CCM Kumtumia Tambwe Hiza Kama Muwakilishi: Ni Kudharau Mchakato wa Katiba?

CCM Kumtumia Tambwe Hiza Kama Muwakilishi: Ni Kudharau Mchakato wa Katiba?

Hapa mpaka tuchapane kwanza ndio heshima itakuwepo, hii ngonjera ya amani na utulivu ndio inasababisha wanaume wenye mimba kama Tambwe Hiza badala ya kwenda kujifunguwa anakuja kuleta porojo, i wanna kill light now.

Hv Tambwe ana tumbo kubwa kama la mkuu hapo kwenye picha yako...teh teh
 
kama wanachuo wasingezomea ningewalaumu sana...dk za mwanzo tu alizoongea tambwe hiza zinatosha kujua alienda pale kupoteza muda,bora walivyomfukuza kupisha people with serious minds waongee..
 
Lazima uamuzi huyo utakuwa umefanywa na Y. Makamba...yaani aibu tupu kwani Dk Lamwai yupo wapi labda angewasaidia?
 
CHIMO laiti ungelijua CCBRT inavyo hudumia watoto wenye vilema macho uthingethubutu kuilinganisha na ccm!huwa najiuliza dr slaa alifikiriaje mpaka kuanzisha hudumu ile pamoja na umasikini wake!hili suala la katiba mpya kwa kweli ccm wamelipokea kwa shingo upande tutarajie hila nyingi toka kwao!ila mwisho wao unahesabika
 
Ofcoz ndicho walichomtuma pale kufanya. Kuvuruga utaratibu wa watu walio serious kufanya mambo serious. Ni wazi kuwa kama kuna kitu wanachokiogopa CCM kwa sasa ni ule wasaa - japo mfupi - ambao watanzania wataupata kusikia ukweli, kutafakari kwa fikra zao sahihi bila kuingiliwa na mtu, kujadili kwa kina chanzo cha umaskini na uduni wao na namna ya kujinasua na hatimaye kuamua muskabali wao bila kubugudhiwa na mtu. Pindi wakiona kuna uwezekano wa haya kutokea, iwe ni nyumbani,ukumbini, darasani, uwanjani, msikitini, kanisani au barabarani, watatafuta tu namna ya kutibua. Ndio, wanafahamu kuwa hakuna mtanzania mwenye akili timamu, taarifa sahihi na uhuru wa kuamua anaweza kuikubali CCM walau kwa sasa. Silaha yao ya mwisho ni kuizuia kweli isifike masikioni kwa watu. Wakati fulani walitegemea sana silaha UJINGA miongoni mwa wananchi kama mtaji wao mkuu. Sasa haifanyi kazi tena. Haifanyi kazi kwasababu watu wameamua kwenda maili ya ziada kupata elimu na elimu imeongeza kasi kuwafuata. Hawaipati elimu ya kutosha shuleni, lakini mateso ya maisha wanayoyapata yamewafikirisha bwana, yamewaelimisha bwana. Ulimwengu unafunza kuliko mwalimu kwenye shule ya kata. Wametambua sasa kuwa sahani moja ya wali, fulana na kofia au upande wa khanga hautoshi kukidhi mahitaji kwa miaka mitano,achilia mbali yale ya wajukuu zao baadae. Mikatale ya ujinga imekatika. Wanatambua kwamba hawana uhuru ndani ya nchi yao. Wametawaliwa na waswahili wenzao. Mwisho wa yote ni pale watakapoijua kweli ili kweli iwaweke HURU. Kweli kuwa ipo namna ya kuondokana na ufedhuli huu wa miungu watu waliojipachika uwezo wa kuhodhi nchi na kunyonya rasilimali zake kwa manufaa yao. Kweli kuwa ipo njia ya kuwaweka kando na kurejesha uamuzi wa kesho yetu kwetu wenyewe kama Mungu atupavyo neema. Na zaidi, kweli kuwa Tanzania yenye neema inawezekana bila wao,na kiuhalisia we are better of without them! Hii ndio KWELI ambayo wanajaribu kuizuia kuwafikia wananchi. Haiwezekani kuzuia mvua kwa mikono. Ni uwendawazimu kujaribu. Mtu mwenye akili timamu hawezi kujiingiza kwenye biashara hii ya kijuha! Na ndio maana watu pekee walioweza kukubali kutwishwa kibarua hicho ni mfano wa akina TAMBWE hiza. Mzigo mzito mpe mnyamwezi, zigo la aibu mpe Tambwe. 😛layball:
kama wanachuo wasingezomea ningewalaumu sana...dk za mwanzo tu alizoongea tambwe hiza zinatosha kujua alienda pale kupoteza muda,bora walivyomfukuza kupisha people with serious minds waongee..
 
Unamaanisha nini kusema serious mkuu?.vigezo vp umetumia kujua huyo hakua serious.
Kwa hiyo tunatunga katiba ajili ya maserious na hao wengine.
Main point is just wha..wha...what do you mean by serious?@mshindo
 
Ni utani mkubwa sana kuona watu kama akina Tambwe Hiza ndio washauri wakuu juu ya hatima yetu kitaifa juu ya Katiba huyu wanasheri wetu waliobobea katika fani yao wakiwekwa pembeni kiushauri.
 
Watu serious hasa kwa mazingira yale ya kuzungumzia mswada kuundwa katiba mpya na wala si viraka ni wale wanaozungumza pale wakiwa na picha kubwa wa maslahi ya umma wa Tanzania badala ya kufikiri kwa kupitia tumboni kutetea misingi ya maslahi binafsi.

Mjumbe swali nyingine???

Unamaanisha nini kusema serious mkuu?.vigezo vp umetumia kujua huyo hakua serious.
Kwa hiyo tunatunga katiba ajili ya maserious na hao wengine.
Main point is just wha..wha...what do you mean by serious?@mshindo
 
nimeshangazwa sana na taarifa za kuahirishwa kwa mkutano wa kukusanya maoni kuhusu muswada wa Katiba mpya pale Karimjee. Kwamba mkutano ule umeahirishwa (ITV news, saa 2 usiku) baada ya mtu asiyekubalika CCM wala upinzani, Tambwe Hiza kuchafua hali ya hewa ukumbini.

Lakini najiuliza: katika wakati ambao taifa linashughulikia suala muhimu kama la Katiba ya nchi, CCM inakosa mtu muhimu kweli wa kumtuma kama muwakilishi hata wamteue mtu kama Tambwe Hiza?

Hivi kweli CCM wako serious? Mtu wa propaganda anaweza vipi kuwa muwakilishi wa chama tawala kwenye ishu sensitive kama Katiba ya nchi? Where is CCM taking us? Ama mimi sielewi maana ya propaganda?

Tuwafanye nini hawa CCM?


Tangu lini ccm walikuwa serious? P'se tell me.
 
@ yaa mkama P. Umeongea yale mawazo yangu khasa, maana nakwambia nina wasi wasi mkubwa ikiwa itatokea siku chadema wakawa wanaongoza serikali itakua haruhusiwi mtu hata kukohoa labda yule wa aina yao.

Halafu ukitaka kujua kua wanafunzi wa vyuo vya tanzania kua ni vilaza frm udsm,udom etc. Angalia tu, vipi aje mbunge kutoka mwituni hukoo loliondo aje awashawishi kufanya ujinga na wao wanakubali bila kuhoji. Kweli hao wanastahiki kuitwa wana chuo? Tena udsm? Aibu tupu.
 
Kila mtu ana haki ya kutoa maoni ni aibu kwa wajinga wale wa udsm pale karim jey kutokumpa nafasi tambwe ya kuongea. Ni ujinga mkubwa wa hawa vilaza wa udsm. Kwa vile wengine ninao pamoja nitajaribu kuwaelimisha kua hata tambwe anahaki ya kutoa maoni si dr slaa tu.

Akiongea lipumba wekeni fujo basi muone tutakavo watafuna kama keki. Kudadeki ccm inawalea sio sisi hatutowaacha wehu wakingia ktk anga zetu.

Mbona wewe ndio unaonekana kama mwehu...(Sifa za Mwehu Huongea peke yake) wewe hujui hata unaetaka kupambana nae!!! au waogopa taja huu ndio wakati wake...

CUF ndio inalelewa na CCM hadi imevishwa pete ya uchumba..

katika anga zenu ndio historia inasema CUF walishaingiza majambia yakakamatwa Dogo vita ya Majambia na mapanga ilishapitwa zamani enzi hizo...Au Tindikali bado mwaziwazia?? Utapigwa na Silaha za Moto... Sikulaumu ila Ukikua Utaacha na utaelimika Kasome kwanza... Usije teketezwa.
 
CCM wameanza mambo ya katiba kwa guu baya saaaannaa!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom