CCM ni mfano halisi wa shamba la bibi, Mali za chama ni ulaji wa makada

CCM ni mfano halisi wa shamba la bibi, Mali za chama ni ulaji wa makada

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Wilayani kwetu tangu nikiwa mdogo, kuna kiwanja kilichotengwa kwa ujenzi wa Ofis za Chama Wilaya, kiwanja hiki kilikuwa kwenye prime area kinatazama barabara kuu.

Wakubwa walifika bei na kumuuzia Mwarabu ambae amejenga Hotel. Mpaka sasa ofisi ya CCM ni ile ile iliyokuwa ya TANU. Kuna pesa za ujenzi ziliwafikia, makada walibadilisha madirisha na kupaka rangi, mengine usiulize ila Ofisi ya Chama wilaya Ina vyoo vya shimo tena viwili.

Nape alipigania maslahi ya vijana walio wengi dhidi ya makada wakubwa walionufaika na jengo la Umoja wa Vijana pale Dar. Naye alipopewa ukuu wa Wilaya alinyamaza kimya. Maisha yakaendelea.

Mwalimu Nyerere alipofariki kuna Mzungu mmoja Mark Hastings aliandika chapisho kuhusu maisha ya Nyerere alivyomfahamu tangu akiwa mwanafunzi wa elimu ya juu Edinburgh. Mzungu yule aliichambua sana siasa na sera za Ujamaa na kusema kuwa, miaka ya 80-90 Watanzania waliokuwa na vitambi wengi walikua viongozi wa Chama cha Mapinduzi ambao walikuwa na uhakika wa usafiri kwani walikuwa wanaendeshwa kwenye Landrover 109.

Rais Magufuli alipoingia madharajabu iliundwa kamatiya kuhakiki Mali za Chama. Ile ripoti mpaka kesho haijawekwa hadharani.
 
Ripoti ya Mali za chama haiwezi kuwekwa hadharani maana waliokwepua mali ni wakubwa wenyewe. Kumziba mdomo mchunguzi naye kapewa UKATIBU MKUU. Ngoma inogile.
😂😂😂😂
 
Hiyo report ndio imesababisha hawa makomredi walio karibu na Mwenyekiti kushindwa.

Makomredi walishazoea kujipigia, sasa leo unawaletea mambo ya Control number wapi wapi.
 
Hiyo report ndio imesababisha hawa makomredi walio karibu na Mwenyekiti kushindwa.

Makomredi walishazoea kujipigia, sasa leo unawaletea mambo ya Control number wapi wapi.
Nidhamu CCM itarudi watakapokua chama cha upinzani.
 
Itachukua muda kuwa chama cha Upinzani, ila inavyoonekana Mkuu ata back down. Ata comply na masharti ya Mabeberu. Wajumbe wamempa msg nzito sana kwamba yote anayofanya ni bure watu wanataka pesa mifukoni na sio ndege angani
Nidhamu CCM itarudi watakapokua chama cha upinzani.
 
Itachukua muda kuwa chama cha Upinzani, ila inavyoonekana Mkuu ata back down. Ata comply na masharti ya Mabeberu. Wajumbe wamempa msg nzito sana kwamba yote anayofanya ni bure watu wanataka pesa mifukoni na sio ndege angani
Magufuli anaweza kuwa na nia njema ya kukwamisha ulaji kwenye chama na serikali lakini mambo yote yanafanyika kwa amri kutoka juu, hakuna structure ambayo warithi wake wataifuata.

Manunuzi ya ndege yangekua na tija zaidi Kama kungekuwa na mipango endelevu ya kufufua shirika kwa hatua. Si kujisifu tu kuwa Rais amenunua ndege tena kwa cash money.
 
CAG Assad aliwahi kutuambia kama nchini tuna Strong Personalities na si Institutions.
 
Ripoti ya Mali za chama haiwezi kuwekwa hadharani maana waliokwepua mali ni wakubwa wenyewe. Kumziba mdomo mchunguzi naye kapewa UKATIBU MKUU. Ngoma inogile.
Mali za urithi ndivyo zilivyo.wakubwa wakiwa wanazipiga wewe mdogo ukijifanya unajua kinachoendelea unapoozwa na kitu kidogo unatulia.
 
Back
Top Bottom