Canada yaomba kujiunga na Jumuiya ya Ulaya (EU)

Canada yaomba kujiunga na Jumuiya ya Ulaya (EU)

Imeloa

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2013
Posts
14,885
Reaction score
18,083
Canada imewasilisha ombi la kushtukiza usiku wa kuamkia leo la kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya, likichochewa na matamshi ya Donald Trump kuhusu kuifanya nchi hiyo kuwa jimbo la 51 la Marekani.

Wakati Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alipoangalia kisanduku pokezi chake asubuhi ya leo, hakutarajia kupata barua pepe kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau iliyoandikwa 'HARAKA'.


Le Chou: Canada Applies For EU Membership
 
Hawa wajinga US haifai kuwachekea, wakimaliza huko watageukia huku physically kutwaa makoloni yao
 
Hivi NATO nayo itadumu kweli?!
Mi binafsi nataka Idumu kwa Ulaya, ila Marekani wamuache apigane vita vyake mwenyewe. USA ndiyo inaongoza kuwa na migogoro mingi, na imekuwa ikiwategemea nchi marafiki kumsaidia kupigana vita vyake, hivyo itapunguza fujo akiwa pekeyake na pili itazifanya nchi wanachama kufikiri kujitegemea zaidi kuliko hivi sasa kila kitu wamekuwa wakimtegemea USA.
Vita ya Iraq Marekani ilishirikisha mataifa mengi yeye akiwa kiongozi, lakini nchi marafiki walilazimika kutoa askari kwenda Iraq, na akashinda yeye lakini walipigana wengi.

Sasa kwa kelele za sasa Marekani ingeondolewa kila sehemu, na hata UN ihamishwe kutoka Marekani ipelekwe Bara jingine, na nchi wanachama wachange, tuache utegemezi kwa USA.

Angalia OAU/AU kule Adis Ababa, hawachangi hawakutani hawafanyi chochote kwasababu hakuna pesa, wanataka Marekani na Ulaya ndio watoe pesa wakutane nchi wananchama wa AU.

Kuna mgogoro mdoogo mashariki ya Kongo, wanakimbia kimbia tu, Juzi walikuwa hapa kwenye mkutano wa Pan African Energy Summit, wakakutana kwa dharura baada ya mkutono wao kujadili usalama wa Kongo, badala wamalize wakasema wakutane kama SADC uliwaona juzi Zimbabwe, Jana tumesikia tena Tanzania itaongoza mkutano wa SADC kujadili mgogoro wa mashariki ya Kongo.Tatizo nini, kama ni gharama watumie Zoom au Microsoft Team au njia zingine, kama hizo.

Kama nchi wananchama hawatoi michango, wanataka Taasisis ziendeshwe kwa pesa za nani?

SADC wanahaha, umeona wanakimbia kimbia tu kila nchi haitaki kuandaa mkutano wanakwepa gharama.

Ni vizuri Trump kapiga pin wajitegemee, tutaumia wananchi lakini ndio gharama za maisha zilivyo.
 
Unaandaliwa na taifa tajiri ukanda huu shaka ondoa.
Hakuna utajiri, nchi wanachama walipaswa kushiriki kuandaa mikutano yao, ama kwa internet au kukutana, nchi moja isibebe mzigo wa wengi.
 
Canada imewasilisha ombi la kushtukiza usiku wa kuamkia leo la kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya, likichochewa na matamshi ya Donald Trump kuhusu kuifanya nchi hiyo kuwa jimbo la 51 la Marekani.

Wakati Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alipoangalia kisanduku pokezi chake asubuhi ya leo, hakutarajia kupata barua pepe kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau iliyoandikwa 'HARAKA'.


Le Chou: Canada Applies For EU Membership

Barua iko wapi ? EU ni nchi za Ulaya Canada haipo Ulaya ipo bara la Americas
 
Waende tuu, tuone US atasurvive vp kwa kuipoteza canada
 
Canada imewasilisha ombi la kushtukiza usiku wa kuamkia leo la kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya, likichochewa na matamshi ya Donald Trump kuhusu kuifanya nchi hiyo kuwa jimbo la 51 la Marekani.

Wakati Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alipoangalia kisanduku pokezi chake asubuhi ya leo, hakutarajia kupata barua pepe kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau iliyoandikwa 'HARAKA'.


Le Chou: Canada Applies For EU Membership
Si na hao ni wa malikia
 
Canada imewasilisha ombi la kushtukiza usiku wa kuamkia leo la kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya, likichochewa na matamshi ya Donald Trump kuhusu kuifanya nchi hiyo kuwa jimbo la 51 la Marekani.

Wakati Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alipoangalia kisanduku pokezi chake asubuhi ya leo, hakutarajia kupata barua pepe kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau iliyoandikwa 'HARAKA'.


Le Chou: Canada Applies For EU Membership
Trump trump trump
 
Mtawala wa Canada ni King Charles III. So inaweza kuomba uanachama kupitia mgongo huo.
Cadana sio nchi ya Uingereza (United Kingdom) hii ni nchi inayofuata common wealth lakini sio nchi ya United Kingdom. Wanaweza kufanya lolote. Pili United Kingdom imejitoa EU!
 
Back
Top Bottom