CCM ikitawala miaka 100 bado hatutopata Katiba mpya kwakuwa kila Rais anaamua atakavyo?

CCM ikitawala miaka 100 bado hatutopata Katiba mpya kwakuwa kila Rais anaamua atakavyo?

Wilderness Voice

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2016
Posts
921
Reaction score
1,649
Nasikitika sana, na ninakishangaa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kujiona kuwa kina hati miliki ya nchi na wananchi. Eti CCM kinasema hakina mpango na Katiba mpya. Ambayo hata walio asisi hii nchi, akiwepo Mwalimu Nyerere alikiri kuwa hii Katiba siyo nzuri kwani inampa Rais Madaraka makubwa kiasi kwamba Rais anaweza tumia huo mwanya kufanya atakacho.

Nimshukuru Rais mstaafu Kikwete, kuanzisha mchakato na baadae akauuwa yeye mwenyewe, kwa kuiponda tume na maazimio yaliyofikiwa na hivyo kutupilia mbali mchakato huo wa katiba, lakini alithubutu.

Najua kilichofanya asitishe mchakato huo wa Katiba ni maswala yaliyojitokeza ya Muungano na hasa Serikali tatu. Kwani Rais anaapa kuulinda Muungano wa Tanzania. Hivyo angeruhusu hilo jambo kutokea, ilikuwa ajiuzuru na hivyo kuruhusu serikali ya mpito kuchukua nafasi, kitu ambacho nadhani kingeenda KINYUME na miiko ya CCM. Tunakumbuka yalomfika Abdul Jumbe Mwinyi. Hata hivyo nampa kongole Mhe. J. Kikwete kwa uthubutu huo.

Serikali inayojiita awamu ya sita, japo si awamu ya sita kulingana na katiba tuliyonayo. Hakuna uchaguzi uliyoitishwa, bali Rais aliyopo anaendeleza awamu ya tano mpaka itapofikia ukingoni mwaka 2025. Rais ni wa Sita awamu ya tano. Hivyo tusilazimishwe. Lakini Watanzania uamlishwa kama kuku, ingia ndani tunaingia. Tumejaa ushabiki na undumila kuwili. Mtu akipinga asubiri matusi na kejeri ili tu kumvunja moyo. oK, Tuache hayo!

Tayari Rais wetu Mama Samia, kupitia Katibu mwenezi wa CCM, alieleza serikali ya CCM haina mpango kuruhusu mchakato wa Katiba Mpya. Nacho jiuliza, hivi CCM wana mamlaka gani kikatiba, kukataa kusiwepo mabadiliko ya Katiba? Je, ni kwakua Rais ni wa CCM?
Je kwa style hii ya CCM hata ikitawala miaka 100 ijayo hatutapata katiba mpya kisa CCM na Rais ndo waamuzi? Tena CCM inaongea kwa kujisikia na kutamba kwamba hakuna Katiba mpya! Ni nani kaiweka CCM madarakani? Si wananchi? Ni kwanini leo hawa CCM wanawadharau wananchi kwa kusema hakuna katiba Mpya!

Watanzania, tufikie sehemu, tuihadhibu CCM, si kujipendekeza! Ili kuleta mabadiliko sahihi na kuondokana na mazoea! Hii katiba iliyopo itatuchelewesha kupata maendeleo. Kuna mifumo mingi ambayo inahitajika kufanyiwa marekebisho, ili kuifanya Tanzania ibadilike na iendelee. Nchi nyingi duniani ufanya mabadiliko ya kimfumo ambayo uwa katika katiba kwa maslahi mapana ya nchi. Kwanini CCM ijione ndiyo yenye dhamana katika hili?

Hata Rais Kikwete hakuwa na mamlaka ya kusitisha mambo ambayo tayari yalikuwa yamepitishwa na Bunge la Katiba. Rais kwa utashi wake akagoma na kutoa vijembe kwenye Tume kuwa mara katiba ni jitabu kubwa utadhani desa la physics. Ni kweli katiba haikuhitaji kuwa kubwa kama kitabu cha hadithi za Alf lela Ulela! Lakini tulichokihitaji ni mfumo mpya wa katiba. Angewapa muda kufanya usahihi na kisha kwendelea na mchakato kuliko kusitisha kila kitu.

Imefikia wakati sasa, uchaguzi wa 2025 usifanyike kama hatuna katiba mpya. Mikakati ifuatayo ifanyike:
  • Kwenda mahakamani kudai mwendelezo na mchakato wa katiba Mpya wendelee, kwani Rais aliuzuia kimakosa.
  • Viongozi wote wa vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi, NGOs, Asasi mbalimbali za haki za binadamu, Viongozi wa dini lugha iwe moja Katiba Mpya.
  • Maandamano ni haki na msingi wa kudai utendaji haki. Kila mwezi kuwe na siku moja ya maandamano ya amani nchi nzima kudai katiba mpya.
  • Kuwepo kampeni ya kuwasusia viongozi wa Serikali katika mikutano yao, kwani ni wao ndo hawataki uwepo wa katiba mpya. Hata Rais hasusiwe.
  • Tuwatake wabunge wetu wahoji kuhusu katiba mpya Bungeni, kama hawataki, nao tusiwatambue!
Watanzania, tukijifanya kutulia tusahau, katiba mpya. Hakuna Rais wa CCM atakae kubali mabadiliko ya Katiba. Kikwete, alikwepa, Magufuli akasema hata husika nayo, na sasa Mama yetu Rais mama Samia nae kesha sema kupitia katibu mwenezi. Yaani Rais anaamua atakavyo, nasi kwa ushabiki tunashangilia ila hatujui madhara yake. Tusitake chekwa na vizazi vijavyo. Wakatuona tulikuwa mambumbumbu, kwa kuwa na katiba iliyopitwa na wakati. Inabaki kujazwa viraka kwa manufaa ya Chama tawala. Tuliwacheka babu zetu walio danganywa na wakoloni. Enzi za Chief Mangungo! Tusigeuke kuwa Mangungo. Tukadanganywa kwa madaraka na vijisenti, au kwa maneno matamu na ushabiki; ili tusipate katiba mpya. Tusimame kwa masilahi ya nchi na vizazi vijavyo. Tudai kwa nguvu zote katiba mpya.

Safari hii kieleweke. CCM si Mungu wa kutuamlia tutakacho. Shida tumekuwa na wanasiasa wanafiki, ambao hawana uzalendo wao uangalia matumbo yao na familia zao. Ebu tubadilike na tuchukue hatua sasa.

Nimemkumbuka Mch. Mtikila! Kheri yake aliweza kubadili mambo kwa kuishitaki serikali mahakamani, na hata kuhamasisha wananchi. Hata Mstaafu Rais Mwinyi hawezi msahau huyu!

SHIME WATANZANIA TUDAI KATIBA MPYA. WAKATI NI SASA! TUSIPO DAI TUSAHAU!
 
Najua kilichofanya asitishe mchakato huo wa Katiba ni maswala yaliyojitokeza ya Muungano na hasa Serikali tatu. Kwani Rais anaapa kuulinda Muungano wa Tanzania.
Wala siyo muungano ndugu. Sababu ni kwamba katiba mpya inapunguza sana mamlaka ya rais. Lkn pia inaiweka CCM ishindwe namna ya kutumia vyombo vya dola kubakia madarakani.
 
In summary yaaani:

Wananchi wanataka katiba mpya, wananchi wamewaweka ccm madarakani, ccm inawadharau wananchi waliowaweka madarakani, wananchi waache kujipendekeza kwa ccm, kuna uwezekano wa ccm kutawala miaka 100 ijayo, wananchi waisusie ccm walioiweka madarakani.
 
Ubovu wa KATIBA ndio UHAI wa CCM hivyo kibinadamu pana ugumu kidogo hata nakuunga mkono 100%.
CCM na Katiba mpya ni sawa ni kama mbwa na chatu. Kisa cha mbwa kumuogopa chatu ni kitendawili kilichoshinda hata wataalam kukitegua. Kwa kawaida mbwa ana mbio na akiamua kukimbia chatu haoni ndani.

Hata hivyo cha ajabu ni kwamba mbwa akikutana uso kwa uso na chatu anaganda hapo hapo kama vile kapigwa smaku na hata kusogeza mguu hawezi na hivyo chatu humsogelea tu taratibu na kumkamata bila kuhangaika.

Salama ya mbwa ni kuhakikisha kwamba hatii macho kwa chatu la sivyo tayari anageuzwa kitoweo na hivyo hivyo kwa CCM. CCM wanajua fika kwamba wakitia macho tu kwenye katiba mpya hawachomoki, wameliwa asubuhi!

Hivyo salama ya CCM ni kuiogopa Katiba kama ukoma, hawaisogelei, hawaigusi na wala hawaitazami. Wakipata tu habari kwamba huko wanakoelekea kuna uwezekano wa kukutana uso kwa uso na Katiba mpya, wanageuza safari.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ni vema kuanzisha vugyvugu la kudai katiba badala ya kusubiria hisani ya Rais, Serikali au chama cha siasa.
 
Nasikitika sana, na ninakishangaa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kujiona kuwa kina hati miliki ya nchi na wananchi. Eti CCM kinasema hakina mpango na Katiba mpya. Ambayo hata walio asisi hii nchi, akiwepo Mwalimu Nyerere alikiri kuwa hii Katiba siyo nzuri kwani inampa Rais Madaraka makubwa kiasi kwamba Rais anaweza tumia huo mwanya kufanya atakacho.

Nimshukuru Rais mstaafu Kikwete, kuanzisha mchakato na baadae akauuwa yeye mwenyewe, kwa kuiponda tume na maazimio yaliyofikiwa na hivyo kutupilia mbali mchakato huo wa katiba, lakini alithubutu.

Najua kilichofanya asitishe mchakato huo wa Katiba ni maswala yaliyojitokeza ya Muungano na hasa Serikali tatu. Kwani Rais anaapa kuulinda Muungano wa Tanzania. Hivyo angeruhusu hilo jambo kutokea, ilikuwa ajiuzuru na hivyo kuruhusu serikali ya mpito kuchukua nafasi, kitu ambacho nadhani kingeenda KINYUME na miiko ya CCM. Tunakumbuka yalomfika Abdul Jumbe Mwinyi. Hata hivyo nampa kongole Mhe. J. Kikwete kwa uthubutu huo.

Serikali inayojiita awamu ya sita, japo si awamu ya sita kulingana na katiba tuliyonayo. Hakuna uchaguzi uliyoitishwa, bali Rais aliyopo anaendeleza awamu ya tano mpaka itapofikia ukingoni mwaka 2025. Rais ni wa Sita awamu ya tano. Hivyo tusilazimishwe. Lakini Watanzania uamlishwa kama kuku, ingia ndani tunaingia. Tumejaa ushabiki na undumila kuwili. Mtu akipinga asubiri matusi na kejeri ili tu kumvunja moyo. oK, Tuache hayo!

Tayari Rais wetu Mama Samia, kupitia Katibu mwenezi wa CCM, alieleza serikali ya CCM haina mpango kuruhusu mchakato wa Katiba Mpya. Nacho jiuliza, hivi CCM wana mamlaka gani kikatiba, kukataa kusiwepo mabadiliko ya Katiba? Je, ni kwakua Rais ni wa CCM?
Je kwa style hii ya CCM hata ikitawala miaka 100 ijayo hatutapata katiba mpya kisa CCM na Rais ndo waamuzi? Tena CCM inaongea kwa kujisikia na kutamba kwamba hakuna Katiba mpya! Ni nani kaiweka CCM madarakani? Si wananchi? Ni kwanini leo hawa CCM wanawadharau wananchi kwa kusema hakuna katiba Mpya!

Watanzania, tufikie sehemu, tuihadhibu CCM, si kujipendekeza! Ili kuleta mabadiliko sahihi na kuondokana na mazoea! Hii katiba iliyopo itatuchelewesha kupata maendeleo. Kuna mifumo mingi ambayo inahitajika kufanyiwa marekebisho, ili kuifanya Tanzania ibadilike na iendelee. Nchi nyingi duniani ufanya mabadiliko ya kimfumo ambayo uwa katika katiba kwa maslahi mapana ya nchi. Kwanini CCM ijione ndiyo yenye dhamana katika hili?

Hata Rais Kikwete hakuwa na mamlaka ya kusitisha mambo ambayo tayari yalikuwa yamepitishwa na Bunge la Katiba. Rais kwa utashi wake akagoma na kutoa vijembe kwenye Tume kuwa mara katiba ni jitabu kubwa utadhani desa la physics. Ni kweli katiba haikuhitaji kuwa kubwa kama kitabu cha hadithi za Alf lela Ulela! Lakini tulichokihitaji ni mfumo mpya wa katiba. Angewapa muda kufanya usahihi na kisha kwendelea na mchakato kuliko kusitisha kila kitu.

Imefikia wakati sasa, uchaguzi wa 2025 usifanyike kama hatuna katiba mpya. Mikakati ifuatayo ifanyike:
  • Kwenda mahakamani kudai mwendelezo na mchakato wa katiba Mpya wendelee, kwani Rais aliuzuia kimakosa.
  • Viongozi wote wa vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi, NGOs, Asasi mbalimbali za haki za binadamu, Viongozi wa dini lugha iwe moja Katiba Mpya.
  • Maandamano ni haki na msingi wa kudai utendaji haki. Kila mwezi kuwe na siku moja ya maandamano ya amani nchi nzima kudai katiba mpya.
  • Kuwepo kampeni ya kuwasusia viongozi wa Serikali katika mikutano yao, kwani ni wao ndo hawataki uwepo wa katiba mpya. Hata Rais hasusiwe.
  • Tuwatake wabunge wetu wahoji kuhusu katiba mpya Bungeni, kama hawataki, nao tusiwatambue!
Watanzania, tukijifanya kutulia tusahau, katiba mpya. Hakuna Rais wa CCM atakae kubali mabadiliko ya Katiba. Kikwete, alikwepa, Magufuli akasema hata husika nayo, na sasa Mama yetu Rais mama Samia nae kesha sema kupitia katibu mwenezi. Yaani Rais anaamua atakavyo, nasi kwa ushabiki tunashangilia ila hatujui madhara yake. Tusitake chekwa na vizazi vijavyo. Wakatuona tulikuwa mambumbumbu, kwa kuwa na katiba iliyopitwa na wakati. Inabaki kujazwa viraka kwa manufaa ya Chama tawala. Tuliwacheka babu zetu walio danganywa na wakoloni. Enzi za Chief Mangungo! Tusigeuke kuwa Mangungo. Tukadanganywa kwa madaraka na vijisenti, au kwa maneno matamu na ushabiki; ili tusipate katiba mpya. Tusimame kwa masilahi ya nchi na vizazi vijavyo. Tudai kwa nguvu zote katiba mpya.

Safari hii kieleweke. CCM si Mungu wa kutuamlia tutakacho. Shida tumekuwa na wanasiasa wanafiki, ambao hawana uzalendo wao uangalia matumbo yao na familia zao. Ebu tubadilike na tuchukue hatua sasa.

Nimemkumbuka Mch. Mtikila! Kheri yake aliweza kubadili mambo kwa kuishitaki serikali mahakamani, na hata kuhamasisha wananchi. Hata Mstaafu Rais Mwinyi hawezi msahau huyu!

SHIME WATANZANIA TUDAI KATIBA MPYA. WAKATI NI SASA! TUSIPO DAI TUSAHAU!
Mbona hamkumdai Magufuli muone moto wake?
Mnamuonea Samia kwakuwa ni mpole?
Yeye ana dola,na hakuna anachoamua mwenyewe. Mshike adabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
In summary yaaani:

Wananchi wanataka katiba mpya, wananchi wamewaweka ccm madarakani, ccm inawadharau wananchi waliowaweka madarakani, wananchi waache kujipendekeza kwa ccm, kuna uwezekano wa ccm kutawala miaka 100 ijayo, wananchi waisusie ccm walioiweka madarakani.
Ukweli ni kwamba ccm wamejiweka wenyewe madarakani kwa kupanga matokeo nchi mzima kama unategemea maendeleo au katiba kutoka ccm unapoteza muda wako
 
Nimemsikia waziri wa pesa juzi akilalamika kuwa huwezi amini miaka 60 ya uhuru bado kuna maeneo tz hakuna barabara.
Na ndivyo hivyo hivyo watakuwa wanalalamika mwaka 2063.
 
Nasikitika sana, na ninakishangaa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kujiona kuwa kina hati miliki ya nchi na wananchi. Eti CCM kinasema hakina mpango na Katiba mpya. Ambayo hata walio asisi hii nchi, akiwepo Mwalimu Nyerere alikiri kuwa hii Katiba siyo nzuri kwani inampa Rais Madaraka makubwa kiasi kwamba Rais anaweza tumia huo mwanya kufanya atakacho.

Nimshukuru Rais mstaafu Kikwete, kuanzisha mchakato na baadae akauuwa yeye mwenyewe, kwa kuiponda tume na maazimio yaliyofikiwa na hivyo kutupilia mbali mchakato huo wa katiba, lakini alithubutu.

