CCM na Mgogoro wa Kidini Tanzania

CCM na Mgogoro wa Kidini Tanzania

Mkuu Mchambuzi,
Nilipendelea sana kuiangalia mada yako kwa mtazamo mpana, hata hivyo ikibidi nitakuwa naingiza specifics pengine kuleta maana zaidi ya kile nilichokusudia.

Siku za nyuma mtu alikuwa akiitwa mdini ni tusi na kosa. Tuliona viongozi wa dini wakiweka mipaka ya ndimi zao, mafundisho na vitendo katika ulingano. Na kama ulivyosema ujaama ulijaribu sana kuweka hali ikaonekana kuwa sote tulikuwa na adui wakubwa akina ujinga, maradhi na umasikini. Hili umelieleza vema na nisingependa kulirejea.

Uliberali unatoa fursa ya kila kitu kuwa huru na kuamuliwa na soko. Ni nguvu hiyo ambayo tumeipokea bila matayarisho imetufikisha hapa tulipo. Tukakurupuka kuondoa miiko ya uongozi ambayo ilisaidia sana katika vetting ya viongozi bora.
Tukaruhusu kila mtu kuanzisha dhehebu au dini yake kwasababu huo ndio msingi wa uliberali na kwamba nguvu ya soko ndiyo inayoamua.

Kwa kuondoa miiko ya uongozi na maadili ambazo zilikuwa ni thamani zetu '' value'' nguvu ya mfumo wa kiliberali ikachukua mkondo wake. Kwa vile nguvu hiyo huamuliwa na soko, ni soko hilo hilo likawavuta viongozi wa kisiasa. Kwamba, ili wapate uongozi ni lazima waiitike nguvu ya soko ambayo tayari imeshachafuliwa na wajinga wachache.
Ndipo viongozi wakafuata msemo'' if you can't beat them join them.

Viongozi wanaopatikana kwa njia hiyo hawawezi kusimama na kukemea udini kwasababu udini ndiyo nguvu ya soko iliyowapa ulaji. Hapa ndipo tunaona sehemu muhimu kama bunge ikigawanyika kwa misingi ya udini.
Huwezi kuwa na serikali imara ukishakuwa na bunge la hovyo.

Lakini si bungeni, hata kwenye vyama kila mtu anaangalia nguvu ya soko. Ni kwa msingi huo hata chama tawala kimebaki kutoa statement ambazo hazionyeshi suluhu bali kutaka kupendeza kila mmoja.
Yote haya ninaweza 'wrap up'' kwa hoja kuwa uongozi uliopo ni dhaifu sana na umeacha mianya mingi ikiwa ni pamoja na kutupa thamani za taifa.

Leo ukiwauliza sisi kama taifa ni thamani zipi zinatuweka pamoja, wote watakimbia amani na utulivu.
Na kama ulivyosema hawajui kuwa hivyo viliundwa havikuremeka kama mvua. Hawajishughulishi kujiuliza tatizo liko wapi wamebaki kupiga porojo. Hakuna, si ndani ya chama tawala, serikali au bunge. Ikifika hapo ujue kuna tatizo tena kubwa.

Kuhusu maswali yako kwa scramble labda tumpe nafasi ayajibu ili pengine tuone mtazamo wake tofauti.
Kitu kimoja ninachotaka kusema ni kuwa suluhu ya tatizo iangaliwe kuanzia mzizi yake na wala si dalili.

Scramble ameorodhesha mambo mengi, moja ya hoja zake ni ile ya 6 kuhusu ajira za umma.
Scramble anasahau kuwa ajira za umma katika mfumo wa free market ni kitu kidogo sana.

Katika mfumo wa uliberali ni nguvu ya soko tu itakayoamua. Itafika siku kutakuwa na malalamiko makampuni yanaajiri wakristo wengi. Watu watakuwa wamesahau kuwa ni nguvu ya soko inayoamua si watu kama ilivyokuwa nyakati za ujamaa. Tena nguvu hiyo inaweza kuamua ajira apewe Mkenya, Mmalawi n.k.

Nikidokoa hoja moja ya Mchambuzi, kiini cha tatizo ni historia ya ukoloni kuanzia kwa mwarabu hadi mwingereza.
Kila ukoloni ulikuja na mizigo yake na kutuacha na faida au matatizo.
Athari za ukoloni zimekuwa katika nyakati tofauti zikiathiri jamii fulani kwa nyakati fulani.

Elimu inatumika kama kisingizio kwasababu tunajua kuwa kuna jamii zilifanikiwa sana siku za nyuma kwa mambo mengine hata kama si elimu.
Kwahiyo naweza kusema kiini cha mzozo siyo elimu, NECTA n.k. pengine tatizo ni matumizi ya elimu. Niachie hapa kwanza!
 
..........chama tawala kimebaki kutoa statement ambazo hazionyeshi suluhu bali kutaka kupendeza kila mmoja............

.....hilo hapo juu ni tatizo kubwa sana na hasa kwa Rais JK.......juzi kwenye hotuba yake ya mwezi.....katika ku-address matatizo ya udini......badala ya kutoa suluhu yeye akaanza kutoa/kusema lawama........mara oohh vitabu vilikojolewa.....mara oohh makanisa yaliyochomwa......Kama Rais anatakiwa kuchukua msimamo mkali kwa jamii anayoiongoza bila kujali dini......aseme wale wote walioleta fujo/vurugu watachukuliwa hatua kali za kisheria......na kuonya vitendo vya uchochezi kuwa havitavumiliwa......kila mtu aabudu kwa uhuru wake bila kuchokonoa dini ya watu wengine......vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya huyo mtu au kikundi/vikundi.........



.......................Katika mfumo wa uliberali ni nguvu ya soko tu itakayoamua. Itafika siku kutakuwa na malalamiko makampuni yanaajiri wakristo wengi. Watu watakuwa wamesahau kuwa ni nguvu ya soko inayoamua si watu kama ilivyokuwa nyakati za ujamaa. Tena nguvu hiyo inaweza kuamua ajira apewe Mkenya, Mmalawi n.k................

Siku zote nawaambia wanangu......ulimwengu huu hauna huruma....usione mwenzio anakula, kuvaa na kuishi vizuri ukamtazama kwa jicho la husuda.....fanyeni juhudi shuleni ili walau minimum level yenu ya education iwe kama ya kwangu au mama yenu.....

.......Ndgu zangu Waislamu tuache kuficha nyuso zetu mchangani.......mapinduzi ya elimu katika jamii yetu yatatokana na juhudi zetu za kuwahimiza vijana wetu kusoma kwa kwa bidii......matokeo yanaweza yasiwe Generation yetu lakini inabdi tuanze sasa......hakuna shule/chuo/ofisi itakayo chukua watu wasio kuwa na sifa......Mfano Dr. Dau.....watu hata wampige vita vipi...lakini jamaa anabakia kuwa ana sifa stahiki na ni mchapa kazi...period...ukiangalia wanae...na wenyewe mwendo mdundo.......na wana juhudi kweli kweli........na nimeona familia nyingi tu za mifano ya aina hiyo.....
 
Tofauti za kidini zitaendelea kuwepo katika mfumo wowote wa maisha yetu ya kisiasa na kiutawala. Hii ni kwa sababu dini hizi zenyewe zina uasili wa ushindani na tofauti za kimaono. Lakini kubwa ni kuwa dini hizi zote (uislamu na ukristu)zinaubiri jinsi ya kuishi hapa duniani Kama njia ya kufikia maisha ya kheri mbinguni. Jinsi gani ya kuishi hapa duniani na njia ya kueneza dini hizo ndipo tofauti zinapojitokeza.

Kwangu mimi si aina ya mfumo wa utawala wetu bali wasimamizi tuaowachagua kutuongoza wanapaswa kutuunganisha (katika tofauti zetu za kiimani) Kama taifa moja lenye Imani moja ya utaifa wetu. Tatizo tulilonalo ni kuwa watawala (Serkali na chama) wameshidwa na wana woga wa kuchukua hatua staiki zitakazohakikisha utaifa wetu unadumu. Sababu kubwa inatokana na woga wa kuodolewa katika utawala katika siasa hizi za ushindani. Lakini pia inatokana na watawala wenyewe (Kama watu binafsi) kuweka mbele Imani zao za dini kuliko ujenzi wa utaifa wetu.

Mkuu tunapoingia kwenye competitive politics ni lazima tukubali kuwa uwanja wa ushindani unaweza kuwa na sura za aina mbalimbali. Kama nchi chini ya uongozi wa CCM iliyokuwa ya TANU na ASP, tuliamua kuwa watanzania kwanza, na wakristo na waislamu baadaye. Sababu ni kuwa chama kilikuwa weka priorities za mambo wanayohitaji wananchi bila kujali dini, kabila etc etc

Kwa sasa tupo kwenye siasa za ushindani, kadi yoyote inaweza kuchezwa ili mtu apate ushindi. Kwa hiyo tunapofika wakati wa kutokuwa na sera za maana, au kujua nchi inataka nini, au hasa ikifika wakati wanasiasa wako-desperate kuingia madarakani na kuendelea na nyadhifa zao wanatumia karata yoyote.

Ukiangaliwa wabunge, madiwani na baadhi ya wanasiasa ambao wanaface electorares wenye elimu ndogo, ni rahisi kuwarubuni kwa karata ua udini. Lakini matokeo yake kama kawaida ni mabaya sana.
 
Malalamiko au manung'uniko ya upendeleo na uonevu wa serikali kwa misingi ya udini yamekuwa yakitazamwa na Serikali kwa u-rahisi rahisi.
Serikali kwa nafasi yake inapaswa kufanya yafuatayo inapotokea malalamiko ya aina hii;
1. Kama malalamiko ni ya kweli-KUCHUKUA HATUA KUREKEBISHA KASORO ZILIZOPO
2. Kama malalamiko si ya kweli-KUKANUSHA NA KUKEMEA KWA NGUVU UZUSHI WA AINA YOYOTE ULE

Bahati mbaya sana Serikali (Awamu zote zilizofuata baada ya Nyerere) haijawahi kuchukua hatua madhubuti kila mara malalamiko haya yanapotokea na matokeo yake yameanza kukubalika na jamii husika kuwa ni kweli.....na mwishowe sasa mbegu hii imeanza kuzaa chuki dhidi ya upande unaodaiwa kupendelewa. Huwezi kulalamika kuwa mzazi wako anampendelea nduguyo kwa kila kitu bila kuishia kumchukia huyo nduguyo kwa upendeleo huo!

Serikali imeshindwa kusimama katika nafasi yake kama mlezi wa wananchi wake walio na dini na wapagani na badala yake inafanya maamuzi kwa kuangalia upepo unaelekea wapi. Maamuzi yanayofuata sheria & katiba sio kila siku yatakuwa ni maamuzi yatakayopendwa na watu lakini lazima kuyasimamia no matter what! Tatizo la viongozi wetu wanapenda sana kufanya "popular decisions" ambazo mara nyingi haziko kwa mujibu wa sheria.
 
Mkuu tunapoingia kwenye competitive politics ni lazima tukubali kuwa uwanja wa ushindani unaweza kuwa na sura za aina mbalimbali. Kama nchi chini ya uongozi wa CCM iliyokuwa ya TANU na ASP, tuliamua kuwa watanzania kwanza, na wakristo na waislamu baadaye. Sababu ni kuwa chama kilikuwa weka priorities za mambo wanayohitaji wananchi bila kujali dini, kabila etc etcKwa sasa tupo kwenye siasa za ushindani, kadi yoyote inaweza kuchezwa ili mtu apate ushindi. Kwa hiyo tunapofika wakati wa kutokuwa na sera za maana, au kujua nchi inataka nini, au hasa ikifika wakati wanasiasa wako-desperate kuingia madarakani na kuendelea na nyadhifa zao wanatumia karata yoyote.Ukiangaliwa wabunge, madiwani na baadhi ya wanasiasa ambao wanaface electorares wenye elimu ndogo, ni rahisi kuwarubuni kwa karata ua udini. Lakini matokeo yake kama kawaida ni mabaya sana.
BongolanderHuku ni kushindwa, kwa sababu hata wale waliokomaa katika siasa hizi za ushindani Wana vitu au masuala ambayo ni ya muhimu na hasa yale yanayowaunganisha Kama taifa na hukuti wanaenda nje ya hayo mambo. Tatizo ni kuwa tuliingia bila maandalizi na lawama ni kwa chama tawala (CCM)kwa sababu walifikiri na bado wanafikiri kuwa wataendelea kutawala milele na misingi iliyokuwepo wakati wa TANU na CCM ya 70/80 itaendelea kudumu.Tulipaswa kuweka misingi yetu ya kitaifa ambayo kola anayeingia katika sisa anawajibika kutoikuika. Kwa mfano kwa nini turuhusu mtu apige kampeni kwa misingi ya dini au Kabila lake wakati tunajua kabisa madhara yake na tunamwacha!
 
Malalamiko au manung'uniko ya upendeleo na uonevu wa serikali kwa misingi ya udini yamekuwa yakitazamwa na Serikali kwa u-rahisi rahisi.
Serikali kwa nafasi yake inapaswa kufanya yafuatayo inapotokea malalamiko ya aina hii;
1. Kama malalamiko ni ya kweli-KUCHUKUA HATUA KUREKEBISHA KASORO ZILIZOPO
2. Kama malalamiko si ya kweli-KUKANUSHA NA KUKEMEA KWA NGUVU UZUSHI WA AINA YOYOTE ULE

Bahati mbaya sana Serikali (Awamu zote zilizofuata baada ya Nyerere) haijawahi kuchukua hatua madhubuti kila mara malalamiko haya yanapotokea na matokeo yake yameanza kukubalika na jamii husika kuwa ni kweli.....na mwishowe sasa mbegu hii imeanza kuzaa chuki dhidi ya upande unaodaiwa kupendelewa. Huwezi kulalamika kuwa mzazi wako anampendelea nduguyo kwa kila kitu bila kuishia kumchukia huyo nduguyo kwa upendeleo huo!

Serikali imeshindwa kusimama katika nafasi yake kama mlezi wa wananchi wake walio na dini na wapagani na badala yake inafanya maamuzi kwa kuangalia upepo unaelekea wapi. Maamuzi yanayofuata sheria & katiba sio kila siku yatakuwa ni maamuzi yatakayopendwa na watu lakini lazima kuyasimamia no matter what! Tatizo la viongozi wetu wanapenda sana kufanya "popular decisions" ambazo mara nyingi haziko kwa mujibu wa sheria.

Absolutely right!!....heshima mbele
 
Watawala wamesahau kuwa hii "Amani na Utulivu" ilijengwa na ina misingi yake.....sasa hivi ile misingi imewekwa pembeni badla ya kudumishwa.....halafu wananchi tunaambiwa tuvumiliane!!......watawala wanatakiwa wajue uvumilivu una Kikomo na endapo jamii fulani inapoona kero inayoihusu haziwi addressed.....addressed kwa maana ya kwamba Serikali itoe majibu.......isijifiche.......kama kuna tuhuma dhidi ya serikali ya kwamba kuna dhulma na hizo dhuluma zimeainishwa basi serikali itoe majibu ya kina.......

Serikali inashindwa vipi kutoa majibu kuhusu MoU....mbona Dr. Slaa kwa nafasi yake alifafanua.........kwa nini serikali iko kimya......yale majibu ya JK ya kwamba milango iko wazi na jamii nyingine ikitaka yaweza kuwa na MoU hayajibu tuhuma.......

Nakumbuka kipindi cha Mkapa na hata wakati wa Mwinyi.....waliwahi kutoa majibu ya tuhuma zilizokuwa zinatolewa dhidi ya serikali.......baadhi ya vikundi havikuridhika...na wakadai Mkapa (wakati wake) ni agent wa Kikatoliki na mfumo kristo...kuna wakati Mwinyi aliitwa Kafir (eti kwa kuwa alikuwa naingia Makanisani!!!...).......sasa hivi vikundi vimeendelea na mahubiri yao hadi sasa.....JK alitakiwa arejee yale majibu na atoe msisitizo wa yale majibu yaliyotolewa na Mkapa.....na kujibu tuhuma mpya........kukaa kwake kimya kunazidi kujenga chuki na hatimaye uvumilivu kufikia kikomo.........
 
Inasikitisha sana kuona kuwa tuhuma na malalamiko haya yamefikia mpaka hatua ya kuhoji historia ya nchi yetu na mapambano ya kudai uhuru...kwamba historia ya uhuru wetu imebagua dini fulani, lakini Serikali inaendelea kuchekelea mambo haya.

Huko Znz nako hali ni mbaya zaidi...ilianza minong'ono ya chini chini kuwa hawataki muungano sasa mambo yako hadharani zaidi. Mbaya zaidi kauli hizi za kuvunja muungano zinachagizwa na chuki za kidini hata kufikia kutoana uhai! Serikali na vyombo vyake vya usalama inakaa kimya haya yote yakiendelea...

Mwenyezi Mungu atusaidie kwa kweli huko tunakoelekea!
 
