Pre GE2025 CCM Iringa yatoa onyo kwa wanaobeza Rais Samia na Dkt. Mwinyi kugombea Urais 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Naona mambo yanazidi kunoga tu!
===============
Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa kimeonya vikali watu wanaobeza maamuzi ya Mkutano Mkuu wa chama hicho ya kuwateua Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kupeperusha bendera ya urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Aidha, chama hicho kimeonya dhidi ya upotoshaji wa taarifa zinazohusu maamuzi hayo.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Daudi Yasini, ametoa onyo hilo wakati wa matembezi ya kuunga mkono maamuzi hayo, akisema kuwa uamuzi wa kuwateua viongozi hao unazingatia mafanikio makubwa ya utekelezaji wa ilani ya CCM chini ya uongozi wa Rais Samia.

Soma Pia: Wajumbe Mkutano Mkuu CCM wapitisha Rais Samia, Dkt. Mwinyi kugombea Urais 2025

Yasini ameeleza kuwa miradi mikubwa imetekelezwa mkoani Iringa, akitaja mfano wa mradi wa skimu ya umwagiliaji ya Mkombozi katika wilaya ya Iringa, unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 50. Amesema mradi huo unatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa wakulima na kuchangia kukuza uchumi wa mkoa huo.

Your browser is not able to display this video.
 
Hao ni vichaa. Wapuuzwe.
 
Matatizo aliyaanzisha Saa100 mwenyewe,na tatizo lilianzia hapa!
 

Attachments

  • 5938169-3f8437b06df44d0a7c8b8e175f481762.mp4
    23 MB
Ndugu zetu Wahehe mnatuangusha.

kule CDM kuna kale kajamaa kanatumia jina la akina Madaraka ni kachawa promax huku nako kuna hili.....!!
 
Mkutano huo mkuu,ulitoa wapi agenda wakati ,Halmashauri kuu na Kamati kuu,ilikuwa haijakaa na kujadili???😳
 
Ili Mkutano Mkuu wa CCM Taifa uweze kufanyika,ni lazima ,vikao vya chama viwe vimetangulia kukaa ili tutengeneza agenda za mkutano Mkuu.
1. Kamati Kuu
2. Halmashauri Kuu
3. Mkutano Mkuu.


Tuambie agenda ya kupitisha jina la saa100 ilitolewa au kujadiliwa na Kikao kipi kabla ya kupelekwa kwenye mkutano mkuu wa CCM????

Baada ya Kila mjumbe kulipwa Tsh, 2,600,000 walipoteza ufahamu ghafla! Na kuuza nchi kwa miaka 15 kuanzia 2025.
 
 
Wawili hao walichukua shortcut baada ya kuona kwenye ngazi za maamuzi ni
kama huyo Mwenyekiti wa Iringa
 
Jk kazi anayo🤣🤣🤣
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…