Najua kilichofanya asitishe mchakato huo wa Katiba ni maswala yaliyojitokeza ya Muungano na hasa Serikali tatu. Kwani Rais anaapa kuulinda Muungano wa Tanzania. Hivyo angeruhusu hilo jambo kutokea, ilikuwa ajiuzuru na hivyo kuruhusu serikali ya mpito kuchukua nafasi, kitu ambacho nadhani kingeenda KINYUME na miiko ya CCM. Tunakumbuka yalomfika Abdul Jumbe Mwinyi. Hata hivyo nampa kongole Mhe. J. Kikwete kwa uthubutu huo.

Serikali inayojiita awamu ya sita, japo si awamu ya sita kulingana na katiba tuliyonayo. Hakuna uchaguzi uliyoitishwa, bali Rais aliyopo anaendeleza awamu ya tano mpaka itapofikia ukingoni mwaka 2025. Rais ni wa Sita awamu ya tano. Hivyo tusilazimishwe. Lakini Watanzania uamlishwa kama kuku, ingia ndani tunaingia. Tumejaa ushabiki na undumila kuwili. Mtu akipinga asubiri matusi na kejeri ili tu kumvunja moyo. oK, Tuache hayo!

Tayari Rais wetu Mama Samia, kupitia Katibu mwenezi wa CCM, alieleza serikali ya CCM haina mpango kuruhusu mchakato wa Katiba Mpya. Nacho jiuliza, hivi CCM wana mamlaka gani kikatiba, kukataa kusiwepo mabadiliko ya Katiba? Je, ni kwakua Rais ni wa CCM?
Je kwa style hii ya CCM hata ikitawala miaka 100 ijayo hatutapata katiba mpya kisa CCM na Rais ndo waamuzi? Tena CCM inaongea kwa kujisikia na kutamba kwamba hakuna Katiba mpya! Ni nani kaiweka CCM madarakani? Si wananchi? Ni kwanini leo hawa CCM wanawadharau wananchi kwa kusema hakuna katiba Mpya!

Watanzania, tufikie sehemu, tuihadhibu CCM, si kujipendekeza! Ili kuleta mabadiliko sahihi na kuondokana na mazoea! Hii katiba iliyopo itatuchelewesha kupata maendeleo. Kuna mifumo mingi ambayo inahitajika kufanyiwa marekebisho, ili kuifanya Tanzania ibadilike na iendelee. Nchi nyingi duniani ufanya mabadiliko ya kimfumo ambayo uwa katika katiba kwa maslahi mapana ya nchi. Kwanini CCM ijione ndiyo yenye dhamana katika hili?

Hata Rais Kikwete hakuwa na mamlaka ya kusitisha mambo ambayo tayari yalikuwa yamepitishwa na Bunge la Katiba. Rais kwa utashi wake akagoma na kutoa vijembe kwenye Tume kuwa mara katiba ni jitabu kubwa utadhani desa la physics. Ni kweli katiba haikuhitaji kuwa kubwa kama kitabu cha hadithi za Alf lela Ulela! Lakini tulichokihitaji ni mfumo mpya wa katiba. Angewapa muda kufanya usahihi na kisha kwendelea na mchakato kuliko kusitisha kila kitu.

Imefikia wakati sasa, uchaguzi wa 2025 usifanyike kama hatuna katiba mpya. Mikakati ifuatayo ifanyike:
  • Kwenda mahakamani kudai mwendelezo na mchakato wa katiba Mpya wendelee, kwani Rais aliuzuia kimakosa.
  • Viongozi wote wa vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi, NGOs, Asasi mbalimbali za haki za binadamu, Viongozi wa dini lugha iwe moja Katiba Mpya.
  • Maandamano ni haki na msingi wa kudai utendaji haki. Kila mwezi kuwe na siku moja ya maandamano ya amani nchi nzima kudai katiba mpya.
  • Kuwepo kampeni ya kuwasusia viongozi wa Serikali katika mikutano yao, kwani ni wao ndo hawataki uwepo wa katiba mpya. Hata Rais hasusiwe.
  • Tuwatake wabunge wetu wahoji kuhusu katiba mpya Bungeni, kama hawataki, nao tusiwatambue!
Watanzania, tukijifanya kutulia tusahau, katiba mpya. Hakuna Rais wa CCM atakae kubali mabadiliko ya Katiba. Kikwete, alikwepa, Magufuli akasema hata husika nayo, na sasa Mama yetu Rais mama Samia nae kesha sema kupitia katibu mwenezi. Yaani Rais anaamua atakavyo, nasi kwa ushabiki tunashangilia ila hatujui madhara yake. Tusitake chekwa na vizazi vijavyo. Wakatuona tulikuwa mambumbumbu, kwa kuwa na katiba iliyopitwa na wakati. Inabaki kujazwa viraka kwa manufaa ya Chama tawala. Tuliwacheka babu zetu walio danganywa na wakoloni. Enzi za Chief Mangungo! Tusigeuke kuwa Mangungo. Tukadanganywa kwa madaraka na vijisenti, au kwa maneno matamu na ushabiki; ili tusipate katiba mpya. Tusimame kwa masilahi ya nchi na vizazi vijavyo. Tudai kwa nguvu zote katiba mpya.

