CCM nambari wani

CCM nambari wani

tpaul nanyi mnakuja na ngonjera kuwa mtawapatia wananchi maisha bora kumbe ni tamaa ya kushika dola tu. hakuna namna mtaongeza vyanzo vya mapato kuweza kuwapatia watanzania wote maisha bora. picha hizi kama ungezichukua kwa mlinganisho.mfano nyumba mbovu na nyumba bora za kisasa zinazojengwa nchini kote na nssf, na nhc, shida ya maji na juhudi za kutandaza mabomba na miundombinu mingine ya maji, zahanati ya makuti na zahanati bora na zenye vifaa zilizojengwa kwa kipindi chetu hapo ungeeleweka. lakini umefanya makusudi na kujikampenia kwa kuwadanganya watanzania kuwa hali hiyo ndio uhalisia wao kumbe wao wanaona tofauti. wanasafiri kwa barabara za lami, wanalima na wanapata pembejeo kwa wakati, wanauza mazao yao kwenye vyama vyao vya ushirika wanapata umeme wa rea na tanesco, wanapata maji kupitia mamlaka zao za maji wanawapeleka watoto wao wote shule tena sasa hivi zenye maabara na mengineyo mengi tu. wanatumia vipato vyao kujijengea nyumba bora na kujiwekea umeme.hayo uliyotupia ni kaupande kamoja tu ka shilingi tupia upande mmoja wa shilingi na ulinganishe na upande wa pili wa shilingi..usiwahadae watanzania
CCM walianza na ngonjera ya ‘Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania’. Baada ya kuimba ngonjera hii kwa muda wa miaka 5 na kukosa muitikiaji, wakaamua kubalili mapigo na kuibuka na ngonjera mpya waliyoipa jina la ‘Ari mpya, Nguvu mpya na Kasi mpya’ (ANGUKA). Pamoja na usanii huu wote, maisha ya mtanzania yamezidi kuwa duni mwaka nenda mwaka rudi!

View attachment 175945 View attachment 175951 View attachment 175957

Tangu CCM washike madaraka nchi imekuwa haina mwelekeo. CCM inafanana na mtu mwenye jino moja. Mtu kama huyo hata umlishe namna gani hawezi kunenepa. Lazima atakufa kwa njaa kwa kuwa hana meno ya kutafunia chakula.

View attachment 175940

Nchi hii imejaliwa rasilimali nyingi za asili kama vile ardhi, maziwa , bahari na mito, madini, misitu, wanyama, nk. Lakini kwa kuwa CCM haina meno, imewaalika wenye meno (wawekezaji) waje watafune (wakavune) rasilimali hizo huku wakiiacha nchi ikiwa ikiwa tupu! Migogoro katika maeneo ya uchimbaji madini na maeneo yenye ardhi ya rutuba imekuwa ikitokea kila kukicha. Wananchi wamenyanganywa ardhi yao nzuri wamepewa ‘wawekezaji’. Watanzania wanyonge wamegeuka wakimbizi ndani ya nchi yao. Wananchi wamekata tamaa na utawala wa CCM. Hawana hamu nayo!

View attachment 175946 View attachment 175953

Huduma za jamii kama vile maji, umeme, barabara, elimu na afya imekuwa duni kiasi cha kukatisha tamaa. Wanafunzi kusomea chini ya miti ni suala la kawaida kabisa na wale wachache waliobahatika kupata kupata madarasa duni huketi chini ya sakafu ya vumbi au juu ya matofali! Hali hii mpaka lini hasa? CCM wala hawajali kwa kuwa watoto wao husomeshwa kwenye shule nzuri zenye walimu weledi na vifaa vya kufundishia vinavyotosheleza mahitaji.

View attachment 175947View attachment 175948 View attachment 175950 View attachment 175955 View attachment 175956

Mwalimu Nyerere alipokea uongozi wa nchi kutoka kwa wakoloni wakati nchi ikiwa taabani kiuchumi lakini hatukuwahi kushuhudia ugumu wa maisha kama tunavyoshuhudia hivi sasa. Ni lini hasa CCM na mafisadi wake wataboresha huduma za jamii na kuwafanya wananchi waishi maisha yenye utu?

CCM haina tofauti na mtu mzima aliyekabidhiwa kumlea mtoto mdogo badala yake akanywa maziwa ya mtoto na kumuacha mtoto akifa kwa njaa.

View attachment 175944

Hii maana yake ni kwamba CCM imeamimiwa na wananchi wakaikabidhi rasilimali zote wakitegemea iwaletee maendeleo lakini wanaonufaika na rasilimali hizi ni mafisadi wachache ndani ya chama na seerikali huku wananchi wakiishi maisha duni kupindukia.

CCM ni sawa kabisa na mtu mzima anayemtumia mtoto mdogo kama ngazi kwa manufaa yake binafsi. Mtu wa namna hiyo lazima anakuwa na hililafu kichwani mwake.

View attachment 175937

Vivo hivyo, CCM na mafisadi wake huwatumia walalahoi kama ngazi ya kupandia madarakani na wakishayapata hayo madaraka huuwaacha wananchi solemba. Sote ni mashahidi jinsi ambayo CCM inavyowakumbatia mafisadi na makuwadi wa mabeberu wanaokomba rasilimali za taifa na kuiacha nchi ikiwa kama jangwa.

CCM wameishiwa ubunifu wa kuitoa nchi hapa ilipo na kuipeleka mbele. Hata mcheza shoo anawazidi akili maCCM. Mcheza shoo hutumia mwili wake kama rasilimali ya kujiletea maendeleo kwa kuwaburudisha wateja wake na kuwakonga nyoyo zao.Kama vile mcheza shoo anayotumia rasilimali aliyonayo (mauno) kujiletea maendeleo, tulitarajia kwamba CCM watumie rasilimali zilizopo nchini kuwaletea wananchi maendeleo endelevu lakini wao bado wamelala usingizi wa pono.

View attachment 175936

Hata mbuzi anawazidi CCM akili. Wakati wa kiangazi, mbuzi hutumia maarifa yote kuyafikia majani popote yalipo lakini CCM wao wamelala usingizi huku wakitegemea kuombaomba misaada badala ya kutumia rasilimali tulizonazo kuwanufaisha watanzania wote.

View attachment 175935

Nchi hii ina rasilimali lukuki ambazo kama zingetumika vizuri zingeleta manufaa kwa watanzania wote. Kinyume chake rasilimali zote wamekabidhiwa mabeberu (wanaopambwa kwa jina la ‘wawekezaji’) ambao wamemimika kutoka kila pembe ya dunia na kukimbilia kuvuma utajiri uliojaa tele nchini Tanzania.

View attachment 175934

Baada ya CCM kushindwa kuiendeleza nchi, wameamua kuwarubuni wananchi wenye njaa kwa lengo la kuwarejesha madarakani kila uchguzi mkuu uitishwapo. Mgao wa fedha wanazopata kutoka kwa mabepari waliowakabidhi rasilimali zetu, hutumikia kama chambo cha kuwarejesha madarakani kwa kuwapikia chakula, kuwapanga kama ng’ombe kwenye mistari na kuwalisha pilau.

View attachment 175933

Hii ndio kete ya mwisho iliyobaki. Mbinu nyingine zozote ziwazo zimeshindwa kufanya kazi. CCM wamewatia wananchi njaa kwa kutapanya rasilimali zao ili iwe rahisi kuwarubuni kwa kuwalisha chakula, kuwanunulia mbege, mataputapu, t-shirts, kanga, fulana, chumvi, sabuni, nk.

View attachment 175929 View attachment 175930View attachment 175952 View attachment 175978

Na kwa kuwa wananchi hawa wana njaa ya kutisha huamua kugawa kura zao kwa CCM, kisha hukaa na njaa na dhiki zao kwa miaka mingine mitano. Miaka mitano ikiisha CCM huwaendea tena na kuwalisha chakula na kuwapa vizawadi uchwara na hatimaye huwarejesha madarakani tena. Huu ni mzunguko hatari sana ambao kama usipodhibitiwa, wanachi wetu watazidi kutopea kwenye ufukara hadi Yesu atakaporudi. Wakati wa kutafuta kura kwa wananchi, wataingia hadi kwenye mahandaki lakini wakishapata hizo kura hawawakumbuki tena wananchi waliowapa kura.

View attachment 175928 View attachment 175979

Janja ya CCM ni sawa na mfugaji mpumbavu ambaye hamlishi ng’ombe wake lakini kila uchao utamkuta amening’inia kwenye chuchu akimkamua maziwa. Yuko radhi kukamua mpaka damu zitoke kuliko kumlisha na kumnenepesha ng’ombe wake ili apate maziwa mengi zaidi.

View attachment 175926 View attachment 175980

MaCCM hawaboreshi maisha ya wananchi lakini kila mwaka hupandisha kodi za bidhaa na huduma na kuyafanya maisha ya walalahoi yawe magumu zaidi. Kila bajeti isomwapo utasikia bia, soda, mkate, mafuta na bidhaa zingine zikipanda bei wakati uchumi wa watanzania bado upo pale pale!

View attachment 175924 View attachment 175925

Silaha ya mwisho kabisa waliyosalia nayo ni kuwabeba wananchi kwenye malori ya mchanga kuwapeleka kwenye mikutano yao ya siasa pamoja na kuwalipa posho uchwara ili kuwajazia mikutano yao ambayo siku za nyuma ilikuwa ikikosa wasikilizaji/wahudhuriaji. CCM wametufikisha hapa tulipo baada ya kuwafukarisha wananchi ili iwe rahisi kuwatawala.

View attachment 175958

Posho zenyewe wanzopewa ili kuhudhuria mikutano ya CCM huwa ni kidogo sana kiasi cha kupelekea wahudhuriaji kupigana ngumi na mateke wakigombea hayo makombo kidogo wanayoambulia kutoka kwa mafisadi. Hii ndio CCM zaidi ya mnavyoifahamu. CCM oyeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!

View attachment 175977 View attachment 175981

:israel:
 
Kwa hizi picha natamani kulia japo nipoze machungu
 
Kwa upande wangu huu ndio uzi bora kwa 2014 , Mungu akulinde sana mkuu tpaul .
 
attachment.php

Ukitaka BAR yako ife kifo cha mende lete bendi ya VIJANA JAZZ au TOT PLUS , kama unabisha nenda leo PENTAGON - KURASINI MIVINJENI .
 
[TABLE="class: cms_table_tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD]
IMG_5737.JPG
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: cms_table_tr-caption"]Ridhiwani Kikwete mbunge wa Chalinze akigawa ndizi kijini Kwa Msanja
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana

attachment.php
 
ukisoma kwa umakini uzi huu na posti zake ndio utajua kwanini wanasema watanzania wana IQ ndogo. Kuna watu wanapost bila kusoma uzi unahusu nini, akishaona rangi ya kijani ni kuitukana ccm tu hivi hakuna mazuri yaliyofanywa na ccm au ndio mnafikiri kwa akili za kuambiwa?. Uhalisia na maana ya picha hizi hauwakilishi hali ya watanzania sababu unaweza kutumia picha hizi hizi ukatoa ujumbe ulio positive kwa CCM.
tpaul kwanini usiweke uzi wenye mambo mazuri yaliyofanya na wabunge wa chama chako? au hawajafanya lolote?ndessa.jpg
Mzee Ndesa yeye alitoa hii ameweka na ushahidi kabisa hebu tupe za hao wengine
 
Last edited by a moderator:
We ultaka wakuletee hela CCM Kwenu?

No. Nilitaka mafisadi wa CCM wa ESCROW, Meremeta, Richmond, Tangold, Kagoda, etc wabebe pesa kwenye LUMBESA wampelekee JK kama walivyofanya mafisadi wa EPA. Na wakishamkabidhi fedha awaruhusu warudi mtaani (pasipo kuwachukulia hatua) ili waendelee kuiba tena wampelekee. Na asitokee hata mtu mmoja anayehoji wezi hao wanaorejesha fedha ni kina nani, wamerejesha pesa ngapi na zipo wapi! Haya ndiyo MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA ambayo kila mwananchi anayataka. Umeona eeh? CCM oyeeeeeeeeeeeee!!!!
 
No. Nilitaka mafisadi wa CCM wa ESCROW, Meremeta, Richmond, Tangold, Kagoda, etc wabebe pesa kwenye LUMBESA wampelekee JK kama walivyofanya mafisadi wa EPA. Na wakishamkabidhi fedha awaruhusu warudi mtaani (pasipo kuwachukulia hatua) ili waendelee kuiba tena wampelekee. Na asitokee hata mtu mmoja anayehoji wezi hao wanaorejesha fedha ni kina nani, wamerejesha pesa ngapi na zipo wapi! Haya ndiyo MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA ambayo kila mwananchi anayataka. Umeona eeh? CCM oyeeeeeeeeeeeee!!!!
Hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha
 
No. Nilitaka mafisadi wa CCM wa ESCROW, Meremeta, Richmond, Tangold, Kagoda, etc wabebe pesa kwenye LUMBESA wampelekee JK kama walivyofanya mafisadi wa EPA. Na wakishamkabidhi fedha awaruhusu warudi mtaani (pasipo kuwachukulia hatua) ili waendelee kuiba tena wampelekee. Na asitokee hata mtu mmoja anayehoji wezi hao wanaorejesha fedha ni kina nani, wamerejesha pesa ngapi na zipo wapi! Haya ndiyo MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA ambayo kila mwananchi anayataka. Umeona eeh? CCM oyeeeeeeeeeeeee!!!!
Hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha HAHAHA😛eace:Hahaha hahaha
 
Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana

attachment.php

Like father...


attachment.php


...like son!

IMG_5737.JPG


Asante sana mkuu BAK na Mag3 kwa picha za nyongeza. Hapa ndipo CCM na makuwadi wao wa ufisadi walipotufikisha. Ninachoshukuru ni kwamba sasa wananchi wote, mijini na vijijini, wameshaung'amua ulaghai wa CCM na hawako tayati tena kuendelea kuhadaiwa na hawa manyang'au....2015 lazimia kitaeleweka tu. Dawa ya magamba na mafisadi wanaowafuga iko jikoni inachemka.
magamba SINGASINGA.jpg
 
Last edited by a moderator:
Watu wanaiba mabilioni ya fedha halafu wanafutwa kazi tu inaishia hapo...Prof Kikwete aliwahi kuwasamahe wezi wa EPA na kuwabembeleza wamrejeshee fedha na walipofanya hivyo akawaachia huru waende zao mitaani ili waendelee kutuibia. Nchi hii aliyeiloga kafa. Ama kweli CCM ni ukoo wa panya—babu mwizi, baba mwizi, watoto wezi, wajukuu wezi, vitukuu wezi, vilembwe wezi na vining’ina wezi! Ukoo huu wa panya walikuwa wanasafiri katika boti la muhogo, lakini kwa sababu ya uroho wao, walianza kulitafuna boti! Kilichofuata ni ukoo mzima wa kizazi cha panya kuzama na kuangamia.

CCM wameanza kuitafuna nchi tangu mwaka 1961 lakini ukomo wao wa kutafuna rasilimali za nchi ni mwaka 2015 kwani hakuna mtanzania mwenye hamu ya kuongozwa na chama cha kifisadi kama CCM ambacho kimeshindwa kuboresha maisha na ustawi wa watanzania. Wananchi wamechoka kubebeshwa ‘magunia ya misumari’ ya bei ya juu ya umeme, mfumuko wa bei wa kutisha, elimu duni, maisha duni, ufisadi wa kutisha, EPA na matatizo lukuki yanayosababishwa na panya (CCM) hawa wasiokuwa na haya! Kizazi kizima cha CCM kinakaribia kuzama na kusahaulika kabisa katika ardhi ya Tanzania.

It’s a matter of time before CCM dynasty comes to an end, and that’s when magambas will apprehend the significance and power of the people. Desolately, CCM have been ignoring and looking down their noses at common Tanzanians for many years. Time has now come when citizens can no longer endure CCM’s tyranny and corrupt rule. Everybody is tired of living like a slave in a land endowed with an assortment of natural wealth which only benefits the minority fisadis and a few elites in power while majority Tanzanians lead very miserable lives.

What comes around goes around. Let CCM go to hell for good because they have absolutely failed to uplift the living standards of millions of Tanzanians at the expense of a few fisadis whose gargantuan stomachs never fill up! And no one should be blamed for the hatred and grudge that many Tanzanians hold against CCM and their crooked government except fisadis themselves who, horrendously, decided to gnaw the cassava-made boat by which they were sailing!

The only weapon we have today, if we wish to change the history of our country that has been exploitative since independence, is UNITY AND SOLIDARITY. We must understand that our government and the ruling party will not easily accept to quit the state and leave all fruits they are enjoying currently. We must ensure our people join us in this struggle. I believe one day we shall all enjoy living in a country without discrimination, exploitation, suffering and humiliation.

View attachment 213369

kwel uzalendo unashika kasi upo fresh big up
 
No. Nilitaka mafisadi wa CCM wa ESCROW, Meremeta, Richmond, Tangold, Kagoda, etc wabebe pesa kwenye LUMBESA wampelekee JK kama walivyofanya mafisadi wa EPA. Na wakishamkabidhi fedha awaruhusu warudi mtaani (pasipo kuwachukulia hatua) ili waendelee kuiba tena wampelekee. Na asitokee hata mtu mmoja anayehoji wezi hao wanaorejesha fedha ni kina nani, wamerejesha pesa ngapi na zipo wapi! Haya ndiyo MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA ambayo kila mwananchi anayataka. Umeona eeh? CCM oyeeeeeeeeeeeee!!!!


I dont think one could have a better answer than this! Ni jibu SAHIHI kabisa kwa muulizaji! - What a critical mind! Big up!
 
tpaul nanyi mnakuja na ngonjera kuwa mtawapatia wananchi maisha bora kumbe ni tamaa ya kushika dola tu. hakuna namna mtaongeza vyanzo vya mapato kuweza kuwapatia watanzania wote maisha bora. picha hizi kama ungezichukua kwa mlinganisho.mfano nyumba mbovu na nyumba bora za kisasa zinazojengwa nchini kote na nssf, na nhc, shida ya maji na juhudi za kutandaza mabomba na miundombinu mingine ya maji, zahanati ya makuti na zahanati bora na zenye vifaa zilizojengwa kwa kipindi chetu hapo ungeeleweka. lakini umefanya makusudi na kujikampenia kwa kuwadanganya watanzania kuwa hali hiyo ndio uhalisia wao kumbe wao wanaona tofauti. wanasafiri kwa barabara za lami, wanalima na wanapata pembejeo kwa wakati, wanauza mazao yao kwenye vyama vyao vya ushirika wanapata umeme wa rea na tanesco, wanapata maji kupitia mamlaka zao za maji wanawapeleka watoto wao wote shule tena sasa hivi zenye maabara na mengineyo mengi tu. wanatumia vipato vyao kujijengea nyumba bora na kujiwekea umeme.hayo uliyotupia ni kaupande kamoja tu ka shilingi tupia upande mmoja wa shilingi na ulinganishe na upande wa pili wa shilingi..usiwahadae watanzania

Mkuu laiza mbona unachangia kwa uoga sana, hujiamini? Tuliza akili zako upate kuelewa ujumbe ninaotaka kuufikisha kwa watanzania. Haya maswali yote uliyouliza naona umejikanaganya ama kwa makusudi au kwa kutokujua:

1. Vyanzo vya mapato vitaongezwa kwa kuzuia UFISADI wa fedha za umma tofauti na CCM wanaowatetea mafisadi kwa nguvu zao zote. Wewe hujui kwamba mabilioni ya fedha yanayopotea kila siku ni fedha za wananchi ambazo zingetumika kuwaletea maendeleo? Na je unadhani kwamba yale mabilioni ya EPA aliyoyachukua Kikwete kutoka kwa wezi wa EPA yangejenga barabara ngapi kama angeyarejesha kwa wananchi?

2. Pesa za NSSF sio za UMMA...hizi ni fedha za wanachama zinazotumiwa vibaya kujengea miundombinu ya serikali huku wenye fedha zao hawanufaiki na kitu chochote kutokana na vitega uchumi hivyo. Huoni kwamba ni UCHIZI serikali kutegemea fedha za wanachama huku ikiwaachia wezi wanajichotea fedha za umma? Aidha NHC ni shirika la umma linalojiendesha kibiashara na nyumba wanazojenga wanakaa mafisadi huku wananchi wa kawaida wakiwa hawana mahali pa kuishi. Pia, fahamu kwamba zaidi ya 50% ya nyumba zote zilizojengwa na NHC zimeishanyakuliwa na mafisadi...wamejiuzia kwa bei ya kutupa. Ina maana hata hili hilifahamu au umeamua tu kujitoa akili?

3. Shida ya maji nimeishaionglea kwenye uzi mama hapo juu...hebu tazama picha tu kama hujui kusoma. Unataka SHIDA hii ya maji niiongelee mara ngapi?

4. Ni kweli kabisa kwamba haya matatizo niliyotupia humu ni machache ukilinganisha na hali halisi ya maisha ya watanzania. Hali ya maisha ya wananchi ni mbaya kuliko hii inayoonekana kwenye picha hapo juu. Ni juzi tu mwananchi mmoja aliamua kunadi figo lake ili apate fedha za kujikimu....hali ya maisha ya wananchi ni mabaya kuliko kawaida. Nakupongeza kwa kuuona huo ukweli. Ungana na wazalendo tukaikomboe nchi kutoka mikononi mwa mwa wakoloni weusi (CCM) mwezi wa Oktoba mwaka huu wa 2015.
 
Last edited by a moderator:
Ahsante sana Mkuu tpaul kusoma michango kama yako na wengine wengi hapa katika kulinda na kutetea maslahi ya Watanzania na Tanzania kwangu mimi ni motivation kubwa sana ya kuja hapa kila siku na kusoma misimamo yenu kuhusu mustakabali wa nchi yetu, bila michango yenu mimi siku nyingi ningekuwa nimeshasepa hapa mahali. Mbarikiwe sana wote na msichoke kuleta michango yenu ya ina mbali mbali ikiwemo picha kama hizi zinazoonyesha hali ya kusikitisha sehemu nyingi nchini mwetu.

Asante sana mkuu BAK na Mag3 kwa picha za nyongeza. Hapa ndipo CCM na makuwadi wao wa ufisadi walipotufikisha. Ninachoshukuru ni kwamba sasa wananchi wote, mijini na vijijini, wameshaung'amua ulaghai wa CCM na hawako tayati tena kuendelea kuhadaiwa na hawa manyang'au....2015 lazimia kitaeleweka tu. Dawa ya magamba na mafisadi wanaowafuga iko jikoni inachemka.
View attachment 215959
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom