CCM ni chanzo cha mafuriko yanayozikumba kaya zetu

CCM ni chanzo cha mafuriko yanayozikumba kaya zetu

Usitetee uzembe wa serikali. Uhusiano wa serikali na raia ni kama uhusiano wa baba na mwana, na kwa muktadha wa hoja inayojadiliwa, uhusiano huu ni kama wa mzazi na mtoto mdogo ambaye akili haijakomaa. Unamkataza mtoto asitende jambo fulani ni hatari, lakini bado anarudia. Hapo lazima utumie nguvu kwa manufaa ya mtoto. Utetezi kwamba waliambiwa waondoke au waliondoshwa na kulipwa fidia kisha wakarudi ni wa ovyo kabisa. Serikali Ina kila kitu- mamlaka, utaalamu, uwezo wa fedha kutekeleza jambo, rasilimali watu nk.
Ni kama vile unakuta mji unaanza mahali, mji unakuta kido kidogo maka unakuwa mji mkubwa. Pale serikali Ina kusanya kodi kwa wakazi wa eneo lile, watu wakiomba wanaunganishiwa umeme maji etc. Lakini utakutamji huo hauna huduma kama shule ya msingi/sekondari, hakuna Eno la soko, hakuna zahanati/kituo cha afya, Eneo la kuzikia nk. Ni wajibu wa serikali kwanza kutoa idhini kwamba eneo husika linafaa kwa makazi, na iweze kupangilia mji kwa kutenga maeneo kwaajili ya huduma mbalimbali.
Binadamu hamna jema, nguvu ilitumika mtakuja na hoja ya Haki za Binadamu hapa!
 
Raia wengi hawana akili hizo unazofikiria wewe, ndio maana kuna idara za mipango miji na watumishi wanaolipwa huko.
Huu ni utetezi tu, Binadamu mwenye utashi anakosaje hizo akili?
 
Bonde la msimbazi, pale jangwani, na rufiji hapakuwa hatarishi lini? Unawaachia wajenge, unawapelekea umeme, maji, shule zahanati na Kodi ya majengo, siku wakikumbwa na mafuriko serikali inawapa viwanja bure sehemu salama, chakula, malazi, mavazi na fedha za fidia kuondoka mabondenii.
Kama ulinielewa kwenye hoja yangu nilikwambia kuwa si maeneo yote hatarishi yalikuwa hivyo tangu awali, hatari nyingine husababishwa na mabadiliko ya tabia ya Nchi, hali ya hewa na shughuli za kibinadamu, hata hilo Bonde la Msimbazi awali halikuwa hatari kama ilivyo sasa.

Ukiangalia hilo Bonde la Mto Msimbazi utaona kingo za Mto zinameguka na kusababisha Mto kuhama na kuingia kwenye makazi ya Watu na kubomoa Nyumba..
 
Siyo kila kitu ni cha kulaumu Serikali au CCM kama ulivyodai, binafsi nilisikiliza Mahojiano ya Mtangazaji wa Clouds TV na baadhi ya Watu wa maeneo ya Rufiji ambapo kuna Mafuriko, Watu hao wamekiri kuwa Serikali iliwataka wahame maeneo hayo hatarishi siku nyingi za nyuma.

Sambamba na hilo walishapewa hadi viwanja ili wahamie huko, lakini Watu hao licha ya kupewa viwanja eneo lingine ili wahame eneo hilo hatarishi lakini bado wameendelea kurudi maeneo hayo baada ya Mafuriko kuisha.

Ulitaka waondolewe kwa nguvu ili uje una hoja nyingine? Au ulitaka nini kifanyike zaidi ya Elimu iliyotolewa na kupewa viwanja?
Mkuu mbona serikali hiyo hiyo iliwaona watu wa Kimara /Mbezi hadi Kibaha wapo sehemu hatari (service road) na kuamua kuwa bomolea kwa nguvu makazi yao? Tena bila mariposa yeyote.
 
Kuongoza nchi sio kama unavyofikiria.
Tulitarajia kusikia na kuona Rais anawachukulia hatua kali wale wote walisababisha na kuruhusu wananchi kujenga na kuishi maeneo hatarishi kabla na wakati Rais anaagiza waliokumbwa na mafuriko kupewa viwanja/kujengewa sehemu salama. Unataka kusema kamati ya usalama ya kijiji, mtaa, kata, tarafa, wilaya na Mkoa ilikuwa haijui sehemu gani ni salama na wapi ni hatarishi hadi mafuriko yafike na Rais kuagiza?

Hii inaonyesha kuwa viongozi tulionao huku chini are incapable au chama na serikali haviruhusu viongozi wa chini kuwa capable.

Akili ilitumika kutengeneza tatizo haiwezi kutumia kulitaua. CCM ni ileile jana na leo, shida zoooooooote za nchi hii ni mali yake halali. Inatutia hasara na umaskini kila siku. Kwenye kutatua matatizo iliyoyatengeneza kuna upigaji mkubwa pia, vicious cycle.
 
Kama ulinielewa kwenye hoja yangu nilikwambia kuwa si maeneo yote hatarishi yalikuwa hivyo tangu awali, hatari nyingine husababishwa na mabadiliko ya tabia ya Nchi, hali ya hewa na shughuli za kibinadamu, hata hilo Bonde la Msimbazi awali halikuwa hatari kama ilivyo sasa.

Ukiangalia hilo Bonde la Mto Msimbazi utaona kingo za Mto zinameguka na kusababisha Mto kuhama na kuingia kwenye makazi ya Watu na kubomoa Nyumba..
Hakuna familia, ukoo, kabila, jamii na taifa ambalo halina marufuku kwa watu wake. Na katika kila ngazi kuna vyombo vya kusimamia marufuku hizo zitekelezwe kwa hiari au kwa lazima. Hivyo, watoto kugoma kwenda shule, kuvuta bagi na kutukana watu wazima ni udhaifu wa wazazi, na watu kujenga mabondeni, kufanya biashara barabarani popote, miji kuwa michafu, ujenzi holela, raia kukwepa kodi, watoto kukaa chini madarasani, uhaba wa madawa hospitalini na rushwa ni udhaifu wa nani?
 
Usitetee uzembe wa serikali. Uhusiano wa serikali na raia ni kama uhusiano wa baba na mwana, na kwa muktadha wa hoja inayojadiliwa, uhusiano huu ni kama wa mzazi na mtoto mdogo ambaye akili haijakomaa. Unamkataza mtoto asitende jambo fulani ni hatari, lakini bado anarudia. Hapo lazima utumie nguvu kwa manufaa ya mtoto. Utetezi kwamba waliambiwa waondoke au waliondoshwa na kulipwa fidia kisha wakarudi ni wa ovyo kabisa. Serikali Ina kila kitu- mamlaka, utaalamu, uwezo wa fedha kutekeleza jambo, rasilimali watu nk.
Ni kama vile unakuta mji unaanza mahali, mji unakuta kido kidogo maka unakuwa mji mkubwa. Pale serikali Ina kusanya kodi kwa wakazi wa eneo lile, watu wakiomba wanaunganishiwa umeme maji etc. Lakini utakutamji huo hauna huduma kama shule ya msingi/sekondari, hakuna Eno la soko, hakuna zahanati/kituo cha afya, Eneo la kuzikia nk. Ni wajibu wa serikali kwanza kutoa idhini kwamba eneo husika linafaa kwa makazi, na iweze kupangilia mji kwa kutenga maeneo kwaajili ya huduma mbalimbali.
Mbona pale Ikulu hakuna wamachinga wanaotandika mashati na bamia zao chini na kwenye fensi za majengo ya Ikulu? Mbona Mwl. Nyerere aliwahamisha watu kwa nguvu wakati wa kujenga vijiji vya ujamaa? Mbona watu wa bonde la ngorongoro wamehamishwa kutoka Serengeti kwenda ngorongoro na kisha kutoka ngorongoro kwenda Handeni Tanga?

CCM inashinda chaguzi kwa njia za kuruhusu uholela huu au serikali zake ni dhaifu sana?
 
Binadamu hamna jema, nguvu ilitumika mtakuja na hoja ya Haki za Binadamu hapa!
Kumkataza mtu asijenge sehemu hatarishi hakutumii nguvu wala pesa wala kuvunja haki ya binadamu, lakini kumuacha ajenge na kuhamia halafu umuondoe ndiko kunakovunja haki za binadamu na malalamiko. Makosa ya CCM na serikali ni kuwaacha wamalize ujenzi, kuhamia, kupelekewa umeme na maji na kuchukua kodi za majengo kisha unasema ondokeni mmejenga sehemu hatarishi.
 
Mkuu mbona serikali hiyo hiyo iliwaona watu wa Kimara /Mbezi hadi Kibaha wapo sehemu hatari (service road) na kuamua kuwa bomolea kwa nguvu makazi yao? Tena bila mariposa yeyote.
kosa ni kuwaacha wamalize kujenga na kuhamia halafu unasema mlivamia barabara ondoka is a poor governance.
 
Dubai nayo imekumbwa na mafuriko nayo yameletwa na ccm?
sababu/context ni tofauti, sisi hapa viwanja vya kuwapa bure kabisa waliokumbwa na mafuriko vipo na tunajua vilipo lakini tuliwaacha wajenge sehemu hatarishi na kwenye njia za maji. Tumeruhusu watu watumie mkaa na kuni hata kwenye majiji makuu, gesi ya kupikia haipo na ikwepo inauzwa ghali sana kuliko kipato cha mtumishi wa serikali na raia wa kawaida, bei cement ni ghali sana hivyo watu lazima wakate miti na nyasi kujenga nyumba zao, umaskini uko juu sana kiasi cha watu kuiba mifuniko ya chuma ya chemba za majitaka barabarani na vyuma vya madaraja. Hiyo yote ni CCM na serikali zake.
 
Mbona pale Ikulu hakuna wamachinga wanaotandika mashati na bamia zao chini na kwenye fensi za majengo ya Ikulu? Mbona Mwl. Nyerere aliwahamisha watu kwa nguvu wakati wa kujenga vijiji vya ujamaa? Mbona watu wa bonde la ngorongoro wamehamishwa kutoka Serengeti kwenda ngorongoro na kisha kutoka ngorongoro kwenda Handeni Tanga?

CCM inashinda chaguzi kwa njia za kuruhusu uholela huu au serikali zake ni dhaifu sana?
Mkuu,tena walipo pelekwa Gezaulole waliona kama WANAONEWA; lakini leo kijiji hicho cha vijana wasiokuwa na uwezo kimekuwa moja ya mitaa bora haha Dar
 
Mkuu,tena walipo pelekwa Gezaulole waliona kama WANAONEWA; lakini leo kijiji hicho cha vijana wasiokuwa na uwezo kimekuwa moja ya mitaa bora haha Dar
Shida yetu kuu ni kuogopa kukosa kura na kuogopa Chama kushindwa uchaguzi. Kila awamu inabuni mbinu zake za kukiepusha Chama kushindwa hata kama njia na mbinu hizo ni ovu na zenye hasara kubwa Leo na siku za mbeleni. Kiongozi/awamu anashindwa kuwakataza na kuwaondosha watu wanaojenga sehemu hatarishi, wanashindwa kuwaondoa machinga mitaani, wanashindwa kuwapa adhabu bodaboda wanaovunja Sheria z barabarani, wanaogopa kukusanya kodi, wanashindwa kukatia watu umeme wasiolipa.
 
Back
Top Bottom