Safari hii kieleweke. CCM si Mungu wa kutuamlia tutakacho. Shida tumekuwa na wanasiasa wanafiki, ambao hawana uzalendo wao uangalia matumbo yao na familia zao. Ebu tubadilike na tuchukue hatua sasa.

Nimemkumbuka Mch. Mtikila! Kheri yake aliweza kubadili mambo kwa kuishitaki serikali mahakamani, na hata kuhamasisha wananchi. Hata Mstaafu Rais Mwinyi hawezi msahau huyu!

SHIME WATANZANIA TUDAI KATIBA MPYA. WAKATI NI SASA! TUSIPO DAI TUSAHAU!
Wakenya walifanyaje wakapata Katiba mpya? Tujifunze kutoka kwao tupate mahali pa kuanzia ili tupate Katiba mpya mapema iwezekanavyo.
 
Mbona hamkumdai Magufuli muone moto wake?
Mnamuonea Samia kwakuwa ni mpole?
Yeye ana dola,na hakuna anachoamua mwenyewe. Mshike adabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wengine shida, yaani wanapenda mambo ya kulinganisha na ushabiki. Hapa sijaongelea yupi angeombwa. Soma uelewe. Nimeongea Magu aligoma, tukadhani mama atakubali nae tunaona kagoma. Kitukikiendelea utafutiwa ufumbuzi. Sijaja hapa kitimu Magu sitjui timu Samia. Jadili hoja si watu, na ushabiki.
 
Wakenya walifanyaje wakapata Katiba mpya? Tujifunze kutoka kwao tupate mahali pa kuanzia ili tupate Katiba mpya mapema iwezekanavyo.
Kenya Rais anakuwepo kwa Maslahi mapana ya kitaifa na nchi. Ndiye alie ridhia mchakato wa katiba. Ukiwa na Rais asiye penda ni ngumu. Kenyatta anaangalia maslahi mapana ya wakenya.
 
Je kwa style hii ya CCM hata ikitawala miaka 100 ijayo hatutapata katiba mpya kisa CCM na Rais ndo waamuzi? .
Somo la civics education linahitajika sana!. Rais anaongoza nchi kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, kwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama chake. Maadam issue ya katiba haipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, tusimlazimishe Rais Samia!.

Ila hiyo ya CCM kutawala miaka 100, ni kweli...

Infact CCM ni itatawala milele.
P
 
Hivi vitu vinaenda pamoja. Itakuwa ni makosa makubwa sana kuwa na Katiba mpya bila Tume huru ya uchaguzi halafu wale wahuni wa Tume FAKE wakaendelea na uhuni wao.
Ni kweli, CCM wanachanganya katiba mpya na tume huru, sisi kwasasa watupe Katiba kwanza.
 
Watu wengine shida, yaani wanapenda mambo ya kulinganisha na ushabiki. Hapa sijaongelea yupi angeombwa. Soma uelewe. Nimeongea Magu aligoma, tukadhani mama atakubali nae tunaona kagoma. Kitukikiendelea utafutiwa ufumbuzi. Sijaja hapa kitimu Magu sitjui timu Samia. Jadili hoja si watu, na ushabiki.
Na mimi nimeongea reality. Yaani naona wewe na mwenzio Kigogo ndo mnaona na ninyi mnaweza kumpanikisha Samia.
Katiba mpya si ajenda kwasasa. Watu wanataka kuona reli ya SGR inakamilika,umeme unawaka vijijini,maji yanapatikana mijini na vijijini,elimu inatolewa japo nakiri bado sana elimu yetu ni duni,huduma bora za afya japo nako bado.

Watu wanataka maeneo ya kufanya biashara. Mfano ukimuuliza mmachinga leo ni katiba au kubaki mjini?
Najua jibu unalo.

Kigogo nae anasema eti katiba ipatikane kwa jasho na damu,mjinga kabisa. Yeye hata ya kutolea wagonjwa hathubutu,anataka ya nani imwagike?

Endeleeni kupiga ramli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na mimi nimeongea reality. Yaani naona wewe na mwenzio Kigogo ndo mnaona na ninyi mnaweza kumpanikisha Samia.
Katiba mpya si ajenda kwasasa. Watu wanataka kuona reli ya SGR inakamilika,umeme unawaka vijijini,maji yanapatikana mijini na vijijini,elimu inatolewa japo nakiri bado sana elimu yetu ni duni,huduma bora za afya japo nako bado.

Watu wanataka maeneo ya kufanya biashara. Mfano ukimuuliza mmachinga leo ni katiba au kubaki mjini?
Najua jibu unalo.

Kigogo nae anasema eti katiba ipatikane kwa jasho na damu,mjinga kabisa. Yeye hata ya kutolea wagonjwa hathubutu,anataka ya nani imwagike?

Endeleeni kupiga ramli.

Sent using Jamii Forums mo
Swala la kusema ukimuuliza leo mmachinga atasema sijui nini hiyo haiwezi kuzuia kuwepo kwa Katiba mpya. Kikubwa ni wananchi kuelemishwa na kujua umuhimu wa Katiba. Usichukue kutokuelewa kwao kama tiketi ya wananchi kutopata katiba mpya.
Viongozi wapo kuwaelewesha wananchi si kuchukua udhaifu wao wa kutojua mambo ili viongozi wanufaike.
SGR, Umeme, Elimu, na huduma za afya haziwezi zuia katiba. Kwani Rais amekuwa injinia au dakatari, na Mwalimu kusema anafanya kila kitu yeye mwenyewe. Usilete siasa za kizamani.

Mbona Kikwete aliweza kuanzisha mchakato na mambo katika nchi yaliendelea. Mfano tu, Swala la Elimu, afya, na miundo mbinu, yangekuwa yanatekelezwa na serikali za mitaa wala kusingekuwa na tatizo. Shida serikali za mitaa hazijitegemei, japo wanasema ziko huru.
Huu wote ni uzaifu wa katiba tuliyonayo. Rais ni mtu mkubwa si wakufatilia kila kitu. Yeye ni kuhakikisha sera zinatekelezwa. Leo hii Wakurungezi wangekuwa wanapatikana kwa ushindani wa usaili na kuajiliwa na Halmashauri mambo katika Wilaya yangeenda vizuri. Siyo tumegeuza nafasi za ukurugenzi kuwa za kisiasa.

Ebu tuangalie mataifa mengine Local Government zinavyowajibika kuleta maendeleo kwa wananchi. Shule tunashindwa jenga. Wakati hizi local Government wanatakiwa wawe na projection wanafunzi wangapi tutakuwa nao labda miaka mitano ijayo. Hivyo kujenga shule za kudumu. Mbona Ulaya shule hazijengwi kila mwaka? Kwani wanafunzi hawaongezeki?
Kikubwa ni ku plan. Haya mambo yafanywe na serikali za mitaa bila kuingiliwa kisiasa. Kuna haja gani kuwa na Wizara ya Elimu, na Bado unakuwa na Katibu wizara ya Tamisemi anaeshughulikia Elimu. Yaani unakatibu wizara ya Elimu, Una katibu wizara ya Tamisemi wote kazi moja. Unawaziri wa Elimu tena huku waziri TAMISEMi na manaibu wake bado wanashughulikia Elimu. Ndo maana hata hapa majuzi Bungeni waligongana kwenye utoaji wa kauli ya Elimu bure na Michango.

TAMISEMI waachiwe Elimu ya awali, msingi hadi sekondari. Elimu ya juu iwe katika wizara ya Sayansi na Tecknolojia. Ili kuondoa muingiliano.
Tukiwa na Wakurungezi walioomba kazi kwa ushindani katika Halmashauri, itajenga viongozi wa maono na hata kuleta maendeleo siyo siasa za kubebana. Akija huyu anaondoa huyu anaweka huyu. Hivi tutafika kweli?
Ndo maana tunahitaji katiba kubadili hii mifumo ambayo ni ngumu kupata maendeleo ya kweli. Si ushabiki na kujipendekeza,
 
Mkataba wa ccm kuinyonya Tanzania upo kikatiba ndani yao chama chao na mkataba huo udhalimu inaonyesha ccm itainyonya Tanzania kwa muda wa miaka 350 kuanzia 1985[emoji88][emoji88][emoji88][emoji88][emoji88][emoji3090]
 
Somo la civics education linahitajika sana!. Rais anaongoza nchi kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, kwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama chake. Maadam issue ya katiba haipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, tusimlazimishe Rais Samia!.

Ila hiyo ya CCM kutawala miaka 100, ni kweli...

Infact CCM ni itatawala milele.
P
Rais anaongoza kweli kwa Katiba, sheria, taratibu na kanuni mbalimbali ambazo zipo kwa manufaa ya nchi. Japo pia anatekeleza Ilani ya uchaguzi ya Chama chake.
Ukitegemea tu Civics ni ngumu kuelewa mfumo mzima wa utendaji wa kazi za Rais. Kikubwa ni kujiongeza na kujua mbali na yote, nchi uhitaji visionary leader. Rais alie na maono. Anae weza kufikiria nje ya Box na si akili kuishia tu kwenye kile alichopangiwa kufanya. Ukiwa na Rais wa namna hiyo ambae anaangalia tu Ilani, bila kutazama nyakati na mabadiliko ya kimfumo na kidunia basi huyo Rais si mbunifu.
Tunahitaji Rais ambae anaangalia Ilani yake ya Uchaguzi lakini pia anaangalia mahitaji ya kitaifa na kujenga Taifa lisilo na mawaa.

Ndo maana kuna mihimili mingine ambayo ipo kukidhi haja ya kujenga Taifa moja.
Na hii mihimili mingine haina Ilani bali inatekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria na taratibu mbalimbali.
Mfano, Ilani ya CCM haijawai kukubali mgombea binafsi katika uchaguzi wa Tanzania. Lakini katika miaka ya nyuma elfu mbili na kitu, Mahakam Kuu ilitoa maamuzi ya kuwepo mgombea binafsi au wagombea binafsi katika chaguzi. Japo mahakama ya Rufaa ilibatirisha maamuzi hayo kimizengwe.

Hivyo Mahakama, Bunge zinauwezo wa kuelekeza au kutoa maamuzi ya kufanyika kwa jambo japo hilo jambo haliko katika Ilani ya uchaguzi wa CCM. Ndo maana nikasema kwa kutumia hii mifumo tunaweza kupata katiba mpya kwani Rais hatohitaji kukwepa.
Kikwete alivyoanzisha mchakato wa katiba mpya, haikuwa katika Ilani ya uchaguzi. Ila ni kiongozi alie angalia nje ya Box na kuona kuna hitaji hilo kwa wakati huo.

Ni mangapi marais wanafanya na hayako katika Ilani ya uchaguzi? Tusitafute visingizio visio na mantiki. Mabadiliko ya Haki za binadamu yalianza kuwekwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano mwaka 1984, na baadae iliendelea . haya mabadiliko ya kwanza wakati yanafanyika, hayakuwa kwenye Ilani. Ila kutokana na muda na mahitaji katika jamii ilifanyika. Utakumbuka Rais alikuwa na mamlaka ya kumuweka mtu kuzuizini. CCM hawakupenda lakini ilibidi watii.

Mfumo wa Vyama vingi haukuwa katika Ilani, na CCM wengi waliukataa. Lakini kwa busara za Nyerere kwa kuwaza nje ya Box alisema hata wachache wasikilizwe! Akungoja vurugu zitokee, ndo aruhusu vyama vingi. Hakusema hilo alikuwepo katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 1990. Si kila kitu ni Ilani ya Uchaguzi.
Tunahitaji kiongozi mwenye maono, anae waza zaidi nje ya box si kufungwa na visingizio vya Ilani ya CCM. Na hii inadhihirisha udharimu wa CCM kwa wananchi. Wanakwepa kuweka mabadiliko ya Katiba katika Ilani yao kwakua, hawajali kabisa wananchi. Wapo kwa maslahi yao binafsi. Ilani lazima itazame nini pia wananchi wanataka, si kulaghai laghai. Ifike mwisho sasa. TUMECHOKA!
 
Back
Top Bottom