CCM Lumumba zimejaa Toyota Landcruiser mkonga nje za Wenyeviti wa mikoa. Ni vema CHADEMA wakajifunza matumizi mazuri ya ruzuku

Kufanyia Kufanyia ikulu Kunapunguza gharama
Msafara wa mwenyekiti wa chama hasa walinzi na vitu vingine havigharamiwi na chama kwasababu wale wanamlinda rais popote alipo na gharama hazibebwi na Chama.
Sasa kama wakifanyia ikulu wanapunguza gharama kwa nchi ni jambo Jema.
Piga hesabu gharama za msafara wa rais, Makamu wa rais na waziri mkuu.
Halafu njoo kwa wananchi watakaosimamishwa barabarani ili kupisha misafara Hiyo jumlisha masaa yao kwa ujumla ni uzalishaji kiasi gani utakua umesimama.
Kufanyia Ikulu naona inatupunguzia gharama na Bugdha wananchi.
Wafanyie tu Ikulu kwakweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza mgejenga ofisi maanake hamna kabisa ofisi ktk nchi hii. Pili, nina uhakika kuwa hayo magari yalinunuliwa kwa pesa zetu mlizoiba hazina.

Mwisho lkn sio kwa umuhimu, nina uhakika hayo magari hata hayakulipiwa ushuru wakati yanaingizwa humu nchini.

Nyie ni wezi tu hamna lolote na hilo kila mtu anaelewa ila iko siku mtajibu. Leo Kanu haina hata ofisi.
 
Nanusa harufu ya ile 1.5 T .. tunaibiwaaa!!
 

Hizo gari zimeninuliwa kwa fedha za matajiri ambao wamekuwa wakilazimishwa kutoa fedha kila ufikapo uchaguzi mkuu.
 
Umesahau kuwa chadema kazi yetu ni kupenda vitu vizuri? Kama vile kukodi helkopta, kukodi kumbi xa bei kubwa! Na kugawana 10%? Jamaa katuambia ukweli ! Tujitathimin.
 
Umesahau kuwa chadema kazi yetu ni kupenda vitu vizuri? Kama vile kukodi helkopta, kukodi kumbi xa bei kubwa! Na kugawana 10%? Jamaa katuambia ukweli ! Tujitathimin.
Kakuambia wewe mwanachadema labda,Ila kwanza kufikiria kwamba hapa mtu kachukua 10% kwa kila kitu kilichofanywa ni mawazo ya kimaskini,.pili mkutano gani ufanyike wapi na katika mazingira gani inategemea na level ya concentration unayotaka kulingana na umuhimu wa jambo husika.Kwa mfano serikali ya awamu ya tano kuamua vikao ,seminar na washa zote kufanyikia ofisini,ukiwa masikini utadhani ni uamuzi sahihi sana ila kiukweli ni uamuzi wa hovyo uliotokana ama umasikini wa fikra au ukosefu wa exposure maana si tu unapunguza tija bali pia unaua uchumi wa nchi kwa kupunguza mzinguko wa fedha
 
Hizo sababu zote zinatikana na matumizi mabaya ya ruzuku na kuongozwa na unprofessional leaders,ile tu kuwa rais wa nchi ndiye awe mwenyekiti wao ni kurahisisha utekelezaji wa sera yao ya wizi wa mali za umma baada ya kuona mchwa wanakula ruzuku kwa kasi ya ajabu.otherwise mwenyekiti si lazima ndo awe rais
 
Na wewe kwako nje kumejaa nini Madimbwi ya maji machafu yaliyotuama, baada ya mvua kunyesha na kufanya mazalia ya mbua kuongezeka.
 
hizo gari unauhakika gani kama pesa yake imetokana na ruzuku ama wanatumia gari za serikali
 
CAG alisema kuna bilioni ngapi vile ambazo CCM hawakupeleka NSSF?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…