CCM ijitahidi kutenda mambo mazuri ili kutoviharibu vyama vingine vinavyoiga yanayofanywa na CCM

CCM ijitahidi kutenda mambo mazuri ili kutoviharibu vyama vingine vinavyoiga yanayofanywa na CCM

Matongee

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
1,056
Reaction score
2,729
CCM ni baba wa vyama vyote vya siasa Tanzania. Vyama vyote vinaitazama CCM kama kioo chao. Iwe kwenye jema au baya. Mara nyingi huko CHADEMA kukitokea mambo ya kipuuzi hukimbilia kujitetea kuwa CCM wanafanya mabaya zaidi. Kwa mfano ukiuliza kuhusu michango na ruzuku utajibiwa kwa kuambiwa kaulize CCM kuhusu ufisadi.

Kwa sasa ndani ya CHADEMA kuna sakata la rushwa kwenye chaguzi zao ila makada waandamizi wamekimbilia kuitaja CCM inahusika.

Ninakisihi Chama Cha Mapinduzi kusimamia vizuri ilani yake na kuwachukulia hatua makada wake wanaofanya mambo ya hovyo. Hii itasaidia vyama vidogo kama CHADEMA kuiga mema badala ya mabaya.
 
Ccm sio baba wa vyama vyote, sema ni chama kikongwe kuliko vyote hapa nchini kwa sasa. Ccm ni baba wa baadhi ya vyama, na huwa vinajitokeza wakati wa uchaguzi, ama wakati ccm inapitia misikosuko kwa kazi maalumu, hasa ya upotoshaji. Hakuna chama makini kinaiiga ccm, ukiona chama kinaiiga ccm ujue hicho sio chama. Chama kinaweza kufanya mambo yake na yakafanana na ya ccm, lakini sio kwa kuwaiga.
 
Back
Top Bottom