CCM na Watanzania Kuweni Macho; Jamaa Anajiandaa Kuwatoka

CCM na Watanzania Kuweni Macho; Jamaa Anajiandaa Kuwatoka

Sophist

Platinum Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
4,486
Reaction score
3,408
Huu ni uchambuzi mdogo. Msingi wa uchambuzi huu ni matukio yenye shaka katika utawala na siasa za Tanzania kuanzia 2016.

Kuna muda, ndani ya kipindi hicho, wakongwe ndani ya CCM, wakiwemo Pius Msekwa na Benjamin William Mkapa, wamewahi kuonya. Kwamba haifai kwa mtu mmoja ndani ya CCM kujitangazia kuwa ni maarufu zaidi kuliko chama chake kilichompatia fursa ya uongozi.

Wakongwe hao waliona hatari kwa Chama chao siku za usoni. Waliogopa madhara ya kisiasa, kama ilivyowahi kutokea nchini Malawi na kwingineko. Mwaka 2006 aliyekuwa rais wa Malawi, marehemu Bingu wa Mutharika alihama chama chake cha UDF, kisha kuanzisha chama chake cha DPP na kuendelea na cheo chake cha urais. UDF kilirejea kuwa chama cha upinzani.

Maandalizi yanayofanyika kwa sasa hapa nchini yanafikirisha. Ni bahati mbaya kuwa wanachama wengi wa CCM wanalishwa kasumba kuwa umaarufu wa chama chao unatokana na kutegemea umaarufu wa mtu mmoja. Ni bahati mbaya hasa kwa kuwa wengi wa wanachama wa CCM wameendelea kuamini kuwa hivyo ndivyo ilivyo badala ya kinyume chake.

Maandalizi yaliyosukwa kuteua wagombea wa urais, lakini zaidi utaratibu wa kupata ubunge kupitia CCM, ni dhairi kuwa, kwa macho ya uchambuzi kisayansi, wabunge watakaoingia kwenye Bunge la 12, watakuwa wamenyanyuliwa moja kwa moja (handpicked) kwa mkono wa mtu Bwana yule (mmoja siyo mfumo). Hakutarajiwi kuwepo kwa diversity ya wabunge kwa kuzingatia ukongwe na asili ya CCM.

Aidha, jitihada za kunyamazisha vyombo vya habari vyenye sauti mbadala; jitihada za kutengeneza upinzani bandia bungeni uliopewa hadhi mpya ya 'kambi rasmi ya wachache' Bungeni (official minority), [kanuni za Bunge zilirekebishwa siku moja kabla ya Bunge kuvunjwa rasmi] badala ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KUB); jitihada za kusambaratisha asasi za kiraia zenye msimamo wa kujisimamia badala ya kupokea maelekezo kutoka serikalini; jitihada za kusogeza muda wa kustaafu (extend) wa Msajili wa Vyama Vya Siasa (Jaji Francis Mutungi) kwa miaka miwili zaidi; na jitihada zinazofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhakikisha watuele wa Bwana yule ndio pekee wanapitishwa (siyo kuchaguliwa - nitawawekea uchambuzi wa kanuni mpya za uchaguzi mkuu, 2020 zilizoandaliwa na NEC na kwa sasa ziko mbioni kuwa gazetted) ni ishara au viashiria vya kutosha kwa wataalam na wachambuzi wa masuala ya siasa na utawala kubaini mwelekeo wa Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu 2020.

Hii si ramuli ni uchambuzi mdogo wa kisayansi. Tusishangae baada ya uchaguzi mkuu 2020 kuona kinachoitwa CCM mpya kuwa chama tawala kipya hapa nchini na kisha CCM inakuwa chama cha upinzani. Tusubiri yajayo kuhusu utabiri huu.

Ni hayo tu kwa leo
 

Attachments

Huu ni uchambuzi mdogo. Msingi wa uchambuzi ni matukio yenye shaka katika siasa na utawala wa Tanzania kuanzia 2016.

Kuna muda, ndani ya kipindi hicho, wakongwe ndani ya CCM, wakiwemo Pius Msekwa na Benjamin William Mkapa, wamewahi kuonya. Kwamba haifai kwa MTU mmoja ndani ya CCM kujitangazia kuwa ni maarufu zaidi kuliko chama chake kilichompatia fursa ya uongozi.

Waliona hatari kwa Chama chao siku za usoni. Waliogopa madhara ya kisiasa, kama ilivyowahi kutokea nchini Malawi na kwingineko. Mwaka 2006 aliyekuwa rais wa Malawi, marehemu Bingu wa Mutharika alihama chama chake cha UDF, kisha kuanzisha chama chake cha DPP na kuendelea na cheo chake cha urais. UDF ikarejea kuwa chama cha upinzani.

Maandalizi yanayofanyika kwa sasa hapa nchini yanafikirisha. Wanachama wengi wa CCM wanalishwa kasumba kuwa umaarufu wa chama chao unategemea umaarufu wa mtu mmoja. Ni bahati mbaya kuwa wengi wa wa wanachama hao wameamini kuwa hivyo ndivyo badala ya kinyume chake.

Maandalizi yaliyosukwa kuteua wagombea wa urais, lakini zaidi ubunge kupitia CCM, ni dhairi kuwa, kwa macho ya uchambuzi kisayansi, wabunge watakaoingia bungeni kwenye Bunge la 12, watakuwa handpicked na mtu mmoja. Hakutakuwa na diversity ya wabunge Kwa kuzingatia asili ya CCM.

Aidha, jitihada za kunyamazisha vyombo vya habari vyenye sauti mbadala; jitihada za kutengeneza upinzani bandia bungeni Kwa hadhi mpya ya 'kambi rasmi ya wachache' official minority, badala ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KUB); jitihada za kusambaratisha asasi za kiraia zenye msimamo wa kujisimamia badala ya kupokea maelekezo kutoka serikalini; jitihada za kusogeza muda wa kustaafu (extend) wa Msajili wa Vyama Vya Siasa (Jaji Mutungi) Kwa miaka miwili; na jitihada zinazofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhakikisha watuele wa Bwana Yule ndio pekee wanapitishwa (siyo kuchaguliwa, nitawawekea uchambuzi wa kanuni mpya za uchaguzi mkuu, 2020 zilizoandaliwa na NEC na Kwa sasa ziko mbioni kuwa gazetted) ni ishara au viashiria vya kutosha kwa wataalam wa masuala ya siasa na utawala kubaini mwelekeo wa Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu 2020.

Hii si ramuli ni uchambuzi mdogo wa kisayansi. Tusishangae baada ya uchaguzi mkuu 2020 kuona kinachoitwa CCM mpya kuwa chama tawala kipya hapa nchini. Tusubiri yajayo kuhusu utabiri huu.

Ni hayo tu kwa leo
Duu acha tuone
 
Ramli Chonganishi!!!
Mitishamba Imetusaidia Sana Kwenye COVID 19
Waganga Waheshimiwe Ila Akaweka Angalizo!!!
Uchawi Tu Ndiyo Mbaya.
 
Uzuri hata afanye nini, mwisho wa siku atatuachia tu nchi yetu halafu na yeye mwenyewe atajichagulia/atachaguliwa njia nyingine. Iwe kifo cha kawaida/kuuwawa, kurudi kijijini Chato baada ya kustaafu, kufurushwa madarakani kama ilivyomtokea Mugabe, Gaddaf, Saddam Hussein, nk.
 
Na Ile ya mwamba tuvushe?? Je wengine hawana nguvu ya kuivusha Chadema?

Mada zingine ni bule kabisa
 
Mtandao ndio ulikuwa tatizo kubwa kwa nchi hii.

Tunashukuru JPM kwa kuusambaratisha na kukirudisha chama kwa Raia na wanachama wa nchi hii.

Nyinyi mtandao membe endeleeni kulialia, CCM inapiga kazi na nchi inasonga mbele 100KMPH...
Na Ile ya mwamba tuvushe?? Je wengine hawana nguvu ya kuivusha Chadema?

Mada zingine ni bule kabisa
Nadhani humnao uwezo wa kuona mbali kama wa mtoa maada
 
Wangekua na ujasiri wangechukua hatua ile 2016, kwasasa wameshachelewa, sote tuendelee kuminya p*mbu huku tukiomba hadi kufika 2025 nchi itakuwa kwenye one piece.

Mipango waliyonayo mabeberu kama uchaguzi utakua wa hovyo ni balaa tupu.
 
Hii si ramuli ni uchambuzi mdogo wa kisayansi. Tusishangae baada ya uchaguzi mkuu 2020 kuona kinachoitwa CCM mpya kuwa chama tawala kipya hapa nchini na kisha CCM inakuwa chama cha upinzani. Tusubiri yajayo kuhusu utabiri huu.
Mkuu 'Sophist' huo ni uchambuzi/ramli(?) inayofikirisha kidogo.

Lakini mimi nina swali dogo tu la kukuuliza.

Hivi kuna sababu yoyote inayolazimu afanye hayo yote uliyoyaeleza na kwenda mbele zaidi hadi kuwa na "CCM Mpya"?

CCM Mpya ya nini huku matakwa yake yote hakuna anayeweza kuyapinga ndani ya CCM iliyopo?
 
Hata mi navyoona hali inavyoenda kuanzia 2021 januari nchi hii itabadilika sana
 
Mkuu 'Sophist' huo ni uchambuzi/ramli(?) inayofikirisha kidogo.

Lakini mimi nina swali dogo tu la kukuuliza.

Hivi kuna sababu yoyote inayolazimu afanye hayo yote uliyoyaeleza na kwenda mbele zaidi hadi kuwa na "CCM Mpya"?

CCM Mpya ya nini huku matakwa yake yote hakuna anayeweza kuyapinga ndani ya CCM iliyopo?
Kwenye uchambuzi (mdogo) nimeshauri tusubiri. Tafadhali tufanye hivyo. Tuendelee na trend readings.
 
Duuuh hiii lamri ni ngumu kumesa..ngoja aje bia yngu ( USSR )
 
Back
Top Bottom