CCM Lumumba zimejaa Toyota Landcruiser mkonga nje za Wenyeviti wa mikoa. Ni vema CHADEMA wakajifunza matumizi mazuri ya ruzuku

Link CCM imetumia hela yake yenyewe, CCM ilifilisika ilishindwa kulipa mshahara siku ya pili mkuu aliamuru mshahara ilipwe na vyombo vya habari viboreshwe na mungu alitenda.
 
Ya kwamba ni sera isiyoandikwa ila inatekelezwa kwa ukamilifu kabisa
 
I don't know about the Rest but kutumia ikulu Kwa vikao sidhani kama ni tatizo, besides Chama Chao ndio kinaongoza nchi Kwa SASA... unataka ikulu itumiwe na Nani jamani!?... usisahau kwamba Wana ccm no Watanzania pia..vitu vingine tusiwalaumu Sana..they earned it... wangekua wanaenda ikulu na kuondoka na furniture tungelaumu..lakini wakienda kuteta na chairman wao tusifsnye kuwa issue...what is the point of being of the Ruling party kama huna access ya state House !? Mimi hiyo naona ni privilege ambayo vyama vingine vinabidi viipiganie.
 
wewe ni wale wale tu,Kuna tofauti kati ya kazi za chama na kazi ya nchi,na kuna tofauti kati ya mali za chama na mali za umma,kutawala nchi siyo sababu ya kutumia mali za umma kwa shughuli za chama,chama kinapewa ruzuku,kinapaswa kutumia pesa hiyo kufanya shughuli zake,unachosema wewe ni kuwa kwa kuwa wewe ni meneja au director somewhere na baba wa familia kwa hiyo unaweza kutumia resources za ofisini kwako kufanya kazi za familia yako.too unprofessional
 
Wazo zuri ila maendeleo yana chama ni elimu ndogo tu kulijua hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiki si kipaumbele cha ccm,kipaumbele chetu ni kubaki madarakani iwe kwa hiari au kwa nguvu
 
CCHADEMA na vyama vingine vya siasa vimeanza rasmi shughuli za siasa 1993 wakati CCM imeanza 1954 kabla ya hapo ilikuwa TANU na ilikuwa serikali na chama ni kitu kimoja kwa maana kwamba fedha ya serikali na michango ya wananchi vilitumika kwa shughuli za chama kama kujenga ofisi za chama na viwanja mbalimbali vya mpira hivyo kwa fedha za ruzuku ni ngumu kwa vyama vya upinzani kuwa na rasilimani kama za CCM. Labda tuseme ruzuku zao zitumike angalau tuone vitu vyenye thamani na ruzuku walioipata
 
Hivi unakumbuka kuwa chadema walipoweka picha za ford ranger zilizonunuliwa na chama mlikuja na kauli kuwa ni mradi wa mbowe kula ruzuku?
 
Kwani ruzuku ya ccm ni sawa na chadema ni sawa? hujengi shaka hii hali ya kunatana kati ya ccm na serikali wakati taasisi2 tofauti? ila asante kwa tarifa
 
Yaani Chadema wanafanyia kazi ofisi yao Kama kachoo hivi Tena ka village huko alafu unawaambia wanunue gari kweli???
 
..kwanini CCM mnatumia magari ya kifahari wakati kuna wanafunzi wengi wanakaa sakafuni, na shule hazina vyoo?
Ha haha! Umenikumbusha mbunge wao mmoja wa jimbo la Ukonga na niwaziri, aliulizwa na mwananchi wake wa huko kuhusu barabara mbovu.
Jibu lake likawa "kunywa bia wewe! achana na mambo ya barabara"


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kapicha basi
 
..59 billion + ruzuku 14.4 billion = 73.4 billion.

..viongozi wa ccm wasingekuwa walafi na wabinafsi wanachama wa kawaida wangeweza kupata ahueni ktk maisha yao.
Nitajie mwanachama mmoja wa CCM aliyepigika bwashee!
 
Nitajie mwanachama mmoja wa CCM aliyepigika bwashee!

..bilioni 73.4 mnafanyia nini?

..madiwani wenu wa morogoro wamekomba fedha zote zilizolengwa kuwapa mikopo wanawake na vijana.

..mnapata fedha nyingi sana, lakini matumizi yake hayaeleweki.
 
..bilioni 73.4 mnafanyia nini?

..madiwani wenu wa morogoro wamekomba fedha zote zilizolengwa kuwapa mikopo wanawake na vijana.

..mnapata fedha nyingi sana, lakini matumizi yake hayaeleweki.
Tembelea miradi ya chama bwashee utajifunza mengi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…