Tetesi: CCM inawabebembeleza iliowafukuza!!

Tetesi: CCM inawabebembeleza iliowafukuza!!

Mkuu kaa kimya tu, wale madiwani waliohama kule Hai kwa Mbowe, barua zao za kujiuzulu zilikuwa na maudhui sawa ila wakajichanganya kwenye majina. Wakati ule ndio ilikuwa hii project ya nunua wapinzani pazia la usajili limefunguliwa. Sasa hivi hii inayoitwa ccm mpya sterling ni babayenu naye anacheza siasa za kishamba ile mbaya. Bora hata hiyo ccm ya kabla ya 2015 wagombea wa uchaguzi wa ubunge walikuwa wanapatikana kwa ushindani, na sio hii mpya wahamiaji wanakuja na kupewa nafasi, waliofia chama wanabaki kupamba majukwaa ya kuwapokelea akina Msando na kina Kafulila, na kuishia kupeleka viongozi kwa waganga kuvuta nyota ya cdm iende ccm.
Lowassa alipohamia huko kwenu ilikuwaje?? Alipewa haki ya kugombea tena urais akawaacha wapigania chama kuleee!!
 
Lowassa alipohamia huko kwenu ilikuwaje?? Alipewa haki ya kugombea tena urais akawaacha wapigania chama kuleee!!

Ccm ndio mkawaiga ule upuuzi wa cdm juzi kwenye wale wagombea ubunge?
 
unawafukuza wanachama kwa mbwembwe alafu unaenda kuwanunua wapinzani kwa gharama kubwa huku unashangilia
Mantiki iko wazi. Kama unaweza kuweweseka hadi kutumia fedha kuwanunua wapinzani wako ili ionekane kuwa "unakubalika" inakuwaje ngumu kuwabebembeleza wale uliowafukuza "waombe radhi" ambapo haitatumika hata senti tano ya shaba?
 
Wewe una uhusiano hata na kiongozi yeyote yule aliye karibu na Mzee wa Mangula umuulize kama Jumatano ya wiki hii hawajapokea Barua toka kwa waliofukuzwa?

Halafu hii kaulil mbiu yenu ya chama kwanza mtu baadaye si mnayo miaka yote, leo imekuwaje mpya?

Siasa si uadui. Kama una uwezo na hilo linakuuma, waambie waliofukuzwa wakatae kuandika barua
 
Siasa si uadui. Kama una uwezo na hilo linakuuma, waambie waliofukuzwa wakatae kuandika barua
TOT ilishakufa kitambo na Khadija Kopa zama zake zimepita, sidhani kama bado mipasho ina thamani ya zama zile!!
 
TOT ilishakufa kitambo na Khadija Kopa zama zake zimepita, sidhani kama bado mipasho ina thamani ya zama zile!!

Kama akili yako imekutuma huo ni mpasho basi una tafakuri nzuri Sana na hao wanaokubali kulazimishwa kuandika barua badala ya kuhamia chama kingine ni wasaliti wa yale tuyatamaniayo na hilo jambo ni la kidikteta, linaminya demokrasia. Hahahahaha
 
Back
Top Bottom