Hata Tanzania nayo inahitaji watu.

Canada ya leo kuna watu walitoka jasho na damu kuifikisha hapo na ni mababu wa hao unaowaona leo.

Tanzania ili itoke hapa ije kufanana na Canada 2100 inahitaji watu watakaokubali kutoka jasho na damu leo hii ili baadaye wajukuu wafaidi matunda.
Tunahitaji akili tu Mungu katuwekea kila kitu tumekosa tu akili
 
Habari wana Jamii Forum….



Leo napenda kushare na ndugu zangu nyinyi mambo kadha wa kadha juu ya uhamiaji,

Najua Tanzania tuna watu wengi sana wanapenda kufanya kazi nje, pia ukosefu wa ajira ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu, na pia hata walioajiriwa bado hawana tofauti na wasio na ajira(wao pia hulalamika Maisha magumu) afadhali yao na wasio ajiriwa ni moja tu WAMERIDHIKA.

Tanzania ukitaka uenjoy Maisha na ajira hakikisha unakua “single”, usiwe na mtoto, wala usiwe na wanaokutegemea yaani pesa yako ni wewe tu, HAKIKA utafurahia kidogo ulambishwacho.
  • Daktari analia hana ajira na mshara hautoshi
  • Engineer nao wanalia
  • Manesi na wakunga wanalia
  • Wachumi nao wanalia etc etc
Ndugu zangu tuchangamkieni fursa za uhamiaji (INFORMATION IS A POWER) ninayoandika hapa jitahidi ufanye mwenyewe kama utaweza.

CANADA wameongeza “list” ya kuhitaji nguvu kazi katika nchi yao, ni kweli wanahitaji, Watanzania tuchangamke ndugu zanguni, Wahindi wanatumia hizi fursa sana sasa hivi wnaruhusiwa kujiunga na Jeshi kwa walio na Ukazi wa kudumu na hata kingereza ni tatizo ila wanatoboa
View attachment 2419005
View attachment 2419006

Ukifika hapa NAKUHAKIKISHIA baada ya miaka 4 toka umefika tu wewe sio huyo, yaani nyumbani utarudi kutalii tu, mfn ($ in CAD)
  • mshahara wa Dotka kwa mwaka (general doctor) ni $260,000.00
  • Mfamasia $90,000 per year.
  • Nurse $75,000 per year.
  • Engineer $109,000 CAD
  • Teacher $70,000
  • Truck driver $45,000 per year
  • Carpenter $43,100 CAD per year.
  • Mmwaga zege $45,187
  • Mpiga rangi $38,400
  • Kibarua wa ujenzi $38,026
  • IT $100,000
Hapa kuna child support ni
  • $6,997 per year ($583.08 per month) for each eligible child under the age of 6
  • $5,903 per year ($491.91 per month) for each eligible child aged 6 to 17
Hapo huduma za kijamii zote ni uhakika kwa 100%, kwa hapa swala la afya ni changamoto kidogo, Madaktari ni wachache kuliko watu, kwa afya 60%, unaweza Kwenda kumuona daktari saa 3 asubuhi ukatoka saa 10 jioni, hadi umeenda kwa daktari wewe unaumwa kweli, wengi naona huwa wanaenda kutibiwa kwao au wengi wanaenda DUBAI.

Hivi mtu una GPA ya 3.5+ unalia Tanzania,wakati wewe ni lulu kwa Jirani.

Unatakiwa vitu wiwili 2 tu, 1. Nenda British counsil pale kafanye IELTS score band 7+ hakikisha unajiandaa kweli, usiende kupoteza 700,000 yako, Pili unatakiwa uwe na “Educational credential assessment (ECA)” hii ni kama TZS 550,000 ndani ya miezi 5 unakua tayari kwa kuomba “Ukazi wa kudumu”

Watakuja wazee wanaochaji watu TZS 10,000,000 kuwaombea kusema nimekurupuka, bado kuna vitu vingi, hivo vitu vingi kikubwa ni Pesa ya kuonyesha unaweza kuishi mwaka mmoja ambacho wanataka CAD 12,000 sawa na TSH 17,000,000.00 uonyeshe bank (kwa mfanya kazi wa serikali unakopa unaweka bank, kuna wazazi wana pesa wanaweza kuwapa Watoto wao), wengineo anzeni na hivyo vya juu kwanza kuna njia za wahindi wanatumia, nitawaeleza wakati mwingine.

Watakuja tena watu ukiwa na hiyo pesa si bora ubaki bongo, utatoboa, BONGO KUTOBOA MPAKA UIBE na RUSHWA

Siku ukiwa na IELTS 7band nitakuelekeza jinsi ya kuomba LCA, ambayo ni wewe, chuo na Ubalozi wa Canada, malipo unalipoa kwa kadi wala USIJE HANGAIKA LIPA MAMILIONI KUFANYIWA wakati ni vitu rahisi.
kwa namna fulani ni kweli ulichoandika ila si rahisi, siwakatishi tamaa watu kwa hiki nitakachoandika ila nia yangu nikuwapa tu angalizo.. Kuingia canada unahitaji mambo mawili tu 1. PESA AU 2. CONNECTION ili uingie kwenye hii nchi lazima uwe na kimojawapo kati ya hivyo au vyote kwa pamoja na nikuhakikishie tu kwamba kuna mambo ya kuzingatia ili usinyimwe visa wakati upo kwenye mchakato wa kuingia canada 1. hakikisha huna historia ya makosa ya jinai katika nchi unayotoka, 2. hakikisha huna magonjwa magonjwa yaani afya yako iwe safi 3. Uwe na walau kiwanja au nyumba kama assets canada hawataki watu mizigo 4. Walau uwe umeoa/umeolewa (uwe na cheti cha ndoa kuthibitisha) na muwe na mtoto walau mmoja au wawili mimi nakuhakikishia kuwa ukizingatia mambo hayo 100% wanakuona ni mtu unaejielewa na utakuwa umejithibitisha kuwa wewe ni mtu potential katika kukuza uchumi wa nchi yao wanakupa visa chap.

Mbali na hayo tafuta hela za kutosha ingia kwa njia ya kusoma hapo utafanikiwa ukishindwa hiyo tafuta connection ya watu wanaokaa canada tengeneza urafiki then muombe mtu mmoja akusaidie kukualika canada then ukifika yeye ndiye atakuwa anaku-backup japo mnaweza kuelewana namna utakavyokuwa unamtoatoa ili awe anakusaidia kukuhifadhi na kukupa michoro kwa hii utafanikiwa 100%.. nje ya hapo hakuna njia nyingine rahisi njia zote ngumu sana maana zinahitaji uwe na pesa na kutapeliwa ni kwa kiwango cha juu sana. kifupi canada ni nchi nzuri sana, fursa ni nyingi sana na kutoboa ni jambo la siku 365 tu, Uwe na siku njema.
 
Hata Tanzania nayo inahitaji watu.

Canada ya leo kuna watu walitoka jasho na damu kuifikisha hapo na ni mababu wa hao unaowaona leo.

Tanzania ili itoke hapa ije kufanana na Canada 2100 inahitaji watu watakaokubali kutoka jasho na damu leo hii ili baadaye wajukuu wafaidi matunda.
We have one life to live mzee,we km ulizaliwa uje kuibadilisha Tanzania bas kila la heri mkuu
 
Hata Tanzania nayo inahitaji watu.

Canada ya leo kuna watu walitoka jasho na damu kuifikisha hapo na ni mababu wa hao unaowaona leo.

Tanzania ili itoke hapa ije kufanana na Canada 2100 inahitaji watu watakaokubali kutoka jasho na damu leo hii ili baadaye wajukuu wafaidi matunda.
Kwa akili zile za "Unajenga majengo, madaraja na mabara bara wakati hali ngumu tunatakiwa tuishi vizuri sasa sio miaka 20 ijayo" usitegemee miujiza hapa nchini.

Walioshabikia huo ujinga leo hii wanatamani hata aliekuwa anajenga jenga angeendelea kuwepo. 😂😂😂 Maana wako gizani, dukani hakuendeki, maji hakuna na tozo kama zote!!!
 
Back
Top Bottom