Elections 2010 CCM Kuilalamikia Chadema NEC

Elections 2010 CCM Kuilalamikia Chadema NEC

Wanadai alianza kampeni kabla ya muda. Wanamsubiri arudishe fomu ndipo wapeleke pingamizi. Mashtaka yameshaandaliwa tayari wanasubiri tu kuyapeleka kunakohusika muda utakapofika. Wamekusanya ushahidi kutoka hotuba zote alizotoa katika kampeni yake ya kusaka wadhamini.

Napenda kuamini kuwa Dr Slaa alikuwa makini na hizo sheria wanazokusudia kutumia, na kuwa hakutoa mwanya wa jambo kama hili kutumika dhidi yake.
 
Watu kwa uzushi mmekosa hoja sasa mnapepesuka mwaka huu mtasema yote, CCM inapumua kwa msaada wa mashine karibu mashine itazimika mnavyo wayawaya hadi mnatia huruma poleni sana.

Nashauri mods kama thread haina ushaidi au source ya kueleweka ifutwe vinginevyo tutakuwa tunapoteza muda kunajadili mambo ya kutunga.
 
ccm wao wenyewe walikuwa wanafanya kampeni sema ndio hivyo wanaona moto wa dr slaa bila kuuzima kwa nguvu ya ziada patakuwa hapatoshi.

waandaemikanda na wao mikanda yao ya hotuba pia imeandaliwa.na dr slaa ndio kwanza kachukua fomu hakuwa amechukuwa fomu pale mwanzo.

ccm wawe makini sana na wanachotaka kukifanya kwani wananchi wanaangalia kila kitu.
 
Kithuku,
Mkuu kwa hili umetia chunvi kwani JK alitangazwa kuwa mgombea kabla ya Dr.Slaa na hata kuchagua mgombea mwenza wakati hatujui Chadema atamsimama nani? Nakumbuka hata Seif alisema hatishwi na kuchaguliwa kwa Dr.Shein, kwa kauli hiyo akiwa na maana tayari alikwisha chaguliwa na kujitangaza kuipambana na Dr.Shein.

Ebu rudia kusoma vizuri JF ktk mada zinazohusiana na watu hawa.
 
Dr. W.P Slaa amedhaminiwa na watu zaidi ya milioni moja. ukichukua 1000,000 gawanya kwa 25 unapata 40000 kwahiyo alidhaminiwa na wanachama Takribani 40000 kila alipopita. Kwa hiyo walitaka awaambie nini wananchama wa CHADEMA au kwa sababu alikutana nao nje kwenye viwanja. tayari tuna kura 1200000 tunatafuta kama 5000000 kila mdhamini akishawishi sita kupiga kura Ngoma inachezwa magogoni BBQ kwa sana.

Kwa Homa hii inahitajika quinini tu. Lazima makamba na Mzee Msekwa wachanganyikiwe. Wazee hawa hawawezi kupambana na Strategy za akina Tindu, Kitila, Zitto hawa ni vijana, siasa zimebadilika sana wanakimbia mbio ambazo hawaziwezi. Republican walifikiri dunia bado ni ya 60s wakashangaa siasa za kibaguzi hazinanafasi Obama ana BBQ DC.

Sisi wote ni watanzania hii ni zamu ya Chadema kuongoza watanzania, CCM tuungeni mkono acheni mizwengwe.
 
Katika taarifa ya habari ya TBC1 saa mbili usiku huu, makamu mwenyekiti wa CCM bara Pius Msekwa amenukuliwa akisema kwamba Chadema wameanza kampeni kabla ya muda.

Kutokana na hilo, katibu wa CCM taifa, Yusufu Makamba atapeleka malalamiko yao huko tume ya taifa ya uchaguzi, yaani NEC.

Mambo yameanza. Ngoma inogile.

Na leo pia nimezisikia hizi habari kwenye magazeti RFA na Clouds FM,

Hivi niwaulize hawa viongozi wetu wa CCM sasa imefika mahali nao shule kama imewapita kushoto ati ivi baaada ya chaguzi pale Kizota Dodoma CCM walifanya nini Uwanja wa Jamuhuri na Kule Zanzibar walifanya nini??

Mbali na Hilo katika pita pita yangu huko mikoani kipindi cha hizo kura za maoni nilijionea mengi tena Dodoma Mabango ya Mchague Jakaya Mrisho Kikwete 2010 yamejaaa mji mzima kwenye milingoti ya taaa za barabarani na chaajabu zaidi ukiwa watokea Dar ukikaribia Bungeni muda wa usiku unakuta yale mabango ya JK ndio yanawaka kwenye nguzo hizo hizo za taa za barabarani lakini taaa za juu haziwaki nilistahajabishwa sana,

Sana ntashangaa hawa viongozi wetu wa CCM wanapo lalama kwenye vyombo vya magazeti na kwenda hadi tume ya uchaguzi huku wao CCM wamesahau kuwa wameyaacha mabango mengi Dodoma na sticker nyingi tu za JK kwenye magari na taxi hapo DODOMA MJINI.

John Tendwa unapo letewa haya malalamiko jaribu kuchunguza hizo tuhuma kwanza

 
WanaCCM wakati wa mabadiliko umefika...
Msikubali kuendelea kuburuzwa na kundi la wachache kwa manufaa yao..
Sote tu waTanzania fanya lililo sahihi sasa..
Chagua Chadema..ili Dr SLAA awe Rais wa Tanzania yenye matumaini mapya..
 
Siwalaumu sana CCM kwa kushikwa na woga............umati kwenye mikutano ya Dr Slaa unatisha ati!
 
Wanadai alianza kampeni kabla ya muda. Wanamsubiri arudishe fomu ndipo wapeleke pingamizi. Mashtaka yameshaandaliwa tayari wanasubiri tu kuyapeleka kunakohusika muda utakapofika. Wamekusanya ushahidi kutoka hotuba zote alizotoa katika kampeni yake ya kusaka wadhamini.

Napenda kuamini kuwa Dr Slaa alikuwa makini na hizo sheria wanazokusudia kutumia, na kuwa hakutoa mwanya wa jambo kama hili kutumika dhidi yake.
na sisi tutamwekea mgombea wao zanzibar hana sifa ya kugombea
 
Katika taarifa ya habari ya TBC1 saa mbili usiku huu, makamu mwenyekiti wa CCM bara Pius Msekwa amenukuliwa akisema kwamba Chadema wameanza kampeni kabla ya muda.

Kutokana na hilo, katibu wa CCM taifa, Yusufu Makamba atapeleka malalamiko yao huko tume ya taifa ya uchaguzi, yaani NEC.

Mambo yameanza. Ngoma inogile.

Mpaka sasa mimi najua CCM inafanya Kmpeni za wazi kabisa. Kwa sababu katika mikutano ile watu walikuwa pia na Tshirt zilizoandikwa" CAHGUA CCM, CHAGUA KIKWETE" na hii ni baada ya JK kuthibitisha kuwa anagombea.
Hizo ndo kampeni ambazo hata CHADEMA watawafunga vema CCM kama watawashitaki

waondoe hofu na waguate sheria tu!
 
WanaCCM wakati wa mabadiliko umefika...
Msikubali kuendelea kuburuzwa na kundi la wachache kwa manufaa yao..
Sote tu waTanzania fanya lililo sahihi sasa..
Chagua Chadema..ili Dr SLAA awe Rais wa Tanzania yenye matumaini mapya..

Waambie watu wote waelewe!

Matumaini yanakuja hata kama polepole
 
Nadhani NEC ya CCM hawatathubuti kumzuia Dr Slaa manake kiama chake hawatasahau milele wakiwa wafu,Nguvu ya UMMA usicheze nayo bwana ,Msekwa Koma ukomae na ujinga wako,tuachie nchi yetu iliyosalama,tokemea nje ya ulingo wa siasa kama umechoka
 
WanaCCM wakati wa mabadiliko umefika...
Msikubali kuendelea kuburuzwa na kundi la wachache kwa manufaa yao..
Sote tu waTanzania fanya lililo sahihi sasa..
Chagua Chadema..ili Dr SLAA awe Rais wa Tanzania yenye matumaini mapya..

Hili ndilo Pambio Kabambe lazima wana CCM waamushwe na kutakaswa mukichwa nchi yetu wote
 
Anywayz kwa malalamiko hayo CCM inataka NEC ichukue maamuzi gani?
 
Kithuku,
Mkuu kwa hili umetia chunvi kwani JK alitangazwa kuwa mgombea kabla ya Dr.Slaa na hata kuchagua mgombea mwenza wakati hatujui Chadema atamsimama nani? Nakumbuka hata Seif alisema hatishwi na kuchaguliwa kwa Dr.Shein, kwa kauli hiyo akiwa na maana tayari alikwisha chaguliwa na kujitangaza kuipambana na Dr.Shein.

Ebu rudia kusoma vizuri JF ktk mada zinazohusiana na watu hawa.

Mkuu Mkandara unayosema ni kweli, lakini ninayosema mimi pia ni kweli. Jamaa wanatapatapa na wamejiandaa tayari kumwekea pingamizi Dr Slaa. Hilo ni kweli lipo wanasubiri muda muafaka. Naona na kina Makamba wameshaanza kuuweka umma tayari ili tusishangae siku tutakaposikia hilo pingamizi, nadhani umesikia leo kuwa Makamba anasema atapeleka malalamiko kwa Tume ya Uchaguzi. Hilo atalifanya (au ameshalifanya), lakini yupo pia alieandaliwa kupeleka petition ya kisheria, mtaiona muda ukifika. Suala lililoko mbele yetu ni kujiuliza tu kama hiyo petition itakuwa na nguvu au la, na kama itakubaliwa au la, lakini wataipeleka kwa sababu imeshaandikwa tayari.

Ninaamini kuwa Dr Slaa na timu yake bila shaka wamejiandaa na hilo na wameweka utetezi wao tayari. Mimi niliangalia taarifa ya habari jana usiku baada ya kuposti hii habari hapa, Dr Slaa alizungumza kama vile anaufahamu huu mpango pia pale aliposema CCM hawajui sheria, ninaamini ana matumaini kuwa katika mpambano wa kisheria atawabwaga. Lakini watajaribu, hilo ni hakika.
 
Mpaka sasa mimi najua CCM inafanya Kmpeni za wazi kabisa. Kwa sababu katika mikutano ile watu walikuwa pia na Tshirt zilizoandikwa" CAHGUA CCM, CHAGUA KIKWETE" na hii ni baada ya JK kuthibitisha kuwa anagombea.
Hizo ndo kampeni ambazo hata CHADEMA watawafunga vema CCM kama watawashitaki

waondoe hofu na waguate sheria tu!

MKUU, TAYARI CCM WAMESHAPELEKA MALALAMIKO, HII NGOMA INAPENDEZA, TUTAONA NINI NEC WATASEMA LAKINI SITOSHANGAA WAKAJA NA MAAMUZI AMBAYO YATAWALIZA WATANZANIA WALIO WENGI, TUSUBIRI HUKU TUKIMUOMBA MUNGU AWAPE NEC WOGA WA KUTOA MAAMUZI YA UPENDELEO.
SOMA HII HABARI HAPA CHINI KWA MUJIBU WA GAZETI LA MWANANCHI
CCM yailalamikia rasmi Chadema
Katika hatua nyingine Sadick Mtulya anaripoti kuwa CCM jana iliwasilisha rasmi malalamiko ya maandishi kwa Tume ya Uchaguzi (Nec), ikidai kuwa Chadema imeanza kampeni kabla ya muda.

Hatua hiyo, imefikiwa baada ya timu ya wanasheria wa CCM juzi usiku, kukamilisha kuandaa malalamiko hayo.

Malalamiko hayo yaliyawasilishwa na ofisi ya katibu mkuu wa CCM, kitengo cha mwanasheria wa chama hicho.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, katika malalamiko hayo, CCM imesema Chadema imevunja maadili ya uchaguzi yaliyotolewa na Nec kwa ajili ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani kwa mwaka huu, yaliyotiwa saini na vyama vyote 18 vya siasa.

CCM inadai katika malalamiko hayo kuwa Chadema imetumia mwanya wa kutafuta wadhamini nchini kote, kufanya kampeni jambo ambalo ni ukiukwaji wa maadili katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

“Pamoja na mambo mengine, malalamiko ya CCM ni kuwa Chadema imetumia mwanya wa kutafuta wadhamini nchini kote, kufanya kampeni jambo ambalo ni ukiukwaji wa maadili katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu,’’ kilisema chanzo chetu.

Kwa mujibu wa Nec, maadili ya uchaguzi yaliyotiwa saini na vyama vya siasa hivi karibuni, yataanza kutumika rasmi kuanzia siku ya kwanza ya kampeni, Agosti 20 hadi kutangazwa kwa matokeo.

Akijibu tuhuma hizo juzi jijini Dar es Salaam mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania urais, Dk Willbrod Slaa alisema umbumbumbu wa CCM wa kuelewa mambo ndio uliowafanya watoe malalamiko hayo .

“CCM tumewazoea. Hawasomi sheria. Hawasomi sera za vyama vingine,” alisema Dk Slaa akifafanua kwamba ilifanya kampeni kwa mabango sehemu mbalimbali za nchi ikiwa ni pamoja na Zanzibar, lakini anashangaa wanavyozungumza juu ya madai hayo.

Hata hivyo, Dk Slaa alikiri kuwa alipokuwa mikoani kutafuta wadhamini, umati mkubwa wa watu ulimfuata na ilibidi aueleze sababu zilizomfanya aamue kuwania nafasi hiyo.

Alifafanua kwamba wao hawakuwa na mabango wala hawakuwalazimisha watu waende kuwasikiliza, ila ile hali ya wananchi kuwa na shauku ya kumsikiliza ndiyo iliyomfanya aonekane kama anafanya kampeni.

“Isitoshe, CCM hawajui sheria kwa maana kwamba sisi kama vyama vya siasa tuna wajibu wa kukutana na wananchi ili kuwaeleza sera zetu,’’ alisema Dk Slaa.

Katika hatua nyingine, CCM imesema Rais Jakaya Kikwete atarejesha fomu za kutetea kiti chake Agosti 19, siku moja kabla ya kuanza rasmi kwa kampeni, zitakazomalizika Oktoba 30.
 
Kwa mujibu wa Nec, maadili ya uchaguzi yaliyotiwa saini na vyama vya siasa hivi karibuni, yataanza kutumika rasmi kuanzia siku ya kwanza ya kampeni, Agosti 20 hadi kutangazwa kwa matokeo.
Kumbe jibu wanalo sasa wanalalamika nini.
 
MKUU, TAYARI CCM WAMESHAPELEKA MALALAMIKO, HII NGOMA INAPENDEZA, TUTAONA NINI NEC WATASEMA LAKINI SITOSHANGAA WAKAJA NA MAAMUZI AMBAYO YATAWALIZA WATANZANIA WALIO WENGI, TUSUBIRI HUKU TUKIMUOMBA MUNGU AWAPE NEC WOGA WA KUTOA MAAMUZI YA UPENDELEO.
SOMA HII HABARI HAPA CHINI KWA MUJIBU WA GAZETI LA MWANANCHI
CCM yailalamikia rasmi Chadema
Katika hatua nyingine Sadick Mtulya anaripoti kuwa CCM jana iliwasilisha rasmi malalamiko ya maandishi kwa Tume ya Uchaguzi (Nec), ikidai kuwa Chadema imeanza kampeni kabla ya muda.

Hatua hiyo, imefikiwa baada ya timu ya wanasheria wa CCM juzi usiku, kukamilisha kuandaa malalamiko hayo.

Malalamiko hayo yaliyawasilishwa na ofisi ya katibu mkuu wa CCM, kitengo cha mwanasheria wa chama hicho.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, katika malalamiko hayo, CCM imesema Chadema imevunja maadili ya uchaguzi yaliyotolewa na Nec kwa ajili ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani kwa mwaka huu, yaliyotiwa saini na vyama vyote 18 vya siasa.

CCM inadai katika malalamiko hayo kuwa Chadema imetumia mwanya wa kutafuta wadhamini nchini kote, kufanya kampeni jambo ambalo ni ukiukwaji wa maadili katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

"Pamoja na mambo mengine, malalamiko ya CCM ni kuwa Chadema imetumia mwanya wa kutafuta wadhamini nchini kote, kufanya kampeni jambo ambalo ni ukiukwaji wa maadili katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu,'' kilisema chanzo chetu.

Kwa mujibu wa Nec, maadili ya uchaguzi yaliyotiwa saini na vyama vya siasa hivi karibuni, yataanza kutumika rasmi kuanzia siku ya kwanza ya kampeni, Agosti 20 hadi kutangazwa kwa matokeo.

Akijibu tuhuma hizo juzi jijini Dar es Salaam mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania urais, Dk Willbrod Slaa alisema umbumbumbu wa CCM wa kuelewa mambo ndio uliowafanya watoe malalamiko hayo .

"CCM tumewazoea. Hawasomi sheria. Hawasomi sera za vyama vingine," alisema Dk Slaa akifafanua kwamba ilifanya kampeni kwa mabango sehemu mbalimbali za nchi ikiwa ni pamoja na Zanzibar, lakini anashangaa wanavyozungumza juu ya madai hayo.

Hata hivyo, Dk Slaa alikiri kuwa alipokuwa mikoani kutafuta wadhamini, umati mkubwa wa watu ulimfuata na ilibidi aueleze sababu zilizomfanya aamue kuwania nafasi hiyo.

Alifafanua kwamba wao hawakuwa na mabango wala hawakuwalazimisha watu waende kuwasikiliza, ila ile hali ya wananchi kuwa na shauku ya kumsikiliza ndiyo iliyomfanya aonekane kama anafanya kampeni.

"Isitoshe, CCM hawajui sheria kwa maana kwamba sisi kama vyama vya siasa tuna wajibu wa kukutana na wananchi ili kuwaeleza sera zetu,'' alisema Dk Slaa.

Katika hatua nyingine, CCM imesema Rais Jakaya Kikwete atarejesha fomu za kutetea kiti chake Agosti 19, siku moja kabla ya kuanza rasmi kwa kampeni, zitakazomalizika Oktoba 30.

Kama hawa wanasheria wana akili vizuri wangeliangalia vitu gani wamevifanya pale dodoma kwani ya Dr. Slaa ni madogo ukilinganisha aliyoyafanya kikwete dodoma. Binafsi hilo jambo mie naliangalia kwa upana zaidi ni kama delaying tactics za CCM uchaguzi usifanyike mwaka huu kwani ikiwa Chadema itakuwa summon kwa hilo jambo pia kuna swali jengine litakuja CCM wamefanyiwaje? Na hilo litapelekea wapelekane mahakamani na hapo uchaguzi utakuwa hamna mwaka huu !!! Time will tell
 
Wahenga walisema ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo, na hili ndilo jambo lililowafika CCM wao hawaoni makalio yao kuwa ni mekundu sanaaa bali wanaona ya wenzao ambayo ni mekundu kidogo tu.

Tatizo la kuwa na genge kubwa la watu wanaojiita chama cha siasa huku kila mmoja kichwani akiwa na nia ya kulinda na kuendeleza ulaji wake ndiyo hii. hawa watendaji wa CCM wanaokurupuka si kwamba hawajua kuwa makalio ya ni mekundu bali wanajua kuwa kwa kukaa kimya bila kulalama kuwa makalio ya wenzao mekundu watakuwa wanahatarisha nafasi zao kwa kuonekana hawatetei kundi na hivyo kuwa-replaced. Tabu itakuwa kwa wale wanasikiliza malalamika maana nao ni walewale wasipoonekana wanasaidia kundi pia watakuwa replaced, hivyo ni dhahiri kabisa kuwa sasa umefika wakati wa kuwa na tume huru itakayokuwa na majukumu na wajibu kwa katiba ya nchi, itakayoweka wazi kuwa watu hawa watoke kwenye, taasisi za kidini na interest groups zote wakithibitishwa na bunge baada ya kuhojiwa public.
 
Back
Top Bottom