Bongolander
Huku ni kushindwa, kwa sababu hata wale waliokomaa katika siasa hizi za ushindani Wana vitu au masuala ambayo ni ya muhimu na hasa yale yanayowaunganisha Kama taifa na hukuti wanaenda nje ya hayo mambo. Tatizo ni kuwa tuliingia bila maandalizi na lawama ni kwa chama tawala (CCM)kwa sababu walifikiri na bado wanafikiri kuwa wataendelea kutawala milele na misingi iliyokuwepo wakati wa TANU na CCM ya 70/80.
Tulipaswa kuweka misingi yetu ya kitaifa ambayo kola anayeingia katika sisa anawajibika kutoikuika. Kwa mfano kwa nini turuhusu mtu apige kampeni kwa misingi ya dini au Kabila lake wakati tunajua kabisa madhara yake na tunamwacha!

Mkuu sasa hivi hatuwezi kusema CCM ni Chama, (kwa maana ya kuongoza nchi) isipokuwa ni kundi la watu ambalo linatumia jina la chama kuangalia maslahi yao na usalama wao. Kama ni sera au sheria kuhusu masuala ya umoja na mshikamano wa taifa ziko wazi kabisa.

Kama zingekuwa zinafuatwa na kutekelezwa tusingekuwa tunawaona watu kila siku wanaweka spika na kusema wakristo washenzi, au kusingekuwa na kusema waislamu wajinga, au wapagani washenzi. Lakini siku hizi yanasemwa wazi tena na kuwekewa spika juu. Hata ukiingia kwenye youtube unaweza kuona kuna watu ambao wanalipwa kwa kazi ya kutukana wakristo, na hawafanywi kitu. Si kama wahusika hawajui, wanajua na wanaona, why are they not doing anything? this is a thousand bucks question.

Kibaya zaidi hata kuna redio ambazo zinaleta uchochezi wazi wa kidini. Ukiangalia sheria zetu utaona wazi kuwa hazijakaa kimya, hata mwenendo wa kupiga kampeni nadhani uko wazi kabisa, haya mambo yote tuliyafikiri kama nchi na kama chama zamani sana, na tukayaweka kimaandishi.

Lakini ukisoma vizuri anachosema Mchambuzi unaweza kuona kuwa anachouliza ni, Je kwanini hatuafuati sheria zetu, ni kwanini wanaotakiwa kusimamia mambo kama haya hawafanyi kazi yao, CCM ndio chama tawala kwa sasa kwanini chama kile kile kilichowaunganisha watu wa dini, rangi na makabila tofauti, na sasa chama hicho hicho (wawakilishi wake) wawe wanazunguka na kuwafitinisha watanzania kwa kuwagawa kwa udini?

Ukianza kuangalia kwa undani kwa sasa CCM kama chama hakina uwezo wa kusimamia ilani na sera zake, na kimsingi kimeanza hata kubomoa yale ambacho awamu nyingine zilijenga. This is a fact, Wanachama wamekuwa rogue, wanatumia kila njia ya kulinda nyadhifa zao au hata njia chafu kama za udini. Kwa sasa hivi ukiangalia state of CCM ni kama chama kipo kwenye hatua ya kutafuta njia fulani ya kuboresha sura yake, lakini hakina uwezo wa kudeal na mambo kama hayo.


Kwa sasa labda Rais kwa kutumia presidential decree ndio anaweza kusimamisha vitendi vvya udini. Hata hivyo hii si njia endelevu ya kudeal na suala hili.
 
Malalamiko au manung'uniko ya upendeleo na uonevu wa serikali kwa misingi ya udini yamekuwa yakitazamwa na Serikali kwa u-rahisi rahisi.
Serikali kwa nafasi yake inapaswa kufanya yafuatayo inapotokea malalamiko ya aina hii;
1. Kama malalamiko ni ya kweli-KUCHUKUA HATUA KUREKEBISHA KASORO ZILIZOPO
2. Kama malalamiko si ya kweli-KUKANUSHA NA KUKEMEA KWA NGUVU UZUSHI WA AINA YOYOTE

Bahati mbaya sana Serikali (Awamu zote zilizofuata baada ya Nyerere) haijawahi kuchukua hatua madhubuti kila mara malalamiko haya yanapotokea na matokeo yake yameanza kukubalika na jamii husika kuwa ni kweli.....na mwishowe sasa mbegu hii imeanza kuzaa chuki dhidi ya upande unaodaiwa kupendelewa. Huwezi kulalamika kuwa mzazi wako anampendelea nduguyo kwa kila kitu bila kuishia kumchukia huyo nduguyo kwa upendeleo huo!

Serikali imeshindwa kusimama katika nafasi yake kama mlezi wa wananchi wake walio na dini na wapagani na badala yake inafanya maamuzi kwa kuangalia upepo unaelekea wapi. Maamuzi yanayofuata sheria & katiba sio kila siku yatakuwa ni maamuzi yatakayopendwa na watu lakini lazima kuyasimamia no matter what! Tatizo la viongozi wetu wanapenda sana kufanya "popular decisions" ambazo mara nyingi haziko kwa mujibu wa sheria.

Maoni yako ni sahihi kabisa. Mambo mengi yalihitaji maelezo na msimamo thabiti wa Serkali na yangeishia hapo. Lakini bahati mbaya haikufanyika hivyo kwa sababu ya kuogopa kuwaudhi watu au kundi Fulani. Matokeo yake ndiyo haya na kuwafanya baadhi ya watu kufikiria kuwa Serkali inaunga mkono hoja hizo.
 
Mkuu sasa hivi hatuwezi kusema CCM ni Chama, (kwa maana ya kuongoza nchi) isipokuwa ni kundi la watu ambalo linatumia jina la chama kuangalia maslahi yao na usalama wao. Kama ni sera au sheria kuhusu masuala ya umoja na mshikamano wa taifa ziko wazi kabisa.

Kama zingekuwa zinafuatwa na kutekelezwa tusingekuwa tunawaona watu kila siku wanaweka spika na kusema wakristo washenzi, au kusingekuwa na kusema waislamu wajinga, au wapagani washenzi. Lakini siku hizi yanasemwa wazi tena na kuwekewa spika juu. Hata ukiingia kwenye youtube unaweza kuona kuna watu ambao wanalipwa kwa kazi ya kutukana wakristo, na hawafanywi kitu. Si kama wahusika hawajui, wanajua na wanaona, why are they not doing anything? this is a thousand bucks question.

Kibaya zaidi hata kuna redio ambazo zinaleta uchochezi wazi wa kidini. Ukiangalia sheria zetu utaona wazi kuwa hazijakaa kimya, hata mwenendo wa kupiga kampeni nadhani uko wazi kabisa, haya mambo yote tuliyafikiri kama nchi na kama chama zamani sana, na tukayaweka kimaandishi.:lying:

Lakini ukisoma vizuri anachosema Mchambuzi unaweza kuona kuwa anachouliza ni, Je kwanini hatuafuati sheria zetu, ni kwanini wanaotakiwa kusimamia mambo kama haya hawafanyi kazi yao, CCM ndio chama tawala kwa sasa kwanini chama kile kile kilichowaunganisha watu wa dini, rangi na makabila tofauti, na sasa chama hicho hicho (wawakilishi wake) wawe wanazunguka na kuwafitinisha watanzania kwa kuwagawa kwa udini?

Ukianza kuangalia kwa undani kwa sasa CCM kama chama hakina uwezo wa kusimamia ilani na sera zake, na kimsingi kimeanza hata kubomoa yale ambacho awamu nyingine zilijenga. This is a fact, Wanachama wamekuwa rogue, wanatumia kila njia ya kulinda nyadhifa zao au hata njia chafu kama za udini. Kwa sasa hivi ukiangalia state of CCM ni kama chama kipo kwenye hatua ya kutafuta njia fulani ya kuboresha sura yake, lakini hakina uwezo wa kudeal na mambo kama hayo.


Kwa sasa labda Rais kwa kutumia presidential decree ndio anaweza kusimamisha vitendi vvya udini. Hata hivyo hii si njia endelevu ya kudeal na suala hili.

Naam umenena na hakika hii inathibitisha kuwa hatukujiandaa tulipoingia katika mfumo wa vyama vingi. Tungekuwa tumejiandaa na kuweka taasisi imara CCM wangepaswa kukemewa na kudhibitiwa walipokuwa wanatupeleka huku tuliko sasa katika masuala ya udini. Wanasiasa wanahitaji kudhibitiwa na mifumo imara.
 
Bongolander, Mwalim na Ogah
Kwasasa CCM imepoteza maana ya chama cha siasa. Hili limebaki kuwa genge la watu wanaotaka kumiliki utawala wa nchi na si kuongoza nchi. Haya matatizo na mengine mazito yalishawahi kutokea huko nyuma.
Tofauti na sasa CCM na watangulizi kama TANU walikaa na kuliangalia tatizo kama tatizo.

Kwa vile CCM imegeuka na kuwa genge na hakuna mtu anayethubutu kusimama na kusema kwa masilahi ya taifa.
Nia aibu sana wabunge wa chama tawala wakiwa wamegawanyika katika makundi ya udini.
Hii ni aibu inayothibitisha kuwa ule utashi wa kisiasa ''political will'' hakuna imebaki bora siku ziende.

Upungufu ndani ya CCM haukutokea kwa bahati mbaya. Ni mtiririko uliofuata udhaifu wa serikali iliyopo madarakani.
Tatizo la udini lilionekana na hakik si kubwa kama inavyoonekana.
Ni kubwa kwasababu wendawazimu wachache wameachiwa kutenda wafanyavyo ili lionekane kubwa.

Kuhusu suala la serikali kukemea, kanusha au kukubali madai hilo ni matokeo ya udhaifu wa uongozi ndani ya chama na serikali iliyopo madarakani. Watakaaje kuliongelea tatizo huku tayari wakiwa katika mgawanyiko wa udini?

Pamoja na udhaifu huo mimi ningeshauri kuwa ili kuwepo na uwajibikaji si vema serikali ikakimbizana na watu wachache wajinga. Nashauri dini ziunde jumuiya zao na serikali iwasiliane na viongozi wa dini hizo tu na si kila kikundi cha kichochoroni.

Hapa ndipo nasema serikali vunja BAKWATA, waache waislam waunde jumuiya yao na mkuu wa jumuiya hiyo ndiye awe responsible kwa kila jambo na tukio.
Nasema waislam kwasababu wakristo wana TEC na CCT ambazo hadi sasa zina nguvu sana kuliko wahubiri wafanyabiashara mitaani.

Lakini na sisi wananchi tunasehemu yetu. Kwanini tulumbane na tusiwabane viongozi? Kama hawawezi kusimamia umoja wa kitaifa sisi wananchi bila kujali itikadi zetu tusimame na kuwataka waondoke madarakani.
Hatuwezi kusubiri kuona watu wanauawa kila siku kwa matukio ya kijinga tukisubiri miaka 5.

Leo JK angesikia wananchi wanamtaka ampishe mwenye uwezo sidhani angefanyia mzaha jambo la hatari kama hili.
Kinachomfanya asijali ni kuelewa kuwa mwaka 2015 ndio ataondoka ikulu.

Kwa wenzetu kama south Africa rais angepata ''recall '' kutoka chama chake mambo yanaisha nchi inasonga mbele.
Hivyo sisi ni sehemu ya tatizo kwasababu tumeachia tatizo kwa watu ambao ni tatizo

cc Mchambuzi
 
Mkuu nguruvi3,
Nimepotea kidogo mikoani kutazama nchi yangu Tanzania na kujifunza mawili matatu ndio maana sijarudia hoja nyingi;kuna hoja zako za bandiko la awali ntazirudia ila kwa sasa per post #32,nakubaliana na suala zima la kuvunja bakwata na kuwaachia wahusika wajiundie chombo chao huru kwa mujibu wa mahitaji yao.lakini ni rahisi kusema hivyo,ila je kwa mtazamo wako itatatua matatizo ya msingi yanayopelekea dini kuchanganywa na siasa?

Katika bandiko namba moja nilisema kwamba tatizo sio uwepo wa alternative religious institutions bali marginalization ya baadhi ya taasisi ambapo zipo zinazotambuliwa na zisizotambuliwa kwa vigezo vya kisiasa,je nini mtazamo wako juu ya hoja hii?

Vile vile mtazamo wako kwamba ukristo umeingia biashara na utapeli,je maana yako ni kwamba taasisi nje ya hizo mbili ambazo zina mou na gvnt ni sahihi kuzi marginalize as part of the solution?again in my view,tatizo sio uwepo wa kina kakobe na waumini wao au alternatine muslim institutions nje ya bakwata bali marginalization ya taasisi hizi kama nilivyojadili kwenye bandiko namba moja;hivi sasa tension kubwa ipo kwa waislamu lakini ni possible baadae msuguano ukaingia kwenye ukristo.solution in my view ni kushirikisha waumini wote nchini na taasisi zao,hata zile zinazohusisha waumini wa mizimu.natumia simu so kama sieleweki niwie radhi;ningependa kusikia mawazo yako on this one;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom