GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,880
- 11,134
Wanabodi, Mimi ni mwana ccm na nilitoa hapa ushauri kwenye uzi huu Uchaguzi 2020 - CCM msimjibu Tundu Lissu, Mnavyomjibu ndio anazidi kuongea mengi
Mkutano wa Tundu lissu Tunduma ni dhahiri jinsi viongozi wa CCM wanavyomjibu majukwaani ndivyo watu wanazidi kuhamasika na kumpenda zaidi Tundu lissu
Hoja nyingi za Tundu Lissu hazijibiki kirahisi na hata wanaojibu wanaacha maswali zaidi kuliko majibu mbele za wananchi
Majibu ya hoja za Tundu Lissu sasa yanasababisha watu wanaosikiliza kampeni za CCM kutafuta habari za upande wa Chadema, Kitendo cha viongozi kumuongelea Lissu imepelekea Wanaccm kuanza kumsikiliza Tundu Lissu na kujaa kwenye kampeni zake huko Tunduma
Mosi, Hoja ya uwanja wa ndege kujengwa Chato na Mbuga ya wanyama kuanzishwa huko ,Lisu anahoji mikataba na ni nani aliidhinisha bungeni uwanja kujengwa Chato na pesa hizo ni za nani? Tenda ya ujenzi ilitangazwa wapi na ni nani kapewa tenda hiyo, Kigezo gani kilitumika kumpa Tenda mkandarasi huyo,Huyo mkandarasi ana mahusiano gani na mamlaka?
Pili, Hoja ya mishahara ya watumishi wa Umma, Tundu Lissu anahoji ni sheria ipi imetumika kuwanyima nyongeza ya mishahara walimu na kada zingine,Anahoji majibu ya Mamlaka kuwa hawaongezi mishahara wapo bize na reli,stiglers gorge na barabara,Anahoji watu wa Jeshi la police nao wameumia hawajaongezewa pesa kwa miaka mitano.
Tatu, Anahoji TRA kama wakusanya mapato kupeleka Bank TRA notes za kuzitaka mabenki kufreeze au kumark account za wateja No debit (kuzuia akaunti za wateja pesa isitoke) bali wazitume TRA kiasi cha pesa chochote kilichopo na kinachoingia kwa wakati huo, Anahoji hali hii imepelekea wafanyabiashara kuwa maskini wa kutupwa na kushindwa kuajiri watu
Tundu Lissu anahoji, Maisha ya wakulima anaongelea mazao ya korosho na mahindi watu kuzuiwa kuuza nje kwa bei nzuri na kuambiwa walime kwa ajili ya chakula,Anahoji maisha magumu ya wakulima wa pamba na korosho kutolipwa pesa zao
Tundu Lissu anahoji sheria za utakatishaji pesa na uhujumu uchumi zinavyotumika kukandamiza watu na kutoa hofu kwa wananchi ambao ndio wenye nchi yao,Anahoji yeyote anayepinga serikali anafunguliwa kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji pesa
Tundu Lissu anahoji mifumo ya elimu na ajira hasa maisha ya vijana waliomaliza vyuo kutoajirika
Nini kifanyike kujibu hoja hizi
Ni vyema CCM kama chama kikajikita kwenye sera zake na ilani ya chama,Majibu ya hoja hizi yamezidi kuzaa hasira kwa wananchi
CCM isijibu hoja hizi, Majibu ya hoja hizi kwa week moja hii yameongeza hasira kwa wananchi. Tundu Lissu anazidi kuwaelimisha wananchi hata mambo ambayo hawakuyajua
Tundu Lissu amegeuza kampeni zake kama darasa la kufundisha na kutoa elimu bure kwa wananchi kwa mambo yanayoendelea na wananchi wanamuelewa na kuwa na hasira juu ya CCM
Kwa sasa taarifa zake mitaani ndizo zinazoongeleka zaidi na kutafutwa na kila mwananchi ,Watu wanajadili hoja za lisu mitaani na kuzifurahia
Uchaguzi huu utufundishe wana ccm ni bora kuwaacha watu waongee ya moyoni kuliko kuwafungia,Mpaka sasa tangu mwaka waliofungiwa wangekuwa hawana hoja ya kuzungumza
Ccm ni wakati muafaka wa kujikita kwenye ilani na malengo yetu ya chama,Tuhubiri sera na ilani yetu,Yale tuliyokosea tukubali makosa na kujisahihisha
Mkutano wa Tundu lissu Tunduma ni dhahiri jinsi viongozi wa CCM wanavyomjibu majukwaani ndivyo watu wanazidi kuhamasika na kumpenda zaidi Tundu lissu
Hoja nyingi za Tundu Lissu hazijibiki kirahisi na hata wanaojibu wanaacha maswali zaidi kuliko majibu mbele za wananchi
Majibu ya hoja za Tundu Lissu sasa yanasababisha watu wanaosikiliza kampeni za CCM kutafuta habari za upande wa Chadema, Kitendo cha viongozi kumuongelea Lissu imepelekea Wanaccm kuanza kumsikiliza Tundu Lissu na kujaa kwenye kampeni zake huko Tunduma
Mosi, Hoja ya uwanja wa ndege kujengwa Chato na Mbuga ya wanyama kuanzishwa huko ,Lisu anahoji mikataba na ni nani aliidhinisha bungeni uwanja kujengwa Chato na pesa hizo ni za nani? Tenda ya ujenzi ilitangazwa wapi na ni nani kapewa tenda hiyo, Kigezo gani kilitumika kumpa Tenda mkandarasi huyo,Huyo mkandarasi ana mahusiano gani na mamlaka?
Pili, Hoja ya mishahara ya watumishi wa Umma, Tundu Lissu anahoji ni sheria ipi imetumika kuwanyima nyongeza ya mishahara walimu na kada zingine,Anahoji majibu ya Mamlaka kuwa hawaongezi mishahara wapo bize na reli,stiglers gorge na barabara,Anahoji watu wa Jeshi la police nao wameumia hawajaongezewa pesa kwa miaka mitano.
Tatu, Anahoji TRA kama wakusanya mapato kupeleka Bank TRA notes za kuzitaka mabenki kufreeze au kumark account za wateja No debit (kuzuia akaunti za wateja pesa isitoke) bali wazitume TRA kiasi cha pesa chochote kilichopo na kinachoingia kwa wakati huo, Anahoji hali hii imepelekea wafanyabiashara kuwa maskini wa kutupwa na kushindwa kuajiri watu
Tundu Lissu anahoji, Maisha ya wakulima anaongelea mazao ya korosho na mahindi watu kuzuiwa kuuza nje kwa bei nzuri na kuambiwa walime kwa ajili ya chakula,Anahoji maisha magumu ya wakulima wa pamba na korosho kutolipwa pesa zao
Tundu Lissu anahoji sheria za utakatishaji pesa na uhujumu uchumi zinavyotumika kukandamiza watu na kutoa hofu kwa wananchi ambao ndio wenye nchi yao,Anahoji yeyote anayepinga serikali anafunguliwa kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji pesa
Tundu Lissu anahoji mifumo ya elimu na ajira hasa maisha ya vijana waliomaliza vyuo kutoajirika
Nini kifanyike kujibu hoja hizi
Ni vyema CCM kama chama kikajikita kwenye sera zake na ilani ya chama,Majibu ya hoja hizi yamezidi kuzaa hasira kwa wananchi
CCM isijibu hoja hizi, Majibu ya hoja hizi kwa week moja hii yameongeza hasira kwa wananchi. Tundu Lissu anazidi kuwaelimisha wananchi hata mambo ambayo hawakuyajua
Tundu Lissu amegeuza kampeni zake kama darasa la kufundisha na kutoa elimu bure kwa wananchi kwa mambo yanayoendelea na wananchi wanamuelewa na kuwa na hasira juu ya CCM
Kwa sasa taarifa zake mitaani ndizo zinazoongeleka zaidi na kutafutwa na kila mwananchi ,Watu wanajadili hoja za lisu mitaani na kuzifurahia
Uchaguzi huu utufundishe wana ccm ni bora kuwaacha watu waongee ya moyoni kuliko kuwafungia,Mpaka sasa tangu mwaka waliofungiwa wangekuwa hawana hoja ya kuzungumza
Ccm ni wakati muafaka wa kujikita kwenye ilani na malengo yetu ya chama,Tuhubiri sera na ilani yetu,Yale tuliyokosea tukubali makosa na kujisahihisha