CCM can reclaim her legitimacy, by going back to the roots, SI POROJO ZA MEDIA!

CCM can reclaim her legitimacy, by going back to the roots, SI POROJO ZA MEDIA!

CCM inawezekana kurudi katika misngi yake ya awli, ila inakibidi chama kichukue maamuzi magumu katika kufanikisha hilo jambo, tofauti na hapo tusubiri ndani ya CCM kunatokea chama kingine ambacho kitafuata misingi iliyo wekwa na CCM ya wafanyakazi, wakulima na yenye kujali maslai ya taifa na wananchi wake kwa ujumla.

Mheshimiwa Juma, suala la maamuzi magumu hilo haliwezekani kabisa, limesemwa sana lakini kila kikao cha juu cha chama kikikutana unachosikia baada ya mkutano ni kauli tu. Hakuna uamuzi mgumu wowote uliochukuliwa na kutekelezwa.

Labda tufafanue kidogo tunaposema chama kifanya maamuzi magumu. Maana yake ni kuwa miiko ya uongozi na maadili kwa viongozi wa chama vitekelezwe na kusimamiwa ipasavyo. Hilo likifanyika matatizo mengi yanaweza kupungua, lakini ukiangalia kwa undani, kufuata miiko ya uongozi na maadili yake, nia sawa na kuwaambia mafisadi waache matendo mabaya wanayofanya, na wachukuliwe hatua kutokana na makosa yao. The thing is, who has that courage?

Kuna waheshimiwa ambao hata ndani ya chama wanasifika kwa uchafu lakini hakuna aliyethubutu kuwaondoa, tena hata wanatoa vitisho kuwa mkitufukuza mtakiona. Sana sana kilichotokea ni kusema wajivue gamba, toka hilo limesemwa hadi sasa, ni Rostam peke yake amejiweka pembeni kidogo, amechukua remote control. Wachafu na machafu mengi yanaendelea kuwepo na hakuna cha maana kinachofanyika. Kimsingi mafisadi ndio wana fina say ya mambo ya chama, na kurudi kwenye maadili na miiko kunakwenda kinyume na maslahi yao binafsi.

Kumeguka kwa CCM, kama kukitokea itakuwa ni rehema kutoka kwa Mungu, kuna uwezekano ikatokea CCM ile ambayo tulikuwa nayo miaka 20 iliyopita. CCM ambayo mwenzetu Nape Nnauye anaipigania.
 
Mheshimiwa Juma, suala la maamuzi magumu hilo haliwezekani kabisa, limesemwa sana lakini kila kikao cha juu cha chama kikikutana unachosikia baada ya mkutano ni kauli tu. Hakuna uamuzi mgumu wowote uliochukuliwa na kutekelezwa.

Labda tufafanue kidogo tunaposema chama kifanya maamuzi magumu. Maana yake ni kuwa miiko ya uongozi na maadili kwa viongozi wa chama vitekelezwe na kusimamiwa ipasavyo. Hilo likifanyika matatizo mengi yanaweza kupungua, lakini ukiangalia kwa undani, kufuata miiko ya uongozi na maadili yake, nia sawa na kuwaambia mafisadi waache matendo mabaya wanayofanya, na wachukuliwe hatua kutokana na makosa yao. The thing is, who has that courage?

Kuna waheshimiwa ambao hata ndani ya chama wanasifika kwa uchafu lakini hakuna aliyethubutu kuwaondoa, tena hata wanatoa vitisho kuwa mkitufukuza mtakiona. Sana sana kilichotokea ni kusema wajivue gamba, toka hilo limesemwa hadi sasa, ni Rostam peke yake amejiweka pembeni kidogo, amechukua remote control. Wachafu na machafu mengi yanaendelea kuwepo na hakuna cha maana kinachofanyika. Kimsingi mafisadi ndio wana fina say ya mambo ya chama, na kurudi kwenye maadili na miiko kunakwenda kinyume na maslahi yao binafsi.

Kumeguka kwa CCM, kama kukitokea itakuwa ni rehema kutoka kwa Mungu, kuna uwezekano ikatokea CCM ile ambayo tulikuwa nayo miaka 20 iliyopita. CCM ambayo mwenzetu Nape Nnauye anaipigania.
Mkuu Bongolander, bado tunarudi kwenye hoja yangu ya wali kuwa haiwezekani mabadiliko yakatokea kukiwa na wapenda mabadiliko na wasiopenda mabadiliko. Kwa CCM,kundi la wasiopenda mabadiliko ndilo lenye kisu na limehodhi chama.
Kwa hivyo chama kipo mateka na sijui mateka ana haki gani mbele ya mtekaji wake.

Hili neno maamuzi magumu siliafiki kimatiki. Ni neno lililowekwa na wanasiasa katika jitihada za kupindisha ukweli na kukwepa taratibu, miiko na sheria. Kwanini kuwe na maamuzi magumu iwapo sheria, taratibu na kanuni zipo?

Neno hilo linapotumika humaanisha kuwa kunatakiwa kuwe na maamuzi ya watekwa nyara kupambana na wateka nyara. Kwamba,mtekwaji ameona umuhimu wa kupambana hata kama amefungwa mikono kitu ambacho ni uamuzi mgumu.

Bado tunarudi kule kule kuwa maamuzi magumu kwanza ni kufuata sheria, kanuni na taratibu kusafisha chama na kuondoa elements zote zilizokishika chama mateka kinyume na taratibu.
Baada ya hapo ndipo chama kijitathmini kimejikwaa wapi na kinaelekea wapi.
 
Back
Top Bottom