Uchaguzi 2020 CCM imeshinda uchaguzi kuanzia kwenye uandishi wa ilani, wengine ilani ni za utani

Uchaguzi 2020 CCM imeshinda uchaguzi kuanzia kwenye uandishi wa ilani, wengine ilani ni za utani

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
324
Reaction score
649
ILANI YA CCM INATOA SULUHU YA MASWALI, ACT NA CHADEMA ZINALALAMIKA

Na Elius Ndabila

Nimefanikiwa kuzisoma Ilani za vyama vitatu, yaani Ilani ya CCM, ACT Wazalendo na CHADEMA. Nikiwa ninazipitia Ilani hizi nimegundua utofauti mkubwa kwenye kujibu mahitaji ya Watanzania.

Ilani ya CCM kama chama chenyewe kilivyo kikubwa na kikongwe Afrika basi hata Ilani yake ni kubwa. Ilani ya CCM ina kurasa 308. Ilani ya CCM imeeleza namna serikali ilivyofanya kazi kwa kipindi cha miaka mitano ya 2015/2020 na imeeleza jinsi wanavyopanga kufanya kazi nyingine kubwa mwaka 2020/2025 kama watapewa ridhaa tr 28.

Ilani ya CCM inatoa mwelekeo kama Taifa na kuonyesha namna walivyo jipanga kuendelea kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta mbalimbali za kimaendeleo hasa Elimu, Afya, Mawasiliano, Viwanda, Maji, Michezo n.k. Hata hivyo Ilani inaendelea kusisitiza juu ya kuendelea kusimamia Amani ya Taifa ambayo ni tunu.

Ilani ya CCM ya mwaka huu imeeleza wanategemea kufanya nini kwenye kila Wilaya kwa miaka yao mitano watakapopata ridhaa, zaidi kuendeleza kasi ya kuliletea Taifa Maendeleo.

Lakini ukisoma Ilani ya ACT Wazalendo ambayo ina kurasa 60 na Ilani ya CHADEMA ambayo pia ina kurasa 104 zimejaa kulalamika. Ilani hizi mbili ambazo Utadhani walikaa pamoja na kuziandika mengi yaliyoandikwa kwenye hizo kurasa chache ni:-

Wanalaani ukandamizaji wa demokrasia, wanalaani Uhuru wa vyombo vya habari, Wanalaani watu kubambikiwa kesi na kupelekwa jela, Wanalaani ununuzi wa ndege bila Ridhaa ya Watanzania, Wanaskitika Serikali kukopa fedha na kujenga miradi mikubwa kama SGR na Mradi wa Umeme, Wanalaani Bunge Kuto kuwa mubashara n.k

Baada ya malalamiko wanasema wao wataboresha Kilimo, Uhuru wa habari, kuwatoa watu magerezani, kupunguza madaraka ya Rais n.k Lakini ACT wao wanaongeza kwa kusema watu watakula Bata.

Ukisoma kwa umakini Ilani hizi utaona kuna vyama wanawatania Watanzania, hawako serious. Huwezi kuandika Ilani kwa kulalamika. Ilani inatakiwa kuonyesha matarajio yako ukipata zamani unategemea kufanya nini? Ilani ya upinzani inatakiwa kuonyesha wapi Ilani ya Chama Tawala ilifeli na wao watafanya nini?

Lakini kubwa zaidi Ilani ya Upinzani ilipaswa kuwa kubwa kuliko ya CCM kwa kuwa wao wapo nje na wanaona makosa mengi. Lakini kitendo cha kuwa na ilani ndogo inaonyesha fika CCM imefanya makosa machache hivyo bado tunastahili kuendelea kuongoza.
 
Eliasi Ndabila,

Mdogo wako alipata mkopo wa HESLB?

Vipi umepata ajira?

Vipi pesa za korosho ana yako mdogo alilipwa?
 
Ila CCM akili huwa zinaruka mara nyingine, et lijitu linakwambia tumeibiwa sana wakati nyinyi wenyewe CCM ndiwo mlikuwa mnasaini mikataba na mibovu na wakoloni haohao, misaada hampati toka kwa hao wakoloni basi mnawaita mabeberu.
 
Tume ikiwa huru, CCM hata ikisimama na gunia la viazi mbatata ambalo halina ilani na kampeni haliwezi piga bado tu gunia la viazi mbatata litaibuka kidedea!
Kumbe na wewe ni mchezaji ndio maana umekuja huku?

Kwenda zenu mmeongoza vya kutosha hakuna unafuu zaidi ya umasikini wa kukithiri kwa Watanzania kila uchwao hakuna unafuu.
Wapisheni wengine nao wale bata.
 
Kwa taarifa toka wizara ya kilimo Tanzania tuna deficit ya sukari tani 120,000 kwa mwaka.

Moja ya mambo ya msingi ilitakiwa muda huu wa campaign serikali ije na strategy ya kutafuta visionary local investor kwenye kuzalisha sukari, products za pamba au korosho

Then TIC iwape ardhi ambayo tunayo na wizara ya kilimo au hazina watoe bank guarantee wenye kampuni kukokopa na kuwekeza kwenye sekta hizi ili kuongeza thamani ya pamba au ku-cut down imports ya sukari kwa kukuza uzalishaji wa ndani.

Ahadi pekee za ilani hazitoshi; haya yanahitaji ku-act sasa.

Itazalisha ajira, kukuza exports kama ni mazao ya pamba na korosho, itaongeza tax base na kuongeza forex earnings.
AG anakuwa sehemu ya mchakato toka mwanza na serikali kwa kuweka guarantee inachukua say 40% ya faida ikizalishwa.

Hapa tungekuza uchumi kwa haraka sana.

Otherwise, ilani zimekuwepo nyingi sana ila utekelezaji huwa inahitaji strategy zaidi ili kupata matokea ya haraka.

Usalama, Hazina, TIC, BOT ninyi ni very keyplayers to make this happen.

Wasalaam

Screenshot_20200824-205726-1.jpg
 
Unamaanisha ilani ya CHADEMA inafanana na tiketi ya Dar lux[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
ILANI isiyozingatia UHURU wa watu, HAKI za watu, UTU wa watu, Maendelea ya watu haina maana yoyote.
 
ilani ya CCM haina tija kuwekwa maana nchi inaendeshwa kwa matakwa ya mtu mmoja, hizo ajira milioni nane zilizowekwa kwenye ilani ni upuuzi tu na kuleta vichekesho.
 
Hayo ni maoni yako, nami nna yangu...tofauti kbs na yako!!.
 
Kinacho nishangaza wenye nyuzi za kuunga juhudi wengi wanajitambulisha kwa majina yao halisi! Najiuliza ni coincidence tu au Kuna jambo limepangwa likapangika?
 
Eliasi Ndabila,

Mdogo wako alipata mkopo.wa HESLB?
Vipi umepata ajira.?
Vipi pesa za korosho ana yako mdogo alilipwa?
Kwai ulisikia watu wanadai?
Na mimi nakuuliza pesa za michango ya wabunge kwa ajili ya kampeni ziko wapi?
Naomba jibu hilo tu
 
Wewe Ndabila unatoka Wilaya maskini yenye mahtaji mengi sana..inashangaza kutokuwa na huruma kabsaa ukushabikia ndugu zako wakiendelea kukosa huduma mhimu kwa mda mrefu..tupe mifano ya huduma mhimu zilizopo huko tupime kama Hao unaowashabikia kama wanahitaji ridhaa tena!!roho ya vieo isiwatoe ufahamu!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Wewe Ndabila unatoka Wilaya maskini yenye mahtaji mengi sana..inashangaza kutokuwa na huruma kabsaa ukushabikia ndugu zako wakiendelea kukosa huduma mhimu kwa mda mrefu..tupe mifano ya huduma mhimu zilizopo huko tupime kama Hao unaowashabikia kama wanahitaji ridhaa tena!!roho ya vieo isiwatoe ufahamu!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Yaani Leo ninaletewa barabara ya lami Isongole Kasumulu km 90.7 nishabikie Ilani za kulalamika?

Yaani Leo ninaletewa barabara ya Lami KK-Luswisi-Lubanda-Sange-Ubungu Km 56 nishabikie Ilani za kulialia?
Yaani Leo ninaletewa barabara ya lami mbalizi Shigamba nishabikie ilani za kulialia?

Ni kweli ni ache kushangilia barabara ya Iyula-Mlale- Itumba nianze kununu?

Lakini kweli hujaona mapinduzi makubwa ya Hospital zetu za Ibaba, Lubanda, Isoko na Itumba?

Hujaona mapinduzi ya Elimu Wilayani kwetu?

Leo acha nishabikie CCM kwani Wilaya yetu sasa naona tunakimbia. Vijiji 64 kati ya 71 vimeshawashwa Umeme.

Au utaghendite nakamu mukaya?
 
Uchaguzi huru na haki ni vigumu kushinda hakuna Mtanzania mwenye kujielewa ataipigia ccm kura
 
Back
Top Bottom