CCM na Polisi wanajisiakiaje pale wanaposikia maneno haya ya Hamza akiwasifia Raisi Magufuli na Samia?

CCM na Polisi wanajisiakiaje pale wanaposikia maneno haya ya Hamza akiwasifia Raisi Magufuli na Samia?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kitu kinachoendelea sasa ni jitihada ya Polisi na serikali kujaribu kutoa picha kwa Watanzania kwamba Hamza hakuwa mtu mzuri na Polisi ni watu wanaofanya kazi yao vizuri. Polisi na serikali hata wamekuwa wakijitahidi kuonyesha Hamza alikuwa mtu hatari angeweza kuua raia wengi kama Polisi wasingemuua, jambo ambalo watu wanajua ni uongo.

Tumesikia kauli ya Polisi kwamba Hamza alikuwa mtu wa hovyo hovyo, na kauli toka uongozi wa serikali ukisema kwamba ilikuwa lazima Hamza auwawe siku ya hilo tukio. Polisi pia wanajikita kwenye kufanya watu waone familia ya Hamza pia ni watu wabaya. Kuna kiongozi mmoja wa mtaa alipoishi Hamza alitoa kauli ya kipumbavu sana, labda aliambiwa aseme hivyo, eti inaonekana Hamza hakuwa na tabia nzuri kwa kuwa hakuna mtu aliyekuja kumripoti kwamba ana tabia nzuri!

Na sasa hata kuna propaganda kwamba Hamza alifanya alichofanya kwa msongo wa mawazo baada ya kupata hasara ya Tshs 400m, japo sijajua kwa nini kupata hasara kama hiyo kutasababisha chuki dhidi ya Polisi kama Polisi hawakuwa chanzo cha hasara yenyewe.

La kutisha ni kimya cha CCM juu ya Hamza, kada wao.

Kwa ujumla hakuna kauli toka Polisi, CCM na serikali inayogusia juu ya kwa nini Hamza aliamua alichoamua - kitu katika masuala ya kijamii tunaita cause and effect relationship; kisababishi na matokeo. Kwa nini hatusikii kauli yeyote juu ya nini kilifanya Hamza afanye alichofanya, au aamue lazima awaue Polisi wengi kadiri atakavyoweza?

Lakini huyu mtu ambae Polisi na CCM/viongozi wanataka tumone alikuwa mbaya, alikuwa na kichaa, alikuwa gaidi, alistahili kuuwawa, ndio huyo huyo ambae hapa chini anaongea akiwasifia Raisi Magufuli na Samia.

 
Hoja kubwa hapo ni kwa nini aliwashoot askari tuu!??? Kwa nini walimuua, badala ya kumshikilia akiwa hai!???
Hamza kaibiwa madini yake na Polisiccm walimuua kuficha ushahidi na Aibu kwao, sasa wameamua kuwanyanyasa wazazi wake Hamza kwa visingizio haramu vya kishamba na kishetani ni uonevu ulioje kwani wazazi wa hamza hawana uhusiano na kitendo alichofanya Hamza akiwa peke yake
 
Binadam ni viumbe wa pekee unaposhindwa kuwatendea haki hawata sita kujitoa muhanga, Serikali na jeshi la polisi wajitahidi kutenda haki.
 
Unajua polisi walikuwa na uwezo wa kumkamata yule jamaa akiwa hai,kuna siri nzito hapo kati ya Hamza na Polisi
 
Nashindwa kuelewa kwann vijana wengi was Tanzania wanapenda kushabikia uvunjaji wa sheria.Hamza kama Hamza ,aliharibu sana kufanya mahuhaji ya askari na mlinzi wa private security. Hata kama ,ni kweli tuassume hivyo.Kwann aliua askari wengine wasio na hatia.Hamza alitakiwa kufuatilia kwa ukaribu ,ikiwa ni pamoja na kufika kituo cha polisi kutoa taarifa za kuporwa Mali zake.Kwann alianza kuuwa hovyo askari?Hapo ndipo anapokuwa mharifu.Hapo ndipo anakosa utetezi ,wa watu waungwana na kubaki na watu wasio waungwana. Ambao mnamshabikia Hamza.Je,angeua ndugu zenu ambao ni askari ,mngekuwa bado mnakaa kwenye key board mnashangilia na kuiponda polisi?Hamaza kama Hamza alikosea sana.Na ilikuwa lazima auwawe.Kwa sababu alishaua wengine wasio na hatia.
 
Inaonesha unajua vizuri yaliyojiri.Kwa nini hautoi taarifa kwenye vyombo vya dola ili yafanyiwe kazi?Kurudiarudia sentensi kama hii muda wote uandikapo JF ni upunyufu!
Yamefanyiwa kazi ndiyo maana yuko lupango
 
Orodha ipo haipo!?
=====
Polisi na viongozi wengine wanatakiwa kukaa mbali na kauli ambazo si za kiweledi katika suala zito kama hili ambalo lipo katika uchunguzi. Zitolewe taarifa zinazohusu uchunguzi pekee. Familia ya Aliyesababisha tukio hili nayo ijizuie kutoa kauli ama kujibu chochote hata kama watakuwa provoked kama inavyoonekana kuwa.
 
Back
Top Bottom