Uchaguzi 2020 CCM haikuhitaji kuwa na bango hata moja la kampeni

Uchaguzi 2020 CCM haikuhitaji kuwa na bango hata moja la kampeni

Kwa miaka 5 mfululizo CCM imefanya mambo mengi ambayo yangetosha kuwa mabango yao ya kampeni kwenye uchaguzi wa 2020. Kazi zilizofanyika awamu ya tano pia zilijumuishwa kwenye wimbo wa Harmonize unaoelezea mafanikio ya awamu ya tano, na wimbo huu ulitoka mapema sana na kuchezwa kwenye media zote nchini hata kabla tarehe ya uchaguzi haijatangazwa.

Mafanikio ya awamu ya tano yanaonekana kwa macho ya nyama kwa kila mwenye macho, lakini pia yamehubiriwa sana katika kipindi chote cha miaka 5 katika kila mkutano na kila mwenye masikio amesikia. Mwenye macho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia. Kusema ukweli sikutegemea kuona mabango mengi tena ya kampeni ili hela za mabango zielekezwe kwenye kitu kingine japo hata kwa kuweka nyasi bandia kwenye viwanja vya CCM ili soka lichezwe kwa ufasaha kwenye viwanja vyote.

Hizi gharama za mabango tena sijui ni nani alizipendekeza, kwangu mimi naona mabango hayakuwa na sababu na hayana mchango kwa kampeni za CCM hasa za Urais, maana mafanikio ya CCM na serikali ya awamu ya tano yalishasemwa sana na viongozi wote wa chama na serikali, hata wanapopiga kampeni wanayarudia tena yale yale ya ndege, reli, bwawa, rushwa, umeme na hospitali.

Au wenzangu JF mnaonaje? Gharama hizi za kutengeneza mabango ulikuwa ni ushauri kutoka kwa nani kwa malengo gani? TAKUKURU hebu pitenipiteni huko pia.

Kunywa soda kwa bili yangu
 
Vodacom na umaarufu wake wanamatangazo kila siku kwa TV na radio na mabango kila siku wanaingeza


Unajufunza nini?

Wale wanataka pesa na ni biashara so una maanisha urais ni biashara?
 
Lissu atapata kura za namba za viatu
tapatalk_1601418168188.jpeg
 
CCM mwaka huu sio kwamba wanafanya kampeni kwakua kunaushindani wa kisiasa, uo ni utamaduni wa ccm, walikua walifanya kampeni ata kipindi cha chama kimoja enzi za ndio na hapana.
Enzi izo Mbowe akiwa chipkiz wa ccm, Mwaka huu wangeweza kua na kampeni wikitatu kabla ya uchaguzi ila wengine wange tafsiri ni kama dharau kwa wananchi na ni dalili za kubweteka. Ki uhalisia CCM waliposhinda 2015 wamepata bonus ya 2020, uu uchaguzi ulikwisha 2015 saaizi wanakula faida ya kuchagua JPM 2015.
mmmh uchaguzi wa serika-li z--a mitaa mbona hawakupiga kampeni wala kuweka mabango?
 
Kwa miaka 5 mfululizo CCM imefanya mambo mengi ambayo yangetosha kuwa mabango yao ya kampeni kwenye uchaguzi wa 2020. Kazi zilizofanyika awamu ya tano pia zilijumuishwa kwenye wimbo wa Harmonize unaoelezea mafanikio ya awamu ya tano, na wimbo huu ulitoka mapema sana na kuchezwa kwenye media zote nchini hata kabla tarehe ya uchaguzi haijatangazwa.

Mafanikio ya awamu ya tano yanaonekana kwa macho ya nyama kwa kila mwenye macho, lakini pia yamehubiriwa sana katika kipindi chote cha miaka 5 katika kila mkutano na kila mwenye masikio amesikia. Mwenye macho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia. Kusema ukweli sikutegemea kuona mabango mengi tena ya kampeni ili hela za mabango zielekezwe kwenye kitu kingine japo hata kwa kuweka nyasi bandia kwenye viwanja vya CCM ili soka lichezwe kwa ufasaha kwenye viwanja vyote.

Hizi gharama za mabango tena sijui ni nani alizipendekeza, kwangu mimi naona mabango hayakuwa na sababu na hayana mchango kwa kampeni za CCM hasa za Urais, maana mafanikio ya CCM na serikali ya awamu ya tano yalishasemwa sana na viongozi wote wa chama na serikali, hata wanapopiga kampeni wanayarudia tena yale yale ya ndege, reli, bwawa, rushwa, umeme na hospitali.

Au wenzangu JF mnaonaje? Gharama hizi za kutengeneza mabango ulikuwa ni ushauri kutoka kwa nani kwa malengo gani? TAKUKURU hebu pitenipiteni huko pia.

uchaguzi huu ni wa muhimu sana ccm, tuna jambo letu kwenye katiba
 
Yes, uko sawa kabisa mkuu! Tena hakuhitaji hata kutembea kufanya kampeni bali walihitaji kufanya ufafanuzi tu mdogo kwa kile kipindi cha Dakika 45 za Farhia middle! Ajabu ndio wanaohangaika kuliko vyama vyoote!
 
Kwa miaka 5 mfululizo CCM imefanya mambo mengi ambayo yangetosha kuwa mabango yao ya kampeni kwenye uchaguzi wa 2020. Kazi zilizofanyika awamu ya tano pia zilijumuishwa kwenye wimbo wa Harmonize unaoelezea mafanikio ya awamu ya tano, na wimbo huu ulitoka mapema sana na kuchezwa kwenye media zote nchini hata kabla tarehe ya uchaguzi haijatangazwa.

Mafanikio ya awamu ya tano yanaonekana kwa macho ya nyama kwa kila mwenye macho, lakini pia yamehubiriwa sana katika kipindi chote cha miaka 5 katika kila mkutano na kila mwenye masikio amesikia. Mwenye macho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia. Kusema ukweli sikutegemea kuona mabango mengi tena ya kampeni ili hela za mabango zielekezwe kwenye kitu kingine japo hata kwa kuweka nyasi bandia kwenye viwanja vya CCM ili soka lichezwe kwa ufasaha kwenye viwanja vyote.

Hizi gharama za mabango tena sijui ni nani alizipendekeza, kwangu mimi naona mabango hayakuwa na sababu na hayana mchango kwa kampeni za CCM hasa za Urais, maana mafanikio ya CCM na serikali ya awamu ya tano yalishasemwa sana na viongozi wote wa chama na serikali, hata wanapopiga kampeni wanayarudia tena yale yale ya ndege, reli, bwawa, rushwa, umeme na hospitali.

Au wenzangu JF mnaonaje? Gharama hizi za kutengeneza mabango ulikuwa ni ushauri kutoka kwa nani kwa malengo gani? TAKUKURU hebu pitenipiteni huko pia.
Unapoona mtoto anyejisomea usiku kila siku lakini na ile siku ya mtihani anahangaika kusoma mpaka asuhi ya kwenda chumba cha mtihani bado anasomaga! Juwa huyo ni poyoyo, kichwani ni upepo! CCM haina tija ya kuendelea nayo! Tukikatae kabisa chama kinachobahatisha mambo! Serikali imetumia gharama nyingi mno kujitangaza kwenye vyombo vya habari, ikitangaza miradi na mambo mbali kwa kipindi chote cha miaka 5, Sasa na leo hii kama bado tunaendelea kugharamia vyombo vya habari na kampeni ndeefu kwa kurudia kusimulia yaleyale, basi gharama zote zilizotumika ni kazi bure! Na hii sio bure yawezekana ikawa ni nguvu ya kinyongoa au laana toka kwa makundi yaliyodhulumiwa haki kama watumishi na wengineo!
 
Unazungumzia mabango tu!

1.Thsirt na kofia bure kwa wanaoenda uwanjani kwenye kampeni!
2.Kukodi malori na mabasi kubeba wananchi!

Pamoja na hayo uliyosema,spana zimekubali mpaka mgombea wako anaomba kura kwa kuwapigia magoti wananchi!
Na sasa hapa Kakola wana nunua vitambulisho vya wapiga kura kwa gharama yoyote ili kupunguza kura za Lissu. Wameona kuwapa 5000/ tu haisaidii maana wana pokea wanajaza vichwa uwanjani siku inayo fata wanazipeleka kama sadaka kwa Lissu.
 
Na sasa hapa Kakola wana nunua vitambulisho vya wapiga kura kwa gharama yoyote ili kupunguza kura za Lissu. Wameona kuwapa 5000/ tu haisaidii maana wana pokea wanajaza vichwa uwanjani siku inayo fata wanazipeleka kama sadaka kwa Lissu.
Wanyonge Wana Jambo lao. Hizi shule za kata zinaisaidia jamii kupata wapigakura bora
 
Back
Top Bottom