Elections 2010 CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS

Elections 2010 CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS

QUALITY

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2010
Posts
853
Reaction score
115
CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS
CCM imekazana baada ya kuona maji yamekuwa ya shingo badala ya miguuni!! Usiku wa leo nimetumiwa meseji mbili., moja ilifika saa tisa dakika 26 ikieleza kama ifuatavyo “CCM iliahidi, na imefanya.. tuichague tena. CHAGUA CCM, CHAGUA KIKWETE.

SAA 11.25 ALFAJILI CCM walinitumia sma nyingine inayosema hivi “CCM ni chama cha kimataifa, kimekomboa nchi nyingi barani Afrika” Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Baada ya kusoma SMS hii nilicheka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyekuwa anaongea katika zile picha za Tarime (uchaguzi mdogo) akisema “tumeandaliwa wajinga wengi, ili kundi dogo ndilo liendelee kutawala”.

SMS hii ya CCM kuwa chama cha kimataifa, imeonesha kuwa CCM hawajui kuwa kuna watz ambao wanaelewa. Tangu lini CCM ikakomboa nchi za bara la Africa? Tangu lini CCM ikawa chama cha kimataifa?

Mwaka huu wa 2010, hatudanganyiki. Endeleeni kutuma sms lakini hamuambulii kitu hapa.

Bye CCM, Bye KIKWETE
 
yaani sasa hivi wanaweweseka tu .walitegemea vijijini ndokwenye kura nako hawataki hata kuwasikia
 
Wameona thiatha dha majitaka dhinawapanditha wapindhani thatha wameamua kujipamba wenyewe? Hatudanganyiki!
 
wameona thiatha dha majitaka dhinawapanditha wapindhani thatha wameamua kujipamba wenyewe? Hatudanganyiki!
kweli ccm hoi inavilaza gani hatakutengeneza msg nzuri wanashindwa, ccm kweli namkumbuka mangula katibu wetu!
 
CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS
CCM imekazana baada ya kuona maji yamekuwa ya shingo badala ya miguuni!! Usiku wa leo nimetumiwa meseji mbili., moja ilifika saa tisa dakika 26 ikieleza kama ifuatavyo "CCM iliahidi, na imefanya.. tuichague tena. CHAGUA CCM, CHAGUA KIKWETE.

SAA 11.25 ALFAJILI CCM walinitumia sma nyingine inayosema hivi "CCM ni chama cha kimataifa, kimekomboa nchi nyingi barani Afrika" Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Baada ya kusoma SMS hii nilicheka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyekuwa anaongea katika zile picha za Tarime (uchaguzi mdogo) akisema "tumeandaliwa wajinga wengi, ili kundi dogo ndilo liendelee kutawala".

SMS hii ya CCM kuwa chama cha kimataifa, imeonesha kuwa CCM hawajui kuwa kuna watz ambao wanaelewa. Tangu lini CCM ikakomboa nchi za bara la Africa? Tangu lini CCM ikawa chama cha kimataifa?

Mwaka huu wa 2010, hatudanganyiki. Endeleeni kutuma sms lakini hamuambulii kitu hapa.

Bye CCM, Bye KIKWETE


Ha ha ha you made my day mkuu. Yaani hawa watu wa thithiem nawashangaa mno!! Kwa nini wanatumia nguvu kubwa hivyo kuwahadhaa wananchi? Kama kweli wamefanya mambo mazuri yasiyo ya kifisadi basi wasubiri fainali za ligi kuu ya vyama vya siasa tarhe 31 Oktoba. Yaani zile message za Dr. Slaa zinachekesha sana, hata mtoto wa vidudu/chekechea atawacheka. Poleni sana.
 
Hahahahahhhh ..... na bado wataendelea kuweweseka......
 
CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS
CCM imekazana baada ya kuona maji yamekuwa ya shingo badala ya miguuni!! Usiku wa leo nimetumiwa meseji mbili., moja ilifika saa tisa dakika 26 ikieleza kama ifuatavyo “CCM iliahidi, na imefanya.. tuichague tena. CHAGUA CCM, CHAGUA KIKWETE.

SAA 11.25 ALFAJILI CCM walinitumia sma nyingine inayosema hivi “CCM ni chama cha kimataifa, kimekomboa nchi nyingi barani Afrika” Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Baada ya kusoma SMS hii nilicheka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyekuwa anaongea katika zile picha za Tarime (uchaguzi mdogo) akisema “tumeandaliwa wajinga wengi, ili kundi dogo ndilo liendelee kutawala”.

SMS hii ya CCM kuwa chama cha kimataifa, imeonesha kuwa CCM hawajui kuwa kuna watz ambao wanaelewa. Tangu lini CCM ikakomboa nchi za bara la Africa? Tangu lini CCM ikawa chama cha kimataifa?

Mwaka huu wa 2010, hatudanganyiki. Endeleeni kutuma sms lakini hamuambulii kitu hapa.

Bye CCM, Bye KIKWETE

Duuh inaonekana wakati mwingine hatuelewi. boss mimi pia nilizipata hizo sms, kweli inaonesha ndugu zetu wanahaha, lakini pia ngoja nikueleweshe kidogo.

Hivi Rais wetu wa sasa niwa chama gani? na je Nyerere aliyehusika kwenye kuikomboa nchi yetu na kushiriki kikamilifu kwenye harakati za ukombozi wa nchi zingine za africa alikuwa wa chama gani? kama majibu yako ni CCM. then it is obvious CCM ni chama cha kimataifa na kimeshiriki kuleta ukombozi Africa.

kuwa negative all the time bila ku-analyse issue vizuri wakati mwingine inaonyesha upungufu wa kufikiria.

tutumie JF kusaidiana sio ku ongea bila kuchambua issue vizuri
 
kweli ccm hoi inavilaza gani hatakutengeneza msg nzuri wanashindwa, ccm kweli namkumbuka mangula katibu wetu!

Mkuu wengi wao ni school drop outs, failures, usalama wa taifa na polisi sasa unategemea ujumbe mzuri utokee hapo? Usishangae wengi wao hata Kiswahili sahihi hawawezi kuandika na ndo wamekasimishwa mikoba ya kuongoza kampeni, too sad!!!
 
tehetehetehe wamefulia,wera wera hatuchagui ccm,
 
Poleni thithiem!!! Siku zote huwa najiuliza kwa nini hawa ndugu zetu wanatumia nguvu kubwa sana kujinadi? Tena nyingi zisizokuwa na busara? Always, Chema chajiuza, kibaya chajitembeza.
 
Wakiniletea ujumbe huu nafungua jalada mahakani kwa kukashifiwa na namba yangu kupewa watu wengine bila ridhaa yangu. Lazima hawa Zain na Tigo waheshimu haki yangu ya privacy na namba yangu kutopewa watu hovyo wanaoweza kutuma message za hovyo namna hii
 
Duuh inaonekana wakati mwingine hatuelewi. boss mimi pia nilizipata hizo sms, kweli inaonesha ndugu zetu wanahaha, lakini pia ngoja nikueleweshe kidogo.

Hivi Rais wetu wa sasa niwa chama gani? na je Nyerere aliyehusika kwenye kuikomboa nchi yetu na kushiriki kikamilifu kwenye harakati za ukombozi wa nchi zingine za africa alikuwa wa chama gani? kama majibu yako ni CCM. then it is obvious CCM ni chama cha kimataifa na kimeshiriki kuleta ukombozi Africa.

kuwa negative all the time bila ku-analyse issue vizuri wakati mwingine inaonyesha upungufu wa kufikiria.

tutumie JF kusaidiana sio ku ongea bila kuchambua issue vizuri

Pole Mkuu. Maana ya kuwa international ni nini? Kwa hiyo gharama zilizotumika kukomboa bara la Africa zilitoka CCM? Zilitoka kwa watz, hivyo ni vizuri kutofautisha CCM na Tanzania. Tanzania siyo CCM na CCM siyo Tanzania.
 
Duuh inaonekana wakati mwingine hatuelewi. boss mimi pia nilizipata hizo sms, kweli inaonesha ndugu zetu wanahaha, lakini pia ngoja nikueleweshe kidogo.

Hivi Rais wetu wa sasa niwa chama gani? na je Nyerere aliyehusika kwenye kuikomboa nchi yetu na kushiriki kikamilifu kwenye harakati za ukombozi wa nchi zingine za africa alikuwa wa chama gani? kama majibu yako ni CCM. then it is obvious CCM ni chama cha kimataifa na kimeshiriki kuleta ukombozi Africa.

kuwa negative all the time bila ku-analyse issue vizuri wakati mwingine inaonyesha upungufu wa kufikiria.

tutumie JF kusaidiana sio ku ongea bila kuchambua issue vizuri
Uwezo wako wa kuelewa unaonyesha ni duni sana. Vita ukombozi kusini mwa Africa na kwingineko ilipata msaada kutoka kwa watanzania wote na sio CCM kama unavyotaka kujiaminisha wewe na wengine. Watu walichangia rasilimali zao na hata uhai wao bila kuwa wana CCM. Maana mtasema tena kuwa CCM ilimpiga Idd Amin. Fikirini kabla ya kutamka, watanzania wa leo wameamka.
 
CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS
CCM imekazana baada ya kuona maji yamekuwa ya shingo badala ya miguuni!! Usiku wa leo nimetumiwa meseji mbili., moja ilifika saa tisa dakika 26 ikieleza kama ifuatavyo "CCM iliahidi, na imefanya.. tuichague tena. CHAGUA CCM, CHAGUA KIKWETE.

SAA 11.25 ALFAJILI CCM walinitumia sma nyingine inayosema hivi "CCM ni chama cha kimataifa, kimekomboa nchi nyingi barani Afrika" Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Baada ya kusoma SMS hii nilicheka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyekuwa anaongea katika zile picha za Tarime (uchaguzi mdogo) akisema "tumeandaliwa wajinga wengi, ili kundi dogo ndilo liendelee kutawala".

SMS hii ya CCM kuwa chama cha kimataifa, imeonesha kuwa CCM hawajui kuwa kuna watz ambao wanaelewa. Tangu lini CCM ikakomboa nchi za bara la Africa? Tangu lini CCM ikawa chama cha kimataifa?

Mwaka huu wa 2010, hatudanganyiki. Endeleeni kutuma sms lakini hamuambulii kitu hapa.

Bye CCM, Bye KIKWETE

Umepata kutoka namba gani?Ileile inaomkashifu Slaa?Kama ndiyo hiyo basi washathibitisha kuwa ni ccm ndo waliotuma zile sms.
 
Umepata kutoka namba gani?Ileile inaomkashifu Slaa?Kama ndiyo hiyo basi washathibitisha kuwa ni ccm ndo waliotuma zile sms.

SMS haina namba simu inaandika CCM basi (no number!!!!!) Inawezekana ni kwa msaada wa TCRA na hii ni baada ya kutumia namba ya nje wakapigiwa kelele.
 
"Watu walichangia rasilimali zao na hata uhai wao bila kuwa wana CCM. Maana mtasema tena kuwa CCM ilimpiga Idd Amin. Fikirini kabla ya kutamka, watanzania wa leo wameamka."

Kweli hapo umesema. Anasahau kwanza wakati huo chama kilikuwa kimoja tu na kila mtu awe na chama asiwe nacho wote tulichangia harakati za ukombozi. Tutaelimishana taratibu.
 
Hakuna sababu ya kukataa sana hayo ambayo CCM imefanya. Ila swali muhimu kwa sasa je bado ni political agenda kwa leo? Ni kama ilivyo ukweli kwamba CCM imeleta uhuru. Je, swala la uhuru kwa leo lina maana gani? Leo inapaswa tuzungumzie elimu bora, maji, ajira, usimamizi wa raslimali nk. Mambo ya kukomboa nchi za africa si agenda za leo wala si moja ya matatizo ya Mtanzania wa leo
 
Kumbe nilidhani nimekosea kusoma hiyo taito, mi niliisoma hivi.."CCM ni Chama cha kimafia" nadhani sijui lakini kwamba ndio sahihi
 
Back
Top Bottom