CCM MPs kukutana hadi usiku, MOTO!!!

Halisi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
2,802
Reaction score
614
Wabunge wa CCM wamekutana jana kuanzia saa 11 jioni hadi saa tatu usiku chini ya Mizengo Pinda, kikao ambacho tofauti na siku za nyuma, Mwenyekiti wa kikao hicho (Pinda) anaelezwa kuwapa wabunge uhuru zaidi ya kuzungumza na kuwasilikiliza badala ya yeye kuwataka waseme anavyotaka. Wabunge waliochangia walicharuka na kusema, "Hatutaacha kujadili EPA na Richmond hadi kieleweke" maana kwa sasa hizo ni ajenda za wananchi ambao wanataka majibu sahihi na hatua kuchukuliwa..... Walisema hizo si ajenda za wapinzani kama Waziri mmoja alivyosema...... Mwingine alisema CCM ina matabaka yaani, A,B na C, wakikumbushia kuhusu tuhuma za rushwa dhidi ya wabunge wa CCM Arusha ambao walituhumiwa kutoa rushwa ya Sh 400,000 na walizuiwa na CCM kugombea nafasi ya Uenyekiti mkoa na NEC kupitia mkoa. Wanasema wao bado ni watuhumiwa na walikubali maamuzi ya chama, leo hii wanaotuhumiwa kuhusika Richmond, EPA na Rada tena kwa maamuzi ya BUNGE na WAKAGUZI HALALI wanaendelea kuwa wajumbe wa vikao vya juu vya CCM ikiwa ni pamoja na KAmati Kuu, NEC na mmoja ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Chama!!!!

Kazi mwaka huu ipo....
 

Mkuu Halisi,

Heshima mbele mkuu, tupo ukurasa mmoja, nilisema kwenye dataz huko nyuma kuwa Muungwana amewapiga marufuku viongozi wa juu wa serikali na CCM kuwatisha wabunge, angalau hii italisaidia taifa maana najua kikako kijacho cha bajeti kutakuwa na moto mkali sana, ngoja tuzifuatilie kwa karibu yaaani tha dataz!
 

...Spot on!, inanikumbusha enzi za "usipowajibika ole wako, utakumbwa na fagio la chuma! "

na wasipofanikiwa kuwang'oa kwenye hizi kamati za Chama na zile za Bunge, tumekwisha!!!
 
Wengine sasa tunafungua macho na masikio na kuyaelekeza Dodoma, Bongo, Danganyika.
 
Hii itakuwa safi sana maana wabunge watapata nafasi ya kuonyesha uwezo wao. Haya mambo ya kufuata wanachosema wakubwa yalifanya wabunge wetu waonekane ni mazezete wakati akili wanazo. Ndio nikasema unaweza ukaonyesha utii kwa wakubwa wako bila kuuza uhuru wa kufikiri. Tunataka siasa za nchi yetu ziendeshwe kwa minajiri ya kushindanisha mawazo badala ya ujanjaujanja. Right step in the right direction.
 

SOURCE: http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6898
 
Aliyechokoza alikua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye badala ya kuzungumza mambo yake ya Bajeti, aliwaambia Wabunge wa CCM wajadili bajeti waache kuzungumzia mambo ya Richmond na EPA kwa kuwa hizo ni ajenda za wapinzani, na aliposema kwani wapo wabunge wa CCM wenye ajenda hizo, wakaitikia kwa sauti, "tupooooo!!!!!" na ndipo akasimama Ole Sendeka akasema, "mimi nimetumwa na watu wa Simanjiro, kuwatetea, kuna matatizo ya zahanati, shule na kadhalika, serikali haina fedha, leo kuna fedha bilioni 133 watu wamegawana kama zawadi ya birthday munasema tusizungumze!!. nitasema tu!!!" akashangiliwa sana
 

Mwanzo mzuri! Natumai wabunge hawa watatekeleza hayo wanayosema pembeni, badala ya kuwa na nidhamu ya woga.
 
Inasikitisha sana waziri badala ya kutetea maslahi ya taifa anasema EPA na richmond ni za wapinzani!kwa hiyo kumbe wapinzani ndo wanatetea maslahi ya taifa!Bora wabunge wa CCM wameamka sasa!
 

Good boy! Ole Sendeka.
Huo ndio utetezi wa wananchi tunaohitaji kuusikia,siyo kuwaziba watu midomo na kuwatisha wasiseme klichowapeleka Dodoma na kuwafanya mithili ya wanafunzi wa chekechea.
 
waziri badala ya kutetea maslahi ya taifa anasema EPA na richmond ni za wapinzani!kwa hiyo kumbe wapinzani ndo wanatetea maslahi ya taifa!Bora wabunge wa CCM wameamka sasa!

Huyu waziri ndiye wa kukamata vizuri ana kaufisadi ndani ya moyo wake. Ongera sendeka najua huyu jamaa hana mchezo
 
hivi mmemsahau mustapha mkulo mapema namna hii? ufisadi wake alipokuwa NSSF ulikuwa wa kizenji. nendeni pale mkawaulize waliokuwa naye pale. ,nadhani pesa za kampeni ya ubunge angezipata wapi?
bado safari nin ndefu. na msitegemee mengi toka bunge la dodoma, mafisadi wamejizatiti sana kuliko tunavyodhani.
 


Halafu mtu kama huyu ndo ameteuliwa kuwa waziri wa fedha ambako kuna BOT.

Si ndo atazidi kuzichota? maana wapinzani ndo wamezusha kuwa kuna hela zimechotwa...

Muungwa nakupa pole una kazi sana na hao mawaziri wako. Labda uwapeleke tena Ngurdoto.

Kaazi kwelikweli
 


bwana weye hebu tueleze ndio upi ufisadi wa kizenji?
 

Tusubiri tuone kama wabunge wa CCM watafanya kweli na kuacha kufuata mstari wa chama, maana kikao kilichopita pia tuliambiwa Bunge litawaka moto, na hatukuona moto wowote bali zilikuwa ni cheche tu za hapa na pale.

Si ajabu wameshafundwa kwamba pamoja na kuikosoa serikali, lakini msivuke mipaka na kuiharibu kabisa serikali. Tuwape siku 10 za kwanza tuone kama watakuwa na uhuru wa kweli wa kujadili kero mbali mbali za Watanzania.

Pia tunataka wajadili Kiwira na kuishinikiza serikali irudishe umiliki wa mgodi huu kwa Watanzania na pia ripoti ya madini waijadili na kuishinikiza serikali iyafanyie kazi mapendekezo yaliyotolewa haraka iwezekanavyo.
 
Sasa hivi wataamka kwa sababu tatu kubwa:

i) hakuna anayetarajia uwaziri tena

ii) ule mzuka wa umaarufu wa JK uliokuwa unatisha kila mtu umekwisha. Kwa hiyo sasa kila mtu yupo huru kusema na kumsema JK sio dhambi tena kama ilivyokuwa mwanzoni

iii) wabunge wa CCM wameona wenzao wa upinzani wanavyohusudiwa na wananchi. Hakuna mwanasiasa anayetaka kujenga uadui na wananchi. Ilifika mahala ilikuwa ni aibu kusema mimi ni mbunge wa CCM.

Nasikia pia hata mawaziri wana wakati mgumu sana huku mitaani na hasa mikoani, wananchi wanawadharau sana. Sasa yote haya yanawafanya wabunge waanze kujirudi hasa ukizingatia 2010 ipo karibu.
 
Courtesy of competitively contrasting and combative contesting courtesants.
 

Mimi bado sijawa na imani sana na hii hatua. Maana kadiri hali ninavyoiona ni kwamba chama tawala kiko juu kabisa katika mfumo wa utawala; ikifuatiwa na serikali. Bunge na mahakama vinaburutwa tu.

Labda yawezekana katika kundi la mafisadi elfu, kunaweza kutokea wenye nia njema wawili. Huwezi kujua.
 
CCM ni moja na msitegemee chochote kutoka kwenye hiyo Caucus yao. Kinachofanyika hapo ni kuwekana sawa tu na in the process kutakuwa na wapayukaji kama Sendeka et al but, mwisho wa siku business as usual mwendo mdundo....

By the way its good to see "tamaa ya fisi kumfuata mwanadamu kwa kudhani mikono yake itaanguka" keep good work na endeleeni kuishi in fantasy!
 
CCM ni moja na msitegemee chochote kutoka kwenye hiyo Caucus yao. Kinachofanyika hapo ni kuwekana sawa tu na in the process kutakuwa na wapayukaji kama Sendeka et al but, mwisho wa siku business as usual mwendo mdundo.
jamani hata kwenye maslahi ya taifa?CCM kama chama hakina kosa!ila kuna watu
ndani ya CCM wanatumia huo mwanya kufisadi!sasa waziri kweli anasema EPA ni ya wapinzani jamani!
halafu unasema Sendeka ni mpayukaji!hivi kweli wewe unaesema hivi ni mtanzania